< 2 Samweli 12 >

1 Bwana akamtuma Nathani kwa Daudi. Alipofika kwake akamwambia, “Katika mji mmoja kulikuwepo na watu wawili, mmoja alikuwa tajiri na mwingine alikuwa maskini.
I posla Gospod Natana k Davidu; i on došav k njemu reèe mu: u jednom gradu bijahu dva èovjeka, jedan bogat a drugi siromah.
2 Yule mtu tajiri alikuwa na idadi kubwa sana ya kondoo na ngʼombe,
Bogati imaše ovaca i goveda vrlo mnogo;
3 lakini yule maskini hakuwa na chochote ila kondoo jike mdogo aliyekuwa amemnunua. Akamtunza kondoo huyo, akakulia kwake pamoja na watoto wake. Kondoo huyo alishiriki chakula cha bwana wake na kunywea kikombe chake hata pia huyo kondoo alilala mikononi mwa bwana wake. Kwake alikuwa kama binti yake.
A siromah nemaše ništa do jednu malu ovèicu, koju bješe kupio, i hranjaše je, te odraste uza nj i uz djecu njegovu, i jeðaše od njegova zalogaja, i iz njegove èaše pijaše, i na krilu mu spavaše, i bijaše mu kao kæi.
4 “Siku moja yule tajiri akafikiwa na mgeni, lakini huyo tajiri akaacha kuchukua mmoja wa kondoo au ngʼombe wake mwenyewe amwandalie mgeni. Badala yake akachukua yule kondoo jike mdogo aliyekuwa mali ya yule maskini na kumwandalia yule mgeni wake.”
A doðe putnik k bogatome èovjeku, a njemu bi žao uzeti iz svojih ovaca ili goveda da zgotovi putniku koji doðe k njemu; nego uze ovcu onoga siromaha, i zgotovi je èovjeku, koji doðe k njemu.
5 Daudi akawakwa na hasira dhidi ya mtu huyo tajiri na kumwambia Nathani, “Hakika kama Bwana aishivyo, mtu huyo aliyefanya hivyo anastahili kufa!
Tada se David vrlo razgnjevi na onoga èovjeka, i reèe Natanu: tako živ bio Gospod, zaslužio je smrt onaj koji je to uèinio.
6 Lazima alipe mara nne zaidi, kwa ajili ya kondoo huyo, kwa sababu amefanya jambo kama hilo na hakuwa na huruma.”
I ovcu neka plati uèetvoro, što je to uèinio i nije mu žao bilo.
7 Ndipo Nathani akamwambia Daudi, “Wewe ndiwe huyo mtu! Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikupaka mafuta uwe mfalme juu ya Israeli, nilikuokoa kutokana na mkono wa Sauli.
Tada reèe Natan Davidu: ti si taj. Ovako veli Gospod Bog Izrailjev: ja sam te pomazao za cara nad Izrailjem, i ja sam te izbavio iz ruku Saulovijeh.
8 Nilikupa nyumba ya bwana wako na wake za bwana wako mikononi mwako. Nikakupa nyumba ya Israeli na Yuda. Kama haya yote yalikuwa madogo sana, ningekupa hata zaidi.
I dao sam ti dom gospodara tvojega, i žene gospodara tvojega na krilo tvoje, dao sam ti dom Izrailjev i Judin; i ako je malo, dodao bih ti to i to.
9 Kwa nini ulilidharau neno la Bwana kwa kufanya lililo ovu machoni pake? Ulimuua Uria, Mhiti kwa upanga na kumchukua mke wake awe mkeo. Ulimuua kwa upanga wa Waamoni.
Zašto si prezreo rijeè Gospodnju èineæi što njemu nije po volji? Uriju Hetejina ubio si maèem i uzeo si ženu njegovu sebi za ženu, a njega si ubio maèem sinova Amonovijeh.
10 Basi kwa hiyo, upanga hautaondoka nyumbani mwako kamwe kwa sababu ulinidharau mimi na kumchukua mke wa Uria, Mhiti kuwa mkeo.’
