< 2 Wafalme 7 >

1 Elisha akasema, “Sikiliza neno la Bwana. Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
Élisha: Perwerdigarning sözini anglanglar! Perwerdigar mundaq deydu: — Ete mushu waqitlarda Samariyening derwazisida bir xalta aq un bir shekelge we ikki xalta arpa bir shekelge sétilidu, — dédi.
2 Yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake akamwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Elisha akajibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
Emma padishah bélikini tutup mangghan qoshun emeldari bolsa, Xudaning adimige: Mana, hetta Perwerdigar asman’gha tünglük achsimu, undaq ishning bolushi mumkinmu?! dédi. U: — Sen öz közüng bilen körisen, lékin shuningdin yémeysen, dédi.
3 Basi kulikuwepo na watu wanne wenye ukoma katika ingilio la lango la mji. Wakaambiana, “Kwa nini tukae hapa mpaka tufe?
Emdi derwazining tüwide töt maxaw késili bar adem olturatti. Ular bir-birige: Néme üchün mushu yerde ölümni kütüp olturimiz?
4 Kama tukisema, ‘Tutaingia mjini,’ mjini kuna njaa, nasi tutakufa humo. Kama tukikaa hapa, tutakufa. Kwa hiyo twende kwenye kambi ya Waaramu na tujisalimishe. Kama wakituacha hai, tutaishi; kama wakituua, basi na tufe.”
Sheherge kireyli dések, sheherde acharchiliq bolghachqa, u yerde ölimiz; bu yerde oltursaqmu ölimiz. Qopup Suriylerning leshkergahigha kéteyli. Ular bizni ayisa tirik qalimiz; bizni öltüreyli dése ölimiz, xalas, — déyishti.
5 Wakati wa giza la jioni, wakaondoka na kwenda kwenye kambi ya Waaramu. Walipofika mwanzo wa kambi, hapakuwa na mtu,
Shuni dep ular kechqurun Suriylerning leshkergahigha barghili qopti. Leshkergahining qéshigha yétip kelgende, mana héch kishi yoq idi.
6 kwa kuwa Bwana alilifanya jeshi la Waaramu lisikie sauti kama ya magari ya vita, farasi na jeshi kubwa, kiasi kwamba waliambiana, “Tazama, mfalme wa Israeli ameajiri mfalme wa Wahiti na mfalme wa Wamisri kuja kutushambulia sisi!”
Chünki Perwerdigar Suriylerning leshkergahigha jeng harwiliri, atlar we zor chong qoshunning sadasini anglatqanidi. Shuni anglap ular bir-birige: Mana, Israilning padishahi bishek Hittiylarning padishahlirini we Misirliqlarning padishahlirini üstimizge hujum qilghili yalliwaptu, déyishti;
7 Kwa hiyo wakaondoka na kukimbia wakati wa giza la jioni na kuacha mahema yao, farasi wao na punda wao. Wakakimbia kuokoa maisha yao na kuacha kila kitu ndani ya kambi kama kilivyokuwa.
kechqurun qozghilip chédirlirini, at bilen ésheklirini tashlap leshkergahni shu péti qoyup, öz janlirini qutquzush üchün beder qachqanidi.
8 Wale watu wenye ukoma walipofika mwanzoni mwa kambi, wakaingia kwenye mojawapo ya mahema. Wakala na kunywa, na kuchukua fedha, dhahabu na nguo, wakaenda kuvificha. Wakarudi na kuingia katika hema jingine, na kuchukua baadhi ya vitu kutoka ndani yake na kuvificha pia.
Maxaw késili bar ademler leshkergahning yénigha kélip, bir chédirgha kirip, yep-ichip uningdin kümüsh bilen altunni we kiyimlerni élip yoshurup qoyushti. Andin ular yénip kélip, yene bir chédirgha kirip u yerdiki oljinimu élip yoshurup qoyushti.
9 Kisha wakaambiana, “Hili tunalolifanya sio jema. Hii ni siku ya habari njema, nasi tunakaa kimya. Kama tukisubiri mpaka mapambazuko, maafa yatatupata. Twendeni mara moja tukatoe habari hizi katika jumba la mfalme.”
Andin ular bir-birige: Bizning bundaq qilghinimiz durus emes. Bügün qutluq xewer bar kündur, lékin biz tinmay turuwatimiz. Sehergiche qalsaq bu yamanliq béshimizgha chüshidu. Uning üchün emdi bérip padishahning ordisidikilerge bu xewerni yetküzeyli, dédi.
10 Hivyo wakaenda mjini na kuwaita walinzi wa langoni, wakawaambia, “Tulikwenda katika kambi ya Waaramu lakini hapakuwepo na mtu huko, hata sauti ya mtu yeyote, ila farasi na punda waliofungwa na mahema yaliyoachwa kama yalivyokuwa.”
Shuning bilen ular bérip sheherning derwazisidiki pasibanlarni chaqirip ulargha: Biz Suriylerning leshkergahigha chiqsaq, mana héchkim yoq iken, hetta ademning shepesimu yoqtur; belki atlar baghlaqliq, éshekler baghlaqliq bolup, chédirlar eyni péti turidu, dédi.
