< 2 Wafalme 1 >

1 Baada ya kifo cha Mfalme Ahabu, nchi ya Moabu iliasi dhidi ya Israeli.
Bimmusor ti Moab iti Israel kalpasan iti ipapatay ni Ahab.
2 Basi Ahazia alikuwa ameanguka huko Samaria kutoka baraza ya chumba chake cha juu, akaumia. Hivyo akatuma wajumbe, akiwaambia, “Nendeni mkaulize kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni, mkaone kama nitapona kutokana na kuumia huku.”
Ket natnag ni Ahazias iti balkon iti akingato a siledna idiay Samaria, ket nasugatan. Isu a nangibaon isuna kadagiti mensahero ket kinunana kadakuada, “Mapankayo, makiuman kenni Baal Zebub, a dios ti Ekron, no umimbagak pay manipud iti daytoy a pannakadangran.”
3 Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Mtishbi, “Panda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana mnakwenda kumuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni?’
Ngem kinuna ti anghel ni Yahweh kenni Elias a Tesbita, “Agrubuatka, mapanmo sabtem dagiti mensahero ti ari ti Samaria, ket damagem kadakuada, 'Gapu kadi ta awan ti Dios ti Israel isu a mapankayo makiuman kenni Baal Zebub, a dios ti Ekron?
4 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, ‘Hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!’” Hivyo Eliya akaenda.
Isu a kuna ni Yahweh, “Saankan a makababa iti pagiddaan nga immulliam; ngem ketdi, mataykanto.”'” Ket pimmanaw ni Elias.
5 Wajumbe waliporudi kwa mfalme, akawauliza, “Kwa nini mmerudi?”
Idi nagsubli dagiti mensahero kenni Ahazias, kinunana kadakuada, “Apay a nagsublikayo?”
6 Wakamjibu, “Mtu fulani alikuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Rudini kwa mfalme aliyewatuma na mkamwambie, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana unawatuma watu kwenda kuuliza kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa hiyo hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”’”
Kinunada kenkuana, “Adda ti maysa a tao nga immay simmabat kadakami a nangibaga, 'Agsublikayo iti ari a nangibaon kadakayo, ket ibagayo kenkuana, “Imbaga ni Yahweh daytoy: 'Gapu kadi ta awan ti Dios ti Israel isu a nangibaonka kadagiti lallaki a makiuman kenni Baal Zebub, a dios ti Ekron? Ngarud saankan a makababa iti pagiddaan nga immulliam; ngem ketdi, mataykanto.'”'”
7 Mfalme akawauliza, “Alikuwa mtu wa namna gani ambaye mlikutana naye, akawaambia hili?”
Kinuna ni Ahazias kadagiti mensaherona, “Ania ti langana, ti tao a simmabat ken nangibaga kadagitoy a sasao kadakayo?”
8 Wakamjibu, “Alikuwa mtu aliyekuwa na vazi la manyoya na mkanda wa ngozi kiunoni mwake.” Mfalme akasema, “Huyo alikuwa ni Eliya, Mtishbi.”
Simmungbatda kenkuana, “Nakakawes isuna iti naaramid ti buok ken nakabarikes isuna iti lalat.” Isu nga insungbat ti ari, “Dayta ni Elias a Tesbita.”
9 Ndipo mfalme akamtuma mkuu mmoja wa kikosi pamoja na kikosi chake cha askari hamsini kwa nabii Eliya. Yule mkuu wa kikosi akamwendea Eliya, aliyekuwa ameketi juu ya kilima, na kumwambia, “Mtu wa Mungu, mfalme anasema, ‘Shuka chini!’”
Nangibaon ngarud ti ari iti kapitan nga addaan iti limapulo a soldado a mapan kenni Elias. Simmang-at ti kapitan a napan kenni Elias iti pagtugtugawanna iti tapaw ti turod. Nagsao ti kapitan kenkuana, “Sika, a tao ti Dios, kinuna ti ari, 'Bumabaka.’”
10 Eliya akamjibu yule mkuu wa kikosi, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza yule mkuu wa kikosi pamoja na watu wake.
