< 2 Wafalme 22 >

1 Yosia alikuwa na miaka minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka thelathini na mmoja. Mama yake aliitwa Yedida binti Adaya, kutoka Boskathi.
Josiah was eight years old when he had begun to reign. He reigned for thirty-one years in Jerusalem. The name of his mother was Jedidah, the daughter of Adaiah, from Bozkath.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana na kuenenda katika njia zote za Daudi baba yake. Hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.
And he did what was pleasing before the Lord, and he walked in all the ways of his father David. He did not turn aside to the right, or to the left.
3 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, Mfalme Yosia akamtuma mwandishi Shafani mwana wa Azalia, mwana wa Meshulamu, kwenda katika Hekalu la Bwana. Akasema:
Then, in the eighteenth year of king Josiah, the king sent Shaphan, the son of Azaliah, the son of Meshullam, the scribe of the temple of the Lord, saying to him:
4 “Panda uende kwa Hilkia, kuhani mkuu, umwambie ahesabu zile fedha ambazo zimeletwa katika Hekalu la Bwana, ambazo mabawabu wamekusanya kutoka kwa watu.
“Go to Hilkiah, the high priest, so that the money may be put together which has been brought into the temple of the Lord, which the doorkeepers of the temple have collected from the people.
5 Waambie waikabidhi kwa watu walioteuliwa kusimamia kazi ya Hekalu. Waamuru watu hawa wawalipe wafanyakazi ambao wanakarabati Hekalu la Bwana:
And let it be given, by those in charge of the house of the Lord, to the workers. And let them distribute it to those who are working in the temple of the Lord in order to repair the surfaces of the temple,
6 wale maseremala, wajenzi na waashi. Waambie pia wanunue mbao na mawe yaliyochongwa ili kukarabati Hekalu.
specifically, to carpenters and masons, and to those who mend gaps, and so that wood may be purchased, and stones from the quarries, in order to repair the temple of the Lord.
7 Lakini hawahitajiki kutoa hesabu ya fedha walizokabidhiwa, kwa sababu wanafanya kwa uaminifu.”
Yet truly, let no account be given by them of the money that they receive. Instead, let them have it within their power and trust.”
8 Hilkia kuhani mkuu akamwambia Shafani mwandishi, “Nimekipata Kitabu cha Sheria ndani ya Hekalu la Bwana.” Akampa Shafani, ambaye alikisoma.
Then Hilkiah, the high priest, said to Shaphan, the scribe, “I have found the book of the law in the house of the Lord.” And Hilkiah gave the volume to Shaphan, and he read it.
9 Kisha Shafani mwandishi akamwendea mfalme na kumpa taarifa akisema: “Maafisa wako wametoa ile fedha ambayo ilikuwa ndani ya Hekalu la Bwana na imekabidhiwa mikononi mwa wasimamizi wa marekebisho ya Hekalu.”
Also, Shaphan, the scribe, went to the king, and reported to him what he had instructed. And he said: “Your servants have brought together the money which was found in the house of the Lord. And they have given it so that it would be distributed to the workers by the overseers of the works of the temple of the Lord.”
10 Ndipo Shafani mwandishi akampasha mfalme habari kwamba: “Hilkia kuhani amenipa kitabu hiki.” Naye Shafani akakisoma kile kitabu mbele ya mfalme.
Also, Shaphan, the scribe, explained to the king, saying, “Hilkiah, the priest, gave the book to me.” And when Shaphan had read it before the king,
11 Mfalme aliposikia maneno ya kile Kitabu cha Sheria, akararua mavazi yake.
and the king had heard the words of the book of the law of the Lord, he tore his garments.
12 Akatoa maagizo haya kwa Hilkia kuhani, Ahikamu mwana wa Shafani, Akbori mwana wa Mikaya, Shafani mwandishi, na Asaya mtumishi wa mfalme:
And he instructed Hilkiah, the priest, and Ahikam, the son of Shaphan, and Achbor, the son of Micaiah, and Shaphan, the scribe, and Asaiah, the servant of the king, saying:
13 “Nendeni mkamuulize Bwana kwa ajili yangu, na kwa ajili ya watu na Yuda wote kuhusu yale yaliyoandikwa ndani ya kitabu hiki ambacho kimepatikana. Hasira ya Bwana ni kubwa inayowaka dhidi yetu kwa sababu baba zetu hawakuyatii maneno ya kitabu hiki. Hawajatenda kulingana na yale yote yaliyoandikwa humo kutuhusu sisi.”
“Go and consult the Lord concerning me, and the people, and all of Judah, about the words of this volume which has been found. For the great wrath of the Lord has been kindled against us because our fathers did not listen to the words of this book, so that they would do all that has been written for us.”
14 Hilkia kuhani, Ahikamu, Akbori, Shafani na Asaya wakaenda kuongea na nabii mke Hulda, ambaye alikuwa mke wa Shalumu mwana wa Tikwa, mwana wa Harhasi mtunzaji wa chumba cha mavazi. Hulda aliishi Yerusalemu katika Mtaa wa Pili.
Therefore, Hilkiah, the priest, and Ahikam, and Achbor, and Shaphan, and Asaiah, went to Huldah, the prophetess, the wife of Shallum, the son of Tikvah, the son of Harhas, the keeper of the vestments, who was living in Jerusalem, in the second part. And they spoke with her.
15 Akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambieni yule mtu aliyewatuma ninyi kwangu,
And she responded to them: “Thus says the Lord, the God of Israel: Tell the man who sent you to me:
16 ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Nitaleta maafa juu ya mahali hapa na watu wake, kulingana na kila kitu kilichoandikwa katika kitabu hicho mfalme wa Yuda alichosoma.
Thus says the Lord: Behold, I will lead evils over this place, and over its inhabitants, all the words of the law that the king of Judah has read.
17 Kwa sababu wameniacha mimi na kufukiza uvumba kwa miungu mingine, na kunighadhibisha kwa sanamu zote zilizotengenezwa kwa mikono yao, hasira yangu itawaka dhidi ya mahali hapa, wala haitatulizwa.’
For they have abandoned me, and they have sacrificed to foreign gods, provoking me by all the works of their hands. And so my indignation will be kindled against this place. And it will not be extinguished.
18 Mwambieni mfalme wa Yuda, ambaye amewatuma kumuuliza Bwana, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli, kuhusu maneno uliyoyasikia:
But to the king of Judah, who sent you so that you would consult the Lord, so shall you say: Thus says the Lord, the God of Israel: In so far as you have heard the words of the volume,
19 Kwa kuwa moyo wako ulikuwa msikivu na ulijinyenyekeza mbele za Bwana uliposikia kile nilichosema dhidi ya mahali hapa na watu wake, kwamba wangelaaniwa na kuachwa ukiwa, basi kwa sababu uliyararua mavazi yako na kulia mbele zangu, nimekusikia, asema Bwana.
and your heart was terrified, and you humbled yourself before the Lord, listening to the words against this place and its inhabitants, specifically, that they would become an astonishment and a curse, and because you have torn your garments, and have wept before me: I also have heard you, says the Lord.
20 Kwa hiyo nitakukusanya kwa baba zako, nawe utazikwa kwa amani. Macho yako hayataona maafa yote nitakayoleta juu ya mahali hapa.’” Basi wakapeleka jibu lake kwa mfalme.
For this reason, I will gather you to your fathers, and you will be gathered to your sepulcher in peace, so that your eyes may not see all the evils that I will bring over this place.”

< 2 Wafalme 22 >