< 2 Wafalme 20 >

1 Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Nabii Isaya mwana wa Amozi akaenda kwake na kumwambia, “Hili ndilo asemalo Bwana: Tengeneza mambo ya nyumba yako, kwa sababu utakufa, hutapona.”
En ce temps-là, Ezéchias fut malade à la mort. Le prophète Isaïe, fils d'Amos, vint auprès du lui et lui dit: « Ainsi dit Yahweh: Donne tes ordres à ta maison, car tu vas mourir, et tu ne vivras plus. »
2 Hezekia akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana:
Ezéchias tourna son visage contre le mur, et pria Yahweh en ces termes:
3 “Ee Bwana, kumbuka jinsi nilivyoenenda mbele zako kwa uaminifu na kujitoa kwa moyo wangu wote, na kufanya yaliyo mema machoni pako.” Naye Hezekia akalia kwa uchungu.
« Souvenez-vous, ô Yahweh, que j'ai marché devant votre face avec fidélité et intégrité de cœur, et que j'ai fait ce qui est bien à vos yeux. » Et Ezéchias versa des larmes abondantes.
4 Kabla Isaya hajaondoka katika ua wa kati, neno la Bwana likamjia, akaambiwa:
Isaïe, n'était pas sorti jusqu'à la cour du milieu, lorsque la parole de Yahweh lui fut adressée en ces termes:
5 “Rudi ukamwambie Hezekia, kiongozi wa watu wangu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa baba yako Daudi: Nimeyasikia maombi yako na nimeona machozi yako; nitakuponya. Siku ya tatu kuanzia sasa utapanda kwenda Hekalu la Bwana.
Retourne, et dis à Ezéchias, chef de mon peuple: « Ainsi dit Yahweh, le Dieu de David, ton père: J'ai entendu ta prière et j'ai vu tes larmes; voici que je te guéris; dans trois jours, tu monteras à la maison de Yahweh;
6 Nitakuongezea miaka kumi na mitano katika maisha yako. Nami nitakuokoa wewe pamoja na mji huu mkononi mwa mfalme wa Ashuru. Nitaulinda mji huu kwa ajili yangu, na kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi!’”
j'ajouterai à tes jours quinze années. Je te délivrerai, toi et cette ville, de la main du roi d'Assyrie; je protégerai cette ville à cause de moi et à cause de David mon serviteur. »
7 Kisha Isaya akasema, “Tengenezeni dawa ya kubandika ya tini.” Wakafanya hivyo na kuiweka kwenye jipu, naye akapona.
Isaïe dit: « Prenez une masse de figues. » On la prit, on l'appliqua sur l'ulcère, et Ezéchias guérit.
8 Hezekia alikuwa amemuuliza Isaya, “Kutakuwa na ishara gani kwamba Bwana ataniponya mimi, na kwamba nitapanda kwenda Hekalu la Bwana siku ya tatu tangu leo?”
Ezéchias avait dit à Isaïe: « A quel signe connaîtrai-je que Yahweh me guérira et que je monterai dans trois jours à la maison de Yahweh. »
9 Isaya akajibu, “Hii ndiyo ishara ya Bwana kwako kwamba Bwana atafanya kile alichoahidi: Je, kivuli kiende hatua kumi mbele, au kivuli kirudi nyuma hatua kumi?”
Isaïe dit: « Voici pour toi le signe donné par Yahweh, auquel tu connaîtras que Yahweh accomplira la parole qu'il a dite: l'ombre avancera-t-elle de dix degrés, ou reculera-t-elle de dix degrés? »
10 Hezekia akasema, “Ni jambo rahisi kwa kivuli kutangulia mbele hatua kumi, kuliko kukifanya kirudi nyuma hatua kumi.”
Ezéchias répondit: « C'est peu de chose que l'ombre avance de dix degrés; mais qu'elle recule en arrière de dix degrés! »
11 Ndipo nabii Isaya akamwita Bwana, naye Bwana akakifanya kivuli kurudi nyuma hatua kumi ambazo kilikuwa kimeshuka kwenye ngazi ya Ahazi.
Alors Isaïe, le prophète invoqua Yahweh, qui fit reculer l'ombre en arrière de dix degrés sur les degrés d'Achaz, sur les degrés où elle était descendue.
12 Wakati huo Merodaki-Baladani, mwana wa Baladani mfalme wa Babeli