< 2 Wafalme 3 >

1 Yehoramu mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili.
And Jehoram son of Ahab has reigned over Israel, in Samaria, in the eighteenth year of Jehoshaphat king of Judah, and he reigns twelve years,
2 Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini sio kama baba yake na mama yake walivyokuwa wamefanya. Akaondoa nguzo ya ibada ya Baali ambayo baba yake alikuwa ameitengeneza.
and does evil in the eyes of YHWH, only not like his father, and like his mother, and he turns aside the standing-pillar of Ba‘al that his father made;
3 Hata hivyo akashikamana na dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, wala hakuziacha.
surely he has cleaved to the sins of Jeroboam son of Nebat that he caused Israel to sin; he has not turned aside from it.
4 Basi Mesha mfalme wa Moabu akafuga kondoo, naye akawa ampatie mfalme wa Israeli wana-kondoo 100,000 pamoja na sufu ya kondoo dume 100,000.
And Mesha king of Moab was a sheep-master, and he rendered to the king of Israel one hundred thousand lambs and one hundred thousand rams, [with] wool,
5 Lakini baada ya Ahabu kufa, mfalme wa Moabu aliasi dhidi ya mfalme wa Israeli.
and it comes to pass at the death of Ahab, that the king of Moab transgresses against the king of Israel.
6 Kwa hiyo wakati ule Mfalme Yehoramu akaondoka kutoka Samaria na kukusanya Israeli yote tayari kwenda vitani.
And King Jehoram goes out from Samaria in that day, and inspects all Israel,
7 Akapeleka pia ujumbe ufuatao kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda: “Mfalme wa Moabu ameasi dhidi yangu. Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Moabu?” Akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe. Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
and goes and sends to Jehoshaphat king of Judah, saying, “The king of Moab has transgressed against me; do you go with me to Moab for battle?” And he says, “I go up, as I, so you; as my people, so your people; as my horses, so your horses.”
8 Akauliza, “Je, tutashambulia kupitia njia gani?” Akajibu, “Kupitia Jangwa la Edomu.”
And he says, “Where [is] this—the way we go up?” And he says, “The way of the wilderness of Edom.”
9 Hivyo mfalme wa Israeli akaondoka akiwa pamoja na mfalme wa Yuda na mfalme wa Edomu. Baada ya kuzunguka kwa siku saba, jeshi likawa limeishiwa maji kwa matumizi yao na kwa ajili ya wanyama waliokuwa nao.
And the king of Israel goes, and the king of Judah, and the king of Edom, and they turn around the way seven days, and there has been no water for the camp, and for the livestock that [are] at their feet,
10 Mfalme wa Israeli akamaka, “Nini! Je, Bwana ametuita sisi wafalme watatu ili tu kututia mikononi mwa Moabu?”
and the king of Israel says, “Aah! For YHWH has called for these three kings to give them into the hand of Moab.”
11 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa, ili tuweze kumuuliza Bwana kupitia kwake?” Afisa mmoja wa mfalme wa Israeli akajibu, “Elisha mwana wa Shafati yuko hapa. Ndiye alikuwa akimimina maji juu ya mikono ya Eliya.”
And Jehoshaphat says, “Is there not a prophet of YHWH here, and we seek YHWH by him?” And one of the servants of the king of Israel answers and says, “Here [is] Elisha son of Shaphat, who poured water on the hands of Elijah.”
12 Yehoshafati akasema, “Neno la Bwana liko pamoja naye.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli na Yehoshafati pamoja na mfalme wa Edomu wakamwendea.
And Jehoshaphat says, “The word of YHWH is with him”; and the king of Israel goes down to him, and Jehoshaphat, and the king of Edom.
13 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Nina nini mimi nawe? Nenda kwa manabii wa baba yako na manabii wa mama yako.” Mfalme wa Israeli akajibu, “La hasha, kwa sababu ni Bwana ambaye ametuita pamoja sisi wafalme watatu ili atutie mikononi mwa Moabu.”
And Elisha says to the king of Israel, “And what do I [have to do] with you? Go to the prophets of your father, and to the prophets of your mother”; and the king of Israel says to him, “No, for YHWH has called for these three kings to give them into the hand of Moab.”
14 Elisha akasema, “Hakika, kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo ambaye ninamtumikia, kama si kuheshimu Yehoshafati mfalme wa Yuda, nisingekutazama wala hata kukutupia jicho.
