< 2 Wafalme 8 >

1 Wakati huu, Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa, “Ondoka wewe na jamaa yako ukaishi mahali popote unapoweza kwa kitambo kidogo, kwa sababu Bwana ameamuru njaa katika nchi hii ambayo itadumu kwa miaka saba.”
And Elisha he spoke to the woman whom he had restored to life son her saying arise and go (you *Q(K)*) and household your and sojourn in where you will sojourn for he has called Yahweh for famine and also it will come to the land seven years.
2 Yule mwanamke akafanya kama vile yule mtu wa Mungu alivyosema. Yeye na jamaa yake wakaondoka na kwenda kuishi katika nchi ya Wafilisti kwa miaka saba.
And she arose the woman and she did according to [the] word of [the] man of God and she went she and household her and she sojourned in [the] land of [the] Philistines seven years.
3 Baada ya miaka saba, yule mwanamke akarudi kutoka nchi ya Wafilisti, akaenda kwa mfalme kumsihi kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake.
And it was from [the] end of seven years and she returned the woman from [the] land of [the] Philistines and she went out to cry out to the king concerning house her and concerning field her.
4 Mfalme alikuwa anazungumza na Gehazi, mtumishi wa mtu wa Mungu, naye alikuwa amesema, “Hebu niambie mambo yote makuu yaliyofanywa na Elisha.”
And the king [was] speaking to Gehazi [the] servant of [the] man of God saying recount! please to me all the great [things] which he has done Elisha.
5 Wakati Gehazi alipokuwa akimweleza mfalme jinsi Elisha alivyomfufua mtu, yule mwanamke ambaye mwanawe alikuwa amefufuliwa na Elisha akaja ili amsihi mfalme kwa ajili ya nyumba yake na shamba lake. Gehazi akasema, “Huyu ndiye huyo mwanamke, bwana wangu mfalme, na huyu ndiye mwanawe ambaye Elisha alimfufua.”
And he was he recounting to the king this: he had restored to life the dead [one] and there! the woman whom he had restored to life son her [was] crying out for help to the king on house her and on field her and he said Gehazi O lord my the king this [is] the woman and this [is] son her whom he restored to life Elisha.
6 Mfalme akamuuliza yule mwanamke kuhusu mambo hayo, naye akamweleza. Ndipo akaamuru afisa ashughulikie shauri lake na kumwambia, “Mrudishie huyu mwanamke kila kitu kilichokuwa mali yake, pamoja na mapato yote yaliyotokana na shamba lake tangu siku alipoondoka nchini hadi sasa.”
And he asked the king the woman and she recounted to him and he assigned to her the king a court-official one saying restore all that [belonged] to her and all [the] produce of the field from [the] day [when] she left the land and until now.
7 Elisha akaenda Dameski, naye Ben-Hadadi mfalme wa Aramu alikuwa mgonjwa. Mfalme alipoambiwa, “Mtu wa Mungu ametoka mbali akapanda hadi hapa,”
And he went Elisha Damascus and Ben Hadad [the] king of Aram [was] sick and it was told to him saying he has come [the] man of God to here.
8 mfalme akamwambia Hazaeli. “Chukua zawadi na uende kumlaki huyo mtu wa Mungu. Muulize Bwana kupitia yeye, kwamba, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’”
And he said the king to Hazael take in hand your a gift and go to meet [the] man of God and you will consult Yahweh from him saying ¿ will I live from sickness this.
9 Hazaeli akaenda kumlaki Elisha, akiwa amechukua zawadi ya kila kitu kizuri kilichopatikana Dameski, mizigo iliyobebwa na ngamia arobaini. Akaingia ndani na kusimama mbele yake, akasema, “Mwanao Ben-Hadadi mfalme wa Aramu amenituma niulize, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’”
And he went Hazael to meet him and he took a gift in hand his and every good thing of Damascus [the] load of forty camel[s] and he came and he stood before him and he said son your Ben Hadad [the] king of Aram he has sent me to you saying ¿ will I live from sickness this.
10 Elisha akajibu, “Nenda ukamwambie, ‘Hakika utapona’; lakini Bwana amenifunulia kwamba kweli atakufa.”
And he said to him Elisha go say (to him *Q(K)*) certainly you will live and he has shown me Yahweh that certainly he will die.
11 Elisha akamkazia Hazaeli macho kwa nguvu mpaka akaona aibu. Kisha mtu wa Mungu akaanza kulia.
And he set face his and he set until was ashamed and he wept [the] man of God.
12 Hazaeli akauliza “Kwa nini bwana wangu analia?” Elisha akajibu, “Kwa sababu najua mabaya utakayowatendea Waisraeli. Utachoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, kuwatupa chini kwa nguvu watoto wachanga, na kuwatumbua wanawake wenye mimba.”
And he said Hazael why? [is] lord my weeping and he said for I know this: you will do to [the] people of Israel harm fortifications their you will send in fire and young men their with the sword you will kill and children their you will dash in pieces and pregnant [women] their you will rip open.
