< 2 Wafalme 5 >

1 Wakati huu, Naamani alikuwa jemadari wa jeshi la mfalme wa Aramu. Alikuwa mtu mkuu mbele ya bwana wake na aliyeheshimiwa sana, kwa sababu kupitia kwake, Bwana alikuwa amewapa Aramu ushindi. Alikuwa askari shujaa, lakini alikuwa na ukoma.
پادشاه سوریه برای نعمان فرماندهٔ سپاه خود ارزش و احترام زیادی قائل بود، زیرا خداوند به دست او پیروزیهای بزرگی نصیب سپاه سوریه کرده بود. نعمان دلاوری شجاع بود ولی مرض جذام داشت.
2 Siku hizo vikosi kutoka Aramu vilikuwa vimekwenda na vikawa vimemteka msichana kutoka Israeli, naye akamtumikia mkewe Naamani.
قوای سوریه در یکی از جنگهای خود با اسرائیل، عده‌ای را اسیر کرده بودند. در میان اسرا، دختر کوچکی بود که او را به خانهٔ نعمان بردند و او کنیز زن نعمان شد.
3 Akamwambia bibi yake, “Kama bwana wangu angelimwona nabii aliyeko Samaria! Angemponya ukoma wake.”
روزی آن دختر به بانوی خود گفت: «کاش آقایم به دیدن آن نبی‌ای که در شهر سامره است، می‌رفت. او آقایم را از این مرض جذام شفا می‌داد.»
4 Naamani akaenda kwa bwana wake na kumwambia alichosema yule msichana kutoka Israeli.
نعمان آنچه را که دخترک گفته بود به عرض پادشاه رساند.
5 Mfalme wa Aramu akamjibu, “Hakika, nenda. Nitatuma barua kwa mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo Naamani akaondoka, akiwa amechukua talanta kumi za fedha, shekeli 6,000 za dhahabu, na mivao kumi ya mavazi.
پادشاه سوریه به او گفت: «نزد پادشاه اسرائیل برو. سفارش نامه‌ای نیز می‌نویسم تا برای او ببری.» نعمان با سی هزار مثقال نقره و شش هزار مثقال طلا و ده دست لباس روانه شد.
6 Barua aliyopelekea mfalme wa Israeli iliandikwa hivi: “Pamoja na barua hii ninamtuma mtumishi wangu, Naamani, kwako ili uweze kumponya ukoma wake.”
در نامهٔ پادشاه سوریه به پادشاه اسرائیل چنین نوشته شده بود: «حامل این نامه خدمتگزار من نعمان است. می‌خواهم از مرض جذام او را شفا دهی.»
7 Mara mfalme wa Israeli alipomaliza kuisoma ile barua, akararua mavazi yake na kusema, “Je, mimi ni Mungu? Je, mimi naweza kuua na kufufua tena? Kwa nini huyu mtu anamtuma mtu ili mimi nipate kumponya ukoma wake? Tazama jinsi anavyotafuta kuanzisha ugomvi nami!”
پادشاه اسرائیل وقتی نامه را خواند لباس خود را پاره کرد و گفت: «پادشاه سوریه این مرد جذامی را نزد من فرستاده است تا شفایش دهم! مگر من خدا هستم که بمیرانم و زنده کنم؟ او می‌خواهد با این بهانه باز به ما حمله کند.»
8 Elisha mtu wa Mungu aliposikia kwamba mfalme wa Israeli alikuwa amerarua mavazi yake, akamtumia ujumbe huu: “Kwa nini umerarua mavazi yako? Mwamuru mtu huyo aje kwangu, naye atajua ya kuwa yuko nabii katika Israeli.”
ولی وقتی الیشع نبی از موضوع باخبر شد این پیغام را برای پادشاه اسرائیل فرستاد: «چرا نگران هستی؟ نعمان را نزد من بفرست تا بداند در اسرائیل نبی‌ای هست.»
9 Kwa hiyo Naamani akaenda, akiwa na farasi zake na magari yake, na kusimama mlangoni mwa nyumba ya Elisha.
پس نعمان با اسبان و ارابه‌هایش آمده، نزد در خانهٔ الیشع ایستاد.
10 Elisha akamtuma mjumbe kumwambia, “Nenda uoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itapona, nawe utatakasika.”
الیشع یک نفر را فرستاد تا به او بگوید که برود و هفت مرتبه خود را در رود اردن بشوید تا از مرض جذام شفا پیدا کند.
