< 2 Wafalme 9 >

1 Nabii Elisha akamwita mtu mmoja kutoka kwa wana wa manabii na kumwambia, “Jikaze viuno, uichukue hii chupa ya mafuta, na uende Ramoth-Gileadi.
Profeten Elisa kaldte en af Profetsønnerne til sig og sagde til ham: "Omgjord dine Lænder, tag denne Flaske Olie med og drag til Ramot i Gilead.
2 Ukifika huko, mtafute Yehu mwana wa Yehoshafati, mwana wa Nimshi. Enda kwake, umtenge na wenzake, na umpeleke katika chumba cha ndani.
Når du kommer derhen, opsøg så Jehu, Nimsjis Søn Josjafats Søn; gå hen og få ham til at stå op fra sine Fæller og før ham ind i det inderste Hammer;
3 Kisha chukua hii chupa na umimine mafuta juu ya kichwa chake, nawe utangaze, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli.’ Kisha ufungue mlango na ukimbie; usikawie!”
tag så Olieflasken og gyd Olien ud over hans Hoved med de Ord: Så siger HERREN: Jeg salver dig til Konge over Israel! Derefter skal du lukke Døren op og flygte ufortøvet!"
4 Basi yule kijana nabii akaenda Ramoth-Gileadi.
Den unge Mand, Profetens Tjener, drog så til Ramot i Gilead;
5 Wakati alipofika, akawakuta maafisa wa jeshi wameketi pamoja, akasema, “Nina ujumbe wako, ee jemadari.” Yehu akauliza, “Kwa yupi miongoni mwetu?” Akamjibu, “Kwako wewe, jemadari.”
og da han kom derhen, traf han Hærførerne siddende sammen. Han sagde da: "Jeg har et Ærinde til dig, Hærfører!" Jehu spurgte: "Til hvem af os?" Han svarede: "Til dig, Hærfører!"
6 Yehu akainuka na kuingia ndani ya nyumba. Ndipo yule nabii akamimina mafuta juu ya kichwa cha Yehu na kutangaza, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Bwana, yaani Israeli.
Så rejste han sig og gik ind i Huset; der gød han Olien ud over hans Hoved og sagde til ham: "Så siger HERREN, Israels Gud: Jeg salver dig til Konge over HERRENs Folk, over Israel!
7 Inakupasa uiangamize nyumba ya bwana wako Ahabu, nami nitalipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii na damu ya watumishi wote wa Bwana iliyomwagwa na Yezebeli.
Du skal hugge din Herre Akabs Hus ned, så jeg får Hævn over Jesabel for mine Tjenere Profeternes og alle HERRENsjeneres Blod.
8 Nyumba yote ya Ahabu itaangamia. Nitamkatilia mbali kila mzaliwa wa kiume wa Ahabu katika Israeli, aliye mtumwa ama aliye huru.
Hele Akabs Hus skal omkomme, jeg vil udrydde hvert mandligt Væsen, hver og en af Akabs Slægt i Israel;
9 Nitaifanya nyumba ya Ahabu kuwa kama ile nyumba ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na kama ile nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya.
jeg vil handle med Akabs Hus som med Jeroboams, Nebats Søns, og Ba'sjas, Ahijas Søns, Hus.
10 Kuhusu Yezebeli, mbwa watamla kwenye kiwanja huko Yezreeli, wala hakuna mtu atakayemzika.’” Kisha akafungua mlango na kukimbia.
Og Jesabel skal Hundene æde på Jizre'els Mark, og ingen skal jorde hende!" Derpå lukkede han Døren op og flygtede.
11 Yehu alipotoka nje na kurudi kwenda kwa maafisa wenzake, mmoja wao akamuuliza, “Je, kila kitu ni salama? Kwa nini huyu mwenye wazimu alikuja kwako?” Yehu akajibu, “Wewe unamfahamu huyo mtu, na aina ya mambo ambayo yeye husema.”
