< 2 Petro 2 >

1 Lakini pia waliinuka manabii wa uongo miongoni mwa watu, kama vile watakavyokuwako walimu wa uongo miongoni mwenu. Wataingiza mafundisho yasiyopatana na kweli kwa siri, hata kumkana Bwana wa pekee aliyewanunua, na hivyo kujiletea wenyewe maangamizi ya haraka.
However, there were also false prophets among the people, just as, indeed, there will be false teachers among you, who will introduce destructive heresies, even denying the Owner who bought them (bringing on themselves swift destruction).
2 Hata hivyo, wengi watafuata njia zao za ufisadi, na kwa ajili yao njia ya kweli itatukanwa.
And many will follow their licentious ways, because of which the way of the Truth will be defamed.
3 Nao katika tamaa zao mbaya, walimu hawa watajipatia faida kwenu kwa hadithi walizotunga wenyewe. Lakini hukumu imekwisha kutangazwa dhidi yao tangu zamani, wala uangamivu wao haujalala usingizi.
And in covetousness they will exploit you with deceptive words; since way back the judgment for such people is not slack, and their destruction will not sleep.
4 Kwa maana, kama Mungu hakuwasamehe malaika walipotenda dhambi, bali aliwatupa kuzimu katika vifungo vya giza wakae humo mpaka ije hukumu; (Tartaroō g5020)
Because if God did not spare angels when they sinned, but delivered them into chains of darkness, confining them in Tartarus to be reserved for judgment, (Tartaroō g5020)
5 kama hakuusamehe ulimwengu wa kale alipoleta gharika juu ya watu wale wasiomcha Mungu, bali akamhifadhi Noa, mhubiri wa haki, pamoja na watu wengine saba;
and did not spare the ancient world but preserved Noah, with seven others, a preacher of righteousness, when He brought a flood on the world of the ungodly,
6 kama aliihukumu miji ya Sodoma na Gomora kwa kuiteketeza kwa moto ikawa majivu, na kuifanya kuwa kielelezo kwa yale yatakayowapata wale wasiomcha Mungu;
and condemned the cities of Sodom and Gomorrah to destruction, reducing them to ashes (providing a warning to those who are intent on being ungodly),
7 na kama alimwokoa Loti, mtu mwenye haki, ambaye alihuzunishwa na maisha machafu ya watu wapotovu
while He rescued upright Lot, who was distressed by the licentious lifestyle of the wicked
8 (kwa sababu yale matendo mapotovu aliyoyaona na kuyasikia huyo mtu mwenye haki alipoishi miongoni mwao yalimhuzunisha siku baada ya siku):
(for that upright man, dwelling among them, tormented an upright soul from day to day by seeing and hearing lawless deeds)
9 ikiwa hivyo ndivyo, basi Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa wamchao Mungu kutoka majaribu, na kuwaweka waasi katika adhabu hadi siku ya hukumu.
—then the Lord knows how to deliver the godly out of testings and to reserve the unjust under punishment for the day of judgment,
10 Hii ni hakika hasa kwa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kudharau mamlaka. Kwa ushupavu na kwa kiburi, watu hawa hawaogopi kunena mabaya dhidi ya viumbe vya mbinguni.
and especially those who go after the flesh in the lust for defilement, and despise authority. They are audacious, self-willed; they are not afraid to revile majestic beings,
11 Lakini hata malaika, ingawa wana nguvu na uwezo zaidi, hawaleti mashtaka mabaya dhidi ya viumbe kama hao mbele za Bwana.
whereas angels, though being greater in might and power, do not bring a reviling accusation against them before the Lord.
12 Lakini watu hawa hukufuru katika mambo wasiyoyafahamu. Wao ni kama wanyama wasio na akili, viumbe wanaotawaliwa na hisia za mwili, waliozaliwa ili wakamatwe na kuchinjwa. Hawa nao kama wanyama wataangamizwa pia.
But these, as unreasoning animals, creatures of instinct made to be caught and destroyed, spouting off in matters of which they are ignorant, will be destroyed by their own depravity,
13 Watalipwa madhara kwa ajili ya madhara waliyowatendea wengine. Huhesabu kuwa ni fahari kufanya karamu za ulevi na ulafi mchana peupe. Wao ni mawaa na dosari, wakijifurahisha katika anasa zao wanaposhiriki katika karamu zenu.
receiving the wages of unrighteousness. Counting it a pleasure to carouse in the daytime, they are stains and blemishes, reveling in their own deceptions while they feast with you,
14 Wakiwa na macho yaliyojaa uzinzi, kamwe hawaachi kutenda dhambi. Huwashawishi wale wasio imara. Wao ni hodari kwa kutamani; ni wana wa laana!
having eyes full of adultery and that cannot cease from sin, enticing unstable souls; having a heart trained in greediness they are children of a curse;
15 Wameiacha njia iliyonyooka, wakapotoka na kuifuata njia ya Balaamu mwana wa Beori aliyependa mshahara wa uovu.
having forsaken the right way they have gone astray, having followed the way of Balaam of Bosor, who loved the wages of unrighteousness;
16 Lakini kwa ajili ya uovu wake, alikemewa na punda, mnyama asiyejua kusema, akaongea akitumia sauti ya mwanadamu na kuzuia wazimu wa huyo nabii.
but he got a rebuke for his wrongdoing—a mute donkey speaking with a human voice restrained the insanity of the prophet.
17 Watu hawa ni chemchemi zisizo na maji, na ukungu upeperushwao na tufani. Giza nene limewekwa tayari kwa ajili yao.
These are waterless springs, clouds driven by a storm, for whom the blackest of the darkness has been reserved forever. (questioned)
18 Kwa maana wao hunena maneno makuu mno ya kiburi cha bure, na kwa kuvutia tamaa mbaya za asili ya mwili, huwashawishi watu ambao ndipo tu wamejiondoa miongoni mwa wale wanaoishi katika ufisadi.
Because speaking pompous words of emptiness they entice through fleshly lusts, through licentiousness, those who have actually escaped from those who are living in error,
19 Huwaahidi uhuru hao waliowanasa, wakati wao wenyewe ni watumwa wa ufisadi: kwa maana mtu ni mtumwa wa kitu chochote kinachomtawala.
promising them freedom while they themselves are slaves of corruption; for by whom a person is overcome, by him also he is brought into bondage.
20 Kama wameukimbia upotovu wa dunia kwa kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo, kisha wakanaswa tena humo na kushindwa, hali yao ya mwisho ni mbaya zaidi kuliko ile ya kwanza.
For if, after they have escaped the defilements of the world through the real knowledge of the Lord and Savior Jesus Christ, they are again entangled in them and overcome, the latter circumstances have become worse for them than the first ones.
21 Ingelikuwa afadhali kwao kama wasingeliijua kamwe njia ya haki, kuliko kuijua kisha wakaiacha ile amri takatifu waliyokabidhiwa.
For it would have been better for them not to have really known the way of the righteousness, than having really known it to turn back from the holy commandment delivered to them.
22 Imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli isemayo: “Mbwa huyarudia matapiko yake mwenyewe,” tena, “Nguruwe aliyeoshwa hurudi kugaagaa matopeni.”
But it has happened to them according to the true proverb: a dog returns to its own vomit and a bathed sow to wallowing in mud.

< 2 Petro 2 >