< 2 Samweli 11 >

1 Katika mwanzo wa mwaka mpya, wakati wafalme watokapo kwenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu pamoja na watu wa mfalme na jeshi lote la Israeli. Wakawaangamiza Waamoni na kuuzunguka kwa jeshi mji wa Raba. Lakini Daudi akabaki Yerusalemu.
U početku slijedeće godine, u doba kad kraljevi izlaze u rat, posla David Joaba i s njim svoje ljude i svega Izraela: oni pobiše Amonce i podsjedoše Rabu. A David osta u Jeruzalemu.
2 Ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi aliinuka kitandani mwake na kutembeatembea juu ya paa la jumba lake la kifalme. Kutokea kule kwenye paa, akamwona mwanamke akioga. Mwanamke huyo alikuwa mzuri sana wa sura,
A jednoga dana predveče usta David sa svoje postelje i prošeta se po krovu svoje palače. Opazi s krova ženu gdje se kupa. Ta žena bijaše izvanredno lijepa.
3 naye Daudi akatuma mtu mmoja kuuliza habari za huyo mwanamke. Huyo mtu akamwambia Daudi, “Je, huyu si Bathsheba binti Eliamu, naye ni mke wa Uria, Mhiti?”
David se propita za tu ženu i rekoše mu: “Pa to je Bat-Šeba, kći Eliamova i žena Urije Hetita!”
4 Ndipo Daudi akatuma wajumbe kumleta. Huyo mwanamke akaja kwa Daudi, Daudi akakutana naye kimwili. (Huyo mwanamke ndipo tu alikuwa amejitakasa kutoka siku zake za hedhi.) Kisha akarudi nyumbani kwake.
Nato David posla glasnika da je dovedu k njemu. Kad je došla, leže on s njom, upravo kad se bila očistila od svoje nečistoće. Zatim se ona vrati svojoj kući.
5 Huyo mwanamke akapata mimba akampelekea Daudi ujumbe, kusema, “Mimi ni mjamzito.”
Žena zatrudnje te poruči Davidu: “Trudna sam!”
6 Ndipo Daudi akapeleka ujumbe kwa Yoabu, “Unipelekee Uria, Mhiti.” Naye Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
Tada David posla poruku Joabu: “Pošalji k meni Uriju Hetita!” I Joab posla Uriju k Davidu.
7 Uria alipofika, Daudi akamuuliza habari za Yoabu, hali za askari na vita kwamba inaendeleaje.
Kad je Urija došao k njemu, zapita ga David kako je Joab, kako je vojska i kako napreduje rat.
8 Kisha Daudi akamwambia Uria, “Teremka nyumbani kwako ukanawe miguu yako.” Basi Uria akaondoka kutoka kwenye jumba la kifalme, tena zawadi zikamfuata kutoka kwa mfalme.
Potom David reče Uriji: “Siđi u svoju kuću i operi svoje noge!” Urija iziđe iz kraljeva dvora, a za njim ponesoše dar s kraljeva stola.
9 Lakini Uria akalala kwenye ingilio la jumba la kifalme pamoja na watumishi wote wa bwana wake, na hakuteremka kwenda nyumbani kwake.
Ali Urija osta da spava pred vratima kraljeva dvora sa stražarima svoga gospodara i ne ode svojoj kući.
10 Daudi alipoambiwa kwamba, “Uria hakwenda nyumbani,” Daudi akamuuliza, “Je, si ndiyo tu umefika kutoka safari ya mbali? Kwa nini hukwenda nyumbani?”
Javiše to Davidu govoreći: “Urija nije otišao svojoj kući!” Tada David upita Uriju: “Zar nisi došao s puta? Zašto ne ideš svojoj kući?”
11 Uria akamwambia Daudi, “Sanduku la Mungu, na Israeli na Yuda wanakaa kwenye mahema, naye bwana wangu Yoabu na watu wa bwana wangu wamepiga kambi mahali pa wazi. Ningewezaje kwenda nyumbani kwangu ili nile, ninywe na kukutana na mke wangu? Hakika kama uishivyo sitafanya jambo la namna hiyo!”
A Urija odgovori Davidu: “Kovčeg, Izrael i Juda borave pod šatorima, moj gospodar Joab i straža moga gospodara borave na otvorenu polju, a ja da uđem u svoju kuću da jedem i da pijem i da spavam sa svojom ženom? Živoga mi Jahve, i tako mi tvoga života, zaista neću učiniti nešto takvo!”
12 Ndipo Daudi akamwambia, “Kaa hapa siku moja zaidi, nami kesho nitakutuma urudi.” Kwa hiyo Uria akakaa Yerusalemu siku ile na siku iliyofuata.
Tada David reče Uriji: “Ostani još danas ovdje, a sutra ću te otpustiti.” Tako Urija osta u Jeruzalemu onaj dan.
13 Kwa ukaribisho wa Daudi, Uria akala na kunywa pamoja naye, Daudi akamlevya. Lakini jioni Uria alitoka kwenda kulala juu ya mkeka wake miongoni mwa watumishi wa bwana wake, hakwenda nyumbani.
Sutradan David pozva Uriju da jede i da pije pred njim i on ga opi. A uvečer Urija iziđe i leže na svoju postelju sa stražama svoga gospodara, ali svojoj kući nije otišao.
