< 2 Samweli 11 >
1 Katika mwanzo wa mwaka mpya, wakati wafalme watokapo kwenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu pamoja na watu wa mfalme na jeshi lote la Israeli. Wakawaangamiza Waamoni na kuuzunguka kwa jeshi mji wa Raba. Lakini Daudi akabaki Yerusalemu.
Yuxhxhan qadımee, paççahar dəv'əys qığeebaç'ene gahıl, Davudee Yoav cune insanaaşikayiy gırgıne İzrailyne g'oşunuka dəv'eeqa yəqqı'l ha'a. Manbışe Ammonbışikın hı'ı, manbışda paytaxt Rabba hıqiy-allançe avqaaqqa. Davud vucmee İyerusalimcar axva.
2 Ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi aliinuka kitandani mwake na kutembeatembea juu ya paa la jumba lake la kifalme. Kutokea kule kwenye paa, akamwona mwanamke akioga. Mwanamke huyo alikuwa mzuri sana wa sura,
Sa yiğıl exheeqana, Davud tyuleençe suğotsu, cune paççahaaşine sarayne daxalqa ılqeç'u maa'ar iykar giyğal. Mana daxayle ilyakkımee, mang'uk'le sa zəiyfa əyeexər g'eece. Mana zəiyfa geer uftanna yixha.
3 naye Daudi akatuma mtu mmoja kuuliza habari za huyo mwanamke. Huyo mtu akamwambia Daudi, “Je, huyu si Bathsheba binti Eliamu, naye ni mke wa Uria, Mhiti?”
Zəiyfayne hək'ee qiyghanasva Davudee insan g'ıxele. G'axuvuyne insanee eyhen: – Mana zəiyfa Q'etbışda eyxhene Uriyna xhunaşşe, Eliamnar yiş Bat-Şeva vor.
4 Ndipo Daudi akatuma wajumbe kumleta. Huyo mwanamke akaja kwa Daudi, Daudi akakutana naye kimwili. (Huyo mwanamke ndipo tu alikuwa amejitakasa kutoka siku zake za hedhi.) Kisha akarudi nyumbani kwake.
Davudee insanar g'axuvu mana cusqa ayree'e. Mana zəiyfa Davudusqa arımee, məng'ı'n yadaaşik eyxhenbı manke ç'əveetxha ıxha. Davud məng'ı'ka g'ılexhana. Mançile qiyğa zəiyfa cene xaaqa siyk'al.
5 Huyo mwanamke akapata mimba akampelekea Daudi ujumbe, kusema, “Mimi ni mjamzito.”
Zəiyfa vuxhne eexva. Məng'ee Davudusqa insan g'ıxele «Zı vuxhne vorva» eyhes.
6 Ndipo Daudi akapeleka ujumbe kwa Yoabu, “Unipelekee Uria, Mhiti.” Naye Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
Davudee Yoavne k'anyaqa insan g'axuvu eyhen: – Q'etbışda eyxhena Uriy yizde k'anyaqa g'axıle. Yoavee Uriy Davudne k'anyaqa g'ıxele.
7 Uria alipofika, Daudi akamuuliza habari za Yoabu, hali za askari na vita kwamba inaendeleaje.
Uriy Davudne k'anyaqa arımee, Davudee mang'uke Yoaviy g'oşun nəxübne, dəv'ə nəxübne əlyhəəva qiyghan.
8 Kisha Daudi akamwambia Uria, “Teremka nyumbani kwako ukanawe miguu yako.” Basi Uria akaondoka kutoka kwenye jumba la kifalme, tena zawadi zikamfuata kutoka kwa mfalme.
Qiyğa Davudee Uriyk'le eyhen: – Xaaqa hoora, sık'ırra g'alixhe. Uriy paççahne sarayeençe qığeç'umee, paççahee yı'q'əle mang'us pay g'uxoole.
9 Lakini Uria akalala kwenye ingilio la jumba la kifalme pamoja na watumishi wote wa bwana wake, na hakuteremka kwenda nyumbani kwake.
Uriymee xaaqa ayk'an deş. Mana paççahne manesa nukaraaşika sacigee sarayne akkayne ghalee g'ılexha.
