< 2 Petro 1 >

1 Simoni Petro, mtumishi na mtume wa Yesu Kristo: Kwa wale ambao kwa njia ya haki ya Mungu na Mwokozi wetu Yesu Kristo mmepokea imani iliyo na thamani kama yetu:
Symeon Peter, a servant and apostle of Jesus Christ, to those who have obtained like precious faith with us through the righteousness of our God, and the Saviour Jesus Christ:
2 Neema na amani iwe kwenu kwa wingi katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
Grace and peace be multiplied to you in the knowledge of God, and of Jesus our Lord.
3 Uweza wake wa uungu umetupatia mambo yote tunayohitaji kwa ajili ya uzima na uchaji wa Mungu, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
Seeing that his Divine power hath given to us all things that pertain to life and godliness, through the knowledge of him who called us by his own glory and goodness;
4 Kwa sababu hiyo, ametukirimia ahadi zake kuu na za thamani kupitia mambo haya, ili kupitia hayo mpate kuwa washiriki wa asili ya uungu, na kuokoka kutoka upotovu ulioko duniani unaosababishwa na tamaa mbaya.
through which he hath given us exceedingly great and precious promises, that by these ye may become partakers of the Divine nature, having escaped from the corruption that is in the world through lust;
5 Kwa sababu hii hasa, jitahidini sana katika imani yenu kuongeza wema; na katika wema, maarifa;
even for this very reason, giving all diligence, add to your faith virtue, and to virtue knowledge,
6 katika maarifa, kiasi; katika kiasi, saburi; katika saburi, utauwa;
and to knowledge self-control, and to self-control endurance, and to endurance godliness,
7 katika utauwa, upendano wa ndugu; na katika upendano wa ndugu, upendo.
and to godliness brotherly kindness, and to brotherly kindness love.
8 Kwa maana haya yakiwa ndani yenu kwa wingi na kuzidi kuongezeka, yanawasaidia msikose bidii wala kutozaa matunda katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
For if these things are in you and abound, they make you neither inactive nor unfruitful in gaining the full knowledge of our Lord Jesus Christ.
9 Lakini mtu yeyote asipokuwa na mambo haya haoni mbali, na ni kipofu, naye amesahau kule kutakaswa kutoka dhambi zake za zamani.
But he that lacketh these things is blind, and cannot see afar off, and hath forgotten that he was cleansed from his old sins.
10 Kwa hiyo, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuuthibitisha wito wenu na uteule wenu. Kwa maana mkifanya hivyo, hamtajikwaa kamwe,
Wherefore the rather, brethren, give diligence to make your calling and election sure; for if ye do these things, ye will never fall.
11 na mtajaliwa kwa ukarimu mwingi kuingia katika ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. (aiōnios g166)
For in this way the entrance will be richly furnished you into the everlasting kingdom of our Lord and Saviour Jesus Christ. (aiōnios g166)
12 Hivyo nitawakumbusha mambo haya siku zote, hata ingawa mnayajua na mmethibitishwa katika kweli mliyo nayo.
Wherefore I shall be careful always to remind you of these things, though ye know them, and are established in the truth that is with you.
13 Naona ni vyema kuwakumbusha mambo haya wakati wote niwapo katika hema hili ambalo ni mwili wangu,
Yea, I think it right, as long as I am in this tabernacle, to stir you up by reminding you;
14 kwa sababu najua ya kwamba hivi karibuni nitaliweka kando, kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyoliweka wazi kwangu.
knowing that I must soon put off my tabernacle, even as our Lord Jesus Christ declared to me.
15 Nami nitafanya kila juhudi kuona kwamba baada ya kuondoka kwangu mtaweza kuyakumbuka mambo haya siku zote.
Moreover I shall endeavor that at all times ye may be able, after my departure, to call these things to mind.
16 Tulipowafahamisha juu ya uweza na kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo, hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, bali tulishuhudia kwa macho yetu ukuu wake.
For we did not follow cunningly devised fables, when we made known to you the power and coming of our Lord Jesus Christ, but had been made eye-witnesses of his majesty.
17 Alipewa heshima na utukufu kutoka kwa Mungu Baba, sauti ilipomjia katika Utukufu Mkuu, ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa naye sana.”
For he received from God the Father honor and glory, when such a voice as this was borne to him from the excellent glory: “This is my beloved Son, with whom I am well pleased.”
18 Sisi wenyewe tuliisikia sauti hii ambayo ilitoka mbinguni, wakati tulipokuwa pamoja naye kwenye ule mlima mtakatifu.
And this voice we heard borne from heaven when we were with him in the holy mount.
19 Nasi tunalo pia neno la hakika zaidi la unabii, ambalo mtafanya vyema mkiliangalia kwa bidii, kama vile nuru inavyongʼaa gizani, hadi kupambazuka na nyota ya asubuhi izuke mioyoni mwenu.
And we have more sure the prophetic word, to which ye do well in taking heed, as to a lamp shining in a dark place, until the day dawn, and the day-star arise in your hearts;
20 Zaidi ya yote, yawapasa mjue kwamba hakuna unabii katika Maandiko uliofasiriwa kama alivyopenda nabii mwenyewe.
knowing this first, that no prophecy of the Scripture cometh from private interpretation.
21 Kwa maana unabii haukuja kamwe kwa mapenzi ya mwanadamu, bali watu walinena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
For prophecy never came by the will of man; but moved by the Holy Spirit, men spoke from God.

< 2 Petro 1 >