< 2 Wafalme 25 >
1 Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli, akiwa na jeshi lake lote, alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Akapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
Il arriva donc la neuvième année du règne de Sédécias, le dixième jour du dixième mois, que Nébucadnetsar Roi de Babylone vint avec toute son armée contre Jérusalem, et se campa contr'elle, et ils bâtirent des forts tout autour.
2 Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
Et la ville fut assiégée jusqu'à la onzième année du Roi Sédécias.
3 Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
Et le neuvième jour du [quatrième] mois la famine augmenta dans la ville, de sorte qu'il n'y avait point de pain pour le peuple du pays.
4 Kisha ukuta wa mji ukavunjwa, na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
Alors la brèche fut faite à la ville, et tous les gens de guerre [s'enfuirent] de nuit par le chemin de la porte entre les deux murailles qui [étaient] près du jardin du Roi (or les Caldéens [étaient tout] joignant la ville à l'environ) et le Roi s'en alla par le chemin de la campagne.
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia mfalme na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
Mais l'armée des Caldéens poursuivit le Roi, et quand ils l'eurent atteint dans les campagnes de Jérico, toute son armée se dispersa d'auprès de lui.
6 naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, mahali ambapo hukumu yake ilitangazwa.
Ils prirent donc le Roi, et le firent monter vers le Roi de Babylone à Ribla; où on lui fit son procès.
7 Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Kisha wakayangʼoa macho yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
Et on égorgea les fils de Sédécias en sa présence; après quoi on creva les yeux à Sédécias, et l'ayant lié de doubles chaînes d'airain, on le mena à Babylone.
8 Mnamo siku ya saba ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, afisa wa mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
Et au septième [jour] du cinquième mois, en la dix-neuvième année du Roi Nébucadnetsar, Roi de Babylone, Nébuzar-adan prévôt de l'hôtel, serviteur du Roi de Babylone, entra dans Jérusalem;
9 Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
Et il brûla la maison de l'Eternel, et la maison Royale, et toutes les maisons de Jérusalem, et mit le feu dans toutes les maisons des Grands.
10 Jeshi lote la Wakaldayo, chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme, walivunja kuta zilizoizunguka Yerusalemu.
Et toute l'armée des Caldéens, qui [était] avec le prévôt de l'hôtel, démolit les murailles de Jérusalem tout autour.
11 Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi akawapeleka uhamishoni watu waliokuwa wamebaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
Et Nébuzar-adan prévôt de l'hôtel transporta [à Babylone] le reste du peuple, [savoir] ceux qui étaient demeurés de reste dans la ville, et ceux qui s'étaient allés rendre au Roi de Babylone, et le reste de la multitude.
12 Lakini yule jemadari wa askari walinzi akawaacha baadhi ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
Néanmoins le prévôt de l'hôtel laissa quelques-uns des plus pauvres du pays pour [être] vignerons et laboureurs.
13 Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba na kuipeleka Babeli.
Et les Caldéens mirent en pièces les colonnes d'airain qui [étaient] dans la maison de l'Eternel, et les soubassements, et la mer d'airain qui [était] dans la maison de l'Eternel, et ils en emportèrent l'airain à Babylone.
14 Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
Ils emportèrent aussi les chaudrons, et les racloirs, et les serpes, et les tasses, et tous les ustensiles d'airain dont on faisait le service.
15 Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua vile vyetezo na yale mabakuli ya kunyunyizia, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
Le prévôt de l'hôtel emporta aussi les encensoirs et les bassins; et ce qui était d'or, et ce qui était d'argent.
16 Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
Quant aux deux colonnes, à la mer, et aux soubassements que Salomon avait faits pour la maison de l'Eternel, on ne pesa point l'airain de tous ces vaisseaux.
17 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane. Sehemu ya shaba juu ya nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tatu na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na wavu wake ilifanana na hiyo ya kwanza.
Chaque colonne avait dix-huit coudées de haut, et elle avait un chapiteau d'airain par dessus, dont la hauteur était de trois coudées, outre le rets et les grenades qui étaient autour du chapiteau, le tout d'airain; et la seconde colonne était de même façon, avec le rets.
