< 2 Wafalme 23 >
1 Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
И возвестиша сия глаголы цареви: и посла царь, и собра к себе вся старейшины Иудины и Иерусалимляны,
2 Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na manabii, watu wote wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
и вниде царь в дом Господень, и вси мужие Иудины и вси живущии во Иерусалиме с ним, и жерцы, и пророцы, и вси людие от мала и до велика, и прочте во ушеса их вся словеса книги завета обретшияся в дому Господни:
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo, na kufanya upya agano mbele za Bwana: yaani kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, hivyo kuyathibitisha maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Kisha watu wote wakajifunga wenyewe kwa kiapo katika agano.
и ста царь у столпа и завеща завет пред Господем, еже ходити вслед Господа и хранити заповеди Его и свидения Его и оправдания Его всем сердцем и всею душею, еже возставити словеса завета сего, яже писана в книзе сей. И сташа вси людие в завете.
4 Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani mkuu, makuhani waliomfuata kwa cheo, na mabawabu kuondoa kutoka kwenye Hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali na Ashera na jeshi lote la mianga ya angani! Akavichoma nje ya Yerusalemu katika mashamba ya Bonde la Kidroni, na kuyachukua hayo majivu mpaka Betheli.
И заповеда царь Хелкии жерцу великому и жерцем вторым и стрегущым врат изнести от храма Господня вся сосуды сотвореныя Ваалу и Дубраве и всей силе небесней, и сожже и вне Иерусалима в Садимофе Кедрсте и изверже прах их в Вефиль:
5 Akawafukuza makuhani wa kipagani waliokuwa wameteuliwa na wafalme wa Yuda kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Yuda na ile iliyozunguka Yerusalemu, yaani wale waliofukiza uvumba kwa Baali, kwa jua na mwezi, kwa makundi ya nyota, na jeshi lote la angani.
и сожже хомаримы, ихже даша царие Иудины, и кадяху в высоких и во градех Иудиных и во окрестных Иерусалима, и кадящих Ваалу, и солнцу, и луне, и планетам и всей силе небесней:
6 Akaiondoa nguzo ya Ashera kutoka kwenye Hekalu la Bwana, na kuipeleka kwenye Bonde la Kidroni nje ya Yerusalemu, akaiteketeza huko. Akaisaga hadi ikawa unga na kusambaza hilo vumbi juu ya makaburi ya watu wa kawaida.
и изнесе кумир из храма Господня вне Иерусалима на поток Кедрск, и сожже его в потоце Кедрсте, и истни в прах, и вверже прах их в гробы сынов людских:
7 Akabomoa pia nyumba za mahanithi wa mahali pa ibada za miungu, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana na mahali wanawake walipofuma kwa ajili ya Ashera.
и разруши храм кадисимов, иже бе в храме Господни, идеже жены прядяху ризы кумиру:
8 Yosia akawaleta makuhani wote wa Bwana kutoka miji yote ya Yuda, na kunajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, kuanzia Geba hadi Beer-Sheba, mahali pote ambapo hao makuhani wa miungu walifukiza uvumba. Akabomoa mahali pa kuwekea vitu vya ibada za miungu palipokuwa katika malango, kwenye ingilio la Lango la Yoshua, mtawala wa mji, lililoko upande wa kushoto wa lango la mji.
и возведе вся жерцы от градов Иудиных, и оскверни высокая, идеже кадяху жерцы, от Гаваи да Вирсавеи: и разруши храм врат, иже бе при дверех врат Иисуса князя граднаго, иже ошуюю входящым дверми града.
9 Ingawa makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu hawakuhudumu katika madhabahu ya Bwana katika Yerusalemu, walikula mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
Обаче не вхождаху жерцы высоких ко олтарю Господню во Иерусалиме, но токмо ядяху опресноки посреде братии своея.
10 Kisha mfalme akanajisi Tofethi, palipokuwa katika Bonde la Ben-Hinomu, ili mtu yeyote asiweze kupatumia kumtoa kafara mwanawe au binti yake katika moto kwa mungu Moleki.
И оскверни Тафефа, иже в дебри сынов Еномлих, еже не превести мужу сына своего и мужу дщере своея Молоху сквозе огнь:
11 Akaondoa kutoka kwenye ingilio la Hekalu la Bwana wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye ua karibu na chumba cha afisa aliyeitwa Nathan-Meleki. Basi Yosia akayachoma moto yale magari yaliyokuwa yamewekwa wakfu kwa jua.
и сожже кони, ихже даша царие Иудины солнцу во входе храму Господня, при влагалищи Нафана, царева скопца во Фаруриме: и колесницу солнечную сожже огнем:
12 Alizivunja madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walikuwa wamezijenga kwenye paa la ghorofa ya Ahazi, pia madhabahu alizokuwa amezijenga Manase katika nyua mbili za Hekalu la Bwana. Akaziondoa huko, akazivunja vipande vipande, na kutupa hicho kifusi katika Bonde la Kidroni.
