< 2 Wafalme 3 >
1 Yehoramu mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili.
Or Joram, fils d'Achab, régna sur Israël à Samarie, la dix-huitième année de Josaphat, roi de Juda, et il régna douze ans.
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini sio kama baba yake na mama yake walivyokuwa wamefanya. Akaondoa nguzo ya ibada ya Baali ambayo baba yake alikuwa ameitengeneza.
Il fit ce qui est mal aux yeux de Yahvé, mais non pas comme son père et comme sa mère, car il fit disparaître la statue de Baal que son père avait faite.
3 Hata hivyo akashikamana na dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, wala hakuziacha.
Mais il s'attacha aux péchés de Jéroboam, fils de Nebath, par lesquels il avait fait pécher Israël. Il ne s'en détourna pas.
4 Basi Mesha mfalme wa Moabu akafuga kondoo, naye akawa ampatie mfalme wa Israeli wana-kondoo 100,000 pamoja na sufu ya kondoo dume 100,000.
Or Mesha, roi de Moab, était éleveur de moutons, et il fournissait au roi d'Israël cent mille agneaux et la laine de cent mille béliers.
5 Lakini baada ya Ahabu kufa, mfalme wa Moabu aliasi dhidi ya mfalme wa Israeli.
Mais quand Achab fut mort, le roi de Moab se rebella contre le roi d'Israël.
6 Kwa hiyo wakati ule Mfalme Yehoramu akaondoka kutoka Samaria na kukusanya Israeli yote tayari kwenda vitani.
En ce temps-là, le roi Joram sortit de Samarie et rassembla tout Israël.
7 Akapeleka pia ujumbe ufuatao kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda: “Mfalme wa Moabu ameasi dhidi yangu. Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Moabu?” Akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe. Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
Il alla trouver Josaphat, roi de Juda, et lui dit: « Le roi de Moab s'est révolté contre moi. Veux-tu aller avec moi au combat contre Moab? » Il a dit: « Je vais monter. Je suis comme vous, mon peuple comme votre peuple, mes chevaux comme vos chevaux. »
8 Akauliza, “Je, tutashambulia kupitia njia gani?” Akajibu, “Kupitia Jangwa la Edomu.”
Puis il dit: « Par où monterons-nous? » Jéhoram répondit: « Le chemin du désert d'Édom. »
9 Hivyo mfalme wa Israeli akaondoka akiwa pamoja na mfalme wa Yuda na mfalme wa Edomu. Baada ya kuzunguka kwa siku saba, jeshi likawa limeishiwa maji kwa matumizi yao na kwa ajili ya wanyama waliokuwa nao.
Le roi d'Israël partit avec le roi de Juda et le roi d'Édom, et ils marchèrent pendant sept jours sur un chemin détourné. Il n'y avait pas d'eau pour l'armée ni pour les animaux qui les suivaient.
10 Mfalme wa Israeli akamaka, “Nini! Je, Bwana ametuita sisi wafalme watatu ili tu kututia mikononi mwa Moabu?”
Le roi d'Israël dit: « Hélas! Car Yahvé a convoqué ces trois rois pour les livrer entre les mains de Moab. »
11 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa, ili tuweze kumuuliza Bwana kupitia kwake?” Afisa mmoja wa mfalme wa Israeli akajibu, “Elisha mwana wa Shafati yuko hapa. Ndiye alikuwa akimimina maji juu ya mikono ya Eliya.”
Mais Josaphat dit: « N'y a-t-il pas ici un prophète de Yahvé, afin que nous puissions interroger Yahvé par lui? » L'un des serviteurs du roi d'Israël répondit: « Élisée, fils de Shaphat, qui a versé de l'eau sur les mains d'Élie, est ici. »
12 Yehoshafati akasema, “Neno la Bwana liko pamoja naye.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli na Yehoshafati pamoja na mfalme wa Edomu wakamwendea.
Josaphat dit: « La parole de Yahvé est avec lui. » Et le roi d'Israël, Josaphat et le roi d'Édom descendirent auprès de lui.
13 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Nina nini mimi nawe? Nenda kwa manabii wa baba yako na manabii wa mama yako.” Mfalme wa Israeli akajibu, “La hasha, kwa sababu ni Bwana ambaye ametuita pamoja sisi wafalme watatu ili atutie mikononi mwa Moabu.”
Élisée dit au roi d'Israël: « Qu'ai-je à faire avec toi? Va vers les prophètes de ton père et vers les prophètes de ta mère. » Le roi d'Israël lui répondit: « Non, car Yahvé a convoqué ces trois rois pour les livrer entre les mains de Moab. »
14 Elisha akasema, “Hakika, kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo ambaye ninamtumikia, kama si kuheshimu Yehoshafati mfalme wa Yuda, nisingekutazama wala hata kukutupia jicho.
Élisée dit: « L'Éternel des armées, devant qui je me tiens, est vivant. Si je ne respectais pas la présence de Josaphat, roi de Juda, je ne regarderais pas vers toi et je ne te verrais pas.