18 Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
Le prévôt de l'hôtel emmena aussi Séraja premier Sacrificateur, et Sophonie second Sacrificateur, et les trois gardes des vaisseaux.
19 Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri watano wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
Il emmena aussi de la ville un Eunuque qui avait la charge des hommes de guerre, et cinq hommes de ceux qui voyaient la face du Roi, lesquels furent trouvés dans la ville. [Il emmena] aussi le Secrétaire du Capitaine de l'armée qui enrôlait le peuple du pays, et soixante hommes d'entre le peuple du pays, qui furent trouvés dans la ville.
20 Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
Nébuzar-adan donc prévôt de l'hôtel les prit, et les mena au Roi de Babylone à Ribla.
21 Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
Et le Roi de Babylone les frappa, et les fit mourir à Ribla, au pays de Hamath; ainsi Juda fut transporté hors de sa terre.
22 Nebukadneza mfalme wa Babeli akamteua Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, awe msimamizi wa watu aliowaacha Yuda.
Mais quant au peuple qui était demeuré de reste au pays de Juda, [et] que Nébucadnetsar Roi de Babylone y avait laissé, il établit pour Gouverneur sur eux Guédalia fils d'Ahikam, fils de Saphan.
23 Maafisa wote wa jeshi na watu wao waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemteua Gedalia kuwa mtawala, wakamjia Gedalia huko Mispa. Hawa walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofathi, na Yezania mwana wa Mmaaka, pamoja na watu wao.
Quand tous les Capitaines des gens de guerre, et leurs gens, eurent appris que le Roi de Babylone avait établi Guédalia pour Gouverneur, ils allèrent trouver Guédalia à Mitspa, [savoir]Ismaël fils de Néthania, et Johanan fils de Karéath, et Séraja fils de Tanhumeth Nétophathite, Jaazania fils d'un Mahachathite, eux et leurs gens.
24 Gedalia akaapa ili kuwatia moyo wao na watu wao. Akasema, “Msiwaogope maafisa wa Kikaldayo. Kaeni katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vyema kwenu.”
Et Guédalia leur jura et à leurs gens, et leur dit: Ne faites pas difficulté d'être serviteurs des Caldéens; demeurez au pays, et servez le Roi de Babylone, et vous vous en trouverez bien.
25 Hata hivyo, katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi, nao wakamuua Gedalia, na pia watu wa Yuda, pamoja na Wakaldayo waliokuwa naye huko Mispa.
Mais il arriva au septième mois, qu'Ismaël fils de Néthania, fils d'Elisamah, qui était du sang Royal, et dix hommes avec lui vinrent, et frappèrent Guédalia, dont il mourut. [Ils frappèrent] aussi les Juifs et les Caldéens qui étaient avec lui à Mitspa.
26 Baada ya haya, watu wote kuanzia aliye mdogo sana hadi aliye mkubwa kabisa, pamoja na maafisa wa jeshi, wakakimbilia Misri kwa kuwaogopa Wakaldayo.
Et tout le peuple depuis le plus petit jusqu'au plus grand, avec les capitaines des gens de guerre, se levèrent, et s'en allèrent en Egypte, parce qu'ils avaient peur des Caldéens.
27 Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini kutoka gerezani siku ya ishirini na saba ya mwezi wa kumi na mbili.
Or il arriva la trente-septième année de la captivité de Jéhojachin Roi de Juda, le vingt-septième jour du douzième mois, qu'Evilmérodac, Roi de Babylone, l'année qu'il commença à régner, tira hors de prison Jéhojachin Roi de Juda, et le mit en liberté.
28 Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
Et il lui parla avec douceur, et mit son trône au dessus du trône des Rois qui étaient avec lui à Babylone.
29 Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
Et après qu'il lui eut changé ses vêtements de prison, il mangea du pain ordinairement tout le temps de sa vie en sa présence.
30 Siku kwa siku mfalme alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake.
Et quant à son ordinaire, un ordinaire continuel lui fut établi par le Roi chaque jour, tout le temps de sa vie.