Zato neæe se odmaæi maè od doma tvojega dovijeka, što si me prezreo i uzeo ženu Urije Hetejina da ti bude žena.
11 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kutoka kwa nyumba yako mwenyewe nitaleta maafa juu yako. Mbele ya macho yako mwenyewe nitatwaa wake zako na kumpa yeye aliye wa karibu nawe, naye atakutana kimwili na wake zako mchana mwangavu.
Ovako veli Gospod: evo, ja æu podignuti na te zlo iz doma tvojega, i uzeæu žene tvoje na tvoje oèi, i daæu ih bližnjemu tvojemu, te æe spavati sa ženama tvojim na vidiku svakomu.
12 Ulifanya kwa siri, lakini nitalifanya jambo hili wakati wa mchana mwangavu mbele ya Israeli yote.’”
Jer ti si uèinio tajno, ali æu ja ovo uèiniti pred svijem Izrailjem i svakomu na vidiku.
13 Ndipo Daudi akamjibu Nathani, “Nimefanya dhambi dhidi ya Bwana.” Nathani akamjibu, “Bwana amekuondolea dhambi yako. Hutakufa.
Tada reèe David Natanu: sagriješih Gospodu. A Natan reèe Davidu: i Gospod je pronio grijeh tvoj; neæeš umrijeti.
14 Lakini kwa sababu kwa kufanya hili umefanya adui za Bwana kuonyesha dharau kabisa, mwana atakayezaliwa kwako atakufa.”
Ali što si tijem djelom dao priliku neprijateljima Gospodnjim da hule, zato æe ti umrijeti sin koji ti se rodio.
15 Baada ya Nathani kurudi nyumbani kwake, Bwana akampiga yule mtoto ambaye mke wa Uria alikuwa amemzalia Daudi, akaugua.
Potom Natan otide svojoj kuæi. A Gospod udari dijete koje rodi žena Urijina Davidu, te se razbolje na smrt.
16 Daudi akamwomba Mungu kwa ajili ya mtoto. Akafunga na akaingia ndani ya nyumba yake akawa siku zote analala sakafuni usiku kucha.
I David se moljaše Bogu za dijete, i pošæaše se David, i došavši ležaše preko noæ na zemlji.
17 Wazee wa nyumbani mwake wakamwendea wakasimama karibu naye ili kumwamsha kutoka pale sakafuni, lakini akakataa, wala hakula chochote pamoja nao.
I starješine doma njegova ustaše oko njega da ga podignu sa zemlje, ali on ne htje, niti jede što s njima.
18 Kunako siku ya saba yule mtoto akafa. Watumishi wa Daudi wakaogopa kumwambia kuwa mtoto amekufa, kwa maana walifikiri, “Wakati mtoto alipokuwa angali hai, tulizungumza na Daudi lakini hakutusikiliza. Tutawezaje kumwambia kwamba mtoto amekufa? Anaweza kufanya kitu cha kujidhuru.”
A kad bi sedmi dan, umrije dijete; i ne smijahu sluge Davidove javiti mu da je dijete umrlo, jer govorahu: evo, dok dijete bijaše živo, govorasmo mu, pa nas ne htje poslušati; a kako æemo mu kazati: umrlo je dijete? hoæe ga ucvijeliti.
19 Daudi akaona kuwa watumishi wake wananongʼonezana wenyewe, naye akatambua kuwa mtoto alikuwa amekufa. Akauliza “Je, ni kwamba huyo mtoto amekufa?” Wakamjibu, “Ndiyo, mtoto amekufa.”
A David videæi gdje sluge njegove šapæu meðu sobom, dosjeti se da je umrlo dijete; i reèe David slugama svojim: je li umrlo dijete? A oni rekoše: umrlo je.
20 Basi Daudi akainuka kutoka pale sakafuni. Baada ya kuoga, akajipaka mafuta na kubadilisha nguo zake kisha akaenda ndani ya nyumba ya Bwana, akaabudu. Baada ya hapo akaenda nyumbani kwake kwa kutaka kwake, wakamwandalia chakula, naye akala.
