< 2 Petro 2 >

1 Lakini pia waliinuka manabii wa uongo miongoni mwa watu, kama vile watakavyokuwako walimu wa uongo miongoni mwenu. Wataingiza mafundisho yasiyopatana na kweli kwa siri, hata kumkana Bwana wa pekee aliyewanunua, na hivyo kujiletea wenyewe maangamizi ya haraka.
There were however also false prophets among the people as also among you there will be false teachers, who will stealthily introduce heresies destructive even the having bought them Master denying, bringing upon themselves imminent destruction;
2 Hata hivyo, wengi watafuata njia zao za ufisadi, na kwa ajili yao njia ya kweli itatukanwa.
And many will follow after their (sensuality, *NK(O)*) through whom the way of the truth will be denigrated;
3 Nao katika tamaa zao mbaya, walimu hawa watajipatia faida kwenu kwa hadithi walizotunga wenyewe. Lakini hukumu imekwisha kutangazwa dhidi yao tangu zamani, wala uangamivu wao haujalala usingizi.
And through covetousness with fabricated words you they will exploit, for whom the judgment of long ago not is idle and the destruction of them not (slumbers. *NK(o)*)
4 Kwa maana, kama Mungu hakuwasamehe malaika walipotenda dhambi, bali aliwatupa kuzimu katika vifungo vya giza wakae humo mpaka ije hukumu; (Tartaroō g5020)
If for the God of [the] angels [who] having sinned not spared, but (in chains *NK(O)*) of gloomy darkness to Tartarus He delivered [them] for judgment (being kept, *N(k)O*) (Tartaroō g5020)
5 kama hakuusamehe ulimwengu wa kale alipoleta gharika juu ya watu wale wasiomcha Mungu, bali akamhifadhi Noa, mhubiri wa haki, pamoja na watu wengine saba;
and [the] ancient world not He spared, but one of eight Noah of righteousness a herald preserved [the] flood upon [the] world of [the] ungodly having brought in,
6 kama aliihukumu miji ya Sodoma na Gomora kwa kuiteketeza kwa moto ikawa majivu, na kuifanya kuwa kielelezo kwa yale yatakayowapata wale wasiomcha Mungu;
and [the] cities of Sodom and Gomorrah having reduced to ashes to destruction He condemned [them] an example of what is coming on (ungodly *N(k)O*) having set
7 na kama alimwokoa Loti, mtu mwenye haki, ambaye alihuzunishwa na maisha machafu ya watu wapotovu
and righteous Lot being distressed by the of the lawless in sensuality conduct He rescued;
8 (kwa sababu yale matendo mapotovu aliyoyaona na kuyasikia huyo mtu mwenye haki alipoishi miongoni mwao yalimhuzunisha siku baada ya siku):
through seeing for and hearing that righteous [man] dwelling among them day after day in [his] soul righteous with [their] lawless deeds was tormented;
9 ikiwa hivyo ndivyo, basi Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa wamchao Mungu kutoka majaribu, na kuwaweka waasi katika adhabu hadi siku ya hukumu.
[then] knows [the] Lord [the] devout out of temptation to deliver, [the] unrighteous then unto [the] day of judgment being punished to keep,
10 Hii ni hakika hasa kwa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kudharau mamlaka. Kwa ushupavu na kwa kiburi, watu hawa hawaogopi kunena mabaya dhidi ya viumbe vya mbinguni.
especially then those after [the] flesh in [the] passion of defilement walking and authority despising. Bold, self-willed, glorious ones not they tremble blaspheming;
11 Lakini hata malaika, ingawa wana nguvu na uwezo zaidi, hawaleti mashtaka mabaya dhidi ya viumbe kama hao mbele za Bwana.
whereas angels in strength and in power greater being not they do bring against them ([from the] Lord *N(K)O*) a reviling judgment.
12 Lakini watu hawa hukufuru katika mambo wasiyoyafahamu. Wao ni kama wanyama wasio na akili, viumbe wanaotawaliwa na hisia za mwili, waliozaliwa ili wakamatwe na kuchinjwa. Hawa nao kama wanyama wataangamizwa pia.
