< 2 Wafalme 3 >
1 Yehoramu mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili.
and Joram son: child Ahab to reign upon Israel in/on/with Samaria in/on/with year eight ten to/for Jehoshaphat king Judah and to reign two ten year
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini sio kama baba yake na mama yake walivyokuwa wamefanya. Akaondoa nguzo ya ibada ya Baali ambayo baba yake alikuwa ameitengeneza.
and to make: do [the] bad: evil in/on/with eye: seeing LORD except not like/as father his and like/as mother his and to turn aside: remove [obj] pillar [the] Baal which to make father his
3 Hata hivyo akashikamana na dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, wala hakuziacha.
except in/on/with sin Jeroboam son: child Nebat which to sin [obj] Israel to cleave not to turn aside: depart from her
4 Basi Mesha mfalme wa Moabu akafuga kondoo, naye akawa ampatie mfalme wa Israeli wana-kondoo 100,000 pamoja na sufu ya kondoo dume 100,000.
and Mesha king Moab to be shepherd and to return: return to/for king Israel hundred thousand ram and hundred thousand ram wool
5 Lakini baada ya Ahabu kufa, mfalme wa Moabu aliasi dhidi ya mfalme wa Israeli.
and to be like/as death Ahab and to transgress king Moab in/on/with king Israel
6 Kwa hiyo wakati ule Mfalme Yehoramu akaondoka kutoka Samaria na kukusanya Israeli yote tayari kwenda vitani.
and to come out: come [the] king Joram in/on/with day [the] he/she/it from Samaria and to reckon: list [obj] all Israel
7 Akapeleka pia ujumbe ufuatao kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda: “Mfalme wa Moabu ameasi dhidi yangu. Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Moabu?” Akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe. Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
and to go: went and to send: depart to(wards) Jehoshaphat king Judah to/for to say king Moab to transgress in/on/with me to go: went with me to(wards) Moab to/for battle and to say to ascend: rise like me like you like/as people my like/as people your like/as horse my like/as horse your
8 Akauliza, “Je, tutashambulia kupitia njia gani?” Akajibu, “Kupitia Jangwa la Edomu.”
and to say where? this [the] way: road to ascend: rise and to say way: road wilderness Edom
9 Hivyo mfalme wa Israeli akaondoka akiwa pamoja na mfalme wa Yuda na mfalme wa Edomu. Baada ya kuzunguka kwa siku saba, jeshi likawa limeishiwa maji kwa matumizi yao na kwa ajili ya wanyama waliokuwa nao.
and to go: went king Israel and king Judah and king Edom and to turn: surround way: journey seven day and not to be water to/for camp and to/for animal which in/on/with foot their
10 Mfalme wa Israeli akamaka, “Nini! Je, Bwana ametuita sisi wafalme watatu ili tu kututia mikononi mwa Moabu?”
and to say king Israel alas! for to call: call to LORD to/for three [the] king [the] these to/for to give: give [obj] them in/on/with hand: power Moab
11 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa, ili tuweze kumuuliza Bwana kupitia kwake?” Afisa mmoja wa mfalme wa Israeli akajibu, “Elisha mwana wa Shafati yuko hapa. Ndiye alikuwa akimimina maji juu ya mikono ya Eliya.”
and to say Jehoshaphat nothing here prophet to/for LORD and to seek [obj] LORD from [obj] him and to answer one from servant/slave king Israel and to say here Elisha son: child Shaphat which to pour: pour water upon hand Elijah
12 Yehoshafati akasema, “Neno la Bwana liko pamoja naye.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli na Yehoshafati pamoja na mfalme wa Edomu wakamwendea.
and to say Jehoshaphat there [obj] him word LORD and to go down to(wards) him king Israel and Jehoshaphat and king Edom
13 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Nina nini mimi nawe? Nenda kwa manabii wa baba yako na manabii wa mama yako.” Mfalme wa Israeli akajibu, “La hasha, kwa sababu ni Bwana ambaye ametuita pamoja sisi wafalme watatu ili atutie mikononi mwa Moabu.”
and to say Elisha to(wards) king Israel what? to/for me and to/for you to go: went to(wards) prophet father your and to(wards) prophet mother your and to say to/for him king Israel not for to call: call to LORD to/for three [the] king [the] these to/for to give: give [obj] them in/on/with hand: power Moab
14 Elisha akasema, “Hakika, kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo ambaye ninamtumikia, kama si kuheshimu Yehoshafati mfalme wa Yuda, nisingekutazama wala hata kukutupia jicho.
