< 2 Wafalme 5 >

1 Wakati huu, Naamani alikuwa jemadari wa jeshi la mfalme wa Aramu. Alikuwa mtu mkuu mbele ya bwana wake na aliyeheshimiwa sana, kwa sababu kupitia kwake, Bwana alikuwa amewapa Aramu ushindi. Alikuwa askari shujaa, lakini alikuwa na ukoma.
Naaman, prince of the chyualrye of the kyng of Syrie, was a greet man, and worschipid anentis his lord; for bi hym the Lord yaf helthe to Sirie; sotheli he was a strong man and riche, but leprouse.
2 Siku hizo vikosi kutoka Aramu vilikuwa vimekwenda na vikawa vimemteka msichana kutoka Israeli, naye akamtumikia mkewe Naamani.
Forsothe theues yede out of Sirie, and ledden prisonere fro the lond of Israel a litil damysele, that was in the seruyce of the wijf of Naaman.
3 Akamwambia bibi yake, “Kama bwana wangu angelimwona nabii aliyeko Samaria! Angemponya ukoma wake.”
`Which damysele seide to hir ladi, `Y wolde, that my lord hadde be at the prophete which is in Samarie; sotheli the prophete schulde haue curid hym of the lepre which he hath.
4 Naamani akaenda kwa bwana wake na kumwambia alichosema yule msichana kutoka Israeli.
Therfor Naaman entride to his lord, and telde to hym, and seide, A damysel of the lond of Israel spak so and so.
5 Mfalme wa Aramu akamjibu, “Hakika, nenda. Nitatuma barua kwa mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo Naamani akaondoka, akiwa amechukua talanta kumi za fedha, shekeli 6,000 za dhahabu, na mivao kumi ya mavazi.
Therfor the kyng of Syrie seide to hym, Go thou, and Y schal sende lettris to the kyng of Israel. And whanne he hadde go forth, and hadde take with hym ten talentis of siluer, and sixe thousynde goldun platis, `ether floreyns, and ten chaungyngis of clothis,
6 Barua aliyopelekea mfalme wa Israeli iliandikwa hivi: “Pamoja na barua hii ninamtuma mtumishi wangu, Naamani, kwako ili uweze kumponya ukoma wake.”
he brouyte lettris to the kyng of Israel bi these wordis; Whanne thou hast take this pistle, wite thou, that Y haue sent to thee Naaman, my seruaunt, that thou cure hym of his lepre.
7 Mara mfalme wa Israeli alipomaliza kuisoma ile barua, akararua mavazi yake na kusema, “Je, mimi ni Mungu? Je, mimi naweza kuua na kufufua tena? Kwa nini huyu mtu anamtuma mtu ili mimi nipate kumponya ukoma wake? Tazama jinsi anavyotafuta kuanzisha ugomvi nami!”
And whanne the kyng of Israel hadde red the lettris, he to-rente his clothis, and seide, Whether Y am God, that may sle and quykene, for this kyng sente to me, that Y cure a man of his lepre? Perseyue ye, and se, that he sekith occasiouns ayens me.
8 Elisha mtu wa Mungu aliposikia kwamba mfalme wa Israeli alikuwa amerarua mavazi yake, akamtumia ujumbe huu: “Kwa nini umerarua mavazi yako? Mwamuru mtu huyo aje kwangu, naye atajua ya kuwa yuko nabii katika Israeli.”
And whanne Elisee, the man of God, hadde herd this, that is, that the kyng of Israel hadde to-rente hise clothis, he sente to the kyng, and seide, Whi to-rentist thou thi clothis? come he to me, and wite he, that a prophete is in Israel.
9 Kwa hiyo Naamani akaenda, akiwa na farasi zake na magari yake, na kusimama mlangoni mwa nyumba ya Elisha.
Therfor Naaman cam with horsis and charis, and stood at the dore of the hows of Elisee.
10 Elisha akamtuma mjumbe kumwambia, “Nenda uoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itapona, nawe utatakasika.”
And Elisee sente to hym a messanger, and seide, Go thou, and be thou waischun seuensithis in Jordan; and thi fleisch shal resseyue helthe, and thou schalt be clensid.
