< 2 Samweli 10 >

1 Baada ya muda, mfalme wa Waamoni akafa, naye Hanuni mwanawe akaingia mahali pake.
Hathnukkhu, Ammon siangpahrang teh a due. A capa Hanun ni a na pa e yueng lah siangpahrang a tawk.
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kama vile baba yake alivyonitendea mimi wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kuonyesha wema wake kwa Hanuni kuhusu baba yake. Watu wa Daudi walipofika katika nchi ya Waamoni,
Devit ni Hanun e a na pa Nahash teh kai koe ahawinae a sak dawkvah, pahrennae ka kamnue sak van han telah ati. A na pa a due nah lungpahawi hanelah a sannaw a patoun teh, Devit e sannaw teh Ammonnaw e ram koe a pha awh.
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kukutumia watu ili kuonyesha masikitiko? Je, Daudi hakuwatuma watu hawa kuchunguza na kuupeleleza mji ili kuupindua?”
Ammon miphun kacuenaw ni amamae a bawipa Hanun koevah, Devit ni na barilawa dawkvah, nang koe lungmawng nahanelah, tami a patoun e na yuem maw. Devit ni hete khopui a raphoe thai nahan ka tuet hanelah nang koe a patoun awh nahoehmaw telah atipouh awh.
4 Basi Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa kila mmoja ndevu zake nusu, akakata mavazi yao nyuma katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
Hanun ni Devit e a sannaw a man teh, a pâkhamuen tangawn a ngaw pouh. A khohna hai a laheibaw totouh a a pouh hnukkhu a cei sak.
5 Daudi alipoambiwa jambo hili, akatuma wajumbe ili kwenda kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote ndipo mje.”
Hote kamthang hah Devit ni a thai toteh, ahnimanaw teh a kaya poung dawkvah, ahnimanaw dawn sak hanelah a patoun teh, nangmouh teh pâkhamuen a saw hoehroukrak Jeriko kho dawkvah awm awh. Hahoi torei bout tho awh telah atipouh.
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, wakaajiri askari wa miguu 20,000 Waaramu kutoka Beth-Rehobu na Soba, pia mfalme wa Maaka pamoja na watu 1,000, na vilevile watu 12,000 kutoka Tobu.
Ammonnaw ni vah, maimouh teh Devit e hmaitung panuettho e lah o awh han tie a panue awh teh, taminaw a patoun awh teh, Bethrekhob kho hoi Aramzobah kho e Siria ransa 20,000, hoi siangpahrang Maakah e tami 1,000, hoi Tob ram e tami 12,000 touh hah a hlai awh.
7 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
Devit ni hote kamthang a thai toteh, Joab hoi athakaawme ransanaw hah a patoun.
8 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati Waaramu wa Soba, wa Rehobu, watu wa Tobu na Maaka walikuwa peke yao kwenye eneo la wazi.
Ammonnaw hah a tâco awh teh, kho longkha koe a tungpup awh. Aramzobah kho, Rehob, Tob kho hoi ka tho e Siria tami hoi Maakah siangpahrang e taminaw teh aloukcalah law vah ao awh.
9 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
A hnukhma lahoi tuk hane na kâcai awh tie Joab ni a thai navah, Isarelnaw thung dawk hoi kahawi kahawi e a rawi teh, Sirianaw tuk hanelah namranlah a tumpup awh.
10 Akawaweka waliobaki chini ya uongozi wa Abishai nduguye na kuwapanga dhidi ya Waamoni.
Aloukenaw pueng hah a hmaunawngha Abisai kut dawk koung a hruek teh, Ammon tami tuk hanelah a tumpup sak awh.
11 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itawabidi mje kunisaidia. Lakini kama Waamoni watawazidi nguvu, basi nitakuja kuwasaidia.
Siria taminaw ni kai na tâ pawiteh, nangmouh ni na kabawp han. Ammonnaw ni nangmanaw na tâ pawiteh, kaimouh ni na kabawp han.
12 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
Tarankahawi lah awm awh. Ka taminaw hoi mamae Cathut khonaw hanelah thapatung awh nateh, tuk awh. BAWIPA ni a ngainae patetlah a sak han doeh atipouh.
13 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
Ama koe kaawm e taminaw hoi Siria taminaw tuk hanelah a pâtam awh teh, Sirianaw a yawng awh.
14 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao wakakimbia mbele ya Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi kutoka kupigana na Waamoni na kufika Yerusalemu.
Sirianaw a yawng awh e Ammonnaw ni a hmu awh navah, ahnimouh hai Abisai hmalah a yawng awh teh, kho thung vah a kâen awh. Joab hai Ammon ram hoi a tâco teh Jerusalem kho lah a cei.
15 Baada ya Waaramu kuona wameshindwa na Israeli, wakajikusanya tena.
Sirianaw ni Isarelnaw e a hmalah amamanaw a sung e a kâpanue awh navah bout a kamkhueng awh.
16 Hadadezeri akaagiza Waaramu walioletwa kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakaenda Helamu pamoja na Shobaki jemadari wa jeshi la Hadadezeri akiwaongoza.
Hadadezer ni tami a patoun teh, tui namran lah kaawm e Sirianaw a thokhai teh, Hadadezer ransa kacue e Shobak ni a hrawi awh teh, Helam kho lah a cei awh.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote, wakavuka Mto Yordani, wakaenda Helamu. Waaramu wakapanga vikosi vyao vya askari kukabiliana na kupigana dhidi ya Daudi.
Hote kong Devit koe a dei pouh. Isarelnaw pueng koung a pâkhueng teh, Jordan tui a raka awh teh, Helam kho a pha awh. Sirianaw ni Devit tuk hanelah a kampawp awh teh a tuk awh.
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari mia saba na askari wao wa miguu 40,000. Vilevile alimpiga Shobaki jemadari wa jeshi lao, naye akafa huko.
Sirianaw teh Isarelnaw e hmalah hoi a yawng awh. Devit ni Siria tami leng dawk kâcuinaw 700 hoi marangransanaw 40,000 touh a thei. Ransabawi Shobak hai a thei awh teh hawvah a due.
19 Wafalme wote waliokuwa wanamtumikia Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya amani na Waisraeli na wakawa chini yao. Hivyo Waaramu wakaogopa kuwasaidia Waamoni tena.
Hadadezer koe san ka toung e siangpahrangnaw pueng teh, Isarelnaw e hmaitung vah amamanaw a sung e a kâpanue awh navah, Isarelnaw hoi roumnae a sak awh teh, a thaw a tawk pouh awh. Hottelah Sirianaw ni Ammonnaw hah bout kabawm ngai awh hoeh toe.

< 2 Samweli 10 >