and to say Elisha alive LORD Hosts which to stand: stand to/for face: before his for unless face of Jehoshaphat king Judah I to lift: kindness if: surely no to look to(wards) you and if: surely no to see: see you
15 Lakini sasa, nileteeni mpiga kinubi.” Mpiga kinubi alipokuwa akipiga, mkono wa Bwana ukaja juu ya Elisha,
and now to take: bring to/for me to play and to be like/as to play [the] to play and to be upon him hand: power LORD
16 naye akasema, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Chimbeni bonde hili lijae mahandaki.’
and to say thus to say LORD to make [the] torrent: valley [the] this cistern cistern
17 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana: Hamtaona upepo wala mvua, lakini bonde hili litajaa maji, nanyi pamoja na ngʼombe wenu na wanyama wenu wengine mtakunywa.
for thus to say LORD not to see: see spirit: breath and not to see: see rain and [the] torrent: valley [the] he/she/it to fill water and to drink you(m. p.) and livestock your and animal your
18 Hili ni jambo rahisi machoni pa Bwana. Pia ataitia Moabu mikononi mwenu.
and to lighten this in/on/with eye: seeing LORD and to give: give [obj] Moab in/on/with hand: power your
19 Mtaushinda kila mji wenye ngome na kila mji mkubwa. Mtakata kila mti ulio mzuri, mtaziba chemchemi zote, na kuharibu kila shamba zuri kwa mawe.”
and to smite all city fortification and all city choice and all tree pleasant to fall: fell(trees) and all spring water to close and all [the] portion [the] pleasant to pain in/on/with stone
20 Kesho yake asubuhi, karibu na wakati wa kutoa dhabihu ya asubuhi, tazama, maji yakawa yanatiririka kutoka upande wa Edomu! Nayo nchi ikajaa maji.
and to be in/on/with morning like/as to ascend: offer up [the] offering and behold water to come (in): come from way: direction Edom and to fill [the] land: country/planet [obj] [the] water
21 Basi Wamoabu wote walikuwa wamesikia kuwa wale wafalme wamekuja kupigana dhidi yao. Hivyo kila mtu, kijana na mzee, ambaye angeweza kushika silaha akaitwa na kuwekwa mpakani.
and all Moab to hear: hear for to ascend: rise [the] king to/for to fight in/on/with them and to cry from all to gird belt and above [to] and to stand: stand upon [the] border: boundary
22 Walipoamka asubuhi na mapema, jua likawa linamulika juu ya maji. Wamoabu waliokuwa upande wa pili wakaona maji ni mekundu, kama damu.
and to rise in/on/with morning and [the] sun to rise upon [the] water and to see: see Moab from before [obj] [the] water red like/as blood
23 Wamoabu wakasema, “Ile ni damu! Lazima hao wafalme wamepigana na kuchinjana wao kwa wao. Sasa Moabu, twendeni tukateke nyara!”
and to say blood this to slay to slay [the] king and to smite man: anyone [obj] neighbor his and now to/for spoil Moab
24 Lakini Wamoabu walipofika kwenye kambi ya Israeli, Waisraeli wakainuka na kuwapiga mpaka wakakimbia. Nao Waisraeli wakaivamia nchi na kuwachinja Wamoabu.
and to come (in): come to(wards) camp Israel and to arise: rise Israel and to smite [obj] Moab and to flee from face: before their (and to smite *Q(K)*) in/on/with her and to smite [obj] Moab
25 Wakaiharibu miji, kila mtu akatupa jiwe juu ya kila shamba zuri mpaka likafunikwa. Wakaziba chemchemi zote na kukata kila mti mzuri. Kir-Haresethi peke yake ndio uliobaki na mawe yake yakiwa mahali pake. Lakini hata hivyo watu waliokuwa na makombeo wakauzunguka na kuushambulia vilevile.
and [the] city to overthrow and all portion pleasant to throw man: anyone stone his and to fill her and all spring water to close and all tree pleasant to fall: fell(trees) till to remain stone her in/on/with Kir-hareseth Kir-hareseth and to turn: surround [the] slinger and to smite her
26 Mfalme wa Moabu alipoona kuwa vita vimekuwa vikali dhidi yake, akachukua watu 700 wenye panga ili kuingia kwa mfalme wa Edomu, lakini wakashindwa.
and to see: see king Moab for to strengthen: prevail over from him [the] battle and to take: take with him seven hundred man to draw sword to/for to break up/open to(wards) king Edom and not be able
27 Ndipo akamchukua mwanawe mzaliwa wake wa kwanza, ambaye angekuwa mfalme baada yake, akamtoa kama dhabihu ya kuteketezwa juu ya ukuta wa mji. Ghadhabu ikawa kubwa dhidi ya Israeli; wakajiondoa kwake na kurudi katika nchi yao wenyewe.
and to take: take [obj] son: child his [the] firstborn which to reign underneath: instead him and to ascend: offer up him burnt offering upon [the] wall and to be wrath great: large upon Israel and to set out from upon him and to return: return to/for land: country/planet