< 2 Wafalme 20 >

1 Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Nabii Isaya mwana wa Amozi akaenda kwake na kumwambia, “Hili ndilo asemalo Bwana: Tengeneza mambo ya nyumba yako, kwa sababu utakufa, hutapona.”
Kadagidiay nga al-aldaw, agsaksakit ni Hezekias ket matmatayen. Isu a napan kekuana ni propeta Isaias nga anak ni Amos ket kinunana kenkuana, “Kinuna ni Yahweh, 'Urnosemon ti balaymo; ta mataykan ket saankan nga agbiag.'”
2 Hezekia akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana:
Ket insango ni Hezekias ti rupana iti diding ket nagkararag kenni Yahweh a kinunana,
3 “Ee Bwana, kumbuka jinsi nilivyoenenda mbele zako kwa uaminifu na kujitoa kwa moyo wangu wote, na kufanya yaliyo mema machoni pako.” Naye Hezekia akalia kwa uchungu.
“Pangaasim Yahweh, laglagipem no kasanoak a simmurot a sipupudno kenka iti amin a pusok ken no kasanoak a nagaramid ti naimbag iti panagkitam.” Ket nagsangit iti napigsa ni Hezekias.
4 Kabla Isaya hajaondoka katika ua wa kati, neno la Bwana likamjia, akaambiwa:
Sakbay a makalasat ni Isaias iti akintengnga a paraangan, immay kenkuana ti sao ni Yahweh a kinunana,
5 “Rudi ukamwambie Hezekia, kiongozi wa watu wangu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa baba yako Daudi: Nimeyasikia maombi yako na nimeona machozi yako; nitakuponya. Siku ya tatu kuanzia sasa utapanda kwenda Hekalu la Bwana.
“Agsublika, ket ibagam kenni Hezekias, ti mangidadaulo kadagiti tattaok, 'Daytoy ti kinuna ni Yahweh a Dios ni David a kapuonam: “Nangngegko ti kararagmo, ket nakitak dagiti luam. Agasankanto iti maikatlo nga aldaw, ket sumang-atkanto iti balay ni Yahweh.
6 Nitakuongezea miaka kumi na mitano katika maisha yako. Nami nitakuokoa wewe pamoja na mji huu mkononi mwa mfalme wa Ashuru. Nitaulinda mji huu kwa ajili yangu, na kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi!’”
Nayunak pay ti sangapulo ket lima a tawen ti biagmo, ket ispalenka ken daytoy a siudad manipud iti bileg ti ari ti Asiria, ken salaknibak daytoy a siudad para iti bukodko a dayaw ken gapu iti adipenko a ni David."”'
7 Kisha Isaya akasema, “Tengenezeni dawa ya kubandika ya tini.” Wakafanya hivyo na kuiweka kwenye jipu, naye akapona.
Isu a kinuna ni Isaias, “Mangalakayo iti namekmek nga igos.” Inaramidda ket intapalda iti lettegna, ket immimbag.
8 Hezekia alikuwa amemuuliza Isaya, “Kutakuwa na ishara gani kwamba Bwana ataniponya mimi, na kwamba nitapanda kwenda Hekalu la Bwana siku ya tatu tangu leo?”
Kinuna ni Hezekias kenni Isaias, “Anianto ti pagilasinan nga agasannak ni Yahweh, a makasang-atak idiay templona iti maikatlo nga aldaw?”
9 Isaya akajibu, “Hii ndiyo ishara ya Bwana kwako kwamba Bwana atafanya kile alichoahidi: Je, kivuli kiende hatua kumi mbele, au kivuli kirudi nyuma hatua kumi?”
Simmungbat ni Isaias, “Daytoy ti pagilasinam manipud kenni Yahweh, nga aramidento ni Yahweh ti banag nga imbagana. Agpasangonto kadi ti aniniwan iti sangapulo a tukad wenno bumaba iti sangapulo a tukad?”
10 Hezekia akasema, “Ni jambo rahisi kwa kivuli kutangulia mbele hatua kumi, kuliko kukifanya kirudi nyuma hatua kumi.”
Simmungbat ni Hezekias, “Nalaka a banag para iti aniniwan nga agpasango iti sangapulo a tukad. Pababaen lattan ti aniniwan iti sangapulo a tukad.”
11 Ndipo nabii Isaya akamwita Bwana, naye Bwana akakifanya kivuli kurudi nyuma hatua kumi ambazo kilikuwa kimeshuka kwenye ngazi ya Ahazi.
Isu nga immawag ni Isaias a propeta kenni Yahweh, ket impababana ti aniniwan iti sangapulo a tukad, iti agdan ni Ahaz a nagakaranna.
