< 2 Samweli 10 >

1 Baada ya muda, mfalme wa Waamoni akafa, naye Hanuni mwanawe akaingia mahali pake.
Poslije toga umrije Nahaš, kralj Amonaca, a zakralji se njegov sin Hanun mjesto njega.
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kama vile baba yake alivyonitendea mimi wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kuonyesha wema wake kwa Hanuni kuhusu baba yake. Watu wa Daudi walipofika katika nchi ya Waamoni,
A David reče u sebi: “Želio bih iskazati ljubav Nahaševu sinu Hanunu, kao što je njegov otac iskazao meni.” Zato David posla svoje sluge da mu izraze sućut zbog njegova oca. Ali kad su Davidove sluge došle u zemlju Amonaca,
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kukutumia watu ili kuonyesha masikitiko? Je, Daudi hakuwatuma watu hawa kuchunguza na kuupeleleza mji ili kuupindua?”
rekoše knezovi Amonaca svome gospodaru Hanunu: “Zar misliš da je David poslao ljude da ti izraze sućut zato što bi htio iskazati čast tvome ocu? Nije li možda zato David poslao svoje ljude k tebi da razvide grad da bi doznao njegovu obranu i potom ga oborio?”
4 Basi Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa kila mmoja ndevu zake nusu, akakata mavazi yao nyuma katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
Tada Hanun pograbi Davidove sluge, obrija im pola brade i skrati im haljine dopola, sve do zadnjice, i posla ih natrag.
5 Daudi alipoambiwa jambo hili, akatuma wajumbe ili kwenda kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote ndipo mje.”
Kad su to javili Davidu, posla on čovjeka pred njih, jer su ti ljudi bili teško osramoćeni, i poruči im: “Ostanite u Jerihonu dok vam ne naraste brada, pa se onda vratite!”
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, wakaajiri askari wa miguu 20,000 Waaramu kutoka Beth-Rehobu na Soba, pia mfalme wa Maaka pamoja na watu 1,000, na vilevile watu 12,000 kutoka Tobu.
Tada Amonci uvidješe da su se omrazili s Davidom; zato Amonci poslaše glasnike da za plaću unajme Aramejce iz Bet Rehoba i Aramejce iz Sobe, dvadeset tisuća pješaka, zatim kralja Maake, tisuću ljudi, i ljude iz Toba, dvanaest tisuća vojnika.
7 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
Kad je David to čuo, posla Joaba s vojskom i izabranim junacima.
8 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati Waaramu wa Soba, wa Rehobu, watu wa Tobu na Maaka walikuwa peke yao kwenye eneo la wazi.
Amonci iziđoše i svrstaše se u bojni red pred gradskim vratima, dok su Aramejci iz Sobe i iz Rehoba i ljudi iz Toba i iz Maake stajali zasebno na polju.
9 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
Vidjevši postavljene bojne redove prema sebi sprijeda i straga, probra Joab najvrsnije među Izraelcima i svrsta ih prema Aramejcima.
10 Akawaweka waliobaki chini ya uongozi wa Abishai nduguye na kuwapanga dhidi ya Waamoni.
Ostalu vojsku predade bratu Abišaju da je svrsta prema Amoncima.
11 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itawabidi mje kunisaidia. Lakini kama Waamoni watawazidi nguvu, basi nitakuja kuwasaidia.
I reče mu: “Ako Aramejci budu jači od mene, onda ti meni priskoči u pomoć; ako Amonci budu jači od tebe, ja ću tebi pohrliti u pomoć.
12 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
Budi hrabar i junački se držimo radi naroda i radi gradova svoga Boga; a Jahve neka učini što je dobro u njegovim očima.”
13 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
Tada se Joab i vojska koja je bila s njim počeše primicati da udare na Aramejce, ali oni pobjegoše pred njima.
14 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao wakakimbia mbele ya Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi kutoka kupigana na Waamoni na kufika Yerusalemu.
Kad su Amonci vidjeli da su Aramejci pobjegli, umakoše i oni ispred Abišaja i povukoše se u grad. Tada Joab odustane od rata protiv Amonaca i vrati se u Jeruzalem.
15 Baada ya Waaramu kuona wameshindwa na Israeli, wakajikusanya tena.
Kad su Aramejci vidjeli gdje su ih Izraelci razbili, sabraše ponovo svoje čete.
16 Hadadezeri akaagiza Waaramu walioletwa kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakaenda Helamu pamoja na Shobaki jemadari wa jeshi la Hadadezeri akiwaongoza.
Hadadezer posla glasnike i sabra Aramejce što su s one strane rijeke. Ovi dođoše u Helam pod vodstvom Šobaka, vojvode Hadadezerove vojske.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote, wakavuka Mto Yordani, wakaenda Helamu. Waaramu wakapanga vikosi vyao vya askari kukabiliana na kupigana dhidi ya Daudi.
Pošto su to javili Davidu, on skupi sve Izraelce i, prešavši preko Jordana, dođe u Helam. Aramejci se svrstaše protiv Davida i zametnuše s njime boj.
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari mia saba na askari wao wa miguu 40,000. Vilevile alimpiga Shobaki jemadari wa jeshi lao, naye akafa huko.
Ali Aramejci udariše u bijeg ispred Izraelaca i David im pobi sedam stotina konja od bojnih kola i četrdeset tisuća pješaka; pogubi i njihova vojvodu Šobaka te je ondje umro.
19 Wafalme wote waliokuwa wanamtumikia Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya amani na Waisraeli na wakawa chini yao. Hivyo Waaramu wakaogopa kuwasaidia Waamoni tena.
A kad svi kraljevi, Hadadezerovi vazali, vidješe da ih je razbio Izrael, sklopiše mir s Izraelom i počeše mu služiti. A Aramejci se više nisu usuđivali pomagati Amoncima.

< 2 Samweli 10 >