< 2 Wafalme 23 >

1 Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
Da sendte Kongen Bud og lod alle Judas og Jerusalems Ældste kalde sammen hos sig.
2 Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na manabii, watu wote wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
Derpå gik Kongen op i HERRENs Hus, fulgt af alle Judas Mænd og alle Jerusalems Indbyggere, Præsterne, Profeterne og hele Folket, små og store, og han forelæste dem alt, hvad der stod i Pagtsbogen, som var fundet i HERRENs Hus.
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo, na kufanya upya agano mbele za Bwana: yaani kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, hivyo kuyathibitisha maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Kisha watu wote wakajifunga wenyewe kwa kiapo katika agano.
Så tog Kongen Plads ved Søjlen og sluttede Pagt for HERRENs Åsyn om, at de skulde holde sig til HERREN og holde hans Bud, Vidnesbyrd og Anordninger af hele deres Hjerte og hele deres Sjæl, for at han kunde opfylde denne Pagts Ord, således som de var skrevet i denne Bog. Og alt Folket indgik Pagten.
4 Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani mkuu, makuhani waliomfuata kwa cheo, na mabawabu kuondoa kutoka kwenye Hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali na Ashera na jeshi lote la mianga ya angani! Akavichoma nje ya Yerusalemu katika mashamba ya Bonde la Kidroni, na kuyachukua hayo majivu mpaka Betheli.
Derpå bød Kongen Ypperstepræsten Hilkija og Andenpræsten og Dørvogterne at bringe alle de Ting, der var lavet til Ba'al, Asjera og hele Himmelens Hær, ud af HERRENs Helligdom, og han lod dem opbrænde uden for Jerusalem på Markerne ved Hedron, og Asken lod han bringe til Betel.
5 Akawafukuza makuhani wa kipagani waliokuwa wameteuliwa na wafalme wa Yuda kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Yuda na ile iliyozunguka Yerusalemu, yaani wale waliofukiza uvumba kwa Baali, kwa jua na mwezi, kwa makundi ya nyota, na jeshi lote la angani.
Og han afsatte Afgudspræsterne, som Judas Konger havde indsat, og som havde tændt Offerild på Højene i Judas Byer og Jerusalems Omegn, ligeledes dem, som havde tændt Offerild for Ba'al og for Solen, Månen, Stjernebillederne og hele Himmelens Hær.
6 Akaiondoa nguzo ya Ashera kutoka kwenye Hekalu la Bwana, na kuipeleka kwenye Bonde la Kidroni nje ya Yerusalemu, akaiteketeza huko. Akaisaga hadi ikawa unga na kusambaza hilo vumbi juu ya makaburi ya watu wa kawaida.
Og han lod Asjerastøtten bringe fra HERRENs Hus uden for Jerusalem til Kedrons Dal og opbrænde der, og han lod den knuse til Støv og Støvet kaste hen, hvor Småfolk havde deres Grave.
7 Akabomoa pia nyumba za mahanithi wa mahali pa ibada za miungu, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana na mahali wanawake walipofuma kwa ajili ya Ashera.
Han lod Mandsskøgernes Kamre i HERRENs Hus rive ned, dem i hvilke Kvinderne vævede Kjortler til Asjera.
8 Yosia akawaleta makuhani wote wa Bwana kutoka miji yote ya Yuda, na kunajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, kuanzia Geba hadi Beer-Sheba, mahali pote ambapo hao makuhani wa miungu walifukiza uvumba. Akabomoa mahali pa kuwekea vitu vya ibada za miungu palipokuwa katika malango, kwenye ingilio la Lango la Yoshua, mtawala wa mji, lililoko upande wa kushoto wa lango la mji.
Han lod alle Præsterne hente fra Judas Byer og vanhelligede Offer: højene, hvor Præsterne havde tændt offerild, fra Geba til Be'er-sjeba. Og han lod Portofferhøjen rive ned, som var ved Indgangen til Byøversten Jehosjuas Port til venstre, når man går ind ad Byporten.