и олтари, яже на крове горницы Ахазовы, яже сотвориша царие Иудины и олтари, иже созда Манассиа во двою двору храма Господня, раскопа царь, и сверже оттуду, и всыпа прах их в поток Кедрск:
13 Mfalme pia akanajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, palipokuwa mashariki ya Yerusalemu upande wa kusini wa Kilima cha Uharibifu, pale ambapo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amejenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu mke chukizo la Wasidoni, kwa ajili ya Kemoshi mungu chukizo la Wamoabu, na kwa ajili ya Moleki mungu chukizo la watu wa Amoni.
и храм, иже пред лицем Иерусалима, одесную горы Мосфаф, егоже созда Соломон царь Израилев Астарте мерзости Сидонстей и Хамосу мерзости Моавли и Молхолу мерзости сынов Аммоних, оскверни царь:
14 Yosia akapasua yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Ashera. Kisha akafunika hayo maeneo kwa mifupa ya wanadamu.
и сокруши столпы, и искорени дубравы, и наполни места их костми человеческими:
15 Hata madhabahu yaliyokuwa huko Betheli, mahali pa juu pa kuabudia miungu palipokuwa pamejengwa na Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwafanya Israeli watende dhambi, alibomoa hata hayo madhabahu na mahali pa juu pa kuabudia miungu. Alipateketeza kwa moto hapo mahali pa juu pa kuabudia miungu na kupasaga hadi pakawa vumbi, na kuichoma hiyo nguzo ya Ashera pia.
и олтарь иже во Вефили высокий, егоже сотвори Иеровоам сын Наватов, иже в грех введе Израиля, и олтарь той высокий раскопа, и сокруши камение его, и истни в прах, и сожже кумиры.
16 Kisha Yosia akatazama huku na huko, naye alipoona makaburi yaliyokuwa huko kwenye kilima, akaamuru mifupa itolewe humo na akaichoma juu ya madhabahu ya Betheli ili kupanajisi. Hili lilitokea kulingana na neno la Bwana lililosemwa na mtu wa Mungu ambaye alitangulia kusema mambo haya.
И восклонися Иосиа, и виде гробы сущыя во граде тамо, и посла, и взя кости от гроб, и сожже на олтари, и оскверни его по глаголу Господню, егоже глагола человек Божий, егда стояше Иеровоам в праздник пред олтарем: и обращься возведе очи свои на гроб человека Божия глаголавшаго словеса сия.
17 Mfalme akauliza, “Lile kaburi lenye mnara wa ukumbusho ninaloliona ni kwa ajili gani?” Watu wa mji wakasema, “Hii ni alama ya kaburi la mtu wa Mungu aliyekuja kutoka Yuda, naye akanena dhidi ya hii madhabahu ya Betheli mambo yale yale uliyoifanyia leo.”
И рече: что могила сия, юже аз вижду? И реша ему мужие града: гроб сей человека Божия есть, иже прииде от Иуды и проглагола словеса сия, яже сотворил еси ныне над олтарем, иже в Вефили.
18 Akasema, “Liacheni, msiliguse. Msimruhusu mtu yeyote kuiondoa mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na ile ya yule nabii ambaye alikuwa amekuja kutoka Samaria.
И рече: оставите его, да не подвижет ни един муж костей его. И оставиша кости его с костьми пророка пришедшаго от Самарии.
19 Kama alivyokuwa amefanya huko Betheli, Yosia akabomoa na kunajisi mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu ambapo wafalme wa Israeli walikuwa wamejenga ndani ya miji ya Samaria, ambayo ilikuwa imemghadhibisha Bwana.
Еще и вся храмы высоких сущих во градех Самарийских, яже сотвориша царие Израилевы прогневляюще Господа, отверже Иосиа, и сотвори им вся дела, яже сотвори в Вефили,
20 Yosia akawachinja makuhani wote wa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika madhabahu zao wenyewe, na kuchoma mifupa ya wanadamu juu yake. Kisha akarudi Yerusalemu.
и закла вся жерцы высоких сущыя тамо пред олтарми, и сожже на них кости человечи, и возвратися во Иерусалим.
21 Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Bwana Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
И заповеда царь всем людем, глаголя: сотворите пасху Господеви Богу нашему, якоже писано в книзе завета сего:
22 Hapakuwahi kuwepo na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za Waamuzi walioongoza Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
яко не бысть пасха сия от дний судий, иже судиша Израилеви, и во всех днех царей Израилевых и царей Иудиных:
23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Bwana huko Yerusalemu.
но токмо во осмоенадесять лето царя Иосии бысть пасха Господу во Иерусалиме.