15 Lakini sasa, nileteeni mpiga kinubi.” Mpiga kinubi alipokuwa akipiga, mkono wa Bwana ukaja juu ya Elisha,
Mais maintenant, amène-moi un musicien. » Lorsque le musicien joua, la main de Yahvé se posa sur lui.
16 naye akasema, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Chimbeni bonde hili lijae mahandaki.’
Il dit: « L'Éternel dit: Fais de cette vallée des tranchées.
17 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana: Hamtaona upepo wala mvua, lakini bonde hili litajaa maji, nanyi pamoja na ngʼombe wenu na wanyama wenu wengine mtakunywa.
Car Yahvé dit: 'Tu ne verras pas de vent, ni de pluie, mais cette vallée sera remplie d'eau, et tu boiras, toi, ton bétail et tes autres animaux'.
18 Hili ni jambo rahisi machoni pa Bwana. Pia ataitia Moabu mikononi mwenu.
C'est une chose facile aux yeux de l'Éternel. Il livrera aussi les Moabites entre vos mains.
19 Mtaushinda kila mji wenye ngome na kila mji mkubwa. Mtakata kila mti ulio mzuri, mtaziba chemchemi zote, na kuharibu kila shamba zuri kwa mawe.”
Vous frapperez toutes les villes fortes et toutes les villes de choix, vous abattrez tous les bons arbres, vous arrêterez toutes les sources d'eau et vous marquerez de pierres tout bon terrain.'"
20 Kesho yake asubuhi, karibu na wakati wa kutoa dhabihu ya asubuhi, tazama, maji yakawa yanatiririka kutoka upande wa Edomu! Nayo nchi ikajaa maji.
Le matin, au moment d'offrir le sacrifice, voici que de l'eau arriva par le chemin d'Édom, et le pays fut rempli d'eau.
21 Basi Wamoabu wote walikuwa wamesikia kuwa wale wafalme wamekuja kupigana dhidi yao. Hivyo kila mtu, kijana na mzee, ambaye angeweza kushika silaha akaitwa na kuwekwa mpakani.
Et quand tous les Moabites apprirent que les rois étaient montés pour les combattre, ils se rassemblèrent, tous ceux qui pouvaient se revêtir d'une armure, jeunes et vieux, et ils se tinrent sur la frontière.
22 Walipoamka asubuhi na mapema, jua likawa linamulika juu ya maji. Wamoabu waliokuwa upande wa pili wakaona maji ni mekundu, kama damu.
Ils se levèrent de bon matin, et le soleil brilla sur l'eau. Les Moabites virent l'eau en face d'eux, rouge comme du sang.
23 Wamoabu wakasema, “Ile ni damu! Lazima hao wafalme wamepigana na kuchinjana wao kwa wao. Sasa Moabu, twendeni tukateke nyara!”
Ils dirent: « C'est du sang. Les rois sont certainement détruits, et ils se sont frappés les uns les autres. Maintenant donc, Moab, au pillage! »
24 Lakini Wamoabu walipofika kwenye kambi ya Israeli, Waisraeli wakainuka na kuwapiga mpaka wakakimbia. Nao Waisraeli wakaivamia nchi na kuwachinja Wamoabu.
Lorsqu'ils arrivèrent au camp d'Israël, les Israélites se levèrent et frappèrent les Moabites, de sorte qu'ils prirent la fuite devant eux; ils s'avancèrent dans le pays en attaquant les Moabites.
25 Wakaiharibu miji, kila mtu akatupa jiwe juu ya kila shamba zuri mpaka likafunikwa. Wakaziba chemchemi zote na kukata kila mti mzuri. Kir-Haresethi peke yake ndio uliobaki na mawe yake yakiwa mahali pake. Lakini hata hivyo watu waliokuwa na makombeo wakauzunguka na kuushambulia vilevile.
Ils battirent les villes, et sur tout bon terrain, chacun jeta sa pierre et la remplit. Ils bouchèrent aussi toutes les sources d'eau et coupèrent tous les bons arbres, jusqu'à ce qu'il ne reste à Kir Hareseth que ses pierres; cependant les hommes armés de frondes en firent le tour et l'attaquèrent.
26 Mfalme wa Moabu alipoona kuwa vita vimekuwa vikali dhidi yake, akachukua watu 700 wenye panga ili kuingia kwa mfalme wa Edomu, lakini wakashindwa.
Lorsque le roi de Moab vit que la bataille était trop rude pour lui, il prit avec lui sept cents hommes tirant l'épée, pour percer jusqu'au roi d'Édom; mais ils ne purent pas.
27 Ndipo akamchukua mwanawe mzaliwa wake wa kwanza, ambaye angekuwa mfalme baada yake, akamtoa kama dhabihu ya kuteketezwa juu ya ukuta wa mji. Ghadhabu ikawa kubwa dhidi ya Israeli; wakajiondoa kwake na kurudi katika nchi yao wenyewe.
Alors il prit son fils aîné, qui devait régner à sa place, et l'offrit en holocauste sur la muraille. Il y eut une grande colère contre Israël; ils s'éloignèrent de lui et retournèrent dans leur pays.