< 2 Wafalme 23 >
1 Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
Kral Yoşiya haber gönderip Yahuda ve Yeruşalim'in bütün ileri gelenlerini yanına topladı.
2 Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na manabii, watu wote wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
Sonra Yahudalılar, Yeruşalim'de yaşayanlar, kâhinler, peygamberler, büyük küçük herkesle birlikte RAB'bin Tapınağı'na çıktı. RAB'bin Tapınağı'nda bulunmuş olan Antlaşma Kitabı'nı baştan sona kadar herkesin duyacağı biçimde okudu.
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo, na kufanya upya agano mbele za Bwana: yaani kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, hivyo kuyathibitisha maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Kisha watu wote wakajifunga wenyewe kwa kiapo katika agano.
Sütunun yanında durarak RAB'bin yolunu izleyeceğine, buyruklarını, öğütlerini, kurallarını candan ve yürekten uygulayacağına, bu kitapta yazılı antlaşmanın koşullarını yerine getireceğine ilişkin RAB'bin huzurunda antlaşma yaptı. Bütün halk bu antlaşmayı onayladı.
4 Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani mkuu, makuhani waliomfuata kwa cheo, na mabawabu kuondoa kutoka kwenye Hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali na Ashera na jeshi lote la mianga ya angani! Akavichoma nje ya Yerusalemu katika mashamba ya Bonde la Kidroni, na kuyachukua hayo majivu mpaka Betheli.
Kral Yoşiya Baal, Aşera ve gök cisimleri için yapılmış olan bütün eşyaları RAB'bin Tapınağı'ndan çıkarmak üzere Başkâhin Hilkiya'ya, kâhin yardımcılarına ve kapı nöbetçilerine buyruk verdi. Bunları Yeruşalim'in dışına çıkarıp Kidron Vadisi'nde yaktı, küllerini Beytel'e götürdü.
5 Akawafukuza makuhani wa kipagani waliokuwa wameteuliwa na wafalme wa Yuda kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Yuda na ile iliyozunguka Yerusalemu, yaani wale waliofukiza uvumba kwa Baali, kwa jua na mwezi, kwa makundi ya nyota, na jeshi lote la angani.
Yahuda krallarının kentlerde ve Yeruşalim'in çevresindeki tapınma yerlerinde buhur yaksınlar diye atamış olduğu putperest kâhinleri, Baal'a, güneşe, aya, takımyıldızlara –bütün gök cisimlerine– buhur yakanları ortadan kaldırdı.
6 Akaiondoa nguzo ya Ashera kutoka kwenye Hekalu la Bwana, na kuipeleka kwenye Bonde la Kidroni nje ya Yerusalemu, akaiteketeza huko. Akaisaga hadi ikawa unga na kusambaza hilo vumbi juu ya makaburi ya watu wa kawaida.
Aşera putunu RAB'bin Tapınağı'ndan çıkarıp Yeruşalim'in dışında Kidron Vadisi'nde yaktı, ezip toza çevirdi. Bu tozu sıradan halkın mezarlarına serpti.
7 Akabomoa pia nyumba za mahanithi wa mahali pa ibada za miungu, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana na mahali wanawake walipofuma kwa ajili ya Ashera.
Fuhuş yapan kadın ve erkeklerin RAB'bin Tapınağı alanındaki odalarını yıktı. Kadınlar orada Aşera için kumaş dokurlardı.
8 Yosia akawaleta makuhani wote wa Bwana kutoka miji yote ya Yuda, na kunajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, kuanzia Geba hadi Beer-Sheba, mahali pote ambapo hao makuhani wa miungu walifukiza uvumba. Akabomoa mahali pa kuwekea vitu vya ibada za miungu palipokuwa katika malango, kwenye ingilio la Lango la Yoshua, mtawala wa mji, lililoko upande wa kushoto wa lango la mji.
Yoşiya Yahuda kentlerinden bütün kâhinleri getirtti. Geva'dan Beer-Şeva'ya kadar kâhinlerin buhur yaktıkları tapınma yerlerini kirletti. Adını kent yöneticisinden alan Yeşu Kapısı'nın girişinde, kentin ana kapısının solunda kalan kapılardaki tapınma yerlerini de yıktı.
