< 2 Wafalme 23 >
1 Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
Och Konungen sände bort, och till honom församlades alle de äldste i Juda och Jerusalem.
2 Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na manabii, watu wote wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
Och Konungen gick upp i Herrans hus, och hvar man af Juda, och alle Jerusalems inbyggare med honom, Prester och Propheter, och allt folket, både små och store; och man las för deras öron all förbundsens boks ord, hvilken i Herrans hus funnen var.
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo, na kufanya upya agano mbele za Bwana: yaani kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, hivyo kuyathibitisha maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Kisha watu wote wakajifunga wenyewe kwa kiapo katika agano.
Och Konungen gick in till en stod, och gjorde ett förbund för Herranom, att de skulle vandra efter Herranom, och hålla hans bud, vittnesbörd och rätter, af allt hjerta, och af allo själ, att de skulle upprätta detta förbunds ord, som skrifne stodo uti desso bok; och allt folket trädde uti förbundet.
4 Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani mkuu, makuhani waliomfuata kwa cheo, na mabawabu kuondoa kutoka kwenye Hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali na Ashera na jeshi lote la mianga ya angani! Akavichoma nje ya Yerusalemu katika mashamba ya Bonde la Kidroni, na kuyachukua hayo majivu mpaka Betheli.
Och Konungen böd öfversta Prestenom Hilkia, och Prestenom af det andra skiftet, och dörravaktaromen, att de skulle utkasta af Herrans tempel allahanda tyg, som till Baal och lunden, och all himmelens här gjordt var; och de brände det upp utanför Jerusalem i Kidrons dal, och stoftet deraf vardt buret till BethEl.
5 Akawafukuza makuhani wa kipagani waliokuwa wameteuliwa na wafalme wa Yuda kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Yuda na ile iliyozunguka Yerusalemu, yaani wale waliofukiza uvumba kwa Baali, kwa jua na mwezi, kwa makundi ya nyota, na jeshi lote la angani.
Och han afsatte de Camarim, hvilka Juda Konungar stiktat hade, till att röka på höjderna uti Juda städer, och omkring Jerusalem; desslikes Baals, solenes, månans, planeternas och all himmelens härs rökare;
6 Akaiondoa nguzo ya Ashera kutoka kwenye Hekalu la Bwana, na kuipeleka kwenye Bonde la Kidroni nje ya Yerusalemu, akaiteketeza huko. Akaisaga hadi ikawa unga na kusambaza hilo vumbi juu ya makaburi ya watu wa kawaida.
Och lät föra lunden utu Herrans hus, ut för Jerusalem, i Kidrons bäck; och brände honom upp i Kidrons bäck, och gjorde honom till stoft, och kastade stoftet uppå det meniga folks grifter.
7 Akabomoa pia nyumba za mahanithi wa mahali pa ibada za miungu, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana na mahali wanawake walipofuma kwa ajili ya Ashera.
Och han bröt bort de roffarehus, som voro vid Herrans hus, der qvinnor uti vofvo tapeter till lunden.
8 Yosia akawaleta makuhani wote wa Bwana kutoka miji yote ya Yuda, na kunajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, kuanzia Geba hadi Beer-Sheba, mahali pote ambapo hao makuhani wa miungu walifukiza uvumba. Akabomoa mahali pa kuwekea vitu vya ibada za miungu palipokuwa katika malango, kwenye ingilio la Lango la Yoshua, mtawala wa mji, lililoko upande wa kushoto wa lango la mji.
Och han lät församla alla Presterna utu Juda städer, och orenade de höjder, der Presterna rökte, ifrå Geba allt intill BerSeba; och han bröt bort portaltaren, som voro uti ingångenom i Josua stadsfogdans port, hvilken voro på venstra sidone, der man går till stadsporten.
9 Ingawa makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu hawakuhudumu katika madhabahu ya Bwana katika Yerusalemu, walikula mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
Dock offrade icke höjdernas Prester någon tid på Herrans altare i Jerusalem, utan åto af de osyrade brödena, ibland sina bröder.
10 Kisha mfalme akanajisi Tofethi, palipokuwa katika Bonde la Ben-Hinomu, ili mtu yeyote asiweze kupatumia kumtoa kafara mwanawe au binti yake katika moto kwa mungu Moleki.
Han orenade ock Tophet, uti Hinnoms barnas dal, att ingen skulle låta gå sin son eller sina dotter genom eld för Molech;
11 Akaondoa kutoka kwenye ingilio la Hekalu la Bwana wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye ua karibu na chumba cha afisa aliyeitwa Nathan-Meleki. Basi Yosia akayachoma moto yale magari yaliyokuwa yamewekwa wakfu kwa jua.
Och tog bort de hästar, hvilka Juda Konungar solene uppsatt hade, i ingångenom åt Herrans hus, till NethanMelechs åminnelse, kamererarens, som i Parvarim var; och solenes vagnar brände han upp i eld;
12 Alizivunja madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walikuwa wamezijenga kwenye paa la ghorofa ya Ahazi, pia madhabahu alizokuwa amezijenga Manase katika nyua mbili za Hekalu la Bwana. Akaziondoa huko, akazivunja vipande vipande, na kutupa hicho kifusi katika Bonde la Kidroni.
