< 2 Wafalme 24 >

1 Wakati wa utawala wa Yehoyakimu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliishambulia nchi, naye Yehoyakimu akawa mtumwa wake kwa miaka mitatu. Lakini hatimaye akabadili mawazo yake na kuasi dhidi ya Nebukadneza.
Uti hans tid drog NebucadNezar upp, Konungen i Babel, och Jojakim vardt honom underdånig i tre år. Och han vände sig om, och föll ifrå honom.
2 Bwana akatuma wavamiaji wa Wakaldayo, Waaramu, Wamoabu na Waamoni ili kumshambulia. Aliwatuma kuiangamiza Yuda sawasawa na neno la Bwana lililosemwa na watumishi wake manabii.
Och Herren lät komma öfver honom krigsfolk, utu Chaldeen, utu Syrien, utu Moab, och ifrån Ammons barn; och lät komma dem i Juda, att de skulle förderfva honom, efter Herrans ord, det han talat hade genom sina tjenare Propheterna.
3 Hakika mambo haya yalitokea Yuda kulingana na agizo la Bwana, ili kuwaondoa kutoka machoni pake kwa sababu ya dhambi za Manase na yote aliyoyafanya,
Men det skedde Juda alltså, efter Herrans ord, på det han skulle kasta dem ifrå sitt ansigte för Manasse synds skull, som han gjort hade;
4 ikiwa ni pamoja na kumwaga damu isiyo na hatia. Kwa kuwa aliijaza Yerusalemu kwa damu isiyo na hatia, naye Bwana hakuwa radhi kusamehe.
Och för det oskyldiga blods skull, som han utgöt, och gjorde Jerusalem fullt med oskyldigt blod; och derföre ville Herren icke förlåtat.
5 Matukio mengine ya utawala wa Yehoyakimu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Hvad nu mer af Jojakim sägandes är, och allt det han gjort hafver, si, det är skrifvet uti Juda Konungars Chrönico.
6 Yehoyakimu akalala pamoja na baba zake. Naye Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.
Och Jojakim afsomnade med sina fäder, och hans son Jojachin vardt Konung i hans stad.
7 Mfalme wa Misri hakutoka tena katika nchi yake, kwa sababu mfalme wa Babeli alikuwa ameitwaa himaya yake yote, kuanzia Kijito cha Misri hadi Mto Frati.
Och Konungen i Egypten drog icke mer utu sitt land; förty Konungen i Babel hade honom borttagit allt det som Konungens i Egypten var, ifrån Egypti bäck allt intill den älfven Phrath.
8 Yehoyakini alikuwa na miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani kutoka Yerusalemu.
Aderton åra gammal var Jojachin, då han Konung vardt, och regerade tre månader i Jerusalem; hans moder het Nehustha, Elnathans dotter af Jerusalem.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
Och han gjorde det ondt var för Herranom, såsom hans fader gjort hade.
10 Wakati huo, maafisa wa Nebukadneza mfalme wa Babeli walikuja ili kuishambulia Yerusalemu, nao wakaizunguka kwa jeshi.
På den tiden drogo NebucadNezars Konungens tjenare i Babel upp till Jerusalem, och kringlade staden med bålverk.
11 Nebukadneza mwenyewe akaupandia mji wakati maafisa wake walipokuwa wameuzunguka kwa jeshi.
Och då NebucadNezar kom till staden med sina tjenare, belade han honom.
12 Yehoyakini mfalme wa Yuda, mama yake, wahudumu wake, wakuu na maafisa wake wote wakajisalimisha kwa Nebukadneza. Katika mwaka wa nane wa utawala wa mfalme wa Babeli, akamchukua Yehoyakini kuwa mfungwa.
Men Jojachin, Juda Konung, gick ut till Konungen af Babel med sine moder, med sina tjenare, med sina öfverstar och kamererare. Och Konungen af Babel anammade honom i lians rikes åttonde åre;
13 Kama vile Bwana alivyokuwa amesema, Nebukadneza akaondoa hazina yote kutoka Hekalu la Bwana na kutoka jumba la mfalme, akavichukua vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amevitengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana.
Och tog ut dädan alla håfvor uti Herrans hus, och i Konungshuset; och slog sönder all gyldene kärile, som Salomo, Israels Konung, gjort hade uti Herrans tempel, såsom Herren sagt hade;
14 Akawachukua watu wa Yerusalemu wote kwenda uhamishoni: yaani maafisa wote na mashujaa, watu wenye ustadi na ufundi, jumla yao watu elfu kumi. Watu maskini sana ndio tu waliobaki katika nchi.
Och förde bort hela Jerusalem, alla öfverstar, alla väldiga, tiotusend fångar, och alla timbermän, och alla smeder, och lät intet qvart blifva, utan det ringesta folket i landena;
15 Nebukadneza akamchukua mateka Yehoyakini hadi Babeli. Pia akawachukua utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli mama yake mfalme, wake zake, maafisa wake, na viongozi wote wa nchi.
Och förde bort Jojachin till Babel, Konungens moder, Konungens hustrur, och hans kamererare; desslikes de myndiga i landena förde han ock fångna bort ifrå Jerusalem till Babel;
16 Mfalme wa Babeli pia akawahamishia Babeli mashujaa elfu saba, wenye nguvu na wanaofaa kupigana vita, na watu wenye ustadi na mafundi elfu moja.
Och hvad bästa folket var, sjutusend, och de timbermän och smeder, tusende, alle starke krigsmän. Och Konungen af Babel förde dem till Babel.
17 Akamfanya Matania, ndugu wa baba yake Yehoyakini, kuwa mfalme mahali pake, na akalibadilisha jina lake kuwa Sedekia.
Och Konungen af Babel gjorde Matthania, hans faderbroder, till Konung i hans stad, och förvände hans namn Zedekia.
18 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
Ett och tjugu år gammal var Zedekia, då han vardt Konung, och regerade ellofva år i Jerusalem; hans moder het Hamital, Jeremia dotter af Libna.
19 Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
Och han gjorde det ondt var för Herranom, såsom Jojakim gjort hade.
20 Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.
Ty det skedde alltså med Jerusalem och Juda utaf Herrans vrede, tilldess han kastade dem bort ifrå sitt ansigte. Och Zedekia vardt affällig ifrå Konungenom i Babel.

< 2 Wafalme 24 >