13 Hazaeli akasema, “Itawezekanaje mtumishi wako, aliye mbwa tu, kufanya tendo la ajabu namna hiyo?” Elisha akamjibu, “Bwana amenionyesha kuwa utakuwa mfalme wa Aramu.”
And he said Hazael that what? [is] servant your the dog that he will do the thing great this and he said Elisha he has shown me Yahweh you king over Aram.
14 Kisha Hazaeli akamwacha Elisha na kumrudia bwana wake. Ben-Hadadi akamuuliza, “Elisha alikuambia nini?” Hazaeli akajibu, “Aliniambia kwamba hakika utapona.”
And he went - from with Elisha and he came to master his and he said to him what? did he say to you Elisha and he said he said to me certainly you will live.
15 Lakini kesho yake Hazaeli akachukua nguo nzito, akailoweka ndani ya maji, akaitandaza juu ya uso wa mfalme, hivyo akafa. Kisha Hazaeli akaingia mahali pake kuwa mfalme wa Aramu.
And it was from [the] next day and he took the coverlet and he dipped [it] in water and he spread [it] out over face his and he died and he became king Hazael in place of him.
16 Katika mwaka wa tano wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, wakati huo Yehoshafati akiwa mfalme wa Yuda, Yehoramu mwana wa Yehoshafati akaanza kutawala kama mfalme wa Yuda.
And in year five of Joram [the] son of Ahab [the] king of Israel and Jehoshaphat [was] [the] king of Judah he became king Jehoram [the] son of Jehoshaphat [the] king of Judah.
17 Alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka minane.
A son of thirty and two year[s] he was when became king he and eight (years *Q(K)*) he reigned in Jerusalem.
18 Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alimwoa binti wa Ahabu. Akatenda maovu machoni pa Bwana.
And he walked in [the] way of - [the] kings of Israel just as they did [the] house of Ahab for [the] daughter of Ahab she became of him a wife and he did the evil in [the] eyes of Yahweh.
19 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi mtumishi wake, Bwana hakutaka kuiangamiza Yuda. Alikuwa ameahidi kuidumisha taa kwa ajili ya Daudi na wazao wake milele.
And not he was willing Yahweh to destroy Judah for [the] sake of David servant his just as he had said to him to give to him a lamp to sons his all the days.
20 Wakati wa Yehoramu, Edomu waliasi dhidi ya Yuda na kujiwekea mfalme wao wenyewe.
In days his it rebelled Edom from under [the] hand of Judah and they made king over themselves a king.
21 Basi Yehoramu akaenda Sairi pamoja na magari yake yote ya vita. Waedomu wakamzunguka yeye na majemadari wake wa magari yake ya vita, lakini akaondoka, akapenya usiku na kuwashambulia Waedomu. Hata hivyo, jeshi lake likatorokea nyumbani mwao.
And he passed over Joram Zair towards and all the chariotry [was] with him and it was he he arose night and he struck down Edom which was surrounding him and [the] commanders of the chariotry and it fled the people to tents its.
22 Hadi leo Edomu wameasi dhidi ya Yuda. Libna pia wakaasi wakati huo huo.
And it has rebelled Edom from under [the] hand of Judah until the day this then it rebelled Libnah at the time that.
23 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoramu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
And [the] rest of [the] matters of Joram and all that he did ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Judah.
24 Yehoramu akalala pamoja na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
And he lay down Joram with ancestors his and he was buried with ancestors his in [the] city of David and he became king Ahaziah son his in place of him.
25 Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda alianza kutawala.
In year two [plus] ten year of Joram [the] son of Ahab [the] king of Israel he became king Ahaziah [the] son of Jehoram [the] king of Judah.
26 Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri mfalme wa Israeli.
[was] a son of Twenty and two year[s] Ahaziah when became king he and a year one he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Athaliah [the] daughter of Omri [the] king of Israel.
27 Akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, na kutenda maovu machoni pa Bwana, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa imefanya, kwa kuwa alikuwa ameoa kutoka nyumba ya Ahabu.
And he walked in [the] way of [the] house of Ahab and he did the evil in [the] eyes of Yahweh like [the] house of Ahab for [was] [the] son-in-law of [the] house of Ahab he.
28 Ahazia akaenda vitani na Yoramu mwana wa Ahabu kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
And he went with Joram [the] son of Ahab for battle with Hazael [the] king of Aram at Ramoth Gilead and they wounded [the] Arameans Joram.
29 Hivyo Mfalme Yoramu akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa na Waaramu huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.
And he returned Joram the king to get himself healed in Jezreel from the wounds which they wounded him [the] Arameans at Ramah when fought he with Hazael [the] king of Aram and Ahaziah [the] son of Jehoram [the] king of Judah he went down to see Joram [the] son of Ahab in Jezreel for [was] sick he.

< 2 Wafalme 8 >