< 2 Wafalme 22 >

1 Yosia alikuwa na miaka minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka thelathini na mmoja. Mama yake aliitwa Yedida binti Adaya, kutoka Boskathi.
Ośm lat było Jozyjaszowi, gdy począł królować, a trzydzieści jeden lat królował w Jeruzalemie; a imię matki jego było Jedyda, córka Adaja z Besekatu.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana na kuenenda katika njia zote za Daudi baba yake. Hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.
I czynił, co było dobrego przed oczyma Pańskiemi, chodząc wszystkimi drogami Dawida, ojca swego, a nie uchylał się ani na prawo ani na lewo.
3 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, Mfalme Yosia akamtuma mwandishi Shafani mwana wa Azalia, mwana wa Meshulamu, kwenda katika Hekalu la Bwana. Akasema:
A ośmnastego roku króla Jozyjasza posłał król Safana, syna Azalijaszowego, syna Mesulama, pisarza, do domu Pańskiego, mówiąc:
4 “Panda uende kwa Hilkia, kuhani mkuu, umwambie ahesabu zile fedha ambazo zimeletwa katika Hekalu la Bwana, ambazo mabawabu wamekusanya kutoka kwa watu.
Idź do Helkijasza, kapłana najwyższego, aby zebrał pieniądze, które wnoszono do domu Pańskiego, które wybierali stróżowie progu od ludu.
5 Waambie waikabidhi kwa watu walioteuliwa kusimamia kazi ya Hekalu. Waamuru watu hawa wawalipe wafanyakazi ambao wanakarabati Hekalu la Bwana:
A niech je dawają w ręce rzemieślników, przełożonych nad robotą domu Pańskiego, aby je dawali robotnikom, którzy robili w domu Pańskim, naprawiając skazę domu;
6 wale maseremala, wajenzi na waashi. Waambie pia wanunue mbao na mawe yaliyochongwa ili kukarabati Hekalu.
To jest, budownikom i cieślom, i murarzom, i na zkupowanie drzewa, i kamienia ciosanego ku naprawie domu.
7 Lakini hawahitajiki kutoa hesabu ya fedha walizokabidhiwa, kwa sababu wanafanya kwa uaminifu.”
Wszakże niech nie czynią liczby z pieniędzy, które dawają do rąk ich; bo oni wiernie nimi szafować będą.
8 Hilkia kuhani mkuu akamwambia Shafani mwandishi, “Nimekipata Kitabu cha Sheria ndani ya Hekalu la Bwana.” Akampa Shafani, ambaye alikisoma.
I rzekł Helkijasz, kapłan najwyższy, do Safana pisarza. Księgi zakonu znalazłem w domu Pańskim. I dał Helkijasz one księgi Safanowi, i czytał je (Safan).
9 Kisha Shafani mwandishi akamwendea mfalme na kumpa taarifa akisema: “Maafisa wako wametoa ile fedha ambayo ilikuwa ndani ya Hekalu la Bwana na imekabidhiwa mikononi mwa wasimamizi wa marekebisho ya Hekalu.”
Przyszedłszy tedy Safan pisarz do króla, odniósł to królowi, i rzekł: Zebrali słudzy twoi pieniądze, które się znalazły w domu Pańskim, i oddali je w ręce rzemieślników przełożonych nad robotą w domu Pańskim.
10 Ndipo Shafani mwandishi akampasha mfalme habari kwamba: “Hilkia kuhani amenipa kitabu hiki.” Naye Shafani akakisoma kile kitabu mbele ya mfalme.
Oznajmił też Safan pisarz królowi, mówiąc: Dał mi księgę Helkijasz kapłan; i czytał ją Safan przed królem.
11 Mfalme aliposikia maneno ya kile Kitabu cha Sheria, akararua mavazi yake.
A gdy usłyszał król słowa ksiąg zakonu, rozdarł szaty swe.