Så ock altaren på taken i Ahas sal, den Juda Konungar gjort hade; och de altare, som Manasse gjort hade uti de två gårdar åt Herrans hus, bröt Konungen bort, och lopp dädan, och kastade deras stoft i Kidrons bäck.
13 Mfalme pia akanajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, palipokuwa mashariki ya Yerusalemu upande wa kusini wa Kilima cha Uharibifu, pale ambapo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amejenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu mke chukizo la Wasidoni, kwa ajili ya Kemoshi mungu chukizo la Wamoabu, na kwa ajili ya Moleki mungu chukizo la watu wa Amoni.
Och de höjder, som för Jerusalem voro, på högra sidone, vid berget Mashith, som Salomo Israels Konung byggt hade till Astoreth, Zidons styggelse, och Chemos, Moabs styggelse, och Milcom, Ammons barnas styggelse, orenade Konungen;
14 Yosia akapasua yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Ashera. Kisha akafunika hayo maeneo kwa mifupa ya wanadamu.
Och slog sönder stoderna, och utrotade lundarna, och uppfyllde deras rum med menniskoben;
15 Hata madhabahu yaliyokuwa huko Betheli, mahali pa juu pa kuabudia miungu palipokuwa pamejengwa na Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwafanya Israeli watende dhambi, alibomoa hata hayo madhabahu na mahali pa juu pa kuabudia miungu. Alipateketeza kwa moto hapo mahali pa juu pa kuabudia miungu na kupasaga hadi pakawa vumbi, na kuichoma hiyo nguzo ya Ashera pia.
Sammalunda ock det altaret i BethEl, höjden, som Jerobeam, Nebats son, gjort hade, den Israel hade kommit till att synda; det samma altaret bröt han neder, och höjdena, och brände upp höjdena, och gjorde henne till stoft, och brände upp lunden.
16 Kisha Yosia akatazama huku na huko, naye alipoona makaburi yaliyokuwa huko kwenye kilima, akaamuru mifupa itolewe humo na akaichoma juu ya madhabahu ya Betheli ili kupanajisi. Hili lilitokea kulingana na neno la Bwana lililosemwa na mtu wa Mungu ambaye alitangulia kusema mambo haya.
Och Josia vände sig om, och fick se de grifter, som voro på bergena, och sände bort, och lät hemta benen utu grifterna, och uppbrände dem på altarena, och orenade det, efter Herrans ord, som Guds mannen utropat hade, den detta så föresagt hade,
17 Mfalme akauliza, “Lile kaburi lenye mnara wa ukumbusho ninaloliona ni kwa ajili gani?” Watu wa mji wakasema, “Hii ni alama ya kaburi la mtu wa Mungu aliyekuja kutoka Yuda, naye akanena dhidi ya hii madhabahu ya Betheli mambo yale yale uliyoifanyia leo.”
Och han sade: Hvad är detta för en vård, som jag här ser? Och folket i stadenom sade till honom: Det är den Guds mansens grift, som af Juda kom, och detta utropade, som du gjort hafver med altarena i BethEl.
18 Akasema, “Liacheni, msiliguse. Msimruhusu mtu yeyote kuiondoa mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na ile ya yule nabii ambaye alikuwa amekuja kutoka Samaria.
Och han sade: Låt honom ligga; ingen röre hans ben. Alltså vordo hans ben friade, med den Prophetens ben, som utaf Samarien kommen var.
19 Kama alivyokuwa amefanya huko Betheli, Yosia akabomoa na kunajisi mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu ambapo wafalme wa Israeli walikuwa wamejenga ndani ya miji ya Samaria, ambayo ilikuwa imemghadhibisha Bwana.
Han kastade ock bort all höjders hus uti Samarie städer, som Israels Konungar gjort hade, till att förtörna ( Herran ), och gjorde med dem alldeles såsom han i BethEl gjort hade.
20 Yosia akawachinja makuhani wote wa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika madhabahu zao wenyewe, na kuchoma mifupa ya wanadamu juu yake. Kisha akarudi Yerusalemu.
Och han offrade alla höjdernas Prester, som der voro, på altaren, och brände så menniskoben deruppå, och kom igen till Jerusalem.
21 Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Bwana Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
Och Konungen böd folkena, och sade: Håller Herranom edrom Gud Passah, såsom skrifvet är i denna förbunds bok.
22 Hapakuwahi kuwepo na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za Waamuzi walioongoza Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
Ty intet Passah var så hållet som detta, ifrå de domares tid, som Israel dömde, och i alla Israels Konungars och Juda Konungars tid;
23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Bwana huko Yerusalemu.
Utan i adertonde årena Konungs Josia vardt detta Passah hållet Herranom i Jerusalem.