11 Lakini Naamani akaondoka akiwa amekasirika, akasema, “Hakika nilidhani kwamba angetoka nje, asimame na kuliitia jina la Bwana Mungu wake, na kuweka mkono wake juu ya mahali pagonjwa, aniponye ukoma wangu.
اما نعمان خشمگین شد و گفت: «خیال می‌کردم این مرد نزد من بیرون می‌آید و دست خود را روی محل جذامم تکان داده، نام خداوند، خدای خود را می‌خواند و مرا شفا می‌دهد.
12 Je, Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora zaidi kuliko mito yoyote ya Israeli? Je, nisingeweza kuoga ndani ya hiyo mito na kutakasika?” Basi akageuka na kuondoka kwa hasira kuu.
آیا رودهای ابانه و فرفر دمشق از تمام رودهای اسرائیل بهتر نیستند؟ می‌توانم در آن رودها بدنم را بشویم و از این مرض جذام آزاد شوم.» این را گفت و خشمگین از آنجا رفت.
13 Watumishi wa Naamani wakamwendea na kumwambia, “Baba yangu, kama huyo nabii angekuambia kufanya jambo lililo kubwa, je, usingelifanya? Je, si zaidi sana basi, anapokuambia, ‘Oga na utakasike!’”
ولی همراهانش به او گفتند: «ای سرور ما، اگر آن نبی کار سختی از شما می‌خواست آیا انجام نمی‌دادید؟ شستشو در رودخانه کار سختی نیست. این کار را بکنید و آزاد شوید.»
14 Hivyo akashuka na kujizamisha ndani ya Yordani mara saba, kama vile huyo mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia, nayo nyama ya mwili wake ikapona na kutakasika kama ya mwili wa mvulana mdogo.
پس همان‌گونه که الیشع به او گفته بود، به سوی رود اردن شتافت و هفت بار در آن فرو رفت و شفا یافت و پوست بدنش مانند پوست بدن یک نوزاد، تر و تازه شد.
15 Kisha Naamani na wahudumu wake wote wakarudi kwa yule mtu wa Mungu. Akasimama mbele yake na kusema, “Sasa najua kwamba hakuna Mungu katika ulimwengu wote isipokuwa katika Israeli. Tafadhali sasa upokee zawadi kutoka kwa mtumishi wako.”
او به اتفاق تمام همراهانش نزد الیشع نبی بازگشت و به احترام در حضور او ایستاد و گفت: «حال دریافتم که در سراسر جهان خدایی جز خدای اسرائیل نیست. اکنون خواهش می‌کنم هدایای مرا بپذیر.»
16 Nabii akajibu, “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ninamtumikia, sitapokea kitu hata kimoja.” Ingawa Naamani alimsihi sana, yeye alikataa.
ولی الیشع پاسخ داد: «به خداوند زنده که خدمتش می‌کنم قسم که هدایای تو را قبول نخواهم کرد.» الیشع با وجود اصرار زیاد نعمان، هدایا را نپذیرفت.
17 Naamani akasema, “Ikiwa hutapokea, tafadhali mtumishi wako na apewe udongo kiasi cha mzigo wa kuweza kubebwa na punda wawili, kwa sababu mtumishi wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa na dhabihu kwa mungu mwingine isipokuwa Bwana.
نعمان گفت: «حال که هدایای مرا قبول نمی‌کنی پس دو بارِ قاطر از خاک این سرزمین را به من بده تا با خود به کشورم ببرم؛ زیرا بعد از این دیگر برای خدایان قربانی نخواهم کرد؛ قربانی خود را به خداوند تقدیم خواهم نمود.
18 Lakini Bwana na amsamehe mtumishi wake kwa kitu hiki kimoja: Wakati bwana wangu atakapoingia kwenye hekalu la Rimoni ili kusujudu, naye akiwa anauegemea mkono wangu, nami nikasujudu huko pia, wakati nitakaposujudu ndani ya hekalu la Rimoni, Bwana na amsamehe mtumishi wako kwa ajili ya jambo hili.”
از خداوند می‌خواهم که مرا ببخشد، چون وقتی سرورم پادشاه سوریه برای عبادت به بتخانهٔ رمون می‌رود، به بازوی من تکیه می‌دهد و جلوی بت سجده می‌کند و من هم مجبورم سجده کنم. خداوند این گناه مرا ببخشد.»
19 Elisha akamwambia, “Nenda kwa amani.” Baada ya Naamani kusafiri umbali fulani,
الیشع گفت: «به سلامتی برو.» نعمان رهسپار دیار خود شد.
