< 2 Petro 2 >
1 Lakini pia waliinuka manabii wa uongo miongoni mwa watu, kama vile watakavyokuwako walimu wa uongo miongoni mwenu. Wataingiza mafundisho yasiyopatana na kweli kwa siri, hata kumkana Bwana wa pekee aliyewanunua, na hivyo kujiletea wenyewe maangamizi ya haraka.
But there were false prophets, too, among the people, just as among you also there will be false teachers. These will secretly bring in destructive sects, denying even the Master who bought them, and bringing swift ruin upon themselves.
2 Hata hivyo, wengi watafuata njia zao za ufisadi, na kwa ajili yao njia ya kweli itatukanwa.
Then there will be many who will follow their immorality, because of whom the Way of the Truth will be maligned.
3 Nao katika tamaa zao mbaya, walimu hawa watajipatia faida kwenu kwa hadithi walizotunga wenyewe. Lakini hukumu imekwisha kutangazwa dhidi yao tangu zamani, wala uangamivu wao haujalala usingizi.
In their covetousness, with cunning words, they will make merchandise of you; those whose doom has not been idle from of old, and whose destruction has not been slumbering.
4 Kwa maana, kama Mungu hakuwasamehe malaika walipotenda dhambi, bali aliwatupa kuzimu katika vifungo vya giza wakae humo mpaka ije hukumu; (Tartaroō )
For if God did not spare angels when they sinned, but cast them down to Tartarus, and committed them to chains of darkness, and reserved them for judgment; (Tartaroō )
5 kama hakuusamehe ulimwengu wa kale alipoleta gharika juu ya watu wale wasiomcha Mungu, bali akamhifadhi Noa, mhubiri wa haki, pamoja na watu wengine saba;
if he did not spare the ancient world, but preserved Noah, a herald of righteousness, with seven others, when he brought a flood upon an ungodly world;
6 kama aliihukumu miji ya Sodoma na Gomora kwa kuiteketeza kwa moto ikawa majivu, na kuifanya kuwa kielelezo kwa yale yatakayowapata wale wasiomcha Mungu;
if he condemned the cities of Sodom and Gomorrah and reduced them to ashes, thus holding them up as a warning to all who would live ungodly;
7 na kama alimwokoa Loti, mtu mwenye haki, ambaye alihuzunishwa na maisha machafu ya watu wapotovu
and he delivered righteous Lot who was worn out by the lascivious life of the wicked
8 (kwa sababu yale matendo mapotovu aliyoyaona na kuyasikia huyo mtu mwenye haki alipoishi miongoni mwao yalimhuzunisha siku baada ya siku):
(for that righteous man, living among them, tormented his righteous soul in seeing and hearing, day after day, their lawless deeds),
9 ikiwa hivyo ndivyo, basi Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa wamchao Mungu kutoka majaribu, na kuwaweka waasi katika adhabu hadi siku ya hukumu.
then be sure that the Lord knows how to deliver the godly out of temptation, and to keep the wicked (who are even now enduring punishment) for the "Day of Judgment";
10 Hii ni hakika hasa kwa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kudharau mamlaka. Kwa ushupavu na kwa kiburi, watu hawa hawaogopi kunena mabaya dhidi ya viumbe vya mbinguni.
especially those who spend their lives following the flesh in the lust of defilement, and in despising all authority. Audacious and wilful, they feel no awe in railing against dignities;
11 Lakini hata malaika, ingawa wana nguvu na uwezo zaidi, hawaleti mashtaka mabaya dhidi ya viumbe kama hao mbele za Bwana.
even where angels, though surpassing them in strength and might, do not bring a railing judgment against them before the Lord.
12 Lakini watu hawa hukufuru katika mambo wasiyoyafahamu. Wao ni kama wanyama wasio na akili, viumbe wanaotawaliwa na hisia za mwili, waliozaliwa ili wakamatwe na kuchinjwa. Hawa nao kama wanyama wataangamizwa pia.
But these men, like irrational creatures, mere animals, born to be taken and destroyed, continually rail about matters of which they know nothing. In their corruption they will surely be destroyed,
13 Watalipwa madhara kwa ajili ya madhara waliyowatendea wengine. Huhesabu kuwa ni fahari kufanya karamu za ulevi na ulafi mchana peupe. Wao ni mawaa na dosari, wakijifurahisha katika anasa zao wanaposhiriki katika karamu zenu.
suffering wrong as the wage of wrong which they have done. These are men who count it pleasure to carouse in open daylight; they are spots and blemishes reveling in their deceit, even while they are feasting with you.
14 Wakiwa na macho yaliyojaa uzinzi, kamwe hawaachi kutenda dhambi. Huwashawishi wale wasio imara. Wao ni hodari kwa kutamani; ni wana wa laana!
They have eyes full of harlots, eyes that cannot stop sinning. They entice unsteady souls. Their heart is trained in greed. They are an accursed generation.
15 Wameiacha njia iliyonyooka, wakapotoka na kuifuata njia ya Balaamu mwana wa Beori aliyependa mshahara wa uovu.
They have forsaken the right way; they have lost their way, and followed the road of Balaam, the son of Beor, who loved the wages of wrong-doing.
16 Lakini kwa ajili ya uovu wake, alikemewa na punda, mnyama asiyejua kusema, akaongea akitumia sauti ya mwanadamu na kuzuia wazimu wa huyo nabii.
He was, however, rebuked for his own transgression; a dumb ass spoke with a man’s voice, and stopped the madness of the prophet.
17 Watu hawa ni chemchemi zisizo na maji, na ukungu upeperushwao na tufani. Giza nene limewekwa tayari kwa ajili yao.
Such men are like waterless springs, or mists storm-driven; for them the blackness of darkness has been reserved.
18 Kwa maana wao hunena maneno makuu mno ya kiburi cha bure, na kwa kuvutia tamaa mbaya za asili ya mwili, huwashawishi watu ambao ndipo tu wamejiondoa miongoni mwa wale wanaoishi katika ufisadi.
For speaking great swelling words of vanity, they entangle, by their lasciviousness, in the lusts of the flesh, those who are just about to escape from the men that live in misconduct.
19 Huwaahidi uhuru hao waliowanasa, wakati wao wenyewe ni watumwa wa ufisadi: kwa maana mtu ni mtumwa wa kitu chochote kinachomtawala.
They promise them liberty, while they themselves are slaves of rottenness! (For indeed a man is the slave of anything which masters him.)
20 Kama wameukimbia upotovu wa dunia kwa kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo, kisha wakanaswa tena humo na kushindwa, hali yao ya mwisho ni mbaya zaidi kuliko ile ya kwanza.
For if, after having escaped the pollutions of the world, through the knowledge of our Lord and Saviour Jesus Christ, men are again entangled in them and overpowered, their last state is become worse than their first.
21 Ingelikuwa afadhali kwao kama wasingeliijua kamwe njia ya haki, kuliko kuijua kisha wakaiacha ile amri takatifu waliyokabidhiwa.
Indeed it would have been better for them not to have known the Way of Righteousness, than, after knowing it, to turn back from the holy command delivered to them.
22 Imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli isemayo: “Mbwa huyarudia matapiko yake mwenyewe,” tena, “Nguruwe aliyeoshwa hurudi kugaagaa matopeni.”
In their case it has happened according to the true proverb, The dog returns again to his own vomit, and The sow, after washing, to her wallowing in the mire.