< 2 Wafalme 23 >

1 Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
Wtedy król posłał, aby zebrali się wokół niego wszyscy starsi Judy i Jerozolimy.
2 Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na manabii, watu wote wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
Następnie król udał się do domu PANA, a wraz z nim wszyscy mężczyźni Judy, wszyscy mieszkańcy Jerozolimy, kapłani, prorocy oraz cały lud – od najmniejszych do największych. I czytał do ich uszu wszystkie słowa księgi przymierza, którą znaleziono w domu PANA.
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo, na kufanya upya agano mbele za Bwana: yaani kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, hivyo kuyathibitisha maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Kisha watu wote wakajifunga wenyewe kwa kiapo katika agano.
Potem król stanął przy kolumnie i zawarł przymierze przed PANEM, że będą szli za PANEM i będą przestrzegać jego przykazań, świadectw i nakazów z całego serca i całą duszą i wypełniać słowa przymierza, które zostały napisane w tej księdze. I cały lud przystąpił do przymierza.
4 Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani mkuu, makuhani waliomfuata kwa cheo, na mabawabu kuondoa kutoka kwenye Hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali na Ashera na jeshi lote la mianga ya angani! Akavichoma nje ya Yerusalemu katika mashamba ya Bonde la Kidroni, na kuyachukua hayo majivu mpaka Betheli.
Wtedy król nakazał najwyższemu kapłanowi Chilkiaszowi, kapłanom drugiego rzędu i stróżom progu wynieść ze świątyni PANA wszystkie przedmioty wykonane dla Baala, do gaju i dla całego zastępu niebieskiego. I spalił je poza Jerozolimą na polu Cedronu, i zaniósł ich popiół do Betel.
5 Akawafukuza makuhani wa kipagani waliokuwa wameteuliwa na wafalme wa Yuda kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Yuda na ile iliyozunguka Yerusalemu, yaani wale waliofukiza uvumba kwa Baali, kwa jua na mwezi, kwa makundi ya nyota, na jeshi lote la angani.
Zwolnił też [z urzędu] bałwochwalczych kapłanów, których ustanowili królowie Judy, aby palili kadzidło na wyżynach w miastach Judy i w okolicach Jerozolimy, oraz tych, którzy palili kadzidło Baalowi, słońcu, księżycowi, planetom i całemu zastępowi niebieskiemu.
6 Akaiondoa nguzo ya Ashera kutoka kwenye Hekalu la Bwana, na kuipeleka kwenye Bonde la Kidroni nje ya Yerusalemu, akaiteketeza huko. Akaisaga hadi ikawa unga na kusambaza hilo vumbi juu ya makaburi ya watu wa kawaida.
Wyniósł gaj z domu PANA poza Jerozolimę, do potoku Cedron, i spalił go przy potoku Cedron, starł go na proch i rozrzucił na grobach synów ludu.
7 Akabomoa pia nyumba za mahanithi wa mahali pa ibada za miungu, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana na mahali wanawake walipofuma kwa ajili ya Ashera.
Zburzył też domy Sodomitów, które znajdowały się przy domu PANA, gdzie kobiety tkały zasłony do gaju.
8 Yosia akawaleta makuhani wote wa Bwana kutoka miji yote ya Yuda, na kunajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, kuanzia Geba hadi Beer-Sheba, mahali pote ambapo hao makuhani wa miungu walifukiza uvumba. Akabomoa mahali pa kuwekea vitu vya ibada za miungu palipokuwa katika malango, kwenye ingilio la Lango la Yoshua, mtawala wa mji, lililoko upande wa kushoto wa lango la mji.
I zwołał wszystkich kapłanów z miast Judy, i splugawił wyżyny, na których kapłani palili kadzidło, od Geba aż do Beer-Szeby, i zburzył wyżyny przy bramach [znajdujących się] u wejścia bramy Jozuego, namiestnika miasta, po lewej stronie, gdy się wchodzi przez bramę miejską.
