< 2 Wafalme 25 >

1 Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli, akiwa na jeshi lake lote, alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Akapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
Hahoi a bawinae kum 6 nae thapa yung 10, hnin 10 hnin vah hettelah ao. Babilon siangpahrang Nebukhadnezar hoi a ransanaw pueng hoi Jerusalem taranlahoi a tho awh teh a roe sin awh. A tengpam abuemlah tarantuknae tangkom koung a tai awh.
2 Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
Hottelah siangpahrang Zedekiah a bawinae kum 11 totouh kho teh a kalup awh.
3 Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
Thapa yung 4 nah hnin 9 hnin vah ram thung e taminaw hanelah rawca laipalah ka patawpoung e takang a tho.
4 Kisha ukuta wa mji ukavunjwa, na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
Hahoi khopui kalupnae tapang hah vak a muk awh teh, karum lah tarankatuknaw teh siangpahrang takha teng e kalupnae tapang kahni touh e rahak kalupnae longkha koe lah a yawng awh. Khaldean taminaw ni kho hah king a ring awh teh siangpahrang teh tanghling lam koe lah a cei.
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia mfalme na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
Hatei teh, Khaldean ransanaw ni siangpahrang hah pâlei awh teh, Jeriko tanghling dawk a pha awh, a ransanaw pueng ni dung a yawng takhai awh.
6 naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, mahali ambapo hukumu yake ilitangazwa.
Siangpahrang hah a man awh teh Riblah vah Babilon siangpahrang koe a hrawi awh teh lawk a ceng awh.
7 Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Kisha wakayangʼoa macho yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
Zedekiah e capa hah a mithmu vah a thei awh. Zedekiah e a mitmu hah a cawngkhawi awh teh, king a katek nalaihoi Babilon vah a hrawi awh.
8 Mnamo siku ya saba ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, afisa wa mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
Hottelah Babilon siangpahrang Nebukhadnezar a bawinae kum 9, thapa yung 5, hnin 7 hnin vah Babilon siangpahrang karingkungnaw kahrawikung, Nebuzaradan teh Jerusalem vah a kâen.
9 Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
BAWIPA im hoi siangpahrang im hah hmai a sawi awh teh Jerusalem imnaw pueng im kalennaw pueng hah hmai koung a sawi awh.
10 Jeshi lote la Wakaldayo, chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme, walivunja kuta zilizoizunguka Yerusalemu.
Karingnaw kahrawikungnaw koe kaawm e Khaldean ransanaw pueng ni Jerusalem rapannaw pueng hah a raphoe awh.
11 Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi akawapeleka uhamishoni watu waliokuwa wamebaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
Khopui thung kaawm rae naw pueng hoi, Babilon siangpahrang koe lah kaawm e taminaw pueng hoi, karingkungnaw kahrawikung Nebuzaradan ni san lah a hrawi awh.
12 Lakini yule jemadari wa askari walinzi akawaacha baadhi ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
Hote ram dawk e karoedengnaw, banghai cungkeihoehe naw karingkungnaw kahrawikung ni takhakatawkkungnaw hoi law kaphawnaw lah a ta awh.
13 Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba na kuipeleka Babeli.
Bawipa im dawk e rahum khompui hoi, rahum e tui im, tui kamhluknae naw hah Khaldean taminaw ni rakrak a hem awh teh rahum naw hah Babilon vah a sin awh.
14 Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
Hlaam hoi hraba kawnnae, hmaiim, paitei, pacen hoi, rahum ailo, tongben pueng, thawngnae hnopai pueng koung a la awh.
15 Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua vile vyetezo na yale mabakuli ya kunyunyizia, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
Tongben hoi, hlaam, sui hoi ngun hoi sak e hnopainaw pueng karingkungnaw kahrawikung ni koung a la pouh.
16 Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
Solomon ni BAWIPA im hanelah a sak e khom kahni touh hoi rahum tuiim hoi rahum pâhungnae amkhoung, rahum a ri e teh panue thai hanelah awm hoeh.
17 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane. Sehemu ya shaba juu ya nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tatu na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na wavu wake ilifanana na hiyo ya kwanza.
