< 2 Petro 1 >
1 Simoni Petro, mtumishi na mtume wa Yesu Kristo: Kwa wale ambao kwa njia ya haki ya Mungu na Mwokozi wetu Yesu Kristo mmepokea imani iliyo na thamani kama yetu:
Симон Петр, раб и посланник Иисус Христов, равночистную с нами получившими веру в правде Бога нашего и Спаса Иисуса Христа:
2 Neema na amani iwe kwenu kwa wingi katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
благодать вам и мир да умножится в познании Бога, и Христа Иисуса Господа нашего.
3 Uweza wake wa uungu umetupatia mambo yote tunayohitaji kwa ajili ya uzima na uchaji wa Mungu, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
Яко вся нам Божественныя силы Его, яже к животу и благочестию, подана разумом Призвавшаго нас славою и добродетелию.
4 Kwa sababu hiyo, ametukirimia ahadi zake kuu na za thamani kupitia mambo haya, ili kupitia hayo mpate kuwa washiriki wa asili ya uungu, na kuokoka kutoka upotovu ulioko duniani unaosababishwa na tamaa mbaya.
Имиже честная нам и великая обетования даровашася, да сих ради будете Божественнаго причастницы естества, отбегше, яже в мире, похотныя тли:
5 Kwa sababu hii hasa, jitahidini sana katika imani yenu kuongeza wema; na katika wema, maarifa;
и в самое же сие, тщание все привнесше, подадите в вере вашей добродетель, в добродетели же разум,
6 katika maarifa, kiasi; katika kiasi, saburi; katika saburi, utauwa;
в разуме же воздержание, в воздержании же терпение, в терпении же благочестие,
7 katika utauwa, upendano wa ndugu; na katika upendano wa ndugu, upendo.
во благочестии же братолюбие, в братолюбии же любовь.
8 Kwa maana haya yakiwa ndani yenu kwa wingi na kuzidi kuongezeka, yanawasaidia msikose bidii wala kutozaa matunda katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
Сия бо сущая в вас и множащаяся, не праздных ниже безплодных сотворят вы в Господа нашего Иисуса Христа познание:
9 Lakini mtu yeyote asipokuwa na mambo haya haoni mbali, na ni kipofu, naye amesahau kule kutakaswa kutoka dhambi zake za zamani.
емуже бо несть сих, слеп есть, мжай, забвение приемь очищения древних своих грехов.
10 Kwa hiyo, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuuthibitisha wito wenu na uteule wenu. Kwa maana mkifanya hivyo, hamtajikwaa kamwe,
Темже паче, братие, потщитеся известно ваше звание и избрание творити: сия бо творяще, не имате согрешити никогдаже,
11 na mtajaliwa kwa ukarimu mwingi kuingia katika ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. (aiōnios )
сице бо обилно приподастся вам вход в вечное Царство Господа нашего и Спаса Иисуса Христа. (aiōnios )
12 Hivyo nitawakumbusha mambo haya siku zote, hata ingawa mnayajua na mmethibitishwa katika kweli mliyo nayo.
Сего ради не обленюся воспоминати присно вам о сих, аще и ведите, и утверждени есте в настоящей истине.
13 Naona ni vyema kuwakumbusha mambo haya wakati wote niwapo katika hema hili ambalo ni mwili wangu,
Праведно бо мню, донележе есмь в сем телеси, возставляти вас воспоминанием,
14 kwa sababu najua ya kwamba hivi karibuni nitaliweka kando, kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyoliweka wazi kwangu.
ведый, яко скоро есть отложение телесе моего, якоже и Господь наш Иисус Христос сказа мне.
15 Nami nitafanya kila juhudi kuona kwamba baada ya kuondoka kwangu mtaweza kuyakumbuka mambo haya siku zote.
Потщуся же и всегда имети вас по моем исходе память о сих творити.
16 Tulipowafahamisha juu ya uweza na kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo, hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, bali tulishuhudia kwa macho yetu ukuu wake.
Не ухищренным бо баснем последовавше сказахом вам силу и пришествие Господа нашего Иисуса Христа, но самовидцы бывше величествия Онаго.
17 Alipewa heshima na utukufu kutoka kwa Mungu Baba, sauti ilipomjia katika Utukufu Mkuu, ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa naye sana.”
Прием бо от Бога Отца честь и славу, гласу пришедшу к Нему от велелепныя славы. Сей есть Сын Мой возлюбленный, о Немже Аз благоизволих.
18 Sisi wenyewe tuliisikia sauti hii ambayo ilitoka mbinguni, wakati tulipokuwa pamoja naye kwenye ule mlima mtakatifu.
И сей глас мы слышахом с небесе сшедшь, с Ним суще на горе святей.
19 Nasi tunalo pia neno la hakika zaidi la unabii, ambalo mtafanya vyema mkiliangalia kwa bidii, kama vile nuru inavyongʼaa gizani, hadi kupambazuka na nyota ya asubuhi izuke mioyoni mwenu.
И имамы известнейшее пророческое слово: емуже внимающе якоже светилу сияющу в темнем месте, добре творите, дондеже день озарит, и денница возсияет в сердцах ваших,
20 Zaidi ya yote, yawapasa mjue kwamba hakuna unabii katika Maandiko uliofasiriwa kama alivyopenda nabii mwenyewe.
сие прежде ведуще, яко всяко пророчество книжное по своему сказанию не бывает.
21 Kwa maana unabii haukuja kamwe kwa mapenzi ya mwanadamu, bali watu walinena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
Ни бо волею бысть когда человеком пророчество, но от Святаго Духа просвещаеми глаголаша святии Божии человецы.