< 2 Wafalme 20 >
1 Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Nabii Isaya mwana wa Amozi akaenda kwake na kumwambia, “Hili ndilo asemalo Bwana: Tengeneza mambo ya nyumba yako, kwa sababu utakufa, hutapona.”
Tanī laikā Hizkija palika slims uz miršanu, un pravietis Jesaja, Amoca dēls, nāca pie viņa un uz to sacīja: tā saka Tas Kungs: apkopi savu namu, jo tu mirsi un nepaliksi vesels.
2 Hezekia akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana:
Tad Hizkija savu vaigu pagrieza pret sienu un pielūdza To Kungu un sacīja:
3 “Ee Bwana, kumbuka jinsi nilivyoenenda mbele zako kwa uaminifu na kujitoa kwa moyo wangu wote, na kufanya yaliyo mema machoni pako.” Naye Hezekia akalia kwa uchungu.
Ak Kungs, piemini lūdzams, ka es Tavā priekšā esmu staigājis patiesībā no visas sirds un darījis, kas tev patīk. Un Hizkija gauži raudāja.
4 Kabla Isaya hajaondoka katika ua wa kati, neno la Bwana likamjia, akaambiwa:
Un kad Jesaja vēl nebija izgājis ne pusceļa caur pilsētu, tad Tā Kunga vārds uz viņu notika un sacīja:
5 “Rudi ukamwambie Hezekia, kiongozi wa watu wangu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa baba yako Daudi: Nimeyasikia maombi yako na nimeona machozi yako; nitakuponya. Siku ya tatu kuanzia sasa utapanda kwenda Hekalu la Bwana.
Ej atpakaļ un saki uz Hizkiju, Manas tautas valdnieku: tā saka Tas Kungs, tava tēva Dāvida Dievs: Es tavu lūgšanu esmu klausījis, Es tavas asaras esmu redzējis, redzi, Es tevi darīšu veselu, trešā dienā tu iesi Tā Kunga namā.
6 Nitakuongezea miaka kumi na mitano katika maisha yako. Nami nitakuokoa wewe pamoja na mji huu mkononi mwa mfalme wa Ashuru. Nitaulinda mji huu kwa ajili yangu, na kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi!’”
Un pie tavām dienām Es vēl pielikšu piecpadsmit gadus, un tevi un šo pilsētu Es izpestīšu no Asīrijas ķēniņa rokas un pasargāšu šo pilsētu Sevis labad un Sava kalpa Dāvida labad.
7 Kisha Isaya akasema, “Tengenezeni dawa ya kubandika ya tini.” Wakafanya hivyo na kuiweka kwenye jipu, naye akapona.
Un Jesaja sacīja: ņemiet vīģu rausi. Un tie to ņēma un uzlika uz to trumu, tad viņš palika vesels.
8 Hezekia alikuwa amemuuliza Isaya, “Kutakuwa na ishara gani kwamba Bwana ataniponya mimi, na kwamba nitapanda kwenda Hekalu la Bwana siku ya tatu tangu leo?”
Un Hizkija sacīja uz Jesaju: kāda ir tā zīme, ka Tas Kungs mani darīs veselu, un ka es trešā dienā iešu Tā Kunga namā?
9 Isaya akajibu, “Hii ndiyo ishara ya Bwana kwako kwamba Bwana atafanya kile alichoahidi: Je, kivuli kiende hatua kumi mbele, au kivuli kirudi nyuma hatua kumi?”
Un Jesaja sacīja: šī būs tā zīme no Tā Kunga, ka Tas Kungs šo lietu darīs, ko viņš runājis. Vai ēnai būs iet desmit kāpienus uz priekšu, vai desmit kāpienus atpakaļ?
10 Hezekia akasema, “Ni jambo rahisi kwa kivuli kutangulia mbele hatua kumi, kuliko kukifanya kirudi nyuma hatua kumi.”
Tad Hizkija sacīja: tas ir viegli, ēnai iet desmit kāpienus uz priekšu, - to ne, bet lai ēna iet desmit kāpienus atpakaļ.
11 Ndipo nabii Isaya akamwita Bwana, naye Bwana akakifanya kivuli kurudi nyuma hatua kumi ambazo kilikuwa kimeshuka kwenye ngazi ya Ahazi.
