< 2 Wafalme 24 >

1 Wakati wa utawala wa Yehoyakimu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliishambulia nchi, naye Yehoyakimu akawa mtumwa wake kwa miaka mitatu. Lakini hatimaye akabadili mawazo yake na kuasi dhidi ya Nebukadneza.
در دورهٔ سلطنت یهویاقیم، نِبوکَدنِصَّر، پادشاه بابِل به اورشلیم حمله کرد. یهویاقیم تسلیم شد و سه سال به او باج و خراج پرداخت، اما بعد از آن، سر از فرمان وی پیچید و شورش نمود.
2 Bwana akatuma wavamiaji wa Wakaldayo, Waaramu, Wamoabu na Waamoni ili kumshambulia. Aliwatuma kuiangamiza Yuda sawasawa na neno la Bwana lililosemwa na watumishi wake manabii.
خداوند لشکر بابِلی، سوری، موآبی و عمونی را فرستاد تا همان‌طور که به‌وسیلۀ انبیا خبر داده بود، یهودا را نابود کنند.
3 Hakika mambo haya yalitokea Yuda kulingana na agizo la Bwana, ili kuwaondoa kutoka machoni pake kwa sababu ya dhambi za Manase na yote aliyoyafanya,
بدون شک این بلاها به فرمان خداوند بر یهودا نازل شد. خداوند تصمیم داشت یهودا را به سبب گناهان بی‌شمار مَنَسی طرد کند،
4 ikiwa ni pamoja na kumwaga damu isiyo na hatia. Kwa kuwa aliijaza Yerusalemu kwa damu isiyo na hatia, naye Bwana hakuwa radhi kusamehe.
زیرا مَنَسی اورشلیم را از خون بی‌گناهان پر کرده بود و خداوند نخواست این گناهان را ببخشد.
5 Matukio mengine ya utawala wa Yehoyakimu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
شرح بقیهٔ رویدادهای دوران سلطنت یهویاقیم و کارهای او در کتاب تاریخ پادشاهان یهودا نوشته شده است.
6 Yehoyakimu akalala pamoja na baba zake. Naye Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.
پس از مرگ یهویاقیم پسرش یهویاکین به جای او بر تخت سلطنت نشست.
7 Mfalme wa Misri hakutoka tena katika nchi yake, kwa sababu mfalme wa Babeli alikuwa ameitwaa himaya yake yote, kuanzia Kijito cha Misri hadi Mto Frati.
(پادشاه مصر دیگر از مرزهای خود خارج نشد، زیرا پادشاه بابِل تمام متصرفات مصر را که شامل یهودا هم می‌شد، از نهر مصر تا رود فرات، اشغال نمود.)
8 Yehoyakini alikuwa na miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani kutoka Yerusalemu.
یهویاکین هجده ساله بود که پادشاه یهودا شد و سه ماه در اورشلیم سلطنت کرد. (مادرش نحوشطا، دختر الناتان و از اهالی اورشلیم بود.)
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
یهویاکین مانند پدرش نسبت به خداوند گناه ورزید.
10 Wakati huo, maafisa wa Nebukadneza mfalme wa Babeli walikuja ili kuishambulia Yerusalemu, nao wakaizunguka kwa jeshi.
در دورهٔ سلطنت یهویاکین، لشکر نِبوکَدنِصَّر، پادشاه بابِل، اورشلیم را محاصره کرد.
11 Nebukadneza mwenyewe akaupandia mji wakati maafisa wake walipokuwa wameuzunguka kwa jeshi.
وقتی شهر در محاصره بود، خود نِبوکَدنِصَّر هم به آنجا رسید.
12 Yehoyakini mfalme wa Yuda, mama yake, wahudumu wake, wakuu na maafisa wake wote wakajisalimisha kwa Nebukadneza. Katika mwaka wa nane wa utawala wa mfalme wa Babeli, akamchukua Yehoyakini kuwa mfungwa.
یهویاکین و تمام مقامات و فرماندهان و خدمتگزاران دربارش و ملکهٔ مادر تسلیم نِبوکَدنِصَّر شدند. پادشاه بابِل در سال هشتم سلطنت خود، یهویاکین را زندانی کرد.
13 Kama vile Bwana alivyokuwa amesema, Nebukadneza akaondoa hazina yote kutoka Hekalu la Bwana na kutoka jumba la mfalme, akavichukua vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amevitengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana.
طبق آنچه خداوند فرموده بود، بابِلی‌ها تمام اشیاء قیمتی خانهٔ خداوند، جواهرات کاخ سلطنتی و تمام ظروف طلا را که سلیمان پادشاه برای خانهٔ خداوند ساخته بود، در هم شکستند.
14 Akawachukua watu wa Yerusalemu wote kwenda uhamishoni: yaani maafisa wote na mashujaa, watu wenye ustadi na ufundi, jumla yao watu elfu kumi. Watu maskini sana ndio tu waliobaki katika nchi.
نِبوکَدنِصَّر اهالی اورشلیم را که شامل فرماندهان و سربازان، صنعتگران و آهنگران می‌شدند و تعدادشان به ده هزار نفر می‌رسید به بابِل تبعید کرد، و فقط افراد فقیر را در آن سرزمین باقی گذاشت.
15 Nebukadneza akamchukua mateka Yehoyakini hadi Babeli. Pia akawachukua utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli mama yake mfalme, wake zake, maafisa wake, na viongozi wote wa nchi.
نِبوکَدنِصَّر، یهویاکین را با مادر و زنان او، فرماندهان و مقامات مملکتی به بابِل برد.
16 Mfalme wa Babeli pia akawahamishia Babeli mashujaa elfu saba, wenye nguvu na wanaofaa kupigana vita, na watu wenye ustadi na mafundi elfu moja.
همچنین تمام سربازان جنگ آزموده را که هفت هزار نفر بودند و هزار صنعتگر و آهنگر را اسیر کرده، به بابِل برد.
17 Akamfanya Matania, ndugu wa baba yake Yehoyakini, kuwa mfalme mahali pake, na akalibadilisha jina lake kuwa Sedekia.
بعد پادشاه بابِل متنیا عموی یهویاکین را به جای او به پادشاهی تعیین نمود و نامش را به صدقیا تغییر داد.
18 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
صدقیا بیست و یک ساله بود که پادشاه یهودا شد و یازده سال در اورشلیم سلطنت نمود. (مادرش حموطل، دختر ارمیا و از اهالی لبنه بود.)
19 Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
او مانند یهویاقیم نسبت به خداوند گناه ورزید.
20 Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.
خشم خداوند بر مردم اورشلیم و یهودا افروخته شد و او ایشان را طرد نمود.

< 2 Wafalme 24 >