24 Zaidi ya hayo, Yosia akawaondoa waaguzi, wanaoabudu mizimu, sanamu za kuagulia, sanamu za kuabudiwa, na vitu vingine vyote vya machukizo vilivyoonekana huko Yuda na Yerusalemu. Aliyafanya haya ili kutimiza matakwa ya sheria iliyoandikwa ndani ya kile kitabu ambacho Hilkia kuhani alikipata ndani ya Hekalu la Bwana.
Desslikes rensade Josia ut alla spåmän, tecknatydare, beläte och afgudar, och all styggelse, som i Juda land och i Jerusalem sedde vordo; på det han skulle upprätta lagsens ord, som skrifne stodo i bokene, som Presten Hilkia fann i Herrans hus.
25 Kabla wala baada ya Mfalme Yosia hapakuwepo na mfalme mwingine yeyote ambaye alimpenda Bwana kwa moyo wake wote, kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na Sheria yote ya Mose.
Hans like hade ingen Konung varit för honom, den så af allt hjerta, af allo själ, och alla krafter sig till Herran vände, efter all Mose lag; och efter honom kom ej heller hans like upp.
26 Hata hivyo, Bwana hakuacha ghadhabu yake iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya yale yote ambayo Manase alikuwa amefanya kumghadhibisha.
Dock vände icke Herren sig ifrå sine stora vredes grymhet, der han med öfver Juda förtörnad var, för all de retelses skull, dermed Manasse honom rett hade.
27 Hivyo Bwana akasema, “Nitamwondoa Yuda mbele zangu kama nilivyomwondoa Israeli, nami nitaukataa Yerusalemu, mji niliouchagua, na Hekalu hili, ambalo nilisema, ‘Jina langu litakaa humo.’”
Och Herren sade: Jag vill ock kasta Juda ifrå mitt ansigte, såsom jag Israel bortkastat hafver; och skall förkasta denna staden, som jag utvalt hafver, nämliga Jerusalem, och det hus, der jag om sagt hafver: Mitt Namn skall vara der.
28 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Hvad nu mer af Josia sägandes är, och allt det han gjort hafver, si, det är skrifvet uti Juda Konungars Chrönico.
29 Yosia alipokuwa mfalme, Farao Neko mfalme wa Misri akapanda mpaka Mto Frati kumsaidia mfalme wa Ashuru. Mfalme Yosia akatoka kwenda kupigana naye, lakini Neko akamkabili na kumuua huko Megido.
Uti hans tid drog Pharao Necho, Konungen i Egypten, upp emot Konungen af Assyrien, vid den älfvena Phrat; men Konung Josia drog emot honom, och blef död i Megiddo, då han hade sett honom.
30 Watumishi wa Yosia wakauleta mwili wake katika gari la vita kutoka Megido hadi Yerusalemu, wakamzika kwenye kaburi lake mwenyewe. Nao watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta na kumfanya mfalme mahali pa baba yake.
Och hans tjenare förde honom dödan ifrå Megiddo, och hade honom till Jerusalem, och begrofvo honom i hans graf; och folket i landena togo Joahas, Josia son, och smorde honom, och gjorde honom till Konung i hans faders stad.
31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
Tre och tjugu åra gammal var Joahas, då han vardt Konung, och regerade tre månader i Jerusalem; hans moder het Hamutal, Jeremia dotter af Libna.
32 Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.
Och han gjorde det ondt var för Herranom, såsom hans fäder gjort hade.
33 Farao Neko akamfunga kwa minyororo huko Ribla katika nchi ya Hamathi ili asiweze kutawala huko Yerusalemu, naye akatoza kodi ya talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu katika Yuda.
Men PharaoNecho grep honom i Riblath i Hamaths land, att han icke regera skulle i Jerusalem; och lade en beskattning på landet, hundrade centener silfver, och en centener guld.
34 Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa baba yake Yosia, na kulibadilisha jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafia huko.
Och PharaoNecho gjorde Eliakim, Josia son, till Konung uti hans faders Josia stad, och vände hans namn Jojakim. Men Joahas tog han, och förde in uti Egypten; der blef han död.
35 Yehoyakimu akamlipa Farao Neko ile fedha na dhahabu aliyodai. Ili kuweza kufanya hivyo, Yehoyakimu akatoza nchi kodi na kulipiza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi kulingana na makadrio ya mapato yao.
Och Jojakim gaf Pharao silfret och guldet; dock beskattade han landet, att han sådant silfver gifva kunde efter Pharaos befallning; hvar och en, efter sina förmågo, beskattade han till silfver och guld ibland folket i landena, att han det PharaoNecho gifva skulle.
36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Zebida binti Pedaya kutoka Ruma.
Fem och tjugu åra gammal var Jojakim, då han vardt Konung, och regerade ellofva år i Jerusalem; hans moder het Zebuda, Pedaja dotter af Ruma.
37 Naye akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyokuwa wamefanya.
Och han gjorde det ondt var för Herranom, såsom hans fäder gjort hade.