20 Gehazi, mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu, akajiambia mwenyewe, “Bwana wangu amemwachia kirahisi sana Naamani, huyu Mwaramu, kwa kutokupokea kutoka kwake vile alivyovileta. Hakika kama Bwana aishivyo, nitamkimbilia na kupata kitu kutoka kwake.”
ولی جیحزی، خدمتکار الیشع با خود اندیشید: «ارباب من هدایای نعمان سوری را قبول نکرد، ولی به خداوند زنده قسم که به دنبال او می‌روم و هدیه‌ای از او می‌گیرم.»
21 Hivyo Gehazi akaharakisha kumfuatilia Naamani. Naamani alipomwona akikimbia kumwelekea, akashuka chini kutoka kwenye gari lake na kwenda kumlaki. Akauliza, “Je, mambo yote ni sawa?”
پس جیحزی دوید تا به نعمان رسید. وقتی نعمان دید که او از عقبش می‌دود از ارابه‌اش پایین آمد و به استقبال او شتافت. نعمان از او پرسید: «آیا اتفاقی افتاده است؟»
22 Gehazi akajibu, “Mambo yote ni sawa. Bwana wangu amenituma nikuambie, ‘Vijana wawili kutoka kwa wana wa manabii wamenijia kutoka nchi ya vilima ya Efraimu. Tafadhali wape talanta ya fedha na mivao miwili ya mavazi.’”
جیحزی گفت: «اتفاقی نیفتاده؛ فقط اربابم مرا فرستاده که بگویم دو نفر از انبیای جوان از کوهستان افرایم رسیده‌اند و او سه هزار مثقال نقره و دو دست لباس می‌خواهد تا به آنها بدهد.»
23 Naamani akasema, “Hakika, chukua talanta mbili za fedha.” Akamsihi Gehazi azipokee, kisha akafunga talanta mbili za fedha katika mifuko miwili pamoja na mivao miwili ya mavazi. Akawapa watumishi wake wawili mizigo hiyo, nao wakaibeba wakitangulia mbele ya Gehazi.
نعمان با اصرار گفت: «خواهش می‌کنم شش هزار مثقال نقره ببر.» سپس نقره را در دو کیسه ریخت و دو دست لباس روی دوش دو نفر از خادمانش گذاشت تا همراه جیحزی نزد الیشع ببرند.
24 Gehazi alipofika kwenye kilima, akavichukua vile vitu kutoka kwa wale watumishi na kuvificha ndani ya nyumba. Akawaaga wale watu, nao wakaondoka.
ولی وقتی به تپه‌ای رسیدند که الیشع در آن زندگی می‌کرد، جیحزی هدایا را از خادمان گرفته، آنها را مرخص کرد؛ سپس هدایا را به خانهٔ خود برد و در آنجا پنهان نمود.
25 Kisha akaingia ndani na kusimama mbele ya Elisha bwana wake. Elisha akamuuliza, “Gehazi, ulikuwa wapi?” Gehazi akajibu, “Mtumishi wako hakwenda popote.”
وقتی جیحزی نزد الیشع رفت، الیشع از او پرسید: «جیحزی، کجا بودی؟» او گفت: «جایی نرفته بودم.»
26 Lakini Elisha akamwambia, “Je, roho yangu haikuwa pamoja nawe wakati yule mtu aliposhuka kutoka kwenye gari lake ili kukulaki? Je, huu ni wakati wa kupokea fedha au kupokea nguo, mashamba ya mizeituni, mashamba ya mizabibu, makundi ya kondoo na mbuzi, makundi ya ngʼombe, au watumishi wa kiume na wa kike?
الیشع به او گفت: «آیا خیال می‌کنی وقتی نعمان از ارابه‌اش پیاده شد و به استقبال تو آمد، روحم خبر نداشت؟ آیا حالا وقت گرفتن پول و لباس، باغهای زیتون و تاکستانها، گله‌ها و رمه‌ها، غلامان و کنیزان است؟
27 Ukoma wa Naamani utakushika wewe na wazao wako milele.” Kisha Gehazi akaondoka mbele ya Elisha, mwenye ukoma, mweupe kama theluji.
چون این کار را کرده‌ای مرض جذام نعمان بر تو خواهد آمد و تا به ابد نسل تو را مبتلا خواهد ساخت.» جیحزی از اتاق بیرون رفت در حالی که جذام، پوست بدنش را مثل برف سفید کرده بود.

< 2 Wafalme 5 >