14 Asubuhi yake Daudi akamwandikia Yoabu barua, akamtuma Uria kuipeleka.
Ujutro David napisa pismo Joabu i posla ga po Uriji.
15 Ndani ya barua aliandika, “Mweke Uria mstari wa mbele mahali ambapo mapigano ni makali sana. Kisha wewe uondoke ili Uria aangushwe chini na kuuawa.”
A u tom pismu pisao je ovako: “Postavite Uriju naprijed, gdje je najžešći boj, pa uzmaknite iza njega: neka bude pogođen i neka pogine!”
16 Hivyo Yoabu alipokuwa ameuzingira mji kwa jeshi, akamweka Uria mahali ambapo alijua kuwa ulinzi wa adui ulikuwa imara sana.
Zato Joab, opsjedajući grad, postavi Uriju na mjesto gdje je znao da stoje najhrabriji ratnici.
17 Wakati watu wa mjini walipotoka kwenda kupigana dhidi ya Yoabu, baadhi ya watu katika jeshi la Daudi wakauawa, zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, akafa.
Kad su onda građani provalili van i pobili se s Joabom, pade nekoliko od njegove vojske, od Davidovih ljudi, a pogibe i Urija Hetit.
18 Yoabu akampelekea Daudi maelezo yote ya vita.
Potom Joab posla čovjeka i javi Davidu sve što se dogodilo u boju.
19 Akamwagiza mjumbe hivi, “Utakapokuwa umemaliza kumpa mfalme maelezo ya vita,
I zapovjedi glasniku ovako: “Kad pripovjediš kralju sve što se dogodilo u boju,
20 hasira ya mfalme yaweza kuwaka, naye aweza kukuuliza, ‘Kwa nini mlisogea karibu hivyo na mji kupigana? Hamkujua kuwa wangeweza kuwapiga mishale kutoka ukutani?
možda će se kralj razljutiti pa ti kazati: 'Zašto ste se primakli tako blizu gradu da navalite? Zar niste znali da se obično izmeću strijele sa zida?
21 Ni nani aliyemuua Abimeleki mwana wa Yerub-Besheth? Je, mwanamke hakutupa juu yake jiwe la juu la kusagia kutoka ukutani, kwa hiyo akafa huko Thebesi? Kwa nini mlisogea hivyo karibu ya ukuta?’ Ikiwa atakuuliza hivi, ndipo umwambie, ‘Pia mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa.’”
Tko je ubio Abimeleka, sina Jerubaalova? Nije li jedna žena bacila na njega mlinski kamen, ozgo sa zida, te je poginuo u Tebesu? Zašto ste se primakli tako blizu zidu?' Ako ti tako kaže, a ti mu reci: 'Poginuo je i tvoj sluga Urija Hetit.'”
22 Mjumbe akaondoka. Alipowasili akamwambia Daudi kila kitu alichokuwa ametumwa na Yoabu kusema.
Glasnik krenu na put, dođe k Davidu i pripovjedi mu sve što mu je naložio Joab. A David planu gnjevom na Joaba i reče glasniku: “Zašto ste se primakli tako blizu zidu? Tko je ubio Abimeleka, sina Jerubaalova? Nije li jedna žena bacila na njega mlinski kamen, ozgo sa zida, te je poginuo u Tebesu? Zašto ste se primakli tako blizu zidu?”
23 Mjumbe akamwambia Daudi, “Watu walituzidi nguvu wakatoka nje ya mji dhidi yetu kwenye eneo la wazi, lakini tuliwarudisha nyuma mpaka kwenye ingilio la mji.
Glasnik odgovori Davidu: “Ti su ljudi silovito udarali na nas i izašli su protiv nas na otvoreno polje. Mi smo ih potisnuli natrag do gradskih vrata,
24 Ndipo wapiga upinde walitupa mishale kwa watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watu wa mfalme wakafa. Zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, mtumishi wako amekufa.”
ali su strijelci sa zida stali izmetati strijele na tvoje ljude te ih je poginulo nekoliko između kraljevih slugu; tako je poginuo i tvoj sluga Urija Hetit.”
25 Daudi akamwambia mjumbe, “Ukamwambie Yoabu hivi, ‘Jambo hili lisikutie wasiwasi, upanga hula huyu sawa na ulavyo mwingine. Zidisha mashambulizi dhidi ya mji na uangamize.’ Mwambie Yoabu hivi ili kumtia moyo.”
Tada David reče glasniku: “Ovako reci Joabu: 'Nemoj to uzimati toliko k srcu, jer mač proždire sad ovoga, sad onoga. Udaraj još jače na grad i obori ga!' Tako ćeš mu vratiti srčanost!”
26 Mke wa Uria aliposikia kwamba mumewe amekufa, akamwombolezea.
Kad je Urijina žena čula da je poginuo njezin muž Urija, žalila je za svojim mužem.
27 Baada ya muda wa maombolezo kwisha, Daudi akamtaka aletwe nyumbani kwake, naye akawa mkewe, na akamzalia mwana. Lakini jambo alilokuwa amefanya Daudi lilimchukiza Bwana.
A kad je prošlo vrijeme žalosti, posla David po nju i uze je u svoj dvor, i ona mu posta ženom. I rodi mu sina. Ali djelo koje učini David bijaše zlo u očima Jahvinim.

< 2 Samweli 11 >