9 Ingawa makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu hawakuhudumu katika madhabahu ya Bwana katika Yerusalemu, walikula mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
Dog fik Præsterne ved Højene ikke Adgang til HERRENs Alter i Jerusalem, men de måtte spise usyret Brød blandt deres Brødre.
10 Kisha mfalme akanajisi Tofethi, palipokuwa katika Bonde la Ben-Hinomu, ili mtu yeyote asiweze kupatumia kumtoa kafara mwanawe au binti yake katika moto kwa mungu Moleki.
Han vanhelligede Ildstedet i Hinnoms Søns Dal, så at ingen mere kunde lade sin Søn eller Datter gå igennem Ilden for Molok.
11 Akaondoa kutoka kwenye ingilio la Hekalu la Bwana wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye ua karibu na chumba cha afisa aliyeitwa Nathan-Meleki. Basi Yosia akayachoma moto yale magari yaliyokuwa yamewekwa wakfu kwa jua.
Han fjernede de Heste, Judas Konger havde opstillet for Solen ved Indgangen til HERRENs Hus hen imod Hofmanden Netan Me'leks Kammer i Parvarim, og Solens Vogne lod han opbrænde.
12 Alizivunja madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walikuwa wamezijenga kwenye paa la ghorofa ya Ahazi, pia madhabahu alizokuwa amezijenga Manase katika nyua mbili za Hekalu la Bwana. Akaziondoa huko, akazivunja vipande vipande, na kutupa hicho kifusi katika Bonde la Kidroni.
Altrene, som Judas Konger havde rejst på Taget (Akaz's Tagbygning), og Altrene, som Manasse havde rejst i begge Forgårdene til HERRENs Hus, lod Kongen nebdryde og knuse på Stedet, og Støvet lod han kaste, hen i Kedrons Dal.
13 Mfalme pia akanajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, palipokuwa mashariki ya Yerusalemu upande wa kusini wa Kilima cha Uharibifu, pale ambapo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amejenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu mke chukizo la Wasidoni, kwa ajili ya Kemoshi mungu chukizo la Wamoabu, na kwa ajili ya Moleki mungu chukizo la watu wa Amoni.
Og Offerhøjene østen for Jerusalem på Sydsiden af Fordærvelsens Bjerg, som Kong Salomo af Israel havde bygget for Astarte; Zidoniernes væmmelige Gud, Kemosj, Moabiternes væmmelige Gud, og Milkom, Ammoniternes vederstyggelige Gud, vanhelligede Kongen.
14 Yosia akapasua yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Ashera. Kisha akafunika hayo maeneo kwa mifupa ya wanadamu.
Han lod Stenstøtterne nedbryde og Asjerastøtterne omhugge og Pladsen fylde med Menneskeknogler.
15 Hata madhabahu yaliyokuwa huko Betheli, mahali pa juu pa kuabudia miungu palipokuwa pamejengwa na Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwafanya Israeli watende dhambi, alibomoa hata hayo madhabahu na mahali pa juu pa kuabudia miungu. Alipateketeza kwa moto hapo mahali pa juu pa kuabudia miungu na kupasaga hadi pakawa vumbi, na kuichoma hiyo nguzo ya Ashera pia.
Også Alteret i Betel, den Offerhøj, som Jeroboam, Nebats Søn havde rejst han der forledte Israel til Synd, også det Alter tillige med Offerhøjen lod han nedbryde; Stenene lod han nedrive og knuse til Støv, og Asjerastøtten lod han opbrænde.
16 Kisha Yosia akatazama huku na huko, naye alipoona makaburi yaliyokuwa huko kwenye kilima, akaamuru mifupa itolewe humo na akaichoma juu ya madhabahu ya Betheli ili kupanajisi. Hili lilitokea kulingana na neno la Bwana lililosemwa na mtu wa Mungu ambaye alitangulia kusema mambo haya.
