< 2 Samweli 11 >
1 Katika mwanzo wa mwaka mpya, wakati wafalme watokapo kwenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu pamoja na watu wa mfalme na jeshi lote la Israeli. Wakawaangamiza Waamoni na kuuzunguka kwa jeshi mji wa Raba. Lakini Daudi akabaki Yerusalemu.
And it came to pass, at the return of the year, at the time when kings go out to battle, that David sent Joab, and his servants with him, and all Israel. And they destroyed the sons of Ammon, and besieged Rabbah. But David remained at Jerusalem.
2 Ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi aliinuka kitandani mwake na kutembeatembea juu ya paa la jumba lake la kifalme. Kutokea kule kwenye paa, akamwona mwanamke akioga. Mwanamke huyo alikuwa mzuri sana wa sura,
And it came to pass at evening, that David arose from off his bed, and walked upon the roof of the king's house. And from the roof he saw a woman bathing, and the woman was very beautiful to look upon.
3 naye Daudi akatuma mtu mmoja kuuliza habari za huyo mwanamke. Huyo mtu akamwambia Daudi, “Je, huyu si Bathsheba binti Eliamu, naye ni mke wa Uria, Mhiti?”
And David sent and inquired after the woman. And one said, Is not this Bathsheba, the daughter of Eliam, the wife of Uriah the Hittite?
4 Ndipo Daudi akatuma wajumbe kumleta. Huyo mwanamke akaja kwa Daudi, Daudi akakutana naye kimwili. (Huyo mwanamke ndipo tu alikuwa amejitakasa kutoka siku zake za hedhi.) Kisha akarudi nyumbani kwake.
And David sent messengers, and took her. And she came in to him, and he lay with her (for she was purified from her uncleanness), and she returned to her house.
5 Huyo mwanamke akapata mimba akampelekea Daudi ujumbe, kusema, “Mimi ni mjamzito.”
And the woman conceived. And she sent and told David, and said, I am with child.
6 Ndipo Daudi akapeleka ujumbe kwa Yoabu, “Unipelekee Uria, Mhiti.” Naye Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
And David sent to Joab, saying, Send me Uriah the Hittite. And Joab sent Uriah to David.
7 Uria alipofika, Daudi akamuuliza habari za Yoabu, hali za askari na vita kwamba inaendeleaje.
And when Uriah came to him, David asked of him how Joab did, and how the people fared, and how the war prospered.
8 Kisha Daudi akamwambia Uria, “Teremka nyumbani kwako ukanawe miguu yako.” Basi Uria akaondoka kutoka kwenye jumba la kifalme, tena zawadi zikamfuata kutoka kwa mfalme.
And David said to Uriah, Go down to thy house, and wash thy feet. And Uriah departed out of the king's house, and a gift from the king followed him.
9 Lakini Uria akalala kwenye ingilio la jumba la kifalme pamoja na watumishi wote wa bwana wake, na hakuteremka kwenda nyumbani kwake.
But Uriah slept at the door of the king's house with all the servants of his lord, and did not go down to his house.
10 Daudi alipoambiwa kwamba, “Uria hakwenda nyumbani,” Daudi akamuuliza, “Je, si ndiyo tu umefika kutoka safari ya mbali? Kwa nini hukwenda nyumbani?”
And when they had told David, saying, Uriah did not go down to his house, David said to Uriah, Have thou not come from a journey? Why did thou not go down to thy house?
11 Uria akamwambia Daudi, “Sanduku la Mungu, na Israeli na Yuda wanakaa kwenye mahema, naye bwana wangu Yoabu na watu wa bwana wangu wamepiga kambi mahali pa wazi. Ningewezaje kwenda nyumbani kwangu ili nile, ninywe na kukutana na mke wangu? Hakika kama uishivyo sitafanya jambo la namna hiyo!”
And Uriah said to David, The ark, and Israel, and Judah, abide in booths, and my lord Joab, and the servants of my lord, are encamped in the open field. Shall I then go into my house, to eat and to drink, and to lie with my wife? As thou live, and as thy soul lives, I will not do this thing.
12 Ndipo Daudi akamwambia, “Kaa hapa siku moja zaidi, nami kesho nitakutuma urudi.” Kwa hiyo Uria akakaa Yerusalemu siku ile na siku iliyofuata.
And David said to Uriah, Remain here today also, and tomorrow I will let thee depart. So Uriah abode in Jerusalem that day, and the morrow.
13 Kwa ukaribisho wa Daudi, Uria akala na kunywa pamoja naye, Daudi akamlevya. Lakini jioni Uria alitoka kwenda kulala juu ya mkeka wake miongoni mwa watumishi wa bwana wake, hakwenda nyumbani.