These however like irrational animals (they were born *N(K)O*) as creatures of instinct for capture and destruction, in what they are ignorant of blaspheming in the destruction of them (also *no*) (will be destroyed *N(k)O*)
13 Watalipwa madhara kwa ajili ya madhara waliyowatendea wengine. Huhesabu kuwa ni fahari kufanya karamu za ulevi na ulafi mchana peupe. Wao ni mawaa na dosari, wakijifurahisha katika anasa zao wanaposhiriki katika karamu zenu.
(suffering *N(K)O*) [as the] wage of unrighteousness. [as] pleasure esteeming in daytime carousal, blots and blemishes, reveling in the (deceptions *NK(o)*) of them feasting with you,
14 Wakiwa na macho yaliyojaa uzinzi, kamwe hawaachi kutenda dhambi. Huwashawishi wale wasio imara. Wao ni hodari kwa kutamani; ni wana wa laana!
eyes having full of adultery and unceasing from sin, enticing souls unestablished, a heart exercised (in craving *N(K)O*) having — of a curse children!
15 Wameiacha njia iliyonyooka, wakapotoka na kuifuata njia ya Balaamu mwana wa Beori aliyependa mshahara wa uovu.
(leaving *N(k)O*) (the *k*) straight way they have gone astray, having followed in the way of Balaam [son] of Bosor, who [the] wage of unrighteousness loved,
16 Lakini kwa ajili ya uovu wake, alikemewa na punda, mnyama asiyejua kusema, akaongea akitumia sauti ya mwanadamu na kuzuia wazimu wa huyo nabii.
reproof however he had for his own transgression; [by] a donkey mute in a man’s voice having spoken it restrained the of the prophet madness.
17 Watu hawa ni chemchemi zisizo na maji, na ukungu upeperushwao na tufani. Giza nene limewekwa tayari kwa ajili yao.
These are springs without water (and *no*) (mists *N(k)O*) by storm being driven, for whom gloom of darkness (into age *K*) has been reserved. (questioned)
18 Kwa maana wao hunena maneno makuu mno ya kiburi cha bure, na kwa kuvutia tamaa mbaya za asili ya mwili, huwashawishi watu ambao ndipo tu wamejiondoa miongoni mwa wale wanaoishi katika ufisadi.
Arrogant for of vanity speaking words they entice with [the] passions of [the] flesh to sensuality those (scarcely *N(K)O*) (escaping *N(k)O*) from those in error living,
19 Huwaahidi uhuru hao waliowanasa, wakati wao wenyewe ni watumwa wa ufisadi: kwa maana mtu ni mtumwa wa kitu chochote kinachomtawala.
freedom them promising, themselves slaves being of corruption; By what for anyone has been subdued, by that (and *ko*) he has been enslaved.
20 Kama wameukimbia upotovu wa dunia kwa kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo, kisha wakanaswa tena humo na kushindwa, hali yao ya mwisho ni mbaya zaidi kuliko ile ya kwanza.
If for having escaped the pollutions of the world through [the] knowledge of the Lord (of us *N*) and Savior Jesus Christ, in these now again having been entangled they are subdued, has become to them the last [state] worse than the first.
21 Ingelikuwa afadhali kwao kama wasingeliijua kamwe njia ya haki, kuliko kuijua kisha wakaiacha ile amri takatifu waliyokabidhiwa.
Better for it was being for them not to have known the way of righteousness than having known [it] (to have turned *N(k)O*) from the having been delivered to them holy commandment.
22 Imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli isemayo: “Mbwa huyarudia matapiko yake mwenyewe,” tena, “Nguruwe aliyeoshwa hurudi kugaagaa matopeni.”
Has happened (now *k*) to them the [thing] of the true proverb: A dog having returned to [its] own vomit; and A sow having washed to [her] (rolling place *N(k)O*) in [the] mire.

< 2 Petro 2 >