Da Josias vendte sig om og fik Øje på Gravene på Bjerget, sendte han Folk hen og lod dem tage Benene ud af Gravene og opbrænde dem på Alteret for, at vanhellige det efter HERRENs Ord, som den Guds Mand udråbte, da han kundgjorde disse Ting,
17 Mfalme akauliza, “Lile kaburi lenye mnara wa ukumbusho ninaloliona ni kwa ajili gani?” Watu wa mji wakasema, “Hii ni alama ya kaburi la mtu wa Mungu aliyekuja kutoka Yuda, naye akanena dhidi ya hii madhabahu ya Betheli mambo yale yale uliyoifanyia leo.”
Så sagde han: "Hvad er det for et Gravmæle, jeg ser der?" Byens Folk svarede ham: "Det er den Guds Mands Grav, der kom fra Juda og kundgjorde det, du nu har gjort med Alteret i Betel."
18 Akasema, “Liacheni, msiliguse. Msimruhusu mtu yeyote kuiondoa mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na ile ya yule nabii ambaye alikuwa amekuja kutoka Samaria.
Da sagde han: "Lad ham ligge i Ro, ingen må flytte hans Ben!" Så lod de både hans og Profeten fra Samarias Ben fred.
19 Kama alivyokuwa amefanya huko Betheli, Yosia akabomoa na kunajisi mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu ambapo wafalme wa Israeli walikuwa wamejenga ndani ya miji ya Samaria, ambayo ilikuwa imemghadhibisha Bwana.
Også alle Offerhusene på Højene i Samarias Byer, som Israels Konger havde opført for at krænke HERREN, lod Josias fjerne, og han handlede med dem ganske som han havde gjort i Betel;
20 Yosia akawachinja makuhani wote wa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika madhabahu zao wenyewe, na kuchoma mifupa ya wanadamu juu yake. Kisha akarudi Yerusalemu.
og han lod alle Højenes Præster, som var der ved Altrene, dræbe, og han opbrændte Menneskeknogler på Altrene. Så vendte han tilbage til Jerusalem.
21 Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Bwana Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
Derefter gav Kongen alt Folket, den Befaling: "Hold Påske for HERREN eders Gud, som der er foreskrevet her i Pagtsbogen!"
22 Hapakuwahi kuwepo na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za Waamuzi walioongoza Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
Thi slig en Påske var ikke nogen Sinde blevet holdt i Israels og Judas Kongers Tid, ikke siden Dommerne dømte Israel;
23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Bwana huko Yerusalemu.
men først i Kong Josias's attende Regeringsår blev en sådan Påske fejret for HERREN i Jerusalem.
24 Zaidi ya hayo, Yosia akawaondoa waaguzi, wanaoabudu mizimu, sanamu za kuagulia, sanamu za kuabudiwa, na vitu vingine vyote vya machukizo vilivyoonekana huko Yuda na Yerusalemu. Aliyafanya haya ili kutimiza matakwa ya sheria iliyoandikwa ndani ya kile kitabu ambacho Hilkia kuhani alikipata ndani ya Hekalu la Bwana.
Også Dødemanerne og Sandsigerne, Husguderne, Afgudsbillederne og alle de væmmelige Guder, der var at se i Judas Land og Jerusalem, udryddede Josias for at opfylde Lovens Ord, der stod skrevet i den Bog, Præsten Hilkija havde fundet i HERRENs Hus.
25 Kabla wala baada ya Mfalme Yosia hapakuwepo na mfalme mwingine yeyote ambaye alimpenda Bwana kwa moyo wake wote, kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na Sheria yote ya Mose.
Der havde ikke før været nogen Konge, der som han af hele sit Hjerte og hele sin Sjæl og al sin Kraft omvendte sig til HERREN og fulgte hele Mose Lov; og heller ikke efter ham opstod hans Lige.