Un pravietis Jesaja piesauca To Kungu, un Tas tai ēnai lika iet desmit kāpienus atpakaļ pa tiem pašiem kāpieniem, ko tā bija gājusi uz priekšu pie Ahaza saules stundeņa.
12 Wakati huo Merodaki-Baladani, mwana wa Baladani mfalme wa Babeli, akamtumia Hezekia barua na zawadi, kwa sababu alikuwa amesikia habari za kuugua kwa Hezekia.
Tanī laikā Berodaks Baladans, Baladana dēls, Bābeles ķēniņš, sūtīja grāmatas un dāvanas pie Hizkijas, jo tas bija dzirdējis, ka Hizkija bijis slims.
13 Hezekia akawapokea wale wajumbe na kuwaonyesha vitu vyote vile vilivyokuwa katika ghala zake: yaani fedha, dhahabu, vikolezo na mafuta safi, ghala la silaha na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hapakuwa na kitu chochote katika jumba lake la kifalme au katika ufalme wake wote ambacho Hezekia hakuwaonyesha.
Un Hizkija par tiem priecājās un tiem radīja visu savu mantas namu, sudrabu un zeltu un dārgās zāles un to smalko eļļu un visu savu bruņu namu un visu, kas viņa mantās bija; nekas nebija viņa namā un visā viņa valstī ko Hizkija tiem nebūtu rādījis.
14 Ndipo nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza, “Watu hao walisema nini, na wametoka wapi?” Hezekia akamjibu, “Wametoka nchi ya mbali. Walikuja kutoka Babeli.”
Tad pravietis Jesaja nāca pie ķēniņa Hizkijas un uz to sacīja: ko šie vīri sacījuši un no kurienes tie pie tevis nākuši? Un Hizkija sacīja: tie no tālas zemes atnākuši, no Bābeles.
15 Nabii akauliza, “Waliona nini katika jumba lako la kifalme?” Hezekia akajibu, “Waliona kila kitu katika jumba langu la kifalme. Hakuna kitu chochote katika hazina yangu ambacho sikuwaonyesha.”
Un tas sacīja: ko tie laba redzējuši tavā namā? Un Hizkija sacīja: tie visu redzējuši, kas manā namā; nekā nav no manām mantām, ko es tiem nebūtu rādījis.
16 Ndipo Isaya akamwambia Hezekia, “Sikia neno la Bwana:
Tad Jesaja sacīja uz Hizkiju: klausies Tā Kunga vārdu:
17 Hakika wakati unakuja ambapo vitu vyote katika jumba lako la kifalme, na vyote ambavyo baba zako waliweka akiba mpaka siku hii, vitachukuliwa kwenda Babeli. Hakuna chochote kitakachosalia, asema Bwana.
Redzi, dienas nāks, ka viss, kas ir tavā namā un ko tavi tēvi līdz šai dienai sakrājuši, taps novests uz Bābeli, nekas netaps atlicināts, saka Tas Kungs.
18 Nao baadhi ya wazao wako, nyama yako na damu yako mwenyewe watakaozaliwa kwako, watachukuliwa mbali, nao watakuwa matowashi katika jumba la mfalme wa Babeli.”
Un no taviem bērniem, kas no tevis nāks, ko tu dzemdināsi, taps ņemti, ka tie būs par kambarjunkuriem Bābeles ķēniņa pilī.
19 Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la Bwana ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Lakini si patakuwa na amani na usalama wakati wa uhai wangu?”
Un Hizkija sacīja uz Jesaju: Tā Kunga vārds ir labs, ko tu runājis. Un viņš sacīja: lai notiek, kad tikai miers un drošība pastāv manā laikā.
20 Matukio mengine ya utawala wa Hezekia, mafanikio yake yote, na jinsi alivyotengeneza bwawa na mfereji ambao ulileta maji katika mji, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Un kas vēl par Hizkiju stāstāms, un viss viņa spēks, un ko viņš darījis, un par to dīķi un ūdens grāvi, un ka viņš ūdeni vadījis pilsētā, tas viss ir rakstīts Jūda ķēniņu laiku grāmatā.
21 Hezekia akafa, akazikwa pamoja na baba zake. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.
Un Hizkija aizmiga saviem tēviem pakaļ, un Manasus, viņa dēls, palika par ķēniņu viņa vietā.