< 2 Samweli 10 >
1 Baada ya muda, mfalme wa Waamoni akafa, naye Hanuni mwanawe akaingia mahali pake.
Sometime after this, Nahash, the Ammonite king died and his son Hanun succeeded him.
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kama vile baba yake alivyonitendea mimi wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kuonyesha wema wake kwa Hanuni kuhusu baba yake. Watu wa Daudi walipofika katika nchi ya Waamoni,
David said, “I will be kind to Hanun, son of Nahash, just as his father was kind to me.” So David sent representatives to take his condolences to Hanun regarding his father. But when they arrived in the country of the Ammonites,
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kukutumia watu ili kuonyesha masikitiko? Je, Daudi hakuwatuma watu hawa kuchunguza na kuupeleleza mji ili kuupindua?”
the Ammonite military leaders said to Hanun their king, “Do you really believe David sent condolences to you out of respect for your father? Isn't it more likely that David sent his representatives to scout out the city, spy on it, and then conquer it?”
4 Basi Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa kila mmoja ndevu zake nusu, akakata mavazi yao nyuma katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
So Hanun had David's representatives detained, shaved off half of each man's beard, cut off their clothes at the buttocks, and then sent them back home.
5 Daudi alipoambiwa jambo hili, akatuma wajumbe ili kwenda kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote ndipo mje.”
When David was told about this, he sent messengers to meet them, because they were very embarrassed. The king instructed them, “Stay in Jericho until your beards have re-grown, and then you can return.”
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, wakaajiri askari wa miguu 20,000 Waaramu kutoka Beth-Rehobu na Soba, pia mfalme wa Maaka pamoja na watu 1,000, na vilevile watu 12,000 kutoka Tobu.
When the Ammonites realized they had become like a bad smell to David, they sent a request to the Arameans and hired twenty thousand of their foot soldiers from Beth Rehob and Zobah, as well as one thousand men from the king of Maakah, and also twelve thousand men from Tob.
7 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
When David learned of this, he sent Joab and the entire army to confront them.
8 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati Waaramu wa Soba, wa Rehobu, watu wa Tobu na Maaka walikuwa peke yao kwenye eneo la wazi.
The Ammonites set up their battle lines near the entrance to their town gate, while the Arameans of Zobah and Rehob and the men of Tob and Maacah took up positions by themselves in the open fields.
9 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
Joab realized he would have to fight both in front of him and behind him, he chose some of Israel's best troops and he took charge of them to lead the attack the Arameans.
10 Akawaweka waliobaki chini ya uongozi wa Abishai nduguye na kuwapanga dhidi ya Waamoni.
He put the rest of the army under the command of Abishai, his brother. They were to attack the Ammonites.
11 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itawabidi mje kunisaidia. Lakini kama Waamoni watawazidi nguvu, basi nitakuja kuwasaidia.
Joab told him, “If the Arameans are stronger than me, you come and help me. If the Ammonites are stronger than you, I'll come and help you.
12 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
Be brave, and fight your best for our people and the towns of our God. May the Lord do what he sees as good!”
13 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
Joab attacked the Arameans with his forces and they ran away from him.
14 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao wakakimbia mbele ya Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi kutoka kupigana na Waamoni na kufika Yerusalemu.
When the Ammonites saw that the Arameans had run away, they also ran away from Abishai, and retreated into the town. So Joab went back to Jerusalem after fighting the Ammonites.
15 Baada ya Waaramu kuona wameshindwa na Israeli, wakajikusanya tena.
As soon as the Arameans saw they had been defeated by the Israelites they reassembled their forces.
16 Hadadezeri akaagiza Waaramu walioletwa kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakaenda Helamu pamoja na Shobaki jemadari wa jeshi la Hadadezeri akiwaongoza.
Hadadezer sent for more Arameans to be brought from beyond the Euphrates River. They arrived in Helam under the leadership of Shobach, commander of Hadadezer's army.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote, wakavuka Mto Yordani, wakaenda Helamu. Waaramu wakapanga vikosi vyao vya askari kukabiliana na kupigana dhidi ya Daudi.
When this was reported to David, he assembled all Israel together. He crossed the Jordan and advanced on Helam. The Arameans positioned themselves in battle line against David and fought him.
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari mia saba na askari wao wa miguu 40,000. Vilevile alimpiga Shobaki jemadari wa jeshi lao, naye akafa huko.
But the Aramean army ran away from the Israelites, and David killed 700 charioteers and 40,000 infantry. He also attacked Shobach, their army commander, and he died there.
19 Wafalme wote waliokuwa wanamtumikia Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya amani na Waisraeli na wakawa chini yao. Hivyo Waaramu wakaogopa kuwasaidia Waamoni tena.
When all the kings allied with Hadadezer realized that they had been defeated by Israel, they made peace with David and became subject to him. As a result, the Arameans were afraid to help the Ammonites any more.