10 Daudi alipoambiwa kwamba, “Uria hakwenda nyumbani,” Daudi akamuuliza, “Je, si ndiyo tu umefika kutoka safari ya mbali? Kwa nini hukwenda nyumbani?”
Davuduk'le «Uriy xaaqa ark'ın deşva» uvhumee, mang'vee Uriyke qiyghanan: – Nya'a, ğu yəqqı'le dişde qarı? Nya'a xaaqa idyark'ın?
11 Uria akamwambia Daudi, “Sanduku la Mungu, na Israeli na Yuda wanakaa kwenye mahema, naye bwana wangu Yoabu na watu wa bwana wangu wamepiga kambi mahali pa wazi. Ningewezaje kwenda nyumbani kwangu ili nile, ninywe na kukutana na mke wangu? Hakika kama uishivyo sitafanya jambo la namna hiyo!”
Uriyee Davuduk'le eyhen: – Allahıka mugavilenana q'utye, İzrailybı, Yahuder çadırbışee aaxvamee, yizda xərna eyxhena Yoaviy eskerar g'ab çolbışee aaxvamee, ho'ne zı xaaqa ark'ın otxhan-ulyoğa xhunaşşeyka g'alixhe? Valqaniy yiğne canılqan k'ın ixhen, zı məxdın kar mısacad ha'as deş.
12 Ndipo Daudi akamwambia, “Kaa hapa siku moja zaidi, nami kesho nitakutuma urudi.” Kwa hiyo Uria akakaa Yerusalemu siku ile na siku iliyofuata.
Davudee Uriyk'le eyhen: – Ğu g'iynar inyaa axve, zı ğu g'iyqa yəqqı'l ha'asda. Uriy mane yiğılir, qinne yiğılir İyerusalim axva.
13 Kwa ukaribisho wa Daudi, Uria akala na kunywa pamoja naye, Daudi akamlevya. Lakini jioni Uria alitoka kwenda kulala juu ya mkeka wake miongoni mwa watumishi wa bwana wake, hakwenda nyumbani.
Davudee mana cusqa qort'ul yugda otxhun-ulyoğu'ı keçe xhinne qa'a. Uriy paççahısse exheeqana qığeç'e. Mana g'alixhasva meer cune ögilynecar cigeeqa, paççahne nukaraaşisqa ayk'an. Mana cune xaaqa meer ayk'an deş.
14 Asubuhi yake Daudi akamwandikia Yoabu barua, akamtuma Uria kuipeleka.
Miç'eed qıxhamee, Davudee kağız otk'un, Yoavısqa hixhar he'ecenva Uriysqa qele.
15 Ndani ya barua aliandika, “Mweke Uria mstari wa mbele mahali ambapo mapigano ni makali sana. Kisha wewe uondoke ili Uria aangushwe chini na kuuawa.”
Kağızee inva otk'un eyxhe: «Uriy it'umba dəv'ə əəne cigeeqa yəqqı'l he'e. Mana ögil ulyozar he'e, qiyğa zaraba şu yı'q'əlqa ts'ıts'eepxhe, hasre mana ı'xı' gik'ecen».
16 Hivyo Yoabu alipokuwa ameuzingira mji kwa jeshi, akamweka Uria mahali ambapo alijua kuwa ulinzi wa adui ulikuwa imara sana.
Yoavee şahar hiqiy-allançe avqumee, mang'uk'le şenbışin yugba aldaaxhvananbı nene surak vuxhay ats'anniy. Mançil-allar mang'vee Uriy mane suralqa salat' ha'a.
17 Wakati watu wa mjini walipotoka kwenda kupigana dhidi ya Yoabu, baadhi ya watu katika jeshi la Daudi wakauawa, zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, akafa.
Şaharın insanar Yoavıka səvxəsva, şaharıke g'aqa qığeebaç'e. Manke Davudne g'oşunun sabarabı habat'anbı, habat'anbışde yı'q'nee Q'etbışda eyxhena Uriyer ıxhana.
18 Yoabu akampelekea Daudi maelezo yote ya vita.
Yoavee Davudne k'anyaqa dəv'ə nəxübiy ılğevç'uva xabar ana insan g'ıxele.
