< 2 Petro 1 >
1 Simoni Petro, mtumishi na mtume wa Yesu Kristo: Kwa wale ambao kwa njia ya haki ya Mungu na Mwokozi wetu Yesu Kristo mmepokea imani iliyo na thamani kama yetu:
这封信函来自耶稣基督的仆人和使徒西门·彼得,写给与我们一样,对我们的上帝和救主耶稣基督有着无价信任、真正是良善正义之人。
2 Neema na amani iwe kwenu kwa wingi katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
你们在上帝和我们的主耶稣的知识中成长过程中,愿你们获得更多恩典和平安。
3 Uweza wake wa uungu umetupatia mambo yote tunayohitaji kwa ajili ya uzima na uchaji wa Mungu, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
通过他的神圣力量,我们已获得重要的一切,过上以上帝为中心的生活。这是因为认识他,他以自己的荣耀和善良召唤我们。 通过这种方式,他为我们提供了神奇而无价的承诺。
4 Kwa sababu hiyo, ametukirimia ahadi zake kuu na za thamani kupitia mambo haya, ili kupitia hayo mpate kuwa washiriki wa asili ya uungu, na kuokoka kutoka upotovu ulioko duniani unaosababishwa na tamaa mbaya.
通过这些承诺,你可以分享这神圣的天性,摆脱这个世界邪恶欲望所产生的腐朽。
5 Kwa sababu hii hasa, jitahidini sana katika imani yenu kuongeza wema; na katika wema, maarifa;
正是因为这缘故,要尽你所能!你的善行加上你对上帝和信;你的知识加上你的善行;
6 katika maarifa, kiasi; katika kiasi, saburi; katika saburi, utauwa;
你的自控能力加上你的知识;你的自控能力加上耐心;你的耐心加上敬畏;
7 katika utauwa, upendano wa ndugu; na katika upendano wa ndugu, upendo.
你的敬畏会带来对信徒的爱;对信徒的爱,会带来爱。
8 Kwa maana haya yakiwa ndani yenu kwa wingi na kuzidi kuongezeka, yanawasaidia msikose bidii wala kutozaa matunda katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
你越多地具备这样的品质,那么在认识我们的主耶稣基督时,他们就更不容易变得没有效果和毫无效率。
9 Lakini mtu yeyote asipokuwa na mambo haya haoni mbali, na ni kipofu, naye amesahau kule kutakaswa kutoka dhambi zake za zamani.
因为没有这些品质的人,往往都目光短浅或非常盲目。他们忘记自己已经从过去的罪孽中被洗净。
10 Kwa hiyo, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuuthibitisha wito wenu na uteule wenu. Kwa maana mkifanya hivyo, hamtajikwaa kamwe,
所以兄弟姐妹们,要更坚定地让自己真正“被召唤和被挑选。”你这样做就永远不会坠落。
11 na mtajaliwa kwa ukarimu mwingi kuingia katika ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. (aiōnios )
你将受到热烈欢迎,进入我们主和救世主耶稣基督的永恒国度。 (aiōnios )
12 Hivyo nitawakumbusha mambo haya siku zote, hata ingawa mnayajua na mmethibitishwa katika kweli mliyo nayo.
所以我总是提醒你们这些事情,即使你们已经了然并且坚持你所拥有的真理。
13 Naona ni vyema kuwakumbusha mambo haya wakati wote niwapo katika hema hili ambalo ni mwili wangu,
但我仍然认为,趁我在世之时,通过提醒你们来鼓励你们,这是个好主意。
14 kwa sababu najua ya kwamba hivi karibuni nitaliweka kando, kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyoliweka wazi kwangu.
我知道,我离开今生之日已经不远——我们的主耶稣基督已向我表明这一点。
15 Nami nitafanya kila juhudi kuona kwamba baada ya kuondoka kwangu mtaweza kuyakumbuka mambo haya siku zote.
我会尽其所能,在我离开之后,你们还能时常回忆起这些事。
16 Tulipowafahamisha juu ya uweza na kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo, hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, bali tulishuhudia kwa macho yetu ukuu wake.
当我们对你们说:我们主耶稣基督的大能即将到来,我们所说的并非虚构的神话,我们曾亲眼目睹他的威严。
17 Alipewa heshima na utukufu kutoka kwa Mungu Baba, sauti ilipomjia katika Utukufu Mkuu, ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa naye sana.”
如果听到那庄严荣耀的声音说:“这是我的爱子,是真正令我喜悦的”,就代表从天父上帝那里获得威严荣耀。
18 Sisi wenyewe tuliisikia sauti hii ambayo ilitoka mbinguni, wakati tulipokuwa pamoja naye kwenye ule mlima mtakatifu.
当我们在圣山与他一起时,亲耳听到从天上传来的这个声音。
19 Nasi tunalo pia neno la hakika zaidi la unabii, ambalo mtafanya vyema mkiliangalia kwa bidii, kama vile nuru inavyongʼaa gizani, hadi kupambazuka na nyota ya asubuhi izuke mioyoni mwenu.
我们还有先知的确凿之语,绝对值得信赖,关注它一定会让你受益。它就像一盏灯,照亮黑暗之地,直到天亮;就像晨星,它的光照亮你的思想。
20 Zaidi ya yote, yawapasa mjue kwamba hakuna unabii katika Maandiko uliofasiriwa kama alivyopenda nabii mwenyewe.
最重要的是,你应该意识到,圣经中的任何预言都不能由个人的一时兴起来解释,
21 Kwa maana unabii haukuja kamwe kwa mapenzi ya mwanadamu, bali watu walinena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
因为预言并非起源于人类,而是先知在圣灵的感应下,代表上帝说话。