And when David had called him, he ate and drank before him, and he made him drunk. And at evening he went out to lie on his bed with the servants of his lord, but did not go down to his house.
14 Asubuhi yake Daudi akamwandikia Yoabu barua, akamtuma Uria kuipeleka.
And it came to pass in the morning, that David wrote a letter to Joab, and sent it by the hand of Uriah.
15 Ndani ya barua aliandika, “Mweke Uria mstari wa mbele mahali ambapo mapigano ni makali sana. Kisha wewe uondoke ili Uria aangushwe chini na kuuawa.”
And he wrote in the letter, saying, Set ye Uriah in the forefront of the hottest battle, and retire ye from him, that he may be smitten, and die.
16 Hivyo Yoabu alipokuwa ameuzingira mji kwa jeshi, akamweka Uria mahali ambapo alijua kuwa ulinzi wa adui ulikuwa imara sana.
And it came to pass, when Joab kept watch upon the city, that he assigned Uriah to the place where he knew that valiant men were.
17 Wakati watu wa mjini walipotoka kwenda kupigana dhidi ya Yoabu, baadhi ya watu katika jeshi la Daudi wakauawa, zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, akafa.
And the men of the city went out, and fought with Joab. And there fell some of the people, even of the servants of David, and Uriah the Hittite died also.
18 Yoabu akampelekea Daudi maelezo yote ya vita.
Then Joab sent and told David all the things concerning the war.
19 Akamwagiza mjumbe hivi, “Utakapokuwa umemaliza kumpa mfalme maelezo ya vita,
And he charged the messenger, saying, When thou have made an end of telling all the things concerning the war to the king,
20 hasira ya mfalme yaweza kuwaka, naye aweza kukuuliza, ‘Kwa nini mlisogea karibu hivyo na mji kupigana? Hamkujua kuwa wangeweza kuwapiga mishale kutoka ukutani?
it shall be that, if the king's wrath arise, and he says to thee, Why did ye go so near to the city to fight? Did ye not know that they would shoot from the wall?
21 Ni nani aliyemuua Abimeleki mwana wa Yerub-Besheth? Je, mwanamke hakutupa juu yake jiwe la juu la kusagia kutoka ukutani, kwa hiyo akafa huko Thebesi? Kwa nini mlisogea hivyo karibu ya ukuta?’ Ikiwa atakuuliza hivi, ndipo umwambie, ‘Pia mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa.’”
Who smote Abimelech the son of Jerubbesheth? Did not a woman cast an upper millstone upon him from the wall so that he died at Thebez? Why did ye go so near the wall? Then thou shall say, Thy servant Uriah the Hittite is dead also.
22 Mjumbe akaondoka. Alipowasili akamwambia Daudi kila kitu alichokuwa ametumwa na Yoabu kusema.
So the messenger went, and came and told David all that Joab had sent him.
23 Mjumbe akamwambia Daudi, “Watu walituzidi nguvu wakatoka nje ya mji dhidi yetu kwenye eneo la wazi, lakini tuliwarudisha nyuma mpaka kwenye ingilio la mji.
And the messenger said to David, The men prevailed against us, and came out to us into the field, and we were upon them even to the entrance of the gate.
24 Ndipo wapiga upinde walitupa mishale kwa watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watu wa mfalme wakafa. Zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, mtumishi wako amekufa.”
And the shooters shot at thy servants from off the wall. And some of the king's servants are dead, and thy servant Uriah the Hittite is dead also.
25 Daudi akamwambia mjumbe, “Ukamwambie Yoabu hivi, ‘Jambo hili lisikutie wasiwasi, upanga hula huyu sawa na ulavyo mwingine. Zidisha mashambulizi dhidi ya mji na uangamize.’ Mwambie Yoabu hivi ili kumtia moyo.”
Then David said to the messenger, Thus thou shall say to Joab, Let not this thing displease thee, for the sword devours one as well as another. Make thy battle stronger against the city, and overthrow it. And encourage thou him.
26 Mke wa Uria aliposikia kwamba mumewe amekufa, akamwombolezea.
And when the wife of Uriah heard that Uriah her husband was dead, she made lamentation for her husband.
27 Baada ya muda wa maombolezo kwisha, Daudi akamtaka aletwe nyumbani kwake, naye akawa mkewe, na akamzalia mwana. Lakini jambo alilokuwa amefanya Daudi lilimchukiza Bwana.
And when the mourning was past, David sent and took her home to his house, and she became his wife, and bore him a son. But the thing that David had done displeased Jehovah.