< 2 Wafalme 3 >
1 Yehoramu mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili.
Now Jehoram, filho de Acabe, começou a reinar sobre Israel em Samaria no décimo oitavo ano de Jeosafá, rei de Judá, e reinou doze anos.
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini sio kama baba yake na mama yake walivyokuwa wamefanya. Akaondoa nguzo ya ibada ya Baali ambayo baba yake alikuwa ameitengeneza.
Ele fez o que era mau aos olhos de Iavé, mas não como seu pai e como sua mãe, pois ele afastou o pilar de Baal que seu pai havia feito.
3 Hata hivyo akashikamana na dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, wala hakuziacha.
Nevertheless ele segurou os pecados de Jeroboão, filho de Nebat, com os quais fez Israel pecar. Ele não se afastou deles.
4 Basi Mesha mfalme wa Moabu akafuga kondoo, naye akawa ampatie mfalme wa Israeli wana-kondoo 100,000 pamoja na sufu ya kondoo dume 100,000.
Agora Mesha, rei dos Moab, era um criador de ovelhas; e forneceu ao rei de Israel cem mil cordeiros e a lã de cem mil carneiros.
5 Lakini baada ya Ahabu kufa, mfalme wa Moabu aliasi dhidi ya mfalme wa Israeli.
Mas quando Acabe morreu, o rei dos Moab se rebelou contra o rei de Israel.
6 Kwa hiyo wakati ule Mfalme Yehoramu akaondoka kutoka Samaria na kukusanya Israeli yote tayari kwenda vitani.
O rei Jeorão saiu de Samaria naquela época, e reuniu todo o Israel.
7 Akapeleka pia ujumbe ufuatao kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda: “Mfalme wa Moabu ameasi dhidi yangu. Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Moabu?” Akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe. Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
Ele foi e enviou a Jeosafá o rei de Judá, dizendo: “O rei dos moabitas se rebelou contra mim”. Você irá comigo contra os moabitas para a batalha”? Ele disse: “Eu vou subir”. Eu sou como você é, meu povo como seu povo, meus cavalos como seus cavalos”.
8 Akauliza, “Je, tutashambulia kupitia njia gani?” Akajibu, “Kupitia Jangwa la Edomu.”
Então ele disse: “Para que lado devemos subir?” Jehoram respondeu: “O caminho do deserto de Edom”.
9 Hivyo mfalme wa Israeli akaondoka akiwa pamoja na mfalme wa Yuda na mfalme wa Edomu. Baada ya kuzunguka kwa siku saba, jeshi likawa limeishiwa maji kwa matumizi yao na kwa ajili ya wanyama waliokuwa nao.
Então o rei de Israel foi com o rei de Judá e o rei de Edom, e eles marcharam por sete dias ao longo de uma rota tortuosa. Não havia água para o exército ou para os animais que os seguiam.
10 Mfalme wa Israeli akamaka, “Nini! Je, Bwana ametuita sisi wafalme watatu ili tu kututia mikononi mwa Moabu?”
O rei de Israel disse: “Ai de mim! Pois Javé chamou estes três reis para entregá-los na mão dos moabitas”.
11 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa, ili tuweze kumuuliza Bwana kupitia kwake?” Afisa mmoja wa mfalme wa Israeli akajibu, “Elisha mwana wa Shafati yuko hapa. Ndiye alikuwa akimimina maji juu ya mikono ya Eliya.”
Mas Jehoshaphat disse: “Não há aqui um profeta de Javé, para que possamos perguntar a Javé por ele”? Um dos servos do rei de Israel respondeu: “Eliseu, filho de Shaphat, que derramou água nas mãos de Elias, está aqui”.
12 Yehoshafati akasema, “Neno la Bwana liko pamoja naye.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli na Yehoshafati pamoja na mfalme wa Edomu wakamwendea.
Jehoshaphat disse: “A palavra de Yahweh está com ele”. Então o rei de Israel e Jeosafá e o rei de Edom foram até ele.
13 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Nina nini mimi nawe? Nenda kwa manabii wa baba yako na manabii wa mama yako.” Mfalme wa Israeli akajibu, “La hasha, kwa sababu ni Bwana ambaye ametuita pamoja sisi wafalme watatu ili atutie mikononi mwa Moabu.”
Eliseu disse ao rei de Israel: “O que eu tenho a ver com você? Vai aos profetas de teu pai, e aos profetas de tua mãe”. O rei de Israel lhe disse: “Não, pois Javé chamou estes três reis para entregá-los nas mãos dos moabitas”.
14 Elisha akasema, “Hakika, kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo ambaye ninamtumikia, kama si kuheshimu Yehoshafati mfalme wa Yuda, nisingekutazama wala hata kukutupia jicho.
Eliseu disse: “Como vive Javé dos Exércitos, diante do qual estou, certamente, se não respeitasse a presença de Jeosafá, o rei de Judá, não olharia para você, nem o veria.
