< 2 Samweli 1 >

1 Baada ya kifo cha Sauli, Daudi alipokuwa amerudi kutoka kuwashinda Waamaleki, Daudi alikaa siku mbili huko Siklagi.
Now it came to pass after the death of Saul, when David was returned from the slaughter of the Amalekites, and David had stayed two days in Ziklag;
2 Siku ya tatu akaja mtu mwenye nguo zilizoraruka na mavumbi kichwani mwake kutoka kwenye kambi ya Sauli. Alipomjia Daudi, akajitupa chini ili kumpa heshima.
It came even to pass on the third day, that, behold, a man came out of the camp from Saul with his clothes rent, and earth on his head: and so it was, when he came to David, that he fell to the earth, and did obeisance.
3 Daudi akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?” Akamjibu, “Nimetoroka kutoka kambi ya Waisraeli.”
And David said to him, From where come you? And he said to him, Out of the camp of Israel am I escaped.
4 Daudi akamuuliza, “Ni nini kilichotokea? Niambie.” Akasema, “Watu walikimbia kutoka vitani. Wengi wao walianguka na kufa. Naye Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa.”
And David said to him, How went the matter? I pray you, tell me. And he answered, That the people are fled from the battle, and many of the people also are fallen and dead; and Saul and Jonathan his son are dead also.
5 Ndipo Daudi akamwambia huyo kijana aliyemletea taarifa, “Je, umefahamuje kwamba Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa?”
And David said to the young man that told him, How know you that Saul and Jonathan his son be dead?
6 Yule kijana akasema, “Nilijipata huko Mlima Gilboa, naye Sauli alikuwa huko akiegemea mkuki wake, na magari ya vita na wapanda farasi wa upande wa adui wakawa wamemkaribia sana.
And the young man that told him said, As I happened by chance on mount Gilboa, behold, Saul leaned on his spear; and, see, the chariots and horsemen followed hard after him.
7 Alipogeuka na kuniona, akaniita, nami nikasema, ‘Je, nifanye nini?’
And when he looked behind him, he saw me, and called to me. And I answered, Here am I.
8 “Akaniuliza, ‘Wewe ni nani?’ “Nikamjibu, ‘Mimi ni Mwamaleki.’
And he said to me, Who are you? And I answered him, I am an Amalekite.
9 “Kisha akaniambia, ‘Nikaribie mimi na uniue! Niko katika maumivu makali ya kifo, lakini bado ningali hai.’
He said to me again, Stand, I pray you, on me, and slay me: for anguish is come on me, because my life is yet whole in me.
10 “Kwa hiyo nikamkaribia nikamuua, kwa sababu nilijua kwamba baada ya kuanguka hangeweza kupona. Nami nikachukua lile taji lililokuwa kichwani mwake na utepe uliokuwa mkononi mwake nami nimevileta hapa kwa bwana wangu.”
So I stood on him, and slew him, because I was sure that he could not live after that he was fallen: and I took the crown that was on his head, and the bracelet that was on his arm, and have brought them here to my lord.
11 Ndipo Daudi pamoja na watu wote waliokuwa pamoja naye wakazishika nguo zao na kuzirarua.
Then David took hold on his clothes, and rent them; and likewise all the men that were with him:
12 Wakaomboleza, wakalia pia na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Sauli na Yonathani mwanawe, kwa ajili ya jeshi la Bwana na nyumba ya Israeli, kwa sababu wameanguka kwa upanga.
And they mourned, and wept, and fasted until even, for Saul, and for Jonathan his son, and for the people of the LORD, and for the house of Israel; because they were fallen by the sword.
13 Daudi akamwambia yule kijana aliyemletea taarifa, “Wewe ni mwenyeji wa wapi?” Akamjibu, “Mimi ni mwana wa mgeni, Mwamaleki.”
And David said to the young man that told him, From where are you? And he answered, I am the son of a stranger, an Amalekite.