9 Ingawa makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu hawakuhudumu katika madhabahu ya Bwana katika Yerusalemu, walikula mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
Jednakże kapłani wyżyn nie przystąpili do ołtarza PANA w Jerozolimie, ale mogli jeść przaśne chleby wśród swoich braci.
10 Kisha mfalme akanajisi Tofethi, palipokuwa katika Bonde la Ben-Hinomu, ili mtu yeyote asiweze kupatumia kumtoa kafara mwanawe au binti yake katika moto kwa mungu Moleki.
Splugawił również Tofet, które było w dolinie syna Hinnom, aby nikt więcej nie przeprowadził swego syna ani córki przez ogień [ku czci] Molocha.
11 Akaondoa kutoka kwenye ingilio la Hekalu la Bwana wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye ua karibu na chumba cha afisa aliyeitwa Nathan-Meleki. Basi Yosia akayachoma moto yale magari yaliyokuwa yamewekwa wakfu kwa jua.
Usunął też konie, które królowie Judy poświęcili słońcu u wejścia do domu PANA, obok komnaty dworzanina Natanmeleka, która była na przedmieściu, a rydwany słońca spalił ogniem.
12 Alizivunja madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walikuwa wamezijenga kwenye paa la ghorofa ya Ahazi, pia madhabahu alizokuwa amezijenga Manase katika nyua mbili za Hekalu la Bwana. Akaziondoa huko, akazivunja vipande vipande, na kutupa hicho kifusi katika Bonde la Kidroni.
Król zburzył także ołtarze, które znajdowały się na dachu górnej komnaty Achaza, zbudowane przez królów Judy, oraz ołtarze, które uczynił Manasses w obu dziedzińcach domu PANA. Usunął je stamtąd i wrzucił ich proch do potoku Cedron.
13 Mfalme pia akanajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, palipokuwa mashariki ya Yerusalemu upande wa kusini wa Kilima cha Uharibifu, pale ambapo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amejenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu mke chukizo la Wasidoni, kwa ajili ya Kemoshi mungu chukizo la Wamoabu, na kwa ajili ya Moleki mungu chukizo la watu wa Amoni.
Król splugawił wyżyny, które stały przed Jerozolimą po prawej stronie Góry Zatracenia i które zbudował Salomon, król Izraela, dla Asztarty, obrzydliwości Sydończyków, dla Kemosza, obrzydliwości Moabitów, i dla Milkoma, obrzydliwości synów Ammona.
14 Yosia akapasua yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Ashera. Kisha akafunika hayo maeneo kwa mifupa ya wanadamu.
I pokruszył posągi, powycinał gaje, a ich miejsca napełnił kośćmi ludzkimi.
15 Hata madhabahu yaliyokuwa huko Betheli, mahali pa juu pa kuabudia miungu palipokuwa pamejengwa na Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwafanya Israeli watende dhambi, alibomoa hata hayo madhabahu na mahali pa juu pa kuabudia miungu. Alipateketeza kwa moto hapo mahali pa juu pa kuabudia miungu na kupasaga hadi pakawa vumbi, na kuichoma hiyo nguzo ya Ashera pia.
Ponadto ołtarz, który był w Betel, [i] wyżynę uczynioną przez Jeroboama, syna Nebata, który przywiódł Izraela do grzechu – także ten ołtarz i wyżynę zburzył. Spalił wyżynę, starł na proch i spalił gaj.
16 Kisha Yosia akatazama huku na huko, naye alipoona makaburi yaliyokuwa huko kwenye kilima, akaamuru mifupa itolewe humo na akaichoma juu ya madhabahu ya Betheli ili kupanajisi. Hili lilitokea kulingana na neno la Bwana lililosemwa na mtu wa Mungu ambaye alitangulia kusema mambo haya.