Da Jebu kom ud til sin Herres Folk, spurgte de ham: "Hvorledes står det til? Hvad vilde den gale Mand hos dig?" Han svarede: "I kender jo den Mand og hans Snak!"
12 Wakasema, “Hiyo siyo kweli! Tuambie.” Yehu akasema, “Haya ndiyo aliyoniambia: ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli.’”
Men de sagde: "Udflugter! Sig os det nu!" Da sagde han: "Således sagde han til mig: Så siger HERREN: Jeg salver dig til Konge over Israel!"
13 Wakaharakisha kuvua mavazi yao, na kuyatandaza chini ya Yehu ili akanyage juu kwenye ngazi ya nje. Kisha wakapiga tarumbeta na kupaza sauti wakisema, “Yehu ni mfalme!”
Øjeblikkelig tog de da hver sin Kappe og lagde under ham på selve Trappen, og de stødte i Hornet og udråbte Jehu til Konge.
14 Basi Yehu mwana wa Yehoshafati, mwana wa Nimshi, akafanya shauri baya dhidi ya Yoramu. (Wakati huu, Yoramu na Israeli wote walikuwa wakiilinda Ramoth-Gileadi dhidi ya Hazaeli mfalme wa Aramu,
Således stiftede Jehu, Nimsjis Søn Josjafats Søn, en Sammensværgelse mod Joram. Joram havde med hele Israel forsvaret Ramot i Gilead mod Kong Hazael af Aram;
15 lakini Mfalme Yoramu alikuwa amerudishwa Yezreeli ili kujiuguza kutokana na majeraha ambayo Waaramu walimtia katika vita na Hazaeli mfalme wa Aramu.) Yehu akasema, “Kama hii ndiyo nia yenu, msimruhusu hata mmoja kutoroka nje ya mji kwenda kupeleka habari huko Yezreeli.”
men Kong Joram var vendt tilbage for i Jizre'el at søge Helbredelse for de Sår, Aramæerne havde tilføjet ham, da han kæmpede med Kong Hazael af Aram. Da sagde Jehu: "Vil I som jeg, så lad ikke en eneste slippe ud af Byen og bringe Bud til Jizre'el."
16 Ndipo Yehu akaingia katika gari lake la vita na kuendesha kwenda Yezreeli, kwa sababu Yoramu alikuwa amepumzika huko, na Ahazia mfalme wa Yuda alikuwa ameenda kumwona.
Derpå steg Jehu til Vogns og kørte til Jizre'el; thi der lå Joram syg, og Kong Ahazja af Juda var rejst ned for at se til ham.
17 Mlinzi aliyesimama juu ya kinara cha Yezreeli alipoona askari wa Yehu wanakuja, akaita akisema, “Naona askari wanakuja.” Yoramu akaamuru, “Mtwae mpanda farasi umtume akakutane nao na kuuliza, ‘Je, mmekuja kwa amani?’”
Da Vægteren, som stod på Tårnet i Jizre'el, så Støvskyen efter Jehu, sagde han: "Jeg ser en Støvsky!" Da sagde Joram: "Tag en Rytter og send ham ud imod dem, for at han kan spørge, om de kommer med Fred!"
18 Mpanda farasi akaondoka kwenda kukutana na Yehu na kusema, “Hivi ndivyo asemavyo mfalme: ‘Je, mmekuja kwa amani?’” Yehu akamjibu, “Una nini na amani? Unga msafara nyuma yangu.” Mlinzi akatoa habari, “Mjumbe amewafikia lakini harudi.”
Så red Rytteren ham i Møde og sagde: "Således siger Kongen: Kommer du med Fred?" Jehu svarede: "Hvad vedkommer det dig, om det er med Fred? Omkring, følg mig!" Vægteren meldte: "Sendebudet har nået dem, men han kommer ikke tilbage!"
