< 2 Wafalme 25 >

1 Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli, akiwa na jeshi lake lote, alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Akapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
and to be in/on/with year [the] ninth to/for to reign him in/on/with month [the] tenth in/on/with ten to/for month to come (in): come Nebuchadnezzar king Babylon he/she/it and all strength: soldiers his upon Jerusalem and to camp upon her and to build upon her siegework around
2 Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
and to come (in): besiege [the] city in/on/with siege till eleven ten year to/for king Zedekiah
3 Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
(in/on/with month [the] fourth *X*) in/on/with nine to/for month and to strengthen: strengthen [the] famine in/on/with city and not to be food to/for people [the] land: country/planet
4 Kisha ukuta wa mji ukavunjwa, na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
and to break up/open [the] city and all human [the] battle [the] night way: road gate between [the] wall which upon garden [the] king and Chaldea upon [the] city around and to go: went way: road [the] Arabah
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia mfalme na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
and to pursue strength: soldiers Chaldea after [the] king and to overtake [obj] him in/on/with plain Jericho and all strength: soldiers his to scatter from upon him
6 naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, mahali ambapo hukumu yake ilitangazwa.
and to capture [obj] [the] king and to ascend: establish [obj] him to(wards) king Babylon Riblah [to] and to speak: promise with him justice: judgement
7 Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Kisha wakayangʼoa macho yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
and [obj] son: child Zedekiah to slaughter to/for eye his and [obj] eye: appearance Zedekiah to blind and to bind him in/on/with bronze and to come (in): towards him Babylon
8 Mnamo siku ya saba ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, afisa wa mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
and in/on/with month [the] fifth in/on/with seven to/for month he/she/it year nine ten year to/for king Nebuchadnezzar king Babylon to come (in): come Nebuzaradan chief guard servant/slave king Babylon Jerusalem
9 Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
and to burn [obj] house: temple LORD and [obj] house: palace [the] king and [obj] all house: home Jerusalem and [obj] all house: home great: large to burn in/on/with fire
10 Jeshi lote la Wakaldayo, chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme, walivunja kuta zilizoizunguka Yerusalemu.
and [obj] wall Jerusalem around to tear all strength: soldiers Chaldea which chief guard
11 Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi akawapeleka uhamishoni watu waliokuwa wamebaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
and [obj] remainder [the] people [the] to remain in/on/with city and [obj] [the] to fall: deserting which to fall: deserting upon [the] king Babylon and [obj] remainder [the] crowd to reveal: remove Nebuzaradan chief guard
12 Lakini yule jemadari wa askari walinzi akawaacha baadhi ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
and from poor [the] land: country/planet to remain chief guard to/for to tend vineyards and to/for to till
13 Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba na kuipeleka Babeli.
and [obj] pillar [the] bronze which house: temple LORD and [obj] [the] base and [obj] sea [the] bronze which in/on/with house: temple LORD to break Chaldea and to lift: bear [obj] bronze their Babylon [to]
14 Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
and [obj] [the] pot and [obj] [the] shovel and [obj] [the] snuffer and [obj] [the] palm: dish and [obj] all article/utensil [the] bronze which to minister in/on/with them to take: take
15 Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua vile vyetezo na yale mabakuli ya kunyunyizia, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
and [obj] [the] censer and [obj] [the] bowl which gold gold and which silver: money silver: money to take: take chief guard
16 Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
[the] pillar two [the] sea [the] one and [the] base which to make Solomon to/for house: temple LORD not to be weight to/for bronze all [the] article/utensil [the] these
17 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane. Sehemu ya shaba juu ya nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tatu na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na wavu wake ilifanana na hiyo ya kwanza.
eight ten cubit height [the] pillar [the] one and capital upon him bronze and height [the] capital three (cubit *Q(K)*) and latticework and pomegranate upon [the] capital around [the] all bronze and like/as these to/for pillar [the] second upon [the] latticework
18 Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
and to take: take chief guard [obj] Seraiah priest [the] head: leader and [obj] Zephaniah priest second and [obj] three to keep: guard [the] threshold
19 Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri watano wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
and from [the] city to take: take eunuch one which he/she/it overseer upon human [the] battle and five human from to see: approach face [the] king which to find in/on/with city and [obj] [the] secretary ruler [the] army [the] to serve [obj] people [the] land: country/planet and sixty man from people [the] land: country/planet [the] to find in/on/with city
20 Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
and to take: take [obj] them Nebuzaradan chief guard and to go: take [obj] them upon king Babylon Riblah [to]
21 Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
and to smite [obj] them king Babylon and to die them in/on/with Riblah in/on/with land: country/planet Hamath and to reveal: remove Judah from upon land: soil his
22 Nebukadneza mfalme wa Babeli akamteua Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, awe msimamizi wa watu aliowaacha Yuda.
and [the] people [the] to remain in/on/with land: country/planet Judah which to remain Nebuchadnezzar king Babylon and to reckon: overseer upon them [obj] Gedaliah son: child Ahikam son: child Shaphan
23 Maafisa wote wa jeshi na watu wao waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemteua Gedalia kuwa mtawala, wakamjia Gedalia huko Mispa. Hawa walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofathi, na Yezania mwana wa Mmaaka, pamoja na watu wao.
and to hear: hear all ruler [the] strength: soldiers they(masc.) and [the] human for to reckon: overseer king Babylon [obj] Gedaliah and to come (in): come to(wards) Gedaliah [the] Mizpah and Ishmael son: child Nethaniah and Johanan son: child Kareah and Seraiah son: child Tanhumeth [the] Netophathite and Jezaniah son: child [the] Maacathite they(masc.) and human their
24 Gedalia akaapa ili kuwatia moyo wao na watu wao. Akasema, “Msiwaogope maafisa wa Kikaldayo. Kaeni katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vyema kwenu.”
and to swear to/for them Gedaliah and to/for human their and to say to/for them not to fear from servant/slave [the] Chaldea to dwell in/on/with land: country/planet and to serve [obj] king Babylon and be good to/for you
25 Hata hivyo, katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi, nao wakamuua Gedalia, na pia watu wa Yuda, pamoja na Wakaldayo waliokuwa naye huko Mispa.
and to be in/on/with month [the] seventh to come (in): come Ishmael son: child Nethaniah son: child Elishama from seed: children [the] kingship and ten human with him and to smite [obj] Gedaliah and to die and [obj] [the] Jew and [obj] [the] Chaldea which to be with him in/on/with Mizpah
26 Baada ya haya, watu wote kuanzia aliye mdogo sana hadi aliye mkubwa kabisa, pamoja na maafisa wa jeshi, wakakimbilia Misri kwa kuwaogopa Wakaldayo.
and to arise: rise all [the] people from small and till great: large and ruler [the] strength: soldiers and to come (in): come Egypt for to fear from face of Chaldea
27 Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini kutoka gerezani siku ya ishirini na saba ya mwezi wa kumi na mbili.
and to be in/on/with thirty and seven year to/for captivity Jehoiachin king Judah in/on/with two ten month in/on/with twenty and seven to/for month to lift: kindness Evil-merodach Evil-merodach king Babylon in/on/with year to reign he [obj] head: leader Jehoiachin king Judah from house: home prison
28 Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
and to speak: speak with him welfare and to give: give [obj] throne his from upon throne [the] king which with him in/on/with Babylon
29 Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
and to change [obj] garment prison his and to eat food continually to/for face: before his all day life his
30 Siku kwa siku mfalme alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake.
and ration his ration continually to give: give to/for him from with [the] king word: portion day: daily in/on/with day: daily his all day life his

< 2 Wafalme 25 >