Khom ka rasang poung e teh dong 18 touh a pha teh, a som vah rahum khom pasum e ao. Hate rahum khom pasum e teh dong 3 touh a rasang, rahum khom pasum e dawk rahum em hoi, rahumnaw hoi akawi. Alouke khomnaw hai hottelah ao teh, rahum emnaw hoi akawi.
18 Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
Karingkungnaw kahrawikung ni vaihma bawi Seraiah hoi vaihma Zephaniah hoi tho ka ring e kathum touh a man.
19 Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri watano wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
Taran ka tuk e ransabawi buet touh hoi siangpahrang ouk a kâhmonae khopui dawk hmu e 5 touh hoi cakathutkung hoi khopui thung hmu e naw hah ram thung e 60 touh hoi khopui thung hoi a man awh.
20 Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
Karingkungnaw kahrawikung Nebuzaradan ni Riblah hoi Babilon siangpahrang koevah a ceikhai.
21 Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
Babilon siangpahrang ni Hamath ram e Riblah vah a thei awh. Hahoi teh, Judahnaw teh a ram dawk hoi san lah a hrawi awh.
22 Nebukadneza mfalme wa Babeli akamteua Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, awe msimamizi wa watu aliowaacha Yuda.
Hahoi Babilon siangpahrang Nebukhadnezar ni, Judah ram a ta e tami thung dawk Shaphan capa, Ahikam capa Gadaliah hah bawi lah a ta awh.
23 Maafisa wote wa jeshi na watu wao waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemteua Gedalia kuwa mtawala, wakamjia Gedalia huko Mispa. Hawa walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofathi, na Yezania mwana wa Mmaaka, pamoja na watu wao.
Hahoi teh, ransa kahrawikungnaw pueng hoi a kut rahim e naw ni Babilon siangpahrang ni, Gadaliah teh bawi lah a sak toe tie a panue awh toteh, Mizpah vah Gadaliah koevah a cei awh. Hotnaw teh, Nathaniah capa Ishmael, Kareah capa Johanan, Netophah tami Tanhumeth capa Seraiah, Maakath capa Jaazaniah hoi a kut rahim e naw doeh.
24 Gedalia akaapa ili kuwatia moyo wao na watu wao. Akasema, “Msiwaogope maafisa wa Kikaldayo. Kaeni katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vyema kwenu.”
Gedaliah ni hote taminaw hoi a taminaw koevah, lawkkamnae a sak teh ahnimouh koe Khaldeannaw e san lah o hanelah taket hanh awh. Het ram dawk ma pou awm awh. Babilon siangpahrang kâ ngainae rahim vah awm awh nateh, namamouh hane kahawi han atipouh.
25 Hata hivyo, katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi, nao wakamuua Gedalia, na pia watu wa Yuda, pamoja na Wakaldayo waliokuwa naye huko Mispa.
Hatei thapa yung 7 nah, siangpahrang catoun Elishama capa Nathaniah capa Ishmael ni tami 10 touh a ceikhai teh, Gedaliah teh Mizpah e Judahnaw koe kaawm e Khaldean taminaw hoi a tuk awh teh be a thei awh.
26 Baada ya haya, watu wote kuanzia aliye mdogo sana hadi aliye mkubwa kabisa, pamoja na maafisa wa jeshi, wakakimbilia Misri kwa kuwaogopa Wakaldayo.
Hottelah taminaw pueng kalen, kathoung ransabawinaw hoi a tâco teh, Izip ram vah a cei awh. Bangkongtetpawiteh, Khaldean taminaw, a taki awh dawk doeh.
27 Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini kutoka gerezani siku ya ishirini na saba ya mwezi wa kumi na mbili.
Hahoi Jehoiakhin san lah a onae kum 37, thapa 12, hnin 27 nah Babilon siangpahrang, Evilmerodak ni a bawinae kum nah Judah siangpahrang Jehoiakhin teh, thongim thung hoi a hlout sak.
28 Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
Kahawicalah kho a pouk teh Babilon vah ahni koe kaawm e siangpahrangnaw hlak ka rasang poung e tungkhung a poe.
29 Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
Jehoiakhin teh, thongim a bonae khohna a kâthung teh a hringyung thung pueng siangpahrang hmalah a ca a nei.
30 Siku kwa siku mfalme alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake.
A hringyung thung hnintangkuem a ca hanelah siangpahrang ni a poe teh a coe sak.

< 2 Wafalme 25 >