11 Walinzi wa langoni wakatangaza habari ile kwa sauti kuu, na taarifa hii ikatolewa ndani ya jumba la mfalme.
Derwazidiki pasibanlar shu xewerni towlap élan qilip, padishahning ordisigha xewer yetküzdi.
12 Mfalme akaamka usiku na kuwaambia maafisa wake, “Nitawaambia kile Waaramu walichotufanyia. Wanajua kwamba tuna njaa, hivyo wameacha kambi yao ili kujificha mashambani, wakifikiri, ‘Kwa hakika watatoka nje ya mji, nasi tutawakamata wakiwa hai na kuingia ndani ya mji.’”
Padishah kéchisi qopup xizmetkarlirigha: — Men Suriylerning bizge néme qilmaqchi bolghinini silerge dep bérey. Ular bizning acharchiliqta qalghinimizni bilip, leshkergahdin chiqip dalada mökünüwélip: — Israillar sheherdin chiqsa, biz ularni tirik tutup, andin sheherge kireleymiz, déyishken gep, dédi.
13 Mmoja wa maafisa wake akajibu, “Waamuru watu wachache wakawachukue farasi watano kati ya wale waliobaki katika mji. Hatima yao itakuwa kama ya Waisraeli wote walio hapa. Watakuwa tu kama Waisraeli hawa ambao wanangoja kifo. Hivyo tuwatumeni wajue kumetendeka nini.”
Xizmetkarliridin biri jawab bérip: — Birnechche kishini sheherde qalghan atlardin beshni élip (ularning aqiwiti bu yerde qalghan Israilning barliq kishiliriningkidin, hetta halak bolghanlarningkidin better bolmaydu!), ularni körüp kélishke eweteyli, dédi.
14 Ndipo wakachagua magari mawili ya vita pamoja na farasi wake, naye mfalme akawatuma wafuatilie jeshi la Waaramu. Akawaamuru waendeshaji akisema, “Nendeni mkaone ni nini kilichotokea.”
Shuning bilen ular ikki jeng harwisi bilen ulargha qatidighan atlarni teyyar qildi. Padishah ularni Suriylerning qoshunining keynidin ewetip: — Bérip ehwalni körüp kélinglar, dep buyrudi.
15 Wakawafuatia hadi Yordani, nao wakakuta barabara yote ikiwa imetapakaa nguo na vyombo vya Waaramu walivyokuwa wamevitupa walipokuwa wanatoroka. Basi wale wajumbe wakarudi na kutoa taarifa kwa mfalme.
Bular ularning izidin Iordan deryasighiche qoghlap bardi; we mana, pütkül yol boyi Suriyler aldirap qachqanda tashliwetken kiyim-kéchek we herxil eswab-üsküniler bilen tolghanidi. Elchiler yénip kélip padishahqa shuni xewer qildi.
16 Kisha watu wakatoka na kuteka nyara kambi ya Waaramu. Kwa hiyo kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
U waqitta xelq chiqip Suriylerning leshkergahidin oljilarni talidi; shuning bilen Perwerdigarning éytqan sözidek, bir xalta aq un bir shekelge, ikki xalta arpa bir shekelge sétildi.
17 Basi mfalme alikuwa amemweka yule afisa ambaye mfalme alikuwa anauegemea mkono wake awe msimamizi wa lango. Nao watu wakamkanyaga walipoingia langoni, naye akafa, kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa ametangulia kusema wakati mfalme alipofika nyumbani kwake.
Emdi padishah bilikini tutup mangghan héliqi emeldarni derwazini bashqurushqa teyinlep qoyghanidi. Emdi xalayiq derwazidin [étilip chiqqanda] uni dessep-cheyliwetti we shuning bilen u öldi. Bu ish padishah Xudaning adimini tutmaqchi bolup, uning aldigha barghanda, del Élisha éytqandek boldi.
18 Ikatokea kama vile mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia mfalme: “Wakati kama huu kesho, kipimo kimoja cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli moja ya fedha, na vibaba viwili vya shayiri kwa shekeli moja ya fedha katika lango la Samaria.”
Shuning bilen Xudaning adimi padishahqa éytqan shu söz emelge ashuruldi: «Ete mushu waqitlarda Samariyening derwazisida ikki xalta arpa bir shekelge we bir xalta aq un bir shekelge sétilidu».
19 Yule afisa alikuwa amemwambia yule mtu wa Mungu, “Tazama, hata kama Bwana atafungua madirisha ya mbinguni, je, jambo hili litawezekana?” Naye yule mtu wa Mungu alikuwa amemjibu, “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hutakula chochote kati ya hivyo!”
Emma héliqi emeldar Xudaning adimige: — «Mana, hetta Perwerdigar asman’gha tünglük achsimu, undaq bir ishning bolushi mumkinmu?!» dégenidi. U: — «Sen öz közüng bilen körisen, lékin shuningdin yémeysen», dégenidi.
20 Ndivyo hasa ilivyotokea kwake, kwa kuwa watu walimkanyaga langoni, naye akafa.
Uninggha hem del shundaq boldi; chünki xelq uni derwazida dessep öltürgenidi.

< 2 Wafalme 7 >