< 2 Samweli 10 >
1 Baada ya muda, mfalme wa Waamoni akafa, naye Hanuni mwanawe akaingia mahali pake.
Après cela, le roi des enfants d'Ammon mourut, et Hanun, son fils, régna à sa place.
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kama vile baba yake alivyonitendea mimi wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kuonyesha wema wake kwa Hanuni kuhusu baba yake. Watu wa Daudi walipofika katika nchi ya Waamoni,
Et David dit: J'userai de bonté envers Hanun, fils de Nachash, comme son père a usé de bonté envers moi. David envoya donc ses serviteurs pour le consoler au sujet de son père; et les serviteurs de David vinrent au pays des enfants d'Ammon.
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kukutumia watu ili kuonyesha masikitiko? Je, Daudi hakuwatuma watu hawa kuchunguza na kuupeleleza mji ili kuupindua?”
Mais les chefs d'entre les enfants d'Ammon dirent à Hanun, leur seigneur: Penses-tu que ce soit pour honorer ton père que David t'envoie des consolateurs? N'est-ce pas pour reconnaître exactement la ville, pour l'épier, et la détruire, que David envoie ses serviteurs vers toi?
4 Basi Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa kila mmoja ndevu zake nusu, akakata mavazi yao nyuma katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
Hanun prit donc les serviteurs de David, et leur fit raser la moitié de la barbe, et couper la moitié de leurs habits jusqu'aux hanches; puis il les renvoya.
5 Daudi alipoambiwa jambo hili, akatuma wajumbe ili kwenda kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote ndipo mje.”
Et cela fut rapporté à David, qui envoya au-devant d'eux; car ces hommes étaient dans une grande confusion. Et le roi leur fit dire: Tenez-vous à Jérico jusqu'à ce que votre barbe ait repoussé, et alors vous reviendrez.
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, wakaajiri askari wa miguu 20,000 Waaramu kutoka Beth-Rehobu na Soba, pia mfalme wa Maaka pamoja na watu 1,000, na vilevile watu 12,000 kutoka Tobu.
Or les enfants d'Ammon, voyant qu'ils s'étaient mis en mauvaise odeur auprès de David, envoyèrent lever à leur solde vingt mille hommes de pied chez les Syriens de Beth-Réhob et chez les Syriens de Tsoba, et mille hommes chez le roi de Maaca, et douze mille hommes chez les gens de Tob.
7 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
David, l'ayant appris, envoya Joab et toute l'armée, les plus vaillants hommes.
8 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati Waaramu wa Soba, wa Rehobu, watu wa Tobu na Maaka walikuwa peke yao kwenye eneo la wazi.
Alors les enfants d'Ammon sortirent, et se rangèrent en bataille à l'entrée de la porte; et les Syriens de Tsoba, et de Réhob, et ceux de Tob et de Maaca, étaient à part dans la campagne.
9 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
Et Joab, voyant que leur armée était tournée contre lui devant et derrière, choisit d'entre tous ceux d'Israël des hommes d'élite, et les rangea contre les Syriens.
10 Akawaweka waliobaki chini ya uongozi wa Abishai nduguye na kuwapanga dhidi ya Waamoni.
Et il donna la conduite du reste du peuple à Abishaï, son frère, qui les rangea contre les enfants d'Ammon.
11 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itawabidi mje kunisaidia. Lakini kama Waamoni watawazidi nguvu, basi nitakuja kuwasaidia.
Et il lui dit: Si les Syriens sont plus forts que moi, tu me viendras en aide; et si les enfants d'Ammon sont plus forts que toi, j'irai te délivrer.
12 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
Sois vaillant, et combattons vaillamment pour notre peuple et pour les villes de notre Dieu; et que l'Éternel fasse ce qui lui semblera bon.
13 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
Alors Joab et le peuple qui était avec lui, s'approchèrent pour livrer bataille aux Syriens, et ils s'enfuirent devant lui.
14 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao wakakimbia mbele ya Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi kutoka kupigana na Waamoni na kufika Yerusalemu.
Et les enfants d'Ammon, voyant que les Syriens avaient pris la fuite, s'enfuirent aussi devant Abishaï, et rentrèrent dans la ville. Et Joab s'en retourna de la poursuite des enfants d'Ammon, et vint à Jérusalem.
15 Baada ya Waaramu kuona wameshindwa na Israeli, wakajikusanya tena.
Mais les Syriens, voyant qu'ils avaient été battus par ceux d'Israël, se rallièrent.
16 Hadadezeri akaagiza Waaramu walioletwa kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakaenda Helamu pamoja na Shobaki jemadari wa jeshi la Hadadezeri akiwaongoza.
Et Hadarézer envoya, et fit venir les Syriens d'au delà du fleuve, et ils vinrent à Hélam; et Shobac, chef de l'armée de Hadarézer, les conduisait.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote, wakavuka Mto Yordani, wakaenda Helamu. Waaramu wakapanga vikosi vyao vya askari kukabiliana na kupigana dhidi ya Daudi.
Cela fut rapporté à David, qui assembla tout Israël, passa le Jourdain, et vint à Hélam. Et les Syriens se rangèrent en bataille contre David, et combattirent contre lui.
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari mia saba na askari wao wa miguu 40,000. Vilevile alimpiga Shobaki jemadari wa jeshi lao, naye akafa huko.
Mais les Syriens s'enfuirent devant Israël; et David défit sept cents chars des Syriens et quarante mille cavaliers. Il frappa aussi Shobac, chef de leur armée, qui mourut là.
19 Wafalme wote waliokuwa wanamtumikia Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya amani na Waisraeli na wakawa chini yao. Hivyo Waaramu wakaogopa kuwasaidia Waamoni tena.
Et quand tous les rois, soumis à Hadarézer, virent qu'ils avaient été battus par Israël, ils firent la paix avec les Israélites, et leur furent assujettis; et les Syriens craignirent de donner encore du secours aux enfants d'Ammon.