19 Basi mfalme akamtuma mpanda farasi wa pili. Wakati alipowafikia akasema, “Hivi ndivyo asemavyo mfalme, ‘Je, mmekuja kwa amani?’” Yehu akajibu, “Una nini na amani? Unga msafara nyuma yangu.”
Så sendte han en anden Rytter ud; og da han var kommet hen til dem, sagde han: "Således siger Kongen: Kommer du med Fred?" Jehu svarede: "Hvad vedkommer det dig, om jeg kommer med Fred? Omkring, følg mig!"
20 Yule mlinzi akatoa taarifa akasema, “Mjumbe amewafikia, lakini hata yeye harudi. Uendeshaji ule ni kama wa Yehu mwana wa Nimshi, anaendesha kama mwenye wazimu!”
Vægteren tneldte: "Han har nået dem, men han kommet ikke tilbage. Og de har en Fart på, som var det Jebu, Nimsjis Søn, thi han farer af Sted som rasende."
21 Yoramu akaagiza, akasema, “Weka tayari gari langu la vita.” Na baada ya gari kuwa tayari, Yoramu mfalme wa Israeli, na Ahazia mfalme wa Yuda, wakaondoka kila mmoja kwenye gari lake ili kukutana na Yehu. Walikutana naye katika shamba lililokuwa mali ya Nabothi, Myezreeli.
Da sagde Joram: "Spænd for!" Og da der var spændt for, kørte Kong Joram af Israel og Kong Ahazja af Juda ud hver i sin Vogn. De kørte Jehu i Møde og traf ham ved Jizre'eliten Nabots Mark.
22 Yoramu alipomwona Yehu akauliza, “Je, Yehu, umekuja kwa amani?” Yehu akajibu, “Kunawezaje kuwa na amani wakati ibada za sanamu na uchawi wa mama yako Yezebeli ungaliko?”
Da Joram fik Øje på Jehu, spurgte han: "Kommer du med Fred, Jehu?" Men han svarede: "Hvad! Skulde jeg komme med Fred, så længe det ikke har Ende med din Moder Jesabels Bolen og hendes mange Trolddomskunster!"
23 Yoramu akageuka nyuma na kukimbia, akimwambia Ahazia, “Huu ni uhaini, Ahazia!”
Da drejede Joram omkring og flygtede, idet han roabte tiIAhazja: "Svig, Ahazja!"
24 Kisha Yehu akatwaa upinde wake na kumchoma Yoramu katikati ya mabega. Mshale ukapenya kwenye moyo wake, naye akaanguka ghafula ndani ya gari lake.
Men Jehu greb sin Bue og skød Joram i Ryggen, så at Pilen gik igennem Hjertet, og han sank sammen i Vognen;
25 Yehu akamwambia Bidkari, mwendeshaji wa gari lake, “Mwinue na umtupe katika shamba lililokuwa mali ya Nabothi, Myezreeli. Kumbuka jinsi mimi na wewe tulivyokuwa tukiendesha pamoja magari yetu nyuma ya Ahabu baba yake, wakati Bwana alipotoa unabii huu kumhusu:
og Jehu sagde til sin Høvedsmand Bidkar: "Tag og kast ham hen på Jizre'eliten Nabots Mark, thi det rinder mig i Hu, hvorledes jeg og du kørte sammen bag efter hans Fader Akab, dengang HERREN fremsatte dette Udsagn imod ham:
26 ‘Jana niliona damu ya Nabothi na damu ya wanawe, nami kwa hakika nitakufanya uilipe juu ya shamba hili, asema Bwana.’ Sasa basi, mwinue na umtupe juu ya kiwanja, kulingana na neno la Bwana.”
Sandelig, Nabots og hans Sønners Blod så jeg i Går, lyder det fra HERREN, og jeg bringer Gengældelse over dig her på denne Mark, lyder det fra HERREN! Tag derfor og kast ham hen på Marken efter HERRENs Ord!"