14 Daudi akamuuliza, “Kwa nini hukuogopa kuinua mkono wako ili kumwangamiza mpakwa mafuta wa Bwana?”
And David said to him, How were you not afraid to stretch forth your hand to destroy the LORD’s anointed?
15 Kisha Daudi akamwita mmoja wa watu wake na kumwambia, “Nenda ukamuue!” Kwa hiyo akampiga, naye akafa.
And David called one of the young men, and said, Go near, and fall on him. And he smote him that he died.
16 Kwa maana Daudi alikuwa amemwambia, “Damu yako iwe juu ya kichwa chako mwenyewe. Kinywa chako mwenyewe kimeshuhudia dhidi yako uliposema, ‘Nilimuua mpakwa mafuta wa Bwana.’”
And David said to him, Your blood be on your head; for your mouth has testified against you, saying, I have slain the LORD’s anointed.
17 Daudi akafanya maombolezo haya kuhusu Sauli na Yonathani mwanawe,
And David lamented with this lamentation over Saul and over Jonathan his son:
18 naye akaagiza kwamba watu wa Yuda wafundishwe ombolezo hili la upinde (ambalo limeandikwa katika Kitabu cha Yashari):
(Also he bade them teach the children of Judah the use of the bow: behold, it is written in the book of Jasher.)
19 “Walio fahari yako, ee Israeli, wameuawa juu ya mahali pako palipoinuka. Jinsi wenye nguvu walivyoanguka!
The beauty of Israel is slain on your high places: how are the mighty fallen!
20 “Msilisimulie hili katika Gathi, msilitangaze hili katika barabara za Ashkeloni, binti za Wafilisti wasije wakafurahia, binti za hao wasiotahiriwa wasije wakashangilia.
Tell it not in Gath, publish it not in the streets of Askelon; lest the daughters of the Philistines rejoice, lest the daughters of the uncircumcised triumph.
21 “Enyi milima ya Gilboa, msipate umande wala mvua, wala mashamba yazaayo sadaka ya nafaka. Kwa maana huko ndiko ngao ya mwenye nguvu iliponajisiwa, ngao ya Sauli haitapakwa tena mafuta.
You mountains of Gilboa, let there be no dew, neither let there be rain, on you, nor fields of offerings: for there the shield of the mighty is vilely cast away, the shield of Saul, as though he had not been anointed with oil.
22 Kutokana na damu ya waliouawa, kutokana na miili ya wenye nguvu, ule upinde wa Yonathani haukugeuka nyuma. Upanga wa Sauli haukurudi bure.
From the blood of the slain, from the fat of the mighty, the bow of Jonathan turned not back, and the sword of Saul returned not empty.
23 “Sauli na Yonathani, maishani walipendwa na kuneemeka, na katika kifo hawakutengana. Walikuwa wepesi kuliko tai, walikuwa na nguvu kuliko simba.
Saul and Jonathan were lovely and pleasant in their lives, and in their death they were not divided: they were swifter than eagles, they were stronger than lions.
24 “Enyi binti za Israeli, lieni kwa ajili ya Sauli, ambaye aliwavika nguo nyekundu na maridadi, ambaye aliremba mavazi yenu kwa mapambo ya dhahabu.
You daughters of Israel, weep over Saul, who clothed you in scarlet, with other delights, who put on ornaments of gold on your apparel.
25 “Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka vitani! Yonathani ameuawa mahali pako palipoinuka.
How are the mighty fallen in the middle of the battle! O Jonathan, you were slain in your high places.
26 Nahuzunika kwa ajili yako, Yonathani ndugu yangu, kwangu ulikuwa mpendwa sana. Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, wa ajabu zaidi kuliko ule wa wanawake.
I am distressed for you, my brother Jonathan: very pleasant have you been to me: your love to me was wonderful, passing the love of women.
27 “Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka! Silaha za vita zimeangamia!”
How are the mighty fallen, and the weapons of war perished!

< 2 Samweli 1 >