11 Lakini Naamani akaondoka akiwa amekasirika, akasema, “Hakika nilidhani kwamba angetoka nje, asimame na kuliitia jina la Bwana Mungu wake, na kuweka mkono wake juu ya mahali pagonjwa, aniponye ukoma wangu.
Naaman was wrooth, and yede awei, and seide, Y gesside, that he schulde go out to me, and that he schulde stonde, and clepe the name of `the Lord his God, and that he schulde touche with his hond the place of lepre, and schulde cure me.
12 Je, Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora zaidi kuliko mito yoyote ya Israeli? Je, nisingeweza kuoga ndani ya hiyo mito na kutakasika?” Basi akageuka na kuondoka kwa hasira kuu.
Whether Abana and Pharphar, floodis of Damask, ben not betere than alle the watris of Israel, that Y be waischun in tho, and be clensid?
13 Watumishi wa Naamani wakamwendea na kumwambia, “Baba yangu, kama huyo nabii angekuambia kufanya jambo lililo kubwa, je, usingelifanya? Je, si zaidi sana basi, anapokuambia, ‘Oga na utakasike!’”
Therfor whanne he hadde turned hym silf, and yede awei, hauynge indignacioun, hise seruauntis neiyiden to hym, and spaken to hym, Fadir, thouy the prophete hadde seid to thee a greet thing, certis thou owist to do; hou myche more for now he seide to thee, Be thou waischun, and thou schalt be clensid.
14 Hivyo akashuka na kujizamisha ndani ya Yordani mara saba, kama vile huyo mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia, nayo nyama ya mwili wake ikapona na kutakasika kama ya mwili wa mvulana mdogo.
He yede doun, and waischide hym seuensithis in Jordan, bi the word of the man of God; and his fleisch was restored as the fleisch of a litil child, and he was clensid.
15 Kisha Naamani na wahudumu wake wote wakarudi kwa yule mtu wa Mungu. Akasimama mbele yake na kusema, “Sasa najua kwamba hakuna Mungu katika ulimwengu wote isipokuwa katika Israeli. Tafadhali sasa upokee zawadi kutoka kwa mtumishi wako.”
And he turnede ayen with al his felouschipe to the man of God, and cam, and stood bifor hym; and seide, Verili Y knowe, that noon other God is in al erthe, no but oneli God of Israel; therfor, Y biseche, that thou take blessyng of thi seruaunt.
16 Nabii akajibu, “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ninamtumikia, sitapokea kitu hata kimoja.” Ingawa Naamani alimsihi sana, yeye alikataa.
And he answeride, The Lord lyueth bifor whom Y stonde, for Y schal not take. And whanne he made `strengthe, that is, greet preier, Elisee assentide not outirli.
17 Naamani akasema, “Ikiwa hutapokea, tafadhali mtumishi wako na apewe udongo kiasi cha mzigo wa kuweza kubebwa na punda wawili, kwa sababu mtumishi wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa na dhabihu kwa mungu mwingine isipokuwa Bwana.
Therfor Naaman seide, As thou wolt; but, I biseche, graunte thou to me, thi seruaunt, that Y take of `the lond the birthun of twei burdones; for thi seruaunt schal no more make brent sacrifice, ether slayn sacrifice, to alien goddis, no but to the Lord.
18 Lakini Bwana na amsamehe mtumishi wake kwa kitu hiki kimoja: Wakati bwana wangu atakapoingia kwenye hekalu la Rimoni ili kusujudu, naye akiwa anauegemea mkono wangu, nami nikasujudu huko pia, wakati nitakaposujudu ndani ya hekalu la Rimoni, Bwana na amsamehe mtumishi wako kwa ajili ya jambo hili.”
Forsothe this thing is oneli, of which thou schalt preie the Lord for thi seruaunt, whanne my lord shal entre into the temple of Remmon, that he worschipe, and while he `schal lene on myn hond, if Y worschipe in the temple of Remmon, while he worschipith in the same place, that the Lord foryyue to thi seruaunt for this thing.
