< 2 Samweli 10 >

1 Baada ya muda, mfalme wa Waamoni akafa, naye Hanuni mwanawe akaingia mahali pake.
Forsothe it was doon aftir these thingis, that Naas, kyng of the sones of Amon, diede; and Anoon, his sone, regnede for hym. And Dauid seide,
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kama vile baba yake alivyonitendea mimi wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kuonyesha wema wake kwa Hanuni kuhusu baba yake. Watu wa Daudi walipofika katika nchi ya Waamoni,
Y schal do mercy with Anon, the sone of Naas, as his fadir dide mercy with me. Therfor Dauid sente coumfortynge hym by hise seruauntis on the deeth of the fadir. Sotheli whanne the seruauntis of Dauid hadden come in to the lond of the sones of Amon,
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kukutumia watu ili kuonyesha masikitiko? Je, Daudi hakuwatuma watu hawa kuchunguza na kuupeleleza mji ili kuupindua?”
princes of the sones of Amon seiden to Anon, her lord, Gessist thou that for the onour of thi fadir Dauid sente coumfortouris to thee; and not herfor Dauid sente hise seruauntis to thee, that he schulde aspie, and enserche the citee, and distrie it?
4 Basi Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa kila mmoja ndevu zake nusu, akakata mavazi yao nyuma katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
Therfor Anoon took the seruauntis of Dauid, and schauyde half the part of `the beerd of hem, and he kittide awey the myddil clothis of hem `til to the buttokis; and lefte hem.
5 Daudi alipoambiwa jambo hili, akatuma wajumbe ili kwenda kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote ndipo mje.”
And whanne this was teld to Dauid, he sente in to the comyng of hem, for the men weren schent ful vilensly. And Dauid comaundide to hem, Dwelle ye in Jerico, til youre beerd wexe, and thanne turne ye ayen.
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, wakaajiri askari wa miguu 20,000 Waaramu kutoka Beth-Rehobu na Soba, pia mfalme wa Maaka pamoja na watu 1,000, na vilevile watu 12,000 kutoka Tobu.
Sotheli the sones of Amon sien, that thei hadden do wrong to Dauid, and thei senten, and hiriden bi meede Roob of Sirye, and Soba of Sirie, twenti thousynde of foot men, and of kyng Maacha, a thousynde men, and of Istob twelue thousynde of men.
7 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
And whanne Dauid hadde herd this, he sent Joab and al the oost of fiyteris.
8 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati Waaramu wa Soba, wa Rehobu, watu wa Tobu na Maaka walikuwa peke yao kwenye eneo la wazi.
Therfor the sones of Amon yeden out, and dressiden scheltrun bifor hem in the entryng of the yate. Forsothe Soba, and Roob of Sirie, and Istob, and Maacha weren asidis half in the feeld.
9 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
Therfor Joab siy, that batel was maad redi ayens hym, bothe euene ayens and bihynde the bak; and he chees to hym silf of alle the chosun men of Israel, and ordeynede scheltrun ayens Sirus.
10 Akawaweka waliobaki chini ya uongozi wa Abishai nduguye na kuwapanga dhidi ya Waamoni.
Forsothe he bitook to Abisai, his brothir, the tother part of the puple, which dresside scheltrun ayens the sones of Amon.
11 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itawabidi mje kunisaidia. Lakini kama Waamoni watawazidi nguvu, basi nitakuja kuwasaidia.
And Joab seide, If men of Sirie han the maistrie ayens me, thou schalt be to me in to help; sotheli if the sones of Amon han the maistrie ayens thee, Y schal helpe thee;
12 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
be thou a strong man, and fiyte we for oure puple, and for the citee of oure God; forsothe the Lord schal do that, that is good in his siyt.
13 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
Therfor Joab and his puple that was with hym, bigan batel ayens men of Sirie, whiche fledden anoon fro his face.
14 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao wakakimbia mbele ya Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi kutoka kupigana na Waamoni na kufika Yerusalemu.
Forsothe the sones of Amon sien, that men of Sirie hadden fled; and thei fledden also fro the face of Abisai, and entriden in to the citee; and Joab turnede ayen fro the sones of Amon, and cam in to Jerusalem.
15 Baada ya Waaramu kuona wameshindwa na Israeli, wakajikusanya tena.
Forsothe men of Sirye sien that thei hadden feld bifor Israel, and thei weren gaderid to gidere.
16 Hadadezeri akaagiza Waaramu walioletwa kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakaenda Helamu pamoja na Shobaki jemadari wa jeshi la Hadadezeri akiwaongoza.
And Adadezer sente, and ledde out men of Sirie that weren biyende the flood, and he brouyte the oost of hem; sotheli Sobach, mayster of the chyualrie of Adadezer, was the prince of hem.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote, wakavuka Mto Yordani, wakaenda Helamu. Waaramu wakapanga vikosi vyao vya askari kukabiliana na kupigana dhidi ya Daudi.
And whanne this was teld to Dauid, he drow togidere al Israel, and passide Jordan, and cam in to Helama. And men of Sirie dressiden scheltrun ayens Dauid, and fouyten ayens hym.
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari mia saba na askari wao wa miguu 40,000. Vilevile alimpiga Shobaki jemadari wa jeshi lao, naye akafa huko.
And Sireis fledden fro the face of Israel; and Dauid killide of Sireis seuene hundrid charis, and fourti thousynde of knyytis; and he smoot Sobach, the prince of chyualrie, which was deed anoon.
19 Wafalme wote waliokuwa wanamtumikia Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya amani na Waisraeli na wakawa chini yao. Hivyo Waaramu wakaogopa kuwasaidia Waamoni tena.
Forsothe alle kyngis, that weren in the help of Adadezer, siyen that thei weren ouercomun of Israel, and thei maden pees with Israel, and serueden hem; and Sireis dredden to yyue help to the sones of Amon.

< 2 Samweli 10 >