19 Akamwagiza mjumbe hivi, “Utakapokuwa umemaliza kumpa mfalme maelezo ya vita,
Mang'vee xabar ana g'ıxelene insanıs xət qa'an: – Ğu dəv'əyne hək'ee yuşan hı'ı ç'əvexhemee,
20 hasira ya mfalme yaweza kuwaka, naye aweza kukuuliza, ‘Kwa nini mlisogea karibu hivyo na mji kupigana? Hamkujua kuwa wangeweza kuwapiga mishale kutoka ukutani?
paççahıs sayıb mançike qəl vuxha vake qiyghınee: «Nya'a şu səvxəsva şaharısqa manimee k'ane qeepxha? Nya'a şok'le ats'a dişdiy, manbışe cabırbışile vukbı ahas ıxhay?
21 Ni nani aliyemuua Abimeleki mwana wa Yerub-Besheth? Je, mwanamke hakutupa juu yake jiwe la juu la kusagia kutoka ukutani, kwa hiyo akafa huko Thebesi? Kwa nini mlisogea hivyo karibu ya ukuta?’ Ikiwa atakuuliza hivi, ndipo umwambie, ‘Pia mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa.’”
Şavaane Yerubbeşetna dix Avimelek gik'u? Nya'a, cabırıle dişdiy mang'ulqa sa zəiyfee yöxxəyna g'aye g'a'apçı, mana Tevetsee gik'u? Nya'a şu manimee cabırbışisqa k'ane qeepxha?» Manva paççahee vak'le uvheene, ğu mang'uk'le eyhe: «Yiğna nukar Q'etbışda eyxhena Uriyer qik'una».
22 Mjumbe akaondoka. Alipowasili akamwambia Daudi kila kitu alichokuwa ametumwa na Yoabu kusema.
Xabar ana ı'qqəna insan yəqqı'lqa gexha. Mana qarı Davudusqa hirxhıl, Yoavee cuk'le uvhuyn gırgın mang'us yuşan ha'an.
23 Mjumbe akamwambia Daudi, “Watu walituzidi nguvu wakatoka nje ya mji dhidi yetu kwenye eneo la wazi, lakini tuliwarudisha nyuma mpaka kwenye ingilio la mji.
Xabar ana arıyne insanee Davuduk'le eyhen: – Şen insanar şalqa k'yoptul, şaka saç'uvkasva şaharıke g'aqa qığeepç'ı. Şinab manbı şaharne akkabışisqamee yı'q'əlqa g'ee'epşiynbı.
24 Ndipo wapiga upinde walitupa mishale kwa watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watu wa mfalme wakafa. Zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, mtumishi wako amekufa.”
Vukbı ayhenbışee cabırbışile paççahne eskeraaşilqa vukbı gyoğu'u, paççahne eskeraaşike habat'anbıb vuxhaynbı. Yiğna nukar Q'etbışda eyxhena Uriyer maa'ar qik'una.
25 Daudi akamwambia mjumbe, “Ukamwambie Yoabu hivi, ‘Jambo hili lisikutie wasiwasi, upanga hula huyu sawa na ulavyo mwingine. Zidisha mashambulizi dhidi ya mji na uangamize.’ Mwambie Yoabu hivi ili kumtia moyo.”
Davudee xabar abıyng'uk'le eyhen: – Yoavık'le eyhe: «Mançil-alla aq'va havaxan hıma'acen. G'ılıncın ina-şena geer gik'u. Həşdiyle guc sacigeeqa sav'u, mane şaharılqa sayıb k'yoohre, mana hı'ğəəkar hee'e». Məxüd ğu Yoavıs yik'bı hele.
26 Mke wa Uria aliposikia kwamba mumewe amekufa, akamwombolezea.
Uriyne xhunaşşeyk'le Bat-Şevayk'le Uriy qik'uva g'ayxhımee, mang'us ak' avqaaqqa.
27 Baada ya muda wa maombolezo kwisha, Daudi akamtaka aletwe nyumbani kwake, naye akawa mkewe, na akamzalia mwana. Lakini jambo alilokuwa amefanya Daudi lilimchukiza Bwana.
Ak' ç'əvuvxhayle qiyğa, Davudee insan g'axuvu, Bat-Şeva cune xaaqa qiyelee'e. Məng'ı'ke cus xhunaşşe hee'e. Qiyğa məng'ee Davudus dix uxooxa. Davudee hav'una mana iş Rəbbine yik'eençe vooxhe deş.