Tada David usta sa zemlje, i umi se, i namaza se i preobuèe se; i otide u dom Gospodnji, i pokloni se. Potom opet doðe kuæi svojoj, i zaiska da mu donesu da jede; i jede.
21 Watumishi wake wakamuuliza, “Kwa nini unafanya hivi? Mtoto alipokuwa angali hai, ulifunga na kulia; lakini sasa mtoto amekufa, umeinuka na kula.”
A sluge njegove rekoše mu: šta to radiš? dok bijaše dijete živo, postio si i plakao; a kad umrije dijete, ustao si i jedeš.
22 Akajibu, “Wakati mtoto alipokuwa bado yungali hai, nilifunga na kulia. Nilifikiri, ‘Nani ajuaye? Bwana aweza kunirehemu ili kumwacha mtoto aishi.’
A on reèe: dok dijete bijaše živo, postio sam i plakao, jer govorah: ko zna, može se smilovati Gospod na me da dijete ostane živo.
23 Lakini sasa kwa kuwa amekufa, kwa nini nifunge? Je, naweza kumrudisha tena? Mimi nitakwenda kwake, lakini yeye hatanirudia mimi.”
A sada umrlo je; što bih postio? mogu li ga povratiti? ja æu otiæi k njemu, ali on neæe se vratiti k meni.
24 Ndipo Daudi akamfariji Bathsheba mkewe, akaingia kwake akakutana naye kimwili. Akazaa mwana, wakamwita jina lake Solomoni. Bwana alimpenda Solomoni.
Potom David utješi Vitsaveju ženu svoju, i otide k njoj, i leže s njom. I ona rodi sina, kojemu nadje ime Solomun. I mio bješe Gospodu.
25 Kwa kuwa Bwana alimpenda, akatuma neno kwa Daudi kwa kinywa cha nabii Nathani kuwa mtoto aitwe Yedidia kwa ajili ya Bwana.
I posla Natana proroka, te mu nadje ime Jedidija, radi Gospoda.
26 Wakati huo Yoabu akapigana dhidi ya Raba jamii ya Waamoni na kuteka ngome la kifalme.
A Joav bijuæi Ravu sinova Amonovih, uze carski grad.
27 Kisha Yoabu akatuma wajumbe kwa Daudi, kusema, “Nimepigana dhidi ya Raba, nami nimetwaa chanzo chake cha maji.
I posla poslanike k Davidu, i reèe: bih Ravu, i uzeh grad na vodi.
28 Sasa kusanya vikosi vilivyobaki na ukauzingire mji kwa jeshi na kuuteka. La sivyo, nitauteka mimi, nao utaitwa kwa jina langu.”
Nego sada skupi ostali narod, i stani u oko prema gradu, i uzmi ga, da ga ne bih ja uzeo i moje se ime spominjalo na njemu.
29 Kwa hiyo Daudi akakusanya jeshi lote akaenda Raba, akaushambulia na kuuteka.
I David skupiv sav narod otide na Ravu, i udari na nju, i uze je.
30 Akachukua taji kutoka kwa kichwa cha mfalme wao, lililokuwa na uzito wa talanta moja ya dhahabu, nayo ilizungushiwa vito vya thamani. Ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Alichukua nyara nyingi kutoka mjini huo.
I uze caru njihovu s glave krunu, u kojoj bješe talanat zlata, s dragim kamenjem, i metnuše je na glavu Davidu, i odnese iz grada plijen vrlo velik.
31 Akawatoa watu waliokuwa humo, akawaweka wafanye kazi kwa misumeno, sululu za chuma na mashoka, naye akawaweka kwenye kazi ya kutengeneza matofali. Akafanya hivi kwa miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na jeshi lake lote wakarudi Yerusalemu.
A narod koji bijaše u njemu izvede i metnu ih pod pile i pod brane gvozdene i pod sjekire gvozdene, i sagna ih u peæi gdje se opeke peku. I tako uèini svijem gradovima sinova Amonovijeh. Potom se vrati David sa svijem narodom u Jerusalim.

< 2 Samweli 12 >