< 2 Samweli 10 >

1 Baada ya muda, mfalme wa Waamoni akafa, naye Hanuni mwanawe akaingia mahali pake.
Or, il arriva après cela que le roi des enfants d’Ammon mourut, et Hanon, son fils, régna en sa place.
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kama vile baba yake alivyonitendea mimi wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kuonyesha wema wake kwa Hanuni kuhusu baba yake. Watu wa Daudi walipofika katika nchi ya Waamoni,
Et David dit: Je ferai miséricorde à Hanon, fils de Naas, comme son père m’a fait miséricorde. David envoya donc, le consolant par ses serviteurs de la mort de son père. Mais lorsque les serviteurs de David furent venus dans la terre des enfants d’Ammon,
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kukutumia watu ili kuonyesha masikitiko? Je, Daudi hakuwatuma watu hawa kuchunguza na kuupeleleza mji ili kuupindua?”
Les princes des enfants d’Ammon dirent à Hanon leur seigneur: Pensez-vous que ce soit pour l’honneur de votre père, que David vous ait envoyé des consolateurs, et que ce ne soit pas pour s’enquérir de la ville, l’explorer et la détruire, que David a envoyé ses serviteurs vers vous?
4 Basi Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa kila mmoja ndevu zake nusu, akakata mavazi yao nyuma katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
C’est pourquoi Hanon prit les serviteurs de David, rasa la moitié de leur barbe, coupa la moitié de leurs vêtements jusqu’au haut des cuisses, et les renvoya.
5 Daudi alipoambiwa jambo hili, akatuma wajumbe ili kwenda kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote ndipo mje.”
Lorsque cela eut été annoncé à David, il envoya au-devant d’eux; car ces hommes étaient très honteusement confus, et David leur manda: Demeurez à Jéricho jusqu’à ce que votre barbe croisse, et alors revenez.
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, wakaajiri askari wa miguu 20,000 Waaramu kutoka Beth-Rehobu na Soba, pia mfalme wa Maaka pamoja na watu 1,000, na vilevile watu 12,000 kutoka Tobu.
Mais les enfants d’Ammon, voyant qu’ils avaient fait injure à David, envoyèrent prendre à leur solde des Syriens de Rohob, et des Syriens de Soba, vingt mille hommes de pied, mille du roi de Maacha, et douze mille d’Istob.
7 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
Ce qu’ayant appris David, il envoya Joab et toute l’armée de ses guerriers.
8 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati Waaramu wa Soba, wa Rehobu, watu wa Tobu na Maaka walikuwa peke yao kwenye eneo la wazi.
Les enfants d’Ammon sortirent donc, et rangèrent leur armée en bataille devant l’entrée même de la porte, mais les Syriens de Soba et de Rohob, d’Istob et de Maacha, étaient séparément dans la plaine.
9 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
Joab donc, voyant que la bataille était préparée contre lui et par devant et par derrière, prit de toute l’élite d’Israël, et rangea son armée en bataille contre les Syriens;
10 Akawaweka waliobaki chini ya uongozi wa Abishai nduguye na kuwapanga dhidi ya Waamoni.
Mais le reste du peuple, il le confia à Abisaï son frère, qui le rangea en bataille contre les enfants d’Ammon.
11 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itawabidi mje kunisaidia. Lakini kama Waamoni watawazidi nguvu, basi nitakuja kuwasaidia.
Et Joab dit: Si les Syriens prévalent contre moi, tu me seras en aide; mais si les enfants d’Ammon prévalent contre toi, je te secourrai.
12 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
Sois homme courageux, et combattons pour notre peuple, et la cité de notre Dieu: mais le Seigneur fera ce qui est bon à ses yeux.
13 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
C’est pourquoi Joab et le peuple qui était avec lui engagèrent le combat contre les Syriens, qui aussitôt s’enfuirent devant lui.
14 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao wakakimbia mbele ya Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi kutoka kupigana na Waamoni na kufika Yerusalemu.
Mais les enfants d’Ammon voyant que les Syriens avaient fui, s’enfuirent aussi eux-mêmes devant Abisaï, et ils entrèrent dans la ville; et Joab s’en retourna après la défaite des enfants d’Ammon, et vint à Jérusalem.
15 Baada ya Waaramu kuona wameshindwa na Israeli, wakajikusanya tena.
Les Syriens donc, voyant qu’ils avaient succombé devant Israël, s’assemblèrent tous.
16 Hadadezeri akaagiza Waaramu walioletwa kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakaenda Helamu pamoja na Shobaki jemadari wa jeshi la Hadadezeri akiwaongoza.
Et Adarézer envoya pour faire venir les Syriens, qui étaient au-delà du fleuve, et il amena leur armée; or, Sobach, maître de la milice d’Adarézer, était leur prince.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote, wakavuka Mto Yordani, wakaenda Helamu. Waaramu wakapanga vikosi vyao vya askari kukabiliana na kupigana dhidi ya Daudi.
Lorsque cela eut été annoncé à David, il réunit tout Israël, passa le Jourdain, et vint à Hélam; et les Syriens rangèrent leur armée en bataille contre David, et combattirent contre lui.
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari mia saba na askari wao wa miguu 40,000. Vilevile alimpiga Shobaki jemadari wa jeshi lao, naye akafa huko.
Et les Syriens s’enfuirent devant Israël, et David tua des Syriens sept cents hommes qui étaient sur les chariots, et quarante mille cavaliers; et il frappa Sobach, prince de la milice, lequel mourut sur-le-champ.
19 Wafalme wote waliokuwa wanamtumikia Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya amani na Waisraeli na wakawa chini yao. Hivyo Waaramu wakaogopa kuwasaidia Waamoni tena.
Or, tous les rois qui étaient venus au secours d’Adarézer, voyant qu’ils étaient vaincus par Israël, furent épouvantés, et cinquante-huit mille hommes s’enfuirent devant Israël. Et ils firent la paix avec Israël, et ils les servirent; et les Syriens craignirent de donner encore secours aux enfants d’Ammon.

< 2 Samweli 10 >