27 Wakati Ahazia mfalme wa Yuda alipoona kilichotokea, akakimbia kupitia barabara ya Beth-Hagani. Yehu akamkimbiza akipaza sauti na kusema, “Muue naye pia!” Wakamjeruhi katika gari lake kwenye njia ielekeayo Guri karibu na Ibleamu, lakini akatorokea Megido na akafia huko.
Da Kong Ahazja at Juda så det, flygtede han ad Vejen til BetHagan; men Jehu satte efter ham og råbte: "Også ham!" Og i Gurpasset, i Nærheden afJibleam, skød de ham ned i Vognen. Han undslap til Megiddo, men der døde han.
28 Watumishi wake wakambeba kwa gari la vita na kumpeleka Yerusalemu, wakamzika pamoja na baba zake kwenye kaburi lake katika Mji wa Daudi.
Hans Folk førte ham til Jerusalem og jordede ham i hans Grav hos hans Fædre i Davidsbyen.
29 (Katika mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu, Ahazia alianza kutawala katika Yuda.)
I Akabs Søn Jorams ellevte Regerinsgår blev Ahazja Konge over Juda.
30 Kisha Yehu akaenda Yezreeli. Yezebeli aliposikia habari hii, akayapaka macho yake rangi, akatengeneza nywele zake na kutazama nje dirishani.
Jehu kom nu til Jizre'el. Så snart Jesabel hørte det, sminkede hun sine Øjne og smykkede sit Hoved og bøjede sig ud af Vinduet;
31 Yehu alipokuwa akiingia langoni, Yezebeli akasema, “Je, umekuja kwa amani, Zimri, wewe muuaji wa bwana wako?”
og da Jehu kørte ind igennem Porten, råbte hun: "Kommer du med Fred, Zimri Kongemorder?"
32 Yehu akaangalia juu dirishani na kuita, “Je, ni nani aliye upande wangu? Ni nani?” Matowashi wawili au watatu wakamtazama.
Men han så op til Vinduet og sagde: "Hvem holder med mig? Hvem?" Så var der et Par Hofmænd, som så ud efter ham,
33 Yehu akasema, “Mtupeni huyo mwanamke chini!” Kwa hiyo wakamtupa chini, nayo baadhi ya damu yake ikatapanyika ukutani na nyingine juu ya farasi walipokuwa wakimkanyaga kwa miguu yao.
og han råbte: "Styrt hende ned!" Så styrtede de hende ned. og Blodet sprøjtede op på Muren og på Hestene, og de trådte hende ned.
34 Yehu akaingia ndani, akala na akanywa. Akasema, “Mshughulikieni huyo mwanamke aliyelaaniwa. Mzikeni, kwa sababu alikuwa binti wa mfalme.”
Derpå gik han ind og spiste og drak. Så sagde han: "Tag jer af hende, den forbandede, og jord hende, hun var jo dog en Kongedatter!"
35 Lakini walipotoka kwenda kumzika, hawakukuta kitu chochote isipokuwa fuvu la kichwa, miguu yake na mikono.
Men da de gik ud for at jorde hende, fandt de ikke andet af hende end Hjerneskallen, Fødderne og Hænderne.
36 Wakarudi na kumwambia Yehu, ambaye alisema, “Hili ndilo neno la Bwana alilosema kupitia kinywa cha mtumishi wake Eliya Mtishbi, kwamba: Katika kiwanja cha Yezreeli, mbwa wataikula nyama ya Yezebeli.
Og de kom tilbage og meldte ham det; da sagde han: "Det er det Ord, HERREN talede ved sin Tjener Tisjbiten Elias: På Jizre'els Mark skal Hundene æde Jesabels Legeme!
37 Maiti ya Yezebeli itakuwa kama mavi shambani katika uwanja wa Yezreeli, kwamba hakutakuwepo mtu atakayeweza kusema, ‘Huyu ndiye Yezebeli.’”
og Jesabels Lig skal blive som Gødning på Ageren på Jizre'els Mark, så ingen kan sige: Dette er Jesabel!"

< 2 Wafalme 9 >