A gdy Jozjasz odwrócił się, zobaczył groby, które były tam na górze. Posłał i zabrał kości z tych grobów, i spalił je na ołtarzu, plugawiąc go zgodnie ze słowem PANA wygłoszonym przez męża Bożego, który wypowiedział te rzeczy.
17 Mfalme akauliza, “Lile kaburi lenye mnara wa ukumbusho ninaloliona ni kwa ajili gani?” Watu wa mji wakasema, “Hii ni alama ya kaburi la mtu wa Mungu aliyekuja kutoka Yuda, naye akanena dhidi ya hii madhabahu ya Betheli mambo yale yale uliyoifanyia leo.”
I zapytał: Co to za napis, który widzę? Ludzie z tego miasta odpowiedzieli: To grób męża Bożego, który przyszedł z Judy i zapowiedział rzeczy, które wykonałeś nad ołtarzem w Betel.
18 Akasema, “Liacheni, msiliguse. Msimruhusu mtu yeyote kuiondoa mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na ile ya yule nabii ambaye alikuwa amekuja kutoka Samaria.
Wtedy powiedział: Zostawcie go, niech nikt nie rusza jego kości. Pozostawiono więc jego kości wraz z kośćmi proroka, który przybył z Samarii.
19 Kama alivyokuwa amefanya huko Betheli, Yosia akabomoa na kunajisi mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu ambapo wafalme wa Israeli walikuwa wamejenga ndani ya miji ya Samaria, ambayo ilikuwa imemghadhibisha Bwana.
Jozjasz usunął też wszystkie świątynie na wyżynach, które były w miastach Samarii zbudowanych przez królów Izraela, aby drażnić [PANA]. Postąpił z nimi tak samo, jak uczynił w Betel.
20 Yosia akawachinja makuhani wote wa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika madhabahu zao wenyewe, na kuchoma mifupa ya wanadamu juu yake. Kisha akarudi Yerusalemu.
Pozabijał także wszystkich kapłanów wyżyn, którzy tam [byli] przy ołtarzach, i spalił na nich ludzkie kości. Potem wrócił do Jerozolimy.
21 Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Bwana Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
I król nakazał całemu ludowi: Obchodźcie święto Paschy dla PANA, waszego Boga, tak jak jest napisane w księdze tego przymierza.
22 Hapakuwahi kuwepo na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za Waamuzi walioongoza Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
Takiej Paschy nie obchodzono od czasów sędziów, którzy sądzili Izraela, i przez wszystkie dni królów Izraela i królów Judy.
23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Bwana huko Yerusalemu.
Dopiero w osiemnastym roku króla Jozjasza obchodzono taką Paschę dla PANA w Jerozolimie.
24 Zaidi ya hayo, Yosia akawaondoa waaguzi, wanaoabudu mizimu, sanamu za kuagulia, sanamu za kuabudiwa, na vitu vingine vyote vya machukizo vilivyoonekana huko Yuda na Yerusalemu. Aliyafanya haya ili kutimiza matakwa ya sheria iliyoandikwa ndani ya kile kitabu ambacho Hilkia kuhani alikipata ndani ya Hekalu la Bwana.
Jozjasz usunął również czarowników, wróżbiarzy, posągi, bożki i wszystkie obrzydliwości, które widziano w ziemi Judy i w Jerozolimie, aby wypełnić słowa prawa napisane w księdze, którą znalazł kapłan Chilkiasz w domu PANA.
25 Kabla wala baada ya Mfalme Yosia hapakuwepo na mfalme mwingine yeyote ambaye alimpenda Bwana kwa moyo wake wote, kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na Sheria yote ya Mose.
I nie było przed nim króla podobnego do niego, który by wrócił do PANA z całego swego serca, całą swoją duszą i z całej swojej siły, według całego Prawa Mojżesza, i po nim nie powstał nikt jemu podobny.
26 Hata hivyo, Bwana hakuacha ghadhabu yake iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya yale yote ambayo Manase alikuwa amefanya kumghadhibisha.