And Elisha says, “YHWH of Hosts lives, before whom I have stood; for unless I am lifting up the face of Jehoshaphat king of Judah, I do not look to you, nor see you;
15 Lakini sasa, nileteeni mpiga kinubi.” Mpiga kinubi alipokuwa akipiga, mkono wa Bwana ukaja juu ya Elisha,
and now, bring a musician to me”; and it has been, at the playing of the musician, that the hand of YHWH is on him,
16 naye akasema, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Chimbeni bonde hili lijae mahandaki.’
and he says, “Thus said YHWH: Make this valley ditches—ditches;
17 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana: Hamtaona upepo wala mvua, lakini bonde hili litajaa maji, nanyi pamoja na ngʼombe wenu na wanyama wenu wengine mtakunywa.
for thus said YHWH: You do not see wind, nor do you see rain, and that valley is full of water, and you have drunk—you, and your livestock, and your beasts.
18 Hili ni jambo rahisi machoni pa Bwana. Pia ataitia Moabu mikononi mwenu.
And this has been light in the eyes of YHWH, and he has given Moab into your hand,
19 Mtaushinda kila mji wenye ngome na kila mji mkubwa. Mtakata kila mti ulio mzuri, mtaziba chemchemi zote, na kuharibu kila shamba zuri kwa mawe.”
and you have struck every fortified city, and every choice city, and you cause every good tree to fall, and you stop all fountains of waters, and you mar every good portion with stones.”
20 Kesho yake asubuhi, karibu na wakati wa kutoa dhabihu ya asubuhi, tazama, maji yakawa yanatiririka kutoka upande wa Edomu! Nayo nchi ikajaa maji.
And it comes to pass in the morning, at the ascending of the [morning] present, that behold, waters are coming in from the way of Edom, and the land is filled with the waters,
21 Basi Wamoabu wote walikuwa wamesikia kuwa wale wafalme wamekuja kupigana dhidi yao. Hivyo kila mtu, kijana na mzee, ambaye angeweza kushika silaha akaitwa na kuwekwa mpakani.
and all of Moab has heard that the kings have come up to fight against them, and they are called together, from everyone girding on a girdle and upward, and they stand by the border.
22 Walipoamka asubuhi na mapema, jua likawa linamulika juu ya maji. Wamoabu waliokuwa upande wa pili wakaona maji ni mekundu, kama damu.
And they rise early in the morning, and the sun has shone on the waters, and the Moabites see, from opposite [them], [that] the waters [are] red as blood,
23 Wamoabu wakasema, “Ile ni damu! Lazima hao wafalme wamepigana na kuchinjana wao kwa wao. Sasa Moabu, twendeni tukateke nyara!”
and say, “This [is] blood; the kings have been surely destroyed, and they each strike his neighbor; and now for spoil, Moab!”
24 Lakini Wamoabu walipofika kwenye kambi ya Israeli, Waisraeli wakainuka na kuwapiga mpaka wakakimbia. Nao Waisraeli wakaivamia nchi na kuwachinja Wamoabu.
And they come to the camp of Israel, and Israel rises, and strikes the Moabites, and they flee from their face; and they enter into Moab, so as to strike Moab,
25 Wakaiharibu miji, kila mtu akatupa jiwe juu ya kila shamba zuri mpaka likafunikwa. Wakaziba chemchemi zote na kukata kila mti mzuri. Kir-Haresethi peke yake ndio uliobaki na mawe yake yakiwa mahali pake. Lakini hata hivyo watu waliokuwa na makombeo wakauzunguka na kuushambulia vilevile.
and they break down the cities, and they each cast his stone [on] every good portion, and have filled it, and they stop every fountain of water, and they cause every good tree to fall—until one had left its stones in Kir-Haraseth, and the slingers go around and strike it.
26 Mfalme wa Moabu alipoona kuwa vita vimekuwa vikali dhidi yake, akachukua watu 700 wenye panga ili kuingia kwa mfalme wa Edomu, lakini wakashindwa.
And the king of Moab sees that the battle has been too strong for him, and he takes with him seven hundred men drawing sword, to cleave through to the king of Edom, and they have not been able,
27 Ndipo akamchukua mwanawe mzaliwa wake wa kwanza, ambaye angekuwa mfalme baada yake, akamtoa kama dhabihu ya kuteketezwa juu ya ukuta wa mji. Ghadhabu ikawa kubwa dhidi ya Israeli; wakajiondoa kwake na kurudi katika nchi yao wenyewe.
and he takes his son, the firstborn who reigns in his stead, and causes him to ascend [as] a burnt-offering on the wall, and there is great wrath against Israel, and they journey from off him, and return to the land.

< 2 Wafalme 3 >