“Simmungbat ni Elias ket kinunana iti kapitan, “No taonak ti Dios, bumaba koma ti apuy manipud langit ket puorannaka ken dagiti limapulo a tattaom.” Ket bimmaba ti apuy manipud langit ket naikisap isuna ken dagiti limapulo a tattaona.
11 Aliposikia hili, mfalme akatuma kwa Eliya mkuu wa kikosi mwingine na askari wake hamsini. Yule mkuu wa kikosi akamwambia Eliya, “Mtu wa Mungu, hili ndilo asemalo mfalme, ‘Shuka chini mara moja!’”
Nangibaon manen ni Ari Ahazias iti sabali a kapitan nga addaan iti limapulo a soldado. Kinuna met dayta a kapitan kenni Elias, “Sika, a tao ti Dios, kuna ti ari, 'Bumabaka a dagus.”'
12 Eliya akajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na watu wake hamsini.
“Simmungbat ni Elias ket kinunana kadakuada, “No taonak ti Dios, bumaba koma ti apuy manipud langit ket puorannaka ken dagiti limapulo a tattaom.” Bimmaba manen ti apuy ti Dios manipud langit ket naikisap isuna ken dagiti limapulo a tattaona.
13 Hivyo mfalme akatuma mkuu wa kikosi wa tatu na watu wake hamsini. Huyu mkuu wa kikosi wa tatu akapanda na kupiga magoti mbele ya Eliya, akiomba, “Mtu wa Mungu, tafadhali niachie uhai wangu na uhai wa hawa watu hamsini, watumishi wako!
Nu pay kasta, nangibaon manen ti ari iti maikatlo a bunggoy ti limapulo a mannakigubat. Simmang-at daytoy a kapitan, nagparintumeng isuna iti sangoanan ni Elias, ket nagpakpakaasi ken kinunana kenkuana, “Sika, a tao ti Dios, dawatek kenka, agbalin koma a kailala iti imatangmo ti biagko ken ti biag dagitoy limapulo nga adipenmo.
14 Tazama, moto umeshuka kutoka mbinguni na kuwateketeza wale wakuu wa vikosi viwili vya kwanza pamoja na watu wao. Lakini sasa niachie uhai wangu!”
Kinapudnona, bimmaba ti apuy manipud langit ket inkisapna dagiti dua a kapitan ken dagiti tattaoda, ngem ita, agbalin koma a kailala ti biagko iti imatangmo.”
15 Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, “Shuka pamoja naye, usimwogope.” Hivyo Eliya akainuka na kushuka pamoja naye kwa mfalme.
Isu a kinuna ti anghel ni Yahweh kenni Elias, “Kumuyogka kenkuana. Saanka nga agbuteng kenkuana.” Isu a timmakder ni Elias ket kimmuyog kenkuana a napan iti ari.
16 Akamwambia mfalme, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli wa kumuuliza habari, ndiyo maana ukatuma wajumbe kuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa sababu umefanya hili, kamwe hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”
Saan a nagbayag, kinuna ni Elias kenni Ahazias, “Daytoy ti imbaga ni Yahweh, ‘Nangibaonka kadagiti mensahero a makiuman kenni Baal Zebub, a dios ti Ekron. Gapu kadi ta awan ti Dios ti Israel a pakiumanam? Isu nga ita, saankan a makababa iti pagiddaan nga immulliam; sigurado a mataykanto.”'
17 Hivyo akafa, sawasawa na lile neno la Bwana ambalo Eliya alikuwa amesema. Kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yoramu akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
Isu a natay ni Ahazias a kas iti sao ni Yahweh nga imbaga ni Elias. Nagturay ni Joram a kas kasukatna, iti maikadua a tawen ni Johoram nga anak a lalaki ni Josafat nga ari ti Juda, gapu ta awan ti lalaki nga anak ni Ahazias.
18 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahazia na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Maipanggep met kadagiti dadduma a banbanag maipapan kenni Ahazias, saanda kadi a naisurat iti Libro dagiti Pasamak dagiti Ari ti Israel?

< 2 Wafalme 1 >