< 2 Petro 2 >

1 Lakini pia waliinuka manabii wa uongo miongoni mwa watu, kama vile watakavyokuwako walimu wa uongo miongoni mwenu. Wataingiza mafundisho yasiyopatana na kweli kwa siri, hata kumkana Bwana wa pekee aliyewanunua, na hivyo kujiletea wenyewe maangamizi ya haraka.
But there also came false prophets among the people, as there will also be false teachers among you, who will stealthily bring in destructive sects, even denying the Master who bought them, bringing quick destruction to themselves,
2 Hata hivyo, wengi watafuata njia zao za ufisadi, na kwa ajili yao njia ya kweli itatukanwa.
and many will follow out their destructive ways, because of whom the way of the truth will be spoken of [as] evil,
3 Nao katika tamaa zao mbaya, walimu hawa watajipatia faida kwenu kwa hadithi walizotunga wenyewe. Lakini hukumu imekwisha kutangazwa dhidi yao tangu zamani, wala uangamivu wao haujalala usingizi.
and in covetousness, with forged words, they will make merchandise of you, whose judgment of old is not idle, and their destruction does not slumber.
4 Kwa maana, kama Mungu hakuwasamehe malaika walipotenda dhambi, bali aliwatupa kuzimu katika vifungo vya giza wakae humo mpaka ije hukumu; (Tartaroō g5020)
For if God did not spare messengers having sinned, but having cast [them] down to Tartarus with chains of deepest gloom, delivered [them], having been reserved to judgment, (Tartaroō g5020)
5 kama hakuusamehe ulimwengu wa kale alipoleta gharika juu ya watu wale wasiomcha Mungu, bali akamhifadhi Noa, mhubiri wa haki, pamoja na watu wengine saba;
and did not spare the old world, but kept the eighth person, Noah, a preacher of righteousness, having brought a flood on the world of the impious,
6 kama aliihukumu miji ya Sodoma na Gomora kwa kuiteketeza kwa moto ikawa majivu, na kuifanya kuwa kielelezo kwa yale yatakayowapata wale wasiomcha Mungu;
and having turned the cities of Sodom and Gomorrah to ashes, condemned with an overthrow, having set [them as] an example to those about to be impious,
7 na kama alimwokoa Loti, mtu mwenye haki, ambaye alihuzunishwa na maisha machafu ya watu wapotovu
and He rescued righteous Lot, worn down by the conduct of the lawless in licentiousness,
8 (kwa sababu yale matendo mapotovu aliyoyaona na kuyasikia huyo mtu mwenye haki alipoishi miongoni mwao yalimhuzunisha siku baada ya siku):
for the righteous [man] dwelling among them was tormented in [his] righteous soul, day by day, in seeing and hearing unlawful works—
9 ikiwa hivyo ndivyo, basi Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa wamchao Mungu kutoka majaribu, na kuwaweka waasi katika adhabu hadi siku ya hukumu.
the LORD has known to rescue [the] pious out of temptation, and to keep [the] unrighteous being punished to [the] day of judgment,
10 Hii ni hakika hasa kwa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kudharau mamlaka. Kwa ushupavu na kwa kiburi, watu hawa hawaogopi kunena mabaya dhidi ya viumbe vya mbinguni.
and chiefly those following after the flesh in lust [and] defilement, and despising lordship. Bold, self-pleased, they are not afraid to speak evil of glorious ones,
11 Lakini hata malaika, ingawa wana nguvu na uwezo zaidi, hawaleti mashtaka mabaya dhidi ya viumbe kama hao mbele za Bwana.
whereas messengers, being greater in strength and power, do not bear a slanderous judgment against them before the LORD;
12 Lakini watu hawa hukufuru katika mambo wasiyoyafahamu. Wao ni kama wanyama wasio na akili, viumbe wanaotawaliwa na hisia za mwili, waliozaliwa ili wakamatwe na kuchinjwa. Hawa nao kama wanyama wataangamizwa pia.
and these, as irrational natural beasts, made to be caught and destroyed—in what things they are ignorant of, slandering—in their destruction will be destroyed;
13 Watalipwa madhara kwa ajili ya madhara waliyowatendea wengine. Huhesabu kuwa ni fahari kufanya karamu za ulevi na ulafi mchana peupe. Wao ni mawaa na dosari, wakijifurahisha katika anasa zao wanaposhiriki katika karamu zenu.
doing unjustly, [they will receive] a reward of unrighteousness, esteeming pleasure in the day, [and] luxury—[they are] spots and blemishes, reveling in their deceits, feasting with you,
14 Wakiwa na macho yaliyojaa uzinzi, kamwe hawaachi kutenda dhambi. Huwashawishi wale wasio imara. Wao ni hodari kwa kutamani; ni wana wa laana!
having eyes full of adultery, and unable to cease from sin, enticing unstable souls, having a heart exercised in covetousnesses, children of a curse,
15 Wameiacha njia iliyonyooka, wakapotoka na kuifuata njia ya Balaamu mwana wa Beori aliyependa mshahara wa uovu.
having forsaken a right way, they went astray, having followed in the way of Balaam the [son] of Bosor, who loved a reward of unrighteousness,
16 Lakini kwa ajili ya uovu wake, alikemewa na punda, mnyama asiyejua kusema, akaongea akitumia sauti ya mwanadamu na kuzuia wazimu wa huyo nabii.
and had a rebuke of his own iniquity—a mute donkey, having spoken in man’s voice, forbid the madness of the prophet.
17 Watu hawa ni chemchemi zisizo na maji, na ukungu upeperushwao na tufani. Giza nene limewekwa tayari kwa ajili yao.
These are wells without water, and clouds driven by a storm, to whom the deepest gloom of darkness has been kept throughout the age; (questioned)
18 Kwa maana wao hunena maneno makuu mno ya kiburi cha bure, na kwa kuvutia tamaa mbaya za asili ya mwili, huwashawishi watu ambao ndipo tu wamejiondoa miongoni mwa wale wanaoishi katika ufisadi.
for speaking swollen words of vanity, they entice in desires of the flesh—licentiousness, those who had truly escaped from those conducting themselves in error,
19 Huwaahidi uhuru hao waliowanasa, wakati wao wenyewe ni watumwa wa ufisadi: kwa maana mtu ni mtumwa wa kitu chochote kinachomtawala.
promising liberty to them, themselves being servants of corruption, for by whom anyone has been overcome, he has been brought to servitude to this one also;
20 Kama wameukimbia upotovu wa dunia kwa kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo, kisha wakanaswa tena humo na kushindwa, hali yao ya mwisho ni mbaya zaidi kuliko ile ya kwanza.
for if having escaped from the defilements of the world, in the acknowledging of the LORD and Savior Jesus Christ, and again being entangled by these things, they have been overcome, the last things have become worse to them than the first,
21 Ingelikuwa afadhali kwao kama wasingeliijua kamwe njia ya haki, kuliko kuijua kisha wakaiacha ile amri takatifu waliyokabidhiwa.
for it were better to them not to have acknowledged the way of righteousness, than having acknowledged [it], to turn back from the holy command delivered to them,
22 Imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli isemayo: “Mbwa huyarudia matapiko yake mwenyewe,” tena, “Nguruwe aliyeoshwa hurudi kugaagaa matopeni.”
and that of the true proverb has happened to them: “A dog turned back on his own vomit,” and, “A sow having bathed herself—to rolling in mire.”

< 2 Petro 2 >