19 Elisha akamwambia, “Nenda kwa amani.” Baada ya Naamani kusafiri umbali fulani,
Which Elisee seide to hym, Go thou in pees. `Therfor he yede fro Elisee in a chosun tyme of the lond.
20 Gehazi, mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu, akajiambia mwenyewe, “Bwana wangu amemwachia kirahisi sana Naamani, huyu Mwaramu, kwa kutokupokea kutoka kwake vile alivyovileta. Hakika kama Bwana aishivyo, nitamkimbilia na kupata kitu kutoka kwake.”
And Giezi, the child of the man of God, seide, My lord sparide this Naaman of Syrie, that he took not of hym that, that he brouyte; the Lord lyueth, for Y schal renne aftir hym, and Y schal take of hym sum thing.
21 Hivyo Gehazi akaharakisha kumfuatilia Naamani. Naamani alipomwona akikimbia kumwelekea, akashuka chini kutoka kwenye gari lake na kwenda kumlaki. Akauliza, “Je, mambo yote ni sawa?”
And Giezi suede aftir the bak of Naaman; and whanne Naaman hadde seyn Giezi rennynge to hym, he skippide doun of the chare in to the metyng of Giezi; and seide, Whether alle thingis ben riytfuli?
22 Gehazi akajibu, “Mambo yote ni sawa. Bwana wangu amenituma nikuambie, ‘Vijana wawili kutoka kwa wana wa manabii wamenijia kutoka nchi ya vilima ya Efraimu. Tafadhali wape talanta ya fedha na mivao miwili ya mavazi.’”
And he seide, Riytfuli; my lord sente me to thee, and seide, Twey yonge men of the hille of Effraym, of the sones of prophetis, camen now to me; yyue thou to hem a talent of siluer, and double chaungyng clothis.
23 Naamani akasema, “Hakika, chukua talanta mbili za fedha.” Akamsihi Gehazi azipokee, kisha akafunga talanta mbili za fedha katika mifuko miwili pamoja na mivao miwili ya mavazi. Akawapa watumishi wake wawili mizigo hiyo, nao wakaibeba wakitangulia mbele ya Gehazi.
And Naaman seide, It is betere that thou take twei talentis. And Naaman constreynede hym; and Naaman boond twei talentis of siluer in twei sackis, and double clothis, and puttide on his twey children, `that is, seruauntis, whiche also baren bifor Giezi.
24 Gehazi alipofika kwenye kilima, akavichukua vile vitu kutoka kwa wale watumishi na kuvificha ndani ya nyumba. Akawaaga wale watu, nao wakaondoka.
And whanne he hadde come thanne in the euentid, he took fro the hond of hem, and leide vp in the hows; and he delyuerede the men, and thei yeden.
25 Kisha akaingia ndani na kusimama mbele ya Elisha bwana wake. Elisha akamuuliza, “Gehazi, ulikuwa wapi?” Gehazi akajibu, “Mtumishi wako hakwenda popote.”
Forsothe Giezi entride, and stood bifor his lord. And Elise seide, Giezi, fro whennus comest thou? Which answeride, Thi seruaunt yede not to ony place.
26 Lakini Elisha akamwambia, “Je, roho yangu haikuwa pamoja nawe wakati yule mtu aliposhuka kutoka kwenye gari lake ili kukulaki? Je, huu ni wakati wa kupokea fedha au kupokea nguo, mashamba ya mizeituni, mashamba ya mizabibu, makundi ya kondoo na mbuzi, makundi ya ngʼombe, au watumishi wa kiume na wa kike?
And Elise seide, Whether myn herte was not in present, whanne the man turnede ayen fro his chare in to the metyng of thee? Now therfor thou hast take siluer, and thou hast take clothis, that thou bie places of olyues, and vyneris, and scheep, and oxis, and seruauntis, and handmaydis;
27 Ukoma wa Naamani utakushika wewe na wazao wako milele.” Kisha Gehazi akaondoka mbele ya Elisha, mwenye ukoma, mweupe kama theluji.
but also the lepre of Naaman schal cleue to thee, and to thi seed withouten ende. And Giezi yede leprouse as snow, `fro hym.

< 2 Wafalme 5 >