12 Akatoa maagizo haya kwa Hilkia kuhani, Ahikamu mwana wa Shafani, Akbori mwana wa Mikaya, Shafani mwandishi, na Asaya mtumishi wa mfalme:
I rozkazał król Helkijaszowi kapłanowi, i Ahykamowi, synowi Safanowemu, i Achborowi, synowi Micheaszowemu, i Safanowi pisarzowi, i Asajaszowi, słudze swemu, mówiąc:
13 “Nendeni mkamuulize Bwana kwa ajili yangu, na kwa ajili ya watu na Yuda wote kuhusu yale yaliyoandikwa ndani ya kitabu hiki ambacho kimepatikana. Hasira ya Bwana ni kubwa inayowaka dhidi yetu kwa sababu baba zetu hawakuyatii maneno ya kitabu hiki. Hawajatenda kulingana na yale yote yaliyoandikwa humo kutuhusu sisi.”
Idźcie, poradźcie się Pana o mię, i o lud, i o wszystkiego Judę z strony słów tych ksiąg, które są znalezione; bo wielki jest gniew Pański, który się zapalił przeciwko nam, przeto iż nie posłuchali ojcowie nasi słów tych ksiąg, żeby czynili według wszystkiego, co nam jest napisane.
14 Hilkia kuhani, Ahikamu, Akbori, Shafani na Asaya wakaenda kuongea na nabii mke Hulda, ambaye alikuwa mke wa Shalumu mwana wa Tikwa, mwana wa Harhasi mtunzaji wa chumba cha mavazi. Hulda aliishi Yerusalemu katika Mtaa wa Pili.
A tak poszedł Helkijasz kapłan, i Ahykam, i Achbor, i Safan, i Azajasz, do Huldy prorokini, żony Selluma, syna Tekui, syna Araaszowego, który był stróżem szat; a ona mieszkała w Jeruzalemie na drugiej stronie miasta; i mówili z nią.
15 Akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambieni yule mtu aliyewatuma ninyi kwangu,
Która rzekła do nich: Tak mówi Pan, Bóg Izraelski. Powiedzcie mężowi, który was posłał do mnie;
16 ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Nitaleta maafa juu ya mahali hapa na watu wake, kulingana na kila kitu kilichoandikwa katika kitabu hicho mfalme wa Yuda alichosoma.
Tak mówi Pan: Oto Ja przywiodę złe na to miejsce i na obywateli jego według wszystkich słów ksiąg tych, które czytał król Judzki.
17 Kwa sababu wameniacha mimi na kufukiza uvumba kwa miungu mingine, na kunighadhibisha kwa sanamu zote zilizotengenezwa kwa mikono yao, hasira yangu itawaka dhidi ya mahali hapa, wala haitatulizwa.’
Przeto, że mię opuścili, i kadzili bogom cudzym, aby mię draźnili wszystkiemi sprawami rąk swoich, dla czego rozpaliła się popędliwość moja przeciwko miejscu temu, i nie będzie ugaszona.
18 Mwambieni mfalme wa Yuda, ambaye amewatuma kumuuliza Bwana, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli, kuhusu maneno uliyoyasikia:
A królowi Judzkiemu, który was posłał o radę do Pana, tak powiedzcie: Tak mówi Pan, Bóg Izraelski, o słowach, któreś słyszał:
19 Kwa kuwa moyo wako ulikuwa msikivu na ulijinyenyekeza mbele za Bwana uliposikia kile nilichosema dhidi ya mahali hapa na watu wake, kwamba wangelaaniwa na kuachwa ukiwa, basi kwa sababu uliyararua mavazi yako na kulia mbele zangu, nimekusikia, asema Bwana.
Ponieważ zmiękczone jest serce twoje, a upokorzyłeś się przed obliczem Pańskiem, słysząc, com powiedział przeciwko temu miejscu, i przeciwko obywatelom jego, iż ma przyjść w spustoszenie i w przeklęstwo; rozdarłeś szaty swe, a płakałeś przedemną, i Jam cię też wysłuchał, mówi Pan.
20 Kwa hiyo nitakukusanya kwa baba zako, nawe utazikwa kwa amani. Macho yako hayataona maafa yote nitakayoleta juu ya mahali hapa.’” Basi wakapeleka jibu lake kwa mfalme.
Przetoż oto Ja cię zbiorę do ojców twoich, a będziesz zebrany do grobu twego w pokoju, aby nie oglądały oczy twoje wszystkiego złego, które Ja przywiodę na to miejsce. I odniesiono tę rzecz królowi.

< 2 Wafalme 22 >