24 Zaidi ya hayo, Yosia akawaondoa waaguzi, wanaoabudu mizimu, sanamu za kuagulia, sanamu za kuabudiwa, na vitu vingine vyote vya machukizo vilivyoonekana huko Yuda na Yerusalemu. Aliyafanya haya ili kutimiza matakwa ya sheria iliyoandikwa ndani ya kile kitabu ambacho Hilkia kuhani alikipata ndani ya Hekalu la Bwana.
Еще и волшебники, и вражбиты, и ферафимы, и кумиры, и вся мерзости бывшыя в земли Иудине и во Иерусалиме, искорени царь Иосиа, да утвердит словеса законная писанная в книзе, юже обрете Хелкиа жрец в храме Господни.
25 Kabla wala baada ya Mfalme Yosia hapakuwepo na mfalme mwingine yeyote ambaye alimpenda Bwana kwa moyo wake wote, kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na Sheria yote ya Mose.
Подобен ему не бысть пред ним царь, иже обратися к Господеви всем сердцем своим и всею душею своею и всею силою своею по всему закону Моисеову, и по нем не воста подобен ему.
26 Hata hivyo, Bwana hakuacha ghadhabu yake iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya yale yote ambayo Manase alikuwa amefanya kumghadhibisha.
Обаче не отвратися Господь от ярости гнева Своего великаго, имже возярися гневом на Иуду, на прогневания, имиже прогнева Его Манассиа,
27 Hivyo Bwana akasema, “Nitamwondoa Yuda mbele zangu kama nilivyomwondoa Israeli, nami nitaukataa Yerusalemu, mji niliouchagua, na Hekalu hili, ambalo nilisema, ‘Jina langu litakaa humo.’”
и рече Господь: еще и Иуду отрину от лица Моего, якоже отринух Израиля, и град сей отвергу, егоже избрах, Иерусалима, и храм, о немже рех: будет имя Мое ту.
28 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
И прочая словес Иосиевых, и вся елика сотвори, не сия ли написана в книзе словес дний царей Иудиных?
29 Yosia alipokuwa mfalme, Farao Neko mfalme wa Misri akapanda mpaka Mto Frati kumsaidia mfalme wa Ashuru. Mfalme Yosia akatoka kwenda kupigana naye, lakini Neko akamkabili na kumuua huko Megido.
Во днех же его взыде фараон Нехао царь Египетск на царя Ассирийска на реку Евфрат: и изыде царь Иосиа на сретение ему, и уби его Нехао царь в Магеддоне, егда его узре.
30 Watumishi wa Yosia wakauleta mwili wake katika gari la vita kutoka Megido hadi Yerusalemu, wakamzika kwenye kaburi lake mwenyewe. Nao watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta na kumfanya mfalme mahali pa baba yake.
И взяша его отроцы его мертва из Магеддона и принесоша его во Иерусалим, и погребоша его во гробе его во граде Давидове. И пояша людие земли тоя Иоахаза сына Иосиина и помазаша его, и воцариша его вместо отца его.
31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
Сын двадесяти и триех лет бе Иоахаз, внегда нача царствовати и три месяцы царствова во Иерусалиме. Имя же матери его Амитала, дщи Иеремии из Ловны.
32 Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.
И сотвори лукавое пред очима Господнима, по всем елика сотвориша отцы его.
33 Farao Neko akamfunga kwa minyororo huko Ribla katika nchi ya Hamathi ili asiweze kutawala huko Yerusalemu, naye akatoza kodi ya talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu katika Yuda.
И пресели его фараон Нехао в Ревлаам в землю Емаф, да не царствует во Иерусалиме, и возложи дань на землю ту сто талант сребра и сто талант злата.
34 Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa baba yake Yosia, na kulibadilisha jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafia huko.
И постави царем фараон Нехао над ними Елиакима, сына Иосии царя Иудина, вместо Иосии отца его, и премени имя ему Иоаким: Иоахаза же взя и введе во Египет и умре тамо.
35 Yehoyakimu akamlipa Farao Neko ile fedha na dhahabu aliyodai. Ili kuweza kufanya hivyo, Yehoyakimu akatoza nchi kodi na kulipiza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi kulingana na makadrio ya mapato yao.
И сребро и злато даде Иоаким фараону, обаче написа землю даяти сребро по словеси фараоню: муж по оценению своему даяше сребро и злато от людий земли тоя даяти фараону Нехао.
36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Zebida binti Pedaya kutoka Ruma.
Сын бе двадесяти и пяти лет Иоаким, егда нача царствовати, и единонадесять лет царствова во Иерусалиме. Имя же матери его Иелдаф, дщи Фадаиля, от Румы.
37 Naye akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyokuwa wamefanya.
И сотвори лукавое пред очима Господнима, по всем елика сотвориша отцы его.