< 2 Samweli 10 >
1 Baada ya muda, mfalme wa Waamoni akafa, naye Hanuni mwanawe akaingia mahali pake.
Après cela, il advint que le roi des fils d'Ammon mourut, et qu'Annon, son fils, régna à sa place.
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kama vile baba yake alivyonitendea mimi wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kuonyesha wema wake kwa Hanuni kuhusu baba yake. Watu wa Daudi walipofika katika nchi ya Waamoni,
Et David dit: Je serai compatissant envers Annon, fils de Naas, de même que son père a été compatissant pour moi; en conséquence, il envoya, pour le consoler de la mort de son père, des serviteurs qui allèrent en la contrée des fias d'Ammon.
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kukutumia watu ili kuonyesha masikitiko? Je, Daudi hakuwatuma watu hawa kuchunguza na kuupeleleza mji ili kuupindua?”
Mais, les princes des fils d'Ammon dirent à Annon, leur maître: Est-ce pour glorifier devant toi ton père que David envoie ces consolateurs? N'est-ce point plutôt pour s'informer de ta ville, et pour la reconnaître par eux-mêmes, que David a chargé ses serviteurs de venir auprès de toi.
4 Basi Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa kila mmoja ndevu zake nusu, akakata mavazi yao nyuma katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
Annon saisit donc les serviteurs de David; il leur rasa la barbe, il coupa le bas de leurs manteaux, à partir du milieu des reins, et il les chassa.
5 Daudi alipoambiwa jambo hili, akatuma wajumbe ili kwenda kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote ndipo mje.”
On vint dire à David ce qui leur était arrivé, et il envoya des gens à leur rencontre; car ils étaient cruellement déshonorés, et il leur dit: Demeurez à Jéricho jusqu'à ce que votre barbe ait repoussé; puis, alors vous reviendrez.
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, wakaajiri askari wa miguu 20,000 Waaramu kutoka Beth-Rehobu na Soba, pia mfalme wa Maaka pamoja na watu 1,000, na vilevile watu 12,000 kutoka Tobu.
Les fils d'Ammon, voyant que le peuple de David se tenait pour outragé, firent partir des messagers, et ils enrôlèrent à prix d'or les Syriens de Bethraam, ceux de Suba, ceux de Rhoob, qui leur fournirent vingt mille piétons; le roi d'Amalec en fournit mille, et Istob douze mille.
7 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
David l'apprit et il mit en mouvement Joab avec toute l'armée, et les hommes vaillants.
8 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati Waaramu wa Soba, wa Rehobu, watu wa Tobu na Maaka walikuwa peke yao kwenye eneo la wazi.
Et les fils d'Ammon sortirent; et ils se rangèrent en bataille près de la porte de Suba en Syrie; cependant, Rhoob, Istob et Amalec étaient détachés dans la campagne.
9 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
Joab reconnut qu'il aurait à livrer bataille devant son front et sur ses derrières; il rangea donc en face des Syriens les plus vaillants des jeunes fils d'Israël.
10 Akawaweka waliobaki chini ya uongozi wa Abishai nduguye na kuwapanga dhidi ya Waamoni.
Et il confia à son frère Abessa le reste de l'armée, qui se déploya contre les fils d'Ammon.
11 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itawabidi mje kunisaidia. Lakini kama Waamoni watawazidi nguvu, basi nitakuja kuwasaidia.
Et il dit à son frère: Si les Syriens l'emportent sur moi, tu viendras à mon aide, et si les fils d'Ammon te font plier, j'irai te secourir.
12 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
Sois fort, agissons en hommes, pour l'amour de notre peuple et des villes de notre Dieu; que le Seigneur ensuite fasse à sa volonté.
13 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
Et Joab avec sa troupe tomba sur les Syriens, et ceux-ci s'enfuirent devant lui.
14 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao wakakimbia mbele ya Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi kutoka kupigana na Waamoni na kufika Yerusalemu.
Quand les fils d'Ammon virent que les Syriens fuyaient, ils s'enfuirent eux-mêmes devant Abessa, et ils s'enfermèrent dans leur ville; Joab les y laissa pour revenir à Jérusalem.
15 Baada ya Waaramu kuona wameshindwa na Israeli, wakajikusanya tena.
Mais la Syrie, voyant qu'elle avait échoué devant Israël, se leva tout entière, pour reprendre l'attaque.
16 Hadadezeri akaagiza Waaramu walioletwa kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakaenda Helamu pamoja na Shobaki jemadari wa jeshi la Hadadezeri akiwaongoza.
Adraazar dépêcha des messagers, et il appela les Syriens des rives du fleuve Chalamac, et ils se rendirent à Elam. Et Sobac, général de l'armée d'Adraazar, fut mis à leur tête.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote, wakavuka Mto Yordani, wakaenda Helamu. Waaramu wakapanga vikosi vyao vya askari kukabiliana na kupigana dhidi ya Daudi.
On en instruisit David, qui réunit tout Israël, passa le Jourdain, et atteignit Elam. Et les Syriens se déployèrent devant David, et ils lui livrèrent bataille.
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari mia saba na askari wao wa miguu 40,000. Vilevile alimpiga Shobaki jemadari wa jeshi lao, naye akafa huko.
Les Syriens s'enfuirent devant Israël; David leur détruisit sept cents chars et quarante mille cavaliers; et il frappa mortellement Sobac, général de leur armée, qui mourut sur le lieu même.
19 Wafalme wote waliokuwa wanamtumikia Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya amani na Waisraeli na wakawa chini yao. Hivyo Waaramu wakaogopa kuwasaidia Waamoni tena.
Et tous les rois, serviteurs d'Adraazar, voyant qu'il avait échoué devant Israël, se donnèrent à David; ils lui furent asservis, et la Syrie eut crainte de secourir encore les fils d'Ammon.