26 Hata hivyo, Bwana hakuacha ghadhabu yake iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya yale yote ambayo Manase alikuwa amefanya kumghadhibisha.
Alligevel lagde HERRENs mægtige Vredesglød sig ikke, thi hans Vrede var blusset op mod Juda over alle de Krænkelser, Manasse havde tilføjet ham.
27 Hivyo Bwana akasema, “Nitamwondoa Yuda mbele zangu kama nilivyomwondoa Israeli, nami nitaukataa Yerusalemu, mji niliouchagua, na Hekalu hili, ambalo nilisema, ‘Jina langu litakaa humo.’”
Og HERREN sagde: "Også Juda vil jeg fjerne fra mit Åsyn, ligesom jeg fjernede Israel, og jeg vil forkaste Jerusalem, denne min udvalgte By, og det Hus, om hvilket jeg har sagt: Mit Navn skal være der!"
28 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Hvad der ellers er at fortælle om Josias, alt, hvad han udførte, står jo optegnet i Judas Kongers Krønike.
29 Yosia alipokuwa mfalme, Farao Neko mfalme wa Misri akapanda mpaka Mto Frati kumsaidia mfalme wa Ashuru. Mfalme Yosia akatoka kwenda kupigana naye, lakini Neko akamkabili na kumuua huko Megido.
I hans Dage drog Ægypterkongen Parao Neko op til Eufratfloden imod Assyrerkongen. Kong Josias rykkede imod ham, men Neko fældede ham ved Megiddo, straks han så ham.
30 Watumishi wa Yosia wakauleta mwili wake katika gari la vita kutoka Megido hadi Yerusalemu, wakamzika kwenye kaburi lake mwenyewe. Nao watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta na kumfanya mfalme mahali pa baba yake.
Og hans Folk førte ham død bort fra Megiddo, bragte ham til Jerusalem og jordede ham i hans Grav. Men Folket fra Landet tog Joahaz, Josias's Søn, og salvede og hyldede ham til Bonge i hans Faders Sted.
31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
Joahaz var tre og tyve År gammel, da han blev Konge, og han herskede tre Måneder i Jerusalem. Hans Moder hed Hamutal og var en Datter af Jirmeja fra, Libna.
32 Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.
Han gjorde, hvad der var ondt i HERRENs Øjne, ganske som hans Fædre.
33 Farao Neko akamfunga kwa minyororo huko Ribla katika nchi ya Hamathi ili asiweze kutawala huko Yerusalemu, naye akatoza kodi ya talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu katika Yuda.
Men Farao Neko lod ham fængsle i Ribla i Hamats Land og gjorde dermed Ende på hans Herredømme i Jerusalem og lagde en Skat af hundrede Talenter Sølv og ti Talenter Guld på Landet.
34 Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa baba yake Yosia, na kulibadilisha jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafia huko.
Derpå gjorde Farao Neko Eljakim, Josias's Søn, til Konge i hans Fader Josias's Sted, og han ændrede hans Navn til Jojakim; Joahaz derimod tog han med til Ægypten, og der døde han.
35 Yehoyakimu akamlipa Farao Neko ile fedha na dhahabu aliyodai. Ili kuweza kufanya hivyo, Yehoyakimu akatoza nchi kodi na kulipiza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi kulingana na makadrio ya mapato yao.
Sølvet og Guldet udredede Jojakim til Farao; men for. at kunne udrede Pengeneefter Faraos Befaling satte han Landet i Skat; efter som hver især var sat i Skat, inddrev han Sølvet og Guldet for at give Farao Neko det.
36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Zebida binti Pedaya kutoka Ruma.
Jojakim var fem og tyve År gammel, da han blev Konge, og han herskede elleve År i Jerusalem. Hans Moder hed Zebida og var en Datter af Pedaja fra Ruma.
37 Naye akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyokuwa wamefanya.
Han gjorde, hvad der var ondt i HERRENs Øjne, ganske som hans Fædre.

< 2 Wafalme 23 >