15 Lakini sasa, nileteeni mpiga kinubi.” Mpiga kinubi alipokuwa akipiga, mkono wa Bwana ukaja juu ya Elisha,
Mas agora me traga um músico”. Quando o músico tocou, a mão de Yahweh veio sobre ele.
16 naye akasema, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Chimbeni bonde hili lijae mahandaki.’
Ele disse: “Yahweh diz: 'Faça este vale cheio de trincheiras'.
17 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana: Hamtaona upepo wala mvua, lakini bonde hili litajaa maji, nanyi pamoja na ngʼombe wenu na wanyama wenu wengine mtakunywa.
Para Iavé diz: 'Você não verá vento, nem chuva, mas aquele vale será cheio de água, e você beberá, tanto você como seu gado e seus outros animais'.
18 Hili ni jambo rahisi machoni pa Bwana. Pia ataitia Moabu mikononi mwenu.
Isto é uma coisa fácil à vista de Iavé. Ele também entregará os moabitas em suas mãos.
19 Mtaushinda kila mji wenye ngome na kila mji mkubwa. Mtakata kila mti ulio mzuri, mtaziba chemchemi zote, na kuharibu kila shamba zuri kwa mawe.”
Você atingirá cada cidade fortificada e cada cidade escolhida, e derrubará cada boa árvore, e parará todas as nascentes de água, e martelará com pedras cada bom pedaço de terra”.
20 Kesho yake asubuhi, karibu na wakati wa kutoa dhabihu ya asubuhi, tazama, maji yakawa yanatiririka kutoka upande wa Edomu! Nayo nchi ikajaa maji.
Pela manhã, na hora de oferecer o sacrifício, eis que a água passou pelo caminho de Edom, e o país estava cheio de água.
21 Basi Wamoabu wote walikuwa wamesikia kuwa wale wafalme wamekuja kupigana dhidi yao. Hivyo kila mtu, kijana na mzee, ambaye angeweza kushika silaha akaitwa na kuwekwa mpakani.
Agora, quando todos os moabitas ouviram que os reis tinham subido para lutar contra eles, eles se reuniram, todos os que podiam colocar armaduras, jovens e velhos, e se colocaram na fronteira.
22 Walipoamka asubuhi na mapema, jua likawa linamulika juu ya maji. Wamoabu waliokuwa upande wa pili wakaona maji ni mekundu, kama damu.
Eles se levantaram cedo pela manhã, e o sol brilhava sobre a água, e os moabitas viram a água em frente deles vermelha como sangue.
23 Wamoabu wakasema, “Ile ni damu! Lazima hao wafalme wamepigana na kuchinjana wao kwa wao. Sasa Moabu, twendeni tukateke nyara!”
Eles disseram: “Isto é sangue”. Os reis estão certamente destruídos, e eles se atingiram uns aos outros. Agora, portanto, Moab, ao saque”!
24 Lakini Wamoabu walipofika kwenye kambi ya Israeli, Waisraeli wakainuka na kuwapiga mpaka wakakimbia. Nao Waisraeli wakaivamia nchi na kuwachinja Wamoabu.
Quando chegaram ao acampamento de Israel, os israelitas se levantaram e atacaram os moabitas, de modo que fugiram diante deles; e avançaram para a terra atacando os moabitas.
25 Wakaiharibu miji, kila mtu akatupa jiwe juu ya kila shamba zuri mpaka likafunikwa. Wakaziba chemchemi zote na kukata kila mti mzuri. Kir-Haresethi peke yake ndio uliobaki na mawe yake yakiwa mahali pake. Lakini hata hivyo watu waliokuwa na makombeo wakauzunguka na kuushambulia vilevile.
Eles derrubaram as cidades; e em cada bom pedaço de terra cada homem atirou sua pedra e a encheu. Eles também pararam todas as fontes de água e cortaram todas as árvores boas, até que em Kir Hareseth tudo o que eles deixaram foram suas pedras; no entanto, os homens armados com fundas foram em torno dela e a atacaram.
26 Mfalme wa Moabu alipoona kuwa vita vimekuwa vikali dhidi yake, akachukua watu 700 wenye panga ili kuingia kwa mfalme wa Edomu, lakini wakashindwa.
Quando o rei dos moabitas viu que a batalha era muito severa para ele, levou consigo setecentos homens que desembainharam uma espada, para romper com o rei de Edom; mas eles não conseguiram.
27 Ndipo akamchukua mwanawe mzaliwa wake wa kwanza, ambaye angekuwa mfalme baada yake, akamtoa kama dhabihu ya kuteketezwa juu ya ukuta wa mji. Ghadhabu ikawa kubwa dhidi ya Israeli; wakajiondoa kwake na kurudi katika nchi yao wenyewe.
Então ele levou seu filho mais velho, que teria reinado em seu lugar, e o ofereceu por um holocausto na parede. Houve grande ira contra Israel; e eles se afastaram dele, e voltaram para suas próprias terras.