PAN jednak nie odwrócił się od zapalczywości swego wielkiego gniewu, którym zapłonął przeciwko Judzie z powodu wszelkich zniewag, którymi rozdrażnił go Manasses.
27 Hivyo Bwana akasema, “Nitamwondoa Yuda mbele zangu kama nilivyomwondoa Israeli, nami nitaukataa Yerusalemu, mji niliouchagua, na Hekalu hili, ambalo nilisema, ‘Jina langu litakaa humo.’”
PAN więc powiedział: Również Judę odrzucę sprzed swojego oblicza, jak odrzuciłem Izraela, i wzgardzę tym miastem, które wybrałem, Jerozolimą, i domem tym, o którym powiedziałem: Tam będzie moje imię.
28 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
A pozostałe dzieje Jozjasza i wszystko, co czynił, czy nie są zapisane w księdze kronik królów Judy?
29 Yosia alipokuwa mfalme, Farao Neko mfalme wa Misri akapanda mpaka Mto Frati kumsaidia mfalme wa Ashuru. Mfalme Yosia akatoka kwenda kupigana naye, lakini Neko akamkabili na kumuua huko Megido.
Za jego dni faraon Necho, król Egiptu, wyruszył przeciwko królowi Asyrii nad rzekę Eufrat. Król Jozjasz wyruszył przeciwko niemu, a gdy ten go zobaczył, zabił go w Megiddo.
30 Watumishi wa Yosia wakauleta mwili wake katika gari la vita kutoka Megido hadi Yerusalemu, wakamzika kwenye kaburi lake mwenyewe. Nao watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta na kumfanya mfalme mahali pa baba yake.
I jego słudzy przewieźli go zmarłego z Megiddo, sprowadzili go do Jerozolimy i pogrzebali w jego grobie. Potem lud tej ziemi wziął Jehoachaza, syna Jozjasza, namaścił go i ustanowił go królem w miejsce jego ojca.
31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
Jehoachaz miał dwadzieścia trzy lata, kiedy zaczął królować, i królował trzy miesiące w Jerozolimie. Jego matka miała na imię Chamutal [i była] córką Jeremiasza z Libny.
32 Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.
Czynił on to, co złe w oczach PANA, zupełnie tak, jak czynili jego ojcowie.
33 Farao Neko akamfunga kwa minyororo huko Ribla katika nchi ya Hamathi ili asiweze kutawala huko Yerusalemu, naye akatoza kodi ya talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu katika Yuda.
Faraon Necho uwięził go w Ribla w ziemi Chamat, aby nie królował w Jerozolimie, i nałożył na ziemię daninę w wysokości stu talentów srebra i jednego talentu złota.
34 Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa baba yake Yosia, na kulibadilisha jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafia huko.
Faraon Necho ustanowił królem Eliakima, syna Jozjasza, w miejsce jego ojca Jozjasza, i zmienił jego imię na Joakim, a Jehoachaza zabrał. Ten przyszedł do Egiptu i tam umarł.
35 Yehoyakimu akamlipa Farao Neko ile fedha na dhahabu aliyodai. Ili kuweza kufanya hivyo, Yehoyakimu akatoza nchi kodi na kulipiza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi kulingana na makadrio ya mapato yao.
A Joakim dał faraonowi srebro i złoto, ale opodatkował ziemię, aby mógł oddać pieniądze według rozkazu faraona. Pobierał srebro i złoto od ludu ziemi, od każdego według oszacowania, aby je oddać faraonowi Necho.
36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Zebida binti Pedaya kutoka Ruma.
Joakim miał dwadzieścia pięć lat, kiedy zaczął królować, i królował jedenaście lat w Jerozolimie. Jego matka miała na imię Zebidda [i była] córką Pedajasza z Rumy.
37 Naye akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyokuwa wamefanya.
Czynił on to, co złe w oczach PANA, zupełnie tak, jak czynili jego ojcowie.

< 2 Wafalme 23 >