< 2 Petro 3 >

1 Wapenzi, huu ndio waraka wangu wa pili ninaowaandikia. Katika nyaraka hizi mbili ninajaribu kuziamsha nia zenu safi kwa mawazo makamilifu.
This second epistle, my beloved, I now write unto you; in both which I stir up your sincere mind in remembrance,
2 Nataka ninyi mkumbuke maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu na ile amri ya Bwana na Mwokozi mliyopewa kupitia kwa mitume wenu.
that ye may be mindful of the words formerly spoken by the holy prophets, and of the commandment of us the apostles of the Lord and Saviour: knowing this first,
3 Kwanza kabisa, ni lazima mfahamu ya kwamba siku za mwisho watakuja watu wenye dhihaka, wakidhihaki na kuzifuata tamaa zao mbaya.
that there will come in the last days scoffers,
4 Watasema, “Iko wapi ile ahadi ya kuja kwake? Tangu baba zetu walipofariki, kila kitu kinaendelea kama kilivyokuwa tangu mwanzo wa kuumbwa.”
walking after their own lusts, and saying, Where is the declaration of his coming? for except that the fathers are fallen asleep, all things remain as they were from the beginning of the creation.
5 Lakini wao kwa makusudi hupuuza ukweli huu, ya kwamba kwa neno la Mungu mbingu zilikuwepo tangu zamani, nayo dunia ilifanyizwa kutoka ndani ya maji na kwa maji.
For they are willingly ignorant of this, that by the Word of God the heavens were made of old, and the earth too from the water, and subsisting on the water.
6 Ulimwengu wa wakati ule uligharikishwa kwa hayo maji na kuangamizwa.
Whence the old world being drowned in water perished.
7 Lakini kwa neno lilo hilo, mbingu za sasa na dunia zimewekwa akiba kwa ajili ya moto, zikihifadhiwa hadi siku ile ya hukumu na ya kuangamizwa kwa watu wasiomcha Mungu.
But the heavens and the earth, that now are, by the same Word are kept in store, reserved unto fire on the day of judgement and destruction of ungodly men.
8 Lakini wapenzi, msisahau neno hili: kwamba kwa Bwana, siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.
But, beloved; be not ignorant of this one thing, that one day is with the Lord as a thousand years, and a thousand years as one day.
9 Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama watu wengine wanavyokudhani kukawia. Badala yake, yeye anawavumilia ninyi, maana hataki mtu yeyote aangamie, bali kila mtu afikilie toba.
The Lord is not slow as to his promise (as some count it slowness) but is long-suffering towards us, not willing that any should perish, but that all should come to repentance.
10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi. Ndipo mbingu zitatoweka kwa kishindo kikuu; navyo vitu vya asili vitateketezwa kwa moto, nayo dunia na kila kitu kilichomo ndani yake kitaunguzwa.
But the day of the Lord will come as a thief in the night, in which the heavens shall pass away with a great noise, and the elements being set on fire shall be dissolved, and the earth and the works therein shall be burnt up.
11 Kwa kuwa vitu vyote vitaharibiwa namna hii, je, ninyi imewapasa kuwa watu wa namna gani? Inawapasa kuishi maisha matakatifu na ya kumcha Mungu,
Seeing then that all these things shall be dissolved, what manner of persons ought ye to be in holy conversation and godliness,
12 mkingojea na kuhimiza kuja kwa hiyo siku ya Mungu. Siku hiyo italeta mbingu kuchomwa moto na kutoweka, na vitu vya asili vitayeyuka kwa moto.
expecting and hastening on the coming of the day of God, whereby the heavens being set on fire shall be dissolved, and the burning elements shall be melted.
13 Lakini kufuatana na ahadi yake, sisi tunatazamia mbingu mpya na dunia mpya, ambayo haki hukaa ndani yake.
But we, according to his promise, look for new heavens and a new earth, in which righteousness dwelleth.
14 Kwa sababu hii, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo haya, fanyeni bidii ili awakute katika amani, bila mawaa wala dosari.
Wherefore, beloved, seeing ye expect these things, give diligence to be found of Him in peace, spotless and blameless;
15 Hesabuni uvumilivu wa Bwana kuwa ni wokovu, kama vile ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima ile aliyopewa na Mungu.
and account the long-suffering of our Lord salvation, as our beloved brother Paul also, according to the wisdom given to him, hath written unto you;
16 Huandika vivyo hivyo katika nyaraka zake zote, akizungumzia ndani yake mambo haya. Katika nyaraka zake kuna mambo mengine ambayo ni vigumu kuyaelewa, ambayo watu wajinga na wasio thabiti huyapotosha kwa maangamizi yao wenyewe, kama wapotoshavyo pia Maandiko mengine.
as also in all his epistles, speaking in them of these things: in which are some things hard to be understood, which the illiterate and unstable wrest, as they do also the other scriptures, to their own destruction.
17 Basi, ninyi wapenzi, kwa kuwa mmekwisha kujua mambo haya, jilindeni msije mkachukuliwa na kosa la watu hao waasi na kuanguka kutoka kwenye uthabiti wenu.
Do ye therefore, beloved, as ye know these things before, take heed least being seduced together with them by the error of the wicked, ye should fall from your own stedfastness.
18 Bali kueni katika neema na katika kumjua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na milele! Amen. (aiōn g165)
But grow in grace, and in the knowledge of our Lord and Saviour Jesus Christ: to Him be glory both now and for ever. Amen. (aiōn g165)

< 2 Petro 3 >

The World is Destroyed by Water
The World is Destroyed by Water