< 2 Wafalme 24 >
1 Wakati wa utawala wa Yehoyakimu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliishambulia nchi, naye Yehoyakimu akawa mtumwa wake kwa miaka mitatu. Lakini hatimaye akabadili mawazo yake na kuasi dhidi ya Nebukadneza.
Ahnie se navah Babilon siangpahrang Nebukhadnezar ni a muk. Hatdawkvah Jehoiakim teh san lah kum thum touh a toung. Hathnukkhu, bout a kamlang teh Nebukhadnezar a tuk.
2 Bwana akatuma wavamiaji wa Wakaldayo, Waaramu, Wamoabu na Waamoni ili kumshambulia. Aliwatuma kuiangamiza Yuda sawasawa na neno la Bwana lililosemwa na watumishi wake manabii.
BAWIPA ni a san profetnaw hno lahoi a dei tangcoung e patetlah BAWIPA ni Khaldean tamihu, Siria tamihu, Moab tamihu hoi Ammon tamihu naw hah Judahnaw tuk hane hoi raphoe hanelah a patoun.
3 Hakika mambo haya yalitokea Yuda kulingana na agizo la Bwana, ili kuwaondoa kutoka machoni pake kwa sababu ya dhambi za Manase na yote aliyoyafanya,
Manasseh ni a sak e pueng, tamikayon hoeh e naw a thi palawng e hoi, kayonhoehnaw e thi paling hoi Jerusalem akawi sak dawkvah, BAWIPA ni ngaithoum hane ngai hoeh.
4 ikiwa ni pamoja na kumwaga damu isiyo na hatia. Kwa kuwa aliijaza Yerusalemu kwa damu isiyo na hatia, naye Bwana hakuwa radhi kusamehe.
Judahnaw a hmaitung hoi takhoe hanelah BAWIPA e kâpoelawk teh a pha katang.
5 Matukio mengine ya utawala wa Yehoyakimu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Hottelah Jehoiakim tawksaknae thung hoi kacawiraenaw hoi a kâroenae naw pueng teh Judah siangpahrangnaw e setouknae cauk dawk thut lah ao nahoehmaw.
6 Yehoyakimu akalala pamoja na baba zake. Naye Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.
Jehoiakim teh mintoenaw koe a kâhat teh a capa Jehoiakhin ni a yueng lah a uk.
7 Mfalme wa Misri hakutoka tena katika nchi yake, kwa sababu mfalme wa Babeli alikuwa ameitwaa himaya yake yote, kuanzia Kijito cha Misri hadi Mto Frati.
Izip siangpahrang teh a ram thung hoi tho hoeh toe. Bangkongtetpawiteh, Babilon siangpahrang ni Izip palangnaw koehoi a kamtawng teh Euphrates palang totouh Izip siangpahrang uknae pueng hah koung a la toe.
8 Yehoyakini alikuwa na miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani kutoka Yerusalemu.
Jehoiakhin siangpahrang thaw tawk a kamtawng nah a kum 18 touh a pha. Jerusalem vah thapa yung thum touh a bawi. A manu e min teh Nehushta, Jerusalem kho e Elnathan canu doeh.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
A na pa ni a sak e patetlah BAWIPA mithmu vah thoenae a sak.
10 Wakati huo, maafisa wa Nebukadneza mfalme wa Babeli walikuja ili kuishambulia Yerusalemu, nao wakaizunguka kwa jeshi.
Hatdawkvah Babilon siangpahrang Nebukhadnezar e taminaw Jerusalem lah a ceitakhang awh teh, kho king a kalup awh.
11 Nebukadneza mwenyewe akaupandia mji wakati maafisa wake walipokuwa wameuzunguka kwa jeshi.
Hahoi Babilon siangpahrang Nebukhadnezar khopui dawk a tho navah a sannaw ni khopui teh koung la a kalup awh toe.
12 Yehoyakini mfalme wa Yuda, mama yake, wahudumu wake, wakuu na maafisa wake wote wakajisalimisha kwa Nebukadneza. Katika mwaka wa nane wa utawala wa mfalme wa Babeli, akamchukua Yehoyakini kuwa mfungwa.
Judah siangpahrang Jehoiakhin ni a manu, a sannaw, ukkungnaw hoi a sannaw hoi Babilon siangpahrang koe a tâco awh. Hatdawkvah a bawinae kum 8 nah Babilon siangpahrang ni a man.
13 Kama vile Bwana alivyokuwa amesema, Nebukadneza akaondoa hazina yote kutoka Hekalu la Bwana na kutoka jumba la mfalme, akavichukua vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amevitengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana.
BAWIPA ni a dei tangcoung e patetlah BAWIPA e im dawk e hno hoi siangpahrang im dawk e hnonaw pueng koung a la teh, BAWIPA e bawkim dawk hanelah Isarel siangpahrang Solomon ni a sak e sui hnopai pueng reprep koung a dei pouh.
14 Akawachukua watu wa Yerusalemu wote kwenda uhamishoni: yaani maafisa wote na mashujaa, watu wenye ustadi na ufundi, jumla yao watu elfu kumi. Watu maskini sana ndio tu waliobaki katika nchi.
Jerusalem e tami pueng ka lentoe e taminaw hoi a thakaawme taminaw 10, 000 touh, hnikawng kathoumnaw hoi sumdêikathoumnaw pueng koung a hrawi. Hahoi ram thung e ka roedeng e tami hoi cungkeihoehe tami laipateh pihai cettakhai awh hoeh.
15 Nebukadneza akamchukua mateka Yehoyakini hadi Babeli. Pia akawachukua utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli mama yake mfalme, wake zake, maafisa wake, na viongozi wote wa nchi.
Jehoiakhin e a sannaw hoi hote ram dawk e tami thakaawme taminaw Jerusalem hoi Babilon lah santoung hanlah a ceikhai awh.
16 Mfalme wa Babeli pia akawahamishia Babeli mashujaa elfu saba, wenye nguvu na wanaofaa kupigana vita, na watu wenye ustadi na mafundi elfu moja.
Babilon siangpahrang ni thakasai e tami 7, 000 hni kawng kathoum e hoi sumdêikathoum e tami 1, 000 touh hoi tarantuk kathoumnaw Babilon lah koung a ceikhai.
17 Akamfanya Matania, ndugu wa baba yake Yehoyakini, kuwa mfalme mahali pake, na akalibadilisha jina lake kuwa Sedekia.
Babilon siangpahrang ni Jehoiakhin yueng lah, a panga Mattaniah hah siangpahrang thaw a tawk sak awh teh Zedekiah telah a min a palang pouh awh.
18 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
Zedekiah siangpahrang a tawk navah kum 21 touh a pha. Jerusalem vah kum 11 touh a bawi. A manu e min teh Hamutal, Libnah kho e Jeremiah canu doeh.
19 Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
Jehoiakhin ni a sak e hno pueng a sak teh BAWIPA mithmu vah thoenae a sak.
20 Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.
Judahnaw hoi Jerusalem e taminaw e hmaitung hoi a takhoe hoehroukrak BAWIPA teh a lungkhuek. Hahoi Zedekiah ni Babilon siangpahrang a tuk.