< 2 Samweli 12 >
1 Bwana akamtuma Nathani kwa Daudi. Alipofika kwake akamwambia, “Katika mji mmoja kulikuwepo na watu wawili, mmoja alikuwa tajiri na mwingine alikuwa maskini.
And Jehovah sent Nathan to David. And he came to him, and said to him, There were two men in one city: the one rich, and the other poor.
2 Yule mtu tajiri alikuwa na idadi kubwa sana ya kondoo na ngʼombe,
The rich man had exceedingly many flocks and herds,
3 lakini yule maskini hakuwa na chochote ila kondoo jike mdogo aliyekuwa amemnunua. Akamtunza kondoo huyo, akakulia kwake pamoja na watoto wake. Kondoo huyo alishiriki chakula cha bwana wake na kunywea kikombe chake hata pia huyo kondoo alilala mikononi mwa bwana wake. Kwake alikuwa kama binti yake.
but the poor man had nothing except one little ewe lamb, which he had bought and nourished up. And it grew up together with him, and with his sons. It ate of his own morsel, and drank of his own cup, and lay in his bosom, and was to him as a daughter.
4 “Siku moja yule tajiri akafikiwa na mgeni, lakini huyo tajiri akaacha kuchukua mmoja wa kondoo au ngʼombe wake mwenyewe amwandalie mgeni. Badala yake akachukua yule kondoo jike mdogo aliyekuwa mali ya yule maskini na kumwandalia yule mgeni wake.”
And there came a traveler to the rich man, and he spared to take of his own flock and of his own herd to dress for the wayfaring man who came to him, but took the poor man's lamb, and dressed it for the man who came to him.
5 Daudi akawakwa na hasira dhidi ya mtu huyo tajiri na kumwambia Nathani, “Hakika kama Bwana aishivyo, mtu huyo aliyefanya hivyo anastahili kufa!
And David's anger was greatly kindled against the man, and he said to Nathan, As Jehovah lives, the man who has done this is worthy to die.
6 Lazima alipe mara nne zaidi, kwa ajili ya kondoo huyo, kwa sababu amefanya jambo kama hilo na hakuwa na huruma.”
And he shall restore the lamb fourfold, because he did this thing, and because he had no pity.
7 Ndipo Nathani akamwambia Daudi, “Wewe ndiwe huyo mtu! Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikupaka mafuta uwe mfalme juu ya Israeli, nilikuokoa kutokana na mkono wa Sauli.
And Nathan said to David, Thou are the man. Thus says Jehovah, the God of Israel, I anointed thee king over Israel, and I delivered thee out of the hand of Saul.
8 Nilikupa nyumba ya bwana wako na wake za bwana wako mikononi mwako. Nikakupa nyumba ya Israeli na Yuda. Kama haya yote yalikuwa madogo sana, ningekupa hata zaidi.
And I gave thee thy master's house, and thy master's wives into thy bosom, and gave thee the house of Israel and of Judah. And if that had been too little, I would have added to thee such and such things.
9 Kwa nini ulilidharau neno la Bwana kwa kufanya lililo ovu machoni pake? Ulimuua Uria, Mhiti kwa upanga na kumchukua mke wake awe mkeo. Ulimuua kwa upanga wa Waamoni.
Why have thou despised the word of Jehovah, to do that which is evil in his sight? Thou have smitten Uriah the Hittite with the sword, and have taken his wife to be thy wife, and have slain him with the sword of the sons of Ammon.
10 Basi kwa hiyo, upanga hautaondoka nyumbani mwako kamwe kwa sababu ulinidharau mimi na kumchukua mke wa Uria, Mhiti kuwa mkeo.’
Now therefore the sword shall never depart from thy house, because thou have despised me, and have taken the wife of Uriah the Hittite to be thy wife.
11 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kutoka kwa nyumba yako mwenyewe nitaleta maafa juu yako. Mbele ya macho yako mwenyewe nitatwaa wake zako na kumpa yeye aliye wa karibu nawe, naye atakutana kimwili na wake zako mchana mwangavu.
Thus says Jehovah, Behold, I will raise up evil against thee out of thine own house. And I will take thy wives before thine eyes, and give them to thy neighbor, and he shall lie with thy wives in the sight of this sun.
12 Ulifanya kwa siri, lakini nitalifanya jambo hili wakati wa mchana mwangavu mbele ya Israeli yote.’”
For thou did it secretly, but I will do this thing before all Israel, and before the sun.
13 Ndipo Daudi akamjibu Nathani, “Nimefanya dhambi dhidi ya Bwana.” Nathani akamjibu, “Bwana amekuondolea dhambi yako. Hutakufa.
And David said to Nathan, I have sinned against Jehovah. And Nathan said to David, Jehovah also has put away thy sin; thou shall not die.
14 Lakini kwa sababu kwa kufanya hili umefanya adui za Bwana kuonyesha dharau kabisa, mwana atakayezaliwa kwako atakufa.”
However, because by this deed thou have given great occasion to the enemies of Jehovah to blaspheme, the child also that is born to thee shall surely die.
15 Baada ya Nathani kurudi nyumbani kwake, Bwana akampiga yule mtoto ambaye mke wa Uria alikuwa amemzalia Daudi, akaugua.
And Nathan departed to his house. And Jehovah struck the child that Uriah's wife bore to David, and it was very sick.
16 Daudi akamwomba Mungu kwa ajili ya mtoto. Akafunga na akaingia ndani ya nyumba yake akawa siku zote analala sakafuni usiku kucha.
David therefore besought God for the child. And David fasted, and went in, and lay all night upon the ground.
17 Wazee wa nyumbani mwake wakamwendea wakasimama karibu naye ili kumwamsha kutoka pale sakafuni, lakini akakataa, wala hakula chochote pamoja nao.
And the elders of his house arose, and stood beside him, to raise him up from the ground, but he would not, neither did he eat bread with them.
18 Kunako siku ya saba yule mtoto akafa. Watumishi wa Daudi wakaogopa kumwambia kuwa mtoto amekufa, kwa maana walifikiri, “Wakati mtoto alipokuwa angali hai, tulizungumza na Daudi lakini hakutusikiliza. Tutawezaje kumwambia kwamba mtoto amekufa? Anaweza kufanya kitu cha kujidhuru.”
And it came to pass on the seventh day, that the child died. And the servants of David feared to tell him that the child was dead, for they said, Behold, while the child was yet alive we spoke to him, and he did not hearken to our voice, how will he then vex himself, if we tell him that the child is dead!
19 Daudi akaona kuwa watumishi wake wananongʼonezana wenyewe, naye akatambua kuwa mtoto alikuwa amekufa. Akauliza “Je, ni kwamba huyo mtoto amekufa?” Wakamjibu, “Ndiyo, mtoto amekufa.”
But when David saw that his servants were whispering together, David perceived that the child was dead. And David said to his servants, Is the child dead? And they said, He is dead.
20 Basi Daudi akainuka kutoka pale sakafuni. Baada ya kuoga, akajipaka mafuta na kubadilisha nguo zake kisha akaenda ndani ya nyumba ya Bwana, akaabudu. Baada ya hapo akaenda nyumbani kwake kwa kutaka kwake, wakamwandalia chakula, naye akala.
Then David arose from the earth, and washed, and anointed himself, and changed his apparel. And he came into the house of Jehovah, and worshiped. Then he came to his own house, and when he required, they set bread before him, and he ate.
21 Watumishi wake wakamuuliza, “Kwa nini unafanya hivi? Mtoto alipokuwa angali hai, ulifunga na kulia; lakini sasa mtoto amekufa, umeinuka na kula.”
Then his servants said to him, What thing is this that thou have done? Thou fasted and wept for the child while it was alive, but when the child was dead, thou arose and ate bread.
22 Akajibu, “Wakati mtoto alipokuwa bado yungali hai, nilifunga na kulia. Nilifikiri, ‘Nani ajuaye? Bwana aweza kunirehemu ili kumwacha mtoto aishi.’
And he said, While the child was yet alive, I fasted and wept. For I said, Who knows whether Jehovah will not be gracious to me, that the child may live?
23 Lakini sasa kwa kuwa amekufa, kwa nini nifunge? Je, naweza kumrudisha tena? Mimi nitakwenda kwake, lakini yeye hatanirudia mimi.”
But now he is dead; why should I fast? Can I bring him back again? I shall go to him, but he will not return to me.
24 Ndipo Daudi akamfariji Bathsheba mkewe, akaingia kwake akakutana naye kimwili. Akazaa mwana, wakamwita jina lake Solomoni. Bwana alimpenda Solomoni.
And David comforted Bathsheba his wife, and went in to her, and lay with her. And she bore a son, and he called his name Solomon. And Jehovah loved him,
25 Kwa kuwa Bwana alimpenda, akatuma neno kwa Daudi kwa kinywa cha nabii Nathani kuwa mtoto aitwe Yedidia kwa ajili ya Bwana.
and he sent by the hand of Nathan the prophet. And he called his name Jedidiah, for Jehovah's sake.
26 Wakati huo Yoabu akapigana dhidi ya Raba jamii ya Waamoni na kuteka ngome la kifalme.
Now Joab fought against Rabbah of the sons of Ammon, and took the royal city.
27 Kisha Yoabu akatuma wajumbe kwa Daudi, kusema, “Nimepigana dhidi ya Raba, nami nimetwaa chanzo chake cha maji.
And Joab sent messengers to David, and said, I have fought against Rabbah; yea, I have taken the city of waters.
28 Sasa kusanya vikosi vilivyobaki na ukauzingire mji kwa jeshi na kuuteka. La sivyo, nitauteka mimi, nao utaitwa kwa jina langu.”
Now therefore gather the rest of the people together, and encamp against the city, and take it, lest I take the city, and it be called after my name.
29 Kwa hiyo Daudi akakusanya jeshi lote akaenda Raba, akaushambulia na kuuteka.
And David gathered all the people together, and went to Rabbah, and fought against it, and took it.
30 Akachukua taji kutoka kwa kichwa cha mfalme wao, lililokuwa na uzito wa talanta moja ya dhahabu, nayo ilizungushiwa vito vya thamani. Ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Alichukua nyara nyingi kutoka mjini huo.
And he took the crown of their king from off his head. And the weight of it was a talent of gold, and in it were precious stones. And it was set on David's head. And he brought forth the spoil of the city, exceedingly much.
31 Akawatoa watu waliokuwa humo, akawaweka wafanye kazi kwa misumeno, sululu za chuma na mashoka, naye akawaweka kwenye kazi ya kutengeneza matofali. Akafanya hivi kwa miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na jeshi lake lote wakarudi Yerusalemu.
And he brought forth the people that were in it, and put them under saws, and under harrows of iron, and under axes of iron, and made them pass through the brick-kiln. And thus he did to all the cities of the sons of Ammon. And David and all the people returned to Jerusalem.