12 Wakati huo Merodaki-Baladani, mwana wa Baladani mfalme wa Babeli, akamtumia Hezekia barua na zawadi, kwa sababu alikuwa amesikia habari za kuugua kwa Hezekia.
Iti dayta a tiempo, nangipatulod kadagiti surat ken sagut ni Merodak Baladan nga anak ni Baladan nga ari ti Babilonia kenni Hezekias, ta nadamagna nga agsaksakit ni Hezekias.
13 Hezekia akawapokea wale wajumbe na kuwaonyesha vitu vyote vile vilivyokuwa katika ghala zake: yaani fedha, dhahabu, vikolezo na mafuta safi, ghala la silaha na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hapakuwa na kitu chochote katika jumba lake la kifalme au katika ufalme wake wote ambacho Hezekia hakuwaonyesha.
Dinengngeg ni Hezekias ti linaon dagitoy a surat, kalpasanna, impakitana kadagiti mensahero ti sibubukel a palasio ken ti kinabaknangna, dagiti pirak, dagiti balitok, dagiti rekado ken dagiti napapateg a lana, ken ti pagidulinan dagiti armasna, ken dagiti amin nga adda kadagiti pagidulinanna. Awan ti saan nga impakita ni Hezekias kadakuada nga adda iti balay ken pagarianna.
14 Ndipo nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza, “Watu hao walisema nini, na wametoka wapi?” Hezekia akamjibu, “Wametoka nchi ya mbali. Walikuja kutoka Babeli.”
Kalpasanna, napan ni propeta Isaias kenni Ari Hezekias ket dinamagna, “Ania ti imbaga dagitoy a lallaki kenka? Sadino ti naggapuanda? Kinuna ni Hezekias, “Naggapuda iti adayo a pagilian iti Babilonia.”
15 Nabii akauliza, “Waliona nini katika jumba lako la kifalme?” Hezekia akajibu, “Waliona kila kitu katika jumba langu la kifalme. Hakuna kitu chochote katika hazina yangu ambacho sikuwaonyesha.”
Sinaludsod ni Isaias, “Ania ti nakitada iti uneg ti balaymo?” Simmungbat ni Hezekias, “Nakitada amin nga adda iti uneg ti balayko. Awan kadagiti napapateg a banbanag iti saanko nga impakita kadakuada.”
16 Ndipo Isaya akamwambia Hezekia, “Sikia neno la Bwana:
Isu a kinuna ni Isaias kenni Hezekias, “Denggem ti sao ni Yahweh:
17 Hakika wakati unakuja ambapo vitu vyote katika jumba lako la kifalme, na vyote ambavyo baba zako waliweka akiba mpaka siku hii, vitachukuliwa kwenda Babeli. Hakuna chochote kitakachosalia, asema Bwana.
Kitaem, dumtengto dagiti aldaw a maipan idiay Babilonia dagiti isu amin nga adda iti palasiom, dagiti banbanag nga impempen dagiti kapuonam agingga iti agdama nga aldaw. Awanto pulos iti mabati, kuna ni Yahweh.
18 Nao baadhi ya wazao wako, nyama yako na damu yako mwenyewe watakaozaliwa kwako, watachukuliwa mbali, nao watakuwa matowashi katika jumba la mfalme wa Babeli.”
Italawdanto dagiti annakmo a lallaki, a pinutotmo—ket agbalindanto a eunoko iti palasio ti ari ti Babilonia.”'
19 Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la Bwana ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Lakini si patakuwa na amani na usalama wakati wa uhai wangu?”
Kinuna ni Hezekias kenni Isaias, “Nasayaat ti imbagam a sao ni Yahweh.” Ta impagarupna, “Awanto kadi iti kapia ken kinatalged kadagiti aldawko?”
20 Matukio mengine ya utawala wa Hezekia, mafanikio yake yote, na jinsi alivyotengeneza bwawa na mfereji ambao ulileta maji katika mji, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
No maipapan met kadagiti dadduma a banbanag maipapan kenni Hezekias, ti amin a kinabilegna, no kasano nga inaramidna ti pagurnongan ti danum ken iti usok a pagayusan ti danum, no kasano nga indanonna ti danum idiay siudad— saanda kadi a naisurat Iti Libro Dagiti Pakasaritaan Dagiti Ari-ari iti Juda?
21 Hezekia akafa, akazikwa pamoja na baba zake. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.
Pimmusay ni Hezekias ket ni Manases nga anakna ti nagbalin nga ari a kasukatna.

< 2 Wafalme 20 >