9 Ingawa makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu hawakuhudumu katika madhabahu ya Bwana katika Yerusalemu, walikula mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
Tapınma yerlerinin kâhinleri, Yeruşalim'deki RAB'bin sunağına çıkmaz, ancak öbür kâhinlerle birlikte mayasız ekmek yerlerdi.
10 Kisha mfalme akanajisi Tofethi, palipokuwa katika Bonde la Ben-Hinomu, ili mtu yeyote asiweze kupatumia kumtoa kafara mwanawe au binti yake katika moto kwa mungu Moleki.
Yoşiya, kimse oğlunu ya da kızını ilah Molek için ateşte kurban etmesin diye, Ben-Hinnom Vadisi'ndeki Tofet'i kirletti.
11 Akaondoa kutoka kwenye ingilio la Hekalu la Bwana wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye ua karibu na chumba cha afisa aliyeitwa Nathan-Meleki. Basi Yosia akayachoma moto yale magari yaliyokuwa yamewekwa wakfu kwa jua.
Yahuda krallarının güneşe adamış olduğu atları RAB'bin Tapınağı'nın girişinden kaldırdı. Atlar tapınağın avlusunda, hadım Natan-Melek'in odasının yanındaydı. Yoşiya güneşe adanmış savaş arabalarını da ateşe verdi.
12 Alizivunja madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walikuwa wamezijenga kwenye paa la ghorofa ya Ahazi, pia madhabahu alizokuwa amezijenga Manase katika nyua mbili za Hekalu la Bwana. Akaziondoa huko, akazivunja vipande vipande, na kutupa hicho kifusi katika Bonde la Kidroni.
Ahaz'ın yukarı odasının damında Yahuda krallarının yaptırdığı sunakları da, RAB'bin Tapınağı'nın iki avlusunda Manaşşe'nin yaptırdığı sunakları da yıktı; onları kırıp parçalayarak tozlarını Kidron Vadisi'ne saçtı.
13 Mfalme pia akanajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, palipokuwa mashariki ya Yerusalemu upande wa kusini wa Kilima cha Uharibifu, pale ambapo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amejenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu mke chukizo la Wasidoni, kwa ajili ya Kemoshi mungu chukizo la Wamoabu, na kwa ajili ya Moleki mungu chukizo la watu wa Amoni.
Yeruşalim'in doğusunda, Yıkım Dağı'nın güneyinde İsrail Kralı Süleyman'ın Saydalılar'ın iğrenç putu Aştoret, Moavlılar'ın iğrenç putu Kemoş ve Ammonlular'ın iğrenç putu Molek için yaptırmış olduğu tapınma yerlerini kirletti.
14 Yosia akapasua yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Ashera. Kisha akafunika hayo maeneo kwa mifupa ya wanadamu.
Dikili taşları, Aşera putlarını parçaladı; yerlerini insan kemikleriyle doldurdu.
15 Hata madhabahu yaliyokuwa huko Betheli, mahali pa juu pa kuabudia miungu palipokuwa pamejengwa na Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwafanya Israeli watende dhambi, alibomoa hata hayo madhabahu na mahali pa juu pa kuabudia miungu. Alipateketeza kwa moto hapo mahali pa juu pa kuabudia miungu na kupasaga hadi pakawa vumbi, na kuichoma hiyo nguzo ya Ashera pia.
Bundan başka İsrail'i günaha sürükleyen Nevat oğlu Yarovam'ın yaptırdığı Beytel'deki tapınma yerini ve sunağı bile yıktı. Tapınma yerini ateşe verip toz duman etti. Aşera putunu yaktı.
16 Kisha Yosia akatazama huku na huko, naye alipoona makaburi yaliyokuwa huko kwenye kilima, akaamuru mifupa itolewe humo na akaichoma juu ya madhabahu ya Betheli ili kupanajisi. Hili lilitokea kulingana na neno la Bwana lililosemwa na mtu wa Mungu ambaye alitangulia kusema mambo haya.
Yoşiya çevresine bakındı. Tepedeki mezarları görünce, adamlarını gönderip mezarlardaki kemikleri çıkarttı. Olacakları önceden bildiren Tanrı adamının açıkladığı RAB'bin sözü uyarınca, kemikleri sunağın üzerinde yakarak sunağı kirletti.
17 Mfalme akauliza, “Lile kaburi lenye mnara wa ukumbusho ninaloliona ni kwa ajili gani?” Watu wa mji wakasema, “Hii ni alama ya kaburi la mtu wa Mungu aliyekuja kutoka Yuda, naye akanena dhidi ya hii madhabahu ya Betheli mambo yale yale uliyoifanyia leo.”
Kral, “Orada görünen anıt nedir?” diye sordu. Kent halkı, “Orası Yahuda'dan gelen ve senin Beytel'deki sunağa yaptıklarını bildiren Tanrı adamının mezarıdır” diye yanıtladı.
18 Akasema, “Liacheni, msiliguse. Msimruhusu mtu yeyote kuiondoa mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na ile ya yule nabii ambaye alikuwa amekuja kutoka Samaria.
Kral, “Ona dokunmayın” dedi, “Kimse onun kemiklerini rahatsız etmesin.” Böylece Tanrı adamının kemiklerine de, Samiriye'den gelmiş olan peygamberin kemiklerine de dokunmadılar.
19 Kama alivyokuwa amefanya huko Betheli, Yosia akabomoa na kunajisi mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu ambapo wafalme wa Israeli walikuwa wamejenga ndani ya miji ya Samaria, ambayo ilikuwa imemghadhibisha Bwana.
Yoşiya Beytel'de yaptığı gibi, İsrail krallarının Samiriye kentlerinde yaptırdığı RAB'bi öfkelendiren tapınma yerlerindeki bütün yapıları ortadan kaldırdı.
20 Yosia akawachinja makuhani wote wa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika madhabahu zao wenyewe, na kuchoma mifupa ya wanadamu juu yake. Kisha akarudi Yerusalemu.
O kentlerdeki tapınma yerlerinin bütün kâhinlerini sunakların üzerinde kurban etti. Sunakların üzerinde insan kemikleri yaktıktan sonra Yeruşalim'e döndü.
21 Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Bwana Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
Kral, “Tanrınız RAB için Fısıh Bayramı'nı bu Antlaşma Kitabı'nda yazılanlara uygun biçimde kutlayın” diye halka buyruk verdi.
22 Hapakuwahi kuwepo na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za Waamuzi walioongoza Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
İsrail'e önderlik etmiş olan hâkimler döneminden bu yana, ne İsrail, ne de Yahuda kralları döneminde, böyle bir Fısıh Bayramı kutlanmamıştı.
23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Bwana huko Yerusalemu.
RAB için düzenlenen bu Fısıh Bayramı Kral Yoşiya'nın krallığının on sekizinci yılında Yeruşalim'de kutlandı.
24 Zaidi ya hayo, Yosia akawaondoa waaguzi, wanaoabudu mizimu, sanamu za kuagulia, sanamu za kuabudiwa, na vitu vingine vyote vya machukizo vilivyoonekana huko Yuda na Yerusalemu. Aliyafanya haya ili kutimiza matakwa ya sheria iliyoandikwa ndani ya kile kitabu ambacho Hilkia kuhani alikipata ndani ya Hekalu la Bwana.
Bundan başka Yoşiya, Kâhin Hilkiya'nın RAB'bin Tapınağı'nda bulduğu kitapta yazılı yasanın ilkelerini yerine getirmek amacıyla, cincileri, ruhçuları, aile putlarını, öteki putları, ayrıca Yahuda ve Yeruşalim'de görülen bütün iğrençlikleri silip süpürdü.
25 Kabla wala baada ya Mfalme Yosia hapakuwepo na mfalme mwingine yeyote ambaye alimpenda Bwana kwa moyo wake wote, kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na Sheria yote ya Mose.
Ne ondan önce, ne de sonra onun gibi candan ve yürekten var gücüyle RAB'be yönelen ve Musa'nın yasasına uyan bir kral çıktı.
26 Hata hivyo, Bwana hakuacha ghadhabu yake iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya yale yote ambayo Manase alikuwa amefanya kumghadhibisha.
Oysa Manaşşe işlediği suçlarla RAB'bi öyle öfkelendirmişti ki, RAB Yahuda'ya karşı alevlenen öfkesinden vazgeçmedi
27 Hivyo Bwana akasema, “Nitamwondoa Yuda mbele zangu kama nilivyomwondoa Israeli, nami nitaukataa Yerusalemu, mji niliouchagua, na Hekalu hili, ambalo nilisema, ‘Jina langu litakaa humo.’”
ve “İsrail'i nasıl huzurumdan attımsa, Yahuda'yı da öyle atacağım” dedi, “Seçtiğim bu kenti, Yeruşalim'i ve ‘Orada bulunacağım’ dediğim tapınağı kendimden uzaklaştıracağım.”
28 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Yoşiya'nın krallığı dönemindeki öteki olaylar ve bütün yaptıkları Yahuda krallarının tarihinde yazılıdır.
29 Yosia alipokuwa mfalme, Farao Neko mfalme wa Misri akapanda mpaka Mto Frati kumsaidia mfalme wa Ashuru. Mfalme Yosia akatoka kwenda kupigana naye, lakini Neko akamkabili na kumuua huko Megido.
Yoşiya'nın krallığı sırasında Mısır Firavunu Neko Asur Kralı'na yardım etmek üzere Fırat'a doğru yola çıktı. Kral Yoşiya da Neko'nun üzerine yürüdü. Megiddo'da karşılaştılar. Neko Yoşiya'yı öldürdü.
30 Watumishi wa Yosia wakauleta mwili wake katika gari la vita kutoka Megido hadi Yerusalemu, wakamzika kwenye kaburi lake mwenyewe. Nao watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta na kumfanya mfalme mahali pa baba yake.
Görevlileri Yoşiya'nın cesedini savaş arabasıyla Megiddo'dan Yeruşalim'e getirip mezarına gömdüler. Yahuda halkı Yoşiya'nın oğlu Yehoahaz'ı meshederek babasının yerine kral yaptı.
31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
Yehoahaz yirmi üç yaşında kral oldu ve Yeruşalim'de üç ay krallık yaptı. Annesi Livnalı Yeremya'nın kızı Hamutal'dı.
32 Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.
Yehoahaz ataları gibi RAB'bin gözünde kötü olanı yaptı.
33 Farao Neko akamfunga kwa minyororo huko Ribla katika nchi ya Hamathi ili asiweze kutawala huko Yerusalemu, naye akatoza kodi ya talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu katika Yuda.
Yeruşalim'de krallık yapmasın diye, Firavun Neko, Hama ülkesinde, Rivla'da Yehoahaz'ı zincire vurdu. Ülke halkını yüz talant gümüş ve bir talant altın ödemekle yükümlü kıldı.
34 Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa baba yake Yosia, na kulibadilisha jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafia huko.
Firavun Neko Yoşiya'nın oğlu Elyakim'i babasının yerine kral yaptı ve adını değiştirip Yehoyakim koydu. Sonra Yehoahaz'ı alıp Mısır'a döndü. Yehoahaz orada öldü.
35 Yehoyakimu akamlipa Farao Neko ile fedha na dhahabu aliyodai. Ili kuweza kufanya hivyo, Yehoyakimu akatoza nchi kodi na kulipiza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi kulingana na makadrio ya mapato yao.
Yehoyakim firavunun istediği altın ve gümüşü ödedi. Bu parayı bulmak için firavunun buyruğuna uyarak ülkeyi vergiye bağladı. Firavun Neko'ya verilmek üzere Yahuda halkından herkesin gücü oranında altın ve gümüş topladı.
36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Zebida binti Pedaya kutoka Ruma.
Yehoyakim yirmi beş yaşında kral oldu ve Yeruşalim'de on bir yıl krallık yaptı. Annesi Rumalı Pedaya'nın kızı Zevuda'ydı.
37 Naye akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyokuwa wamefanya.
Yehoyakim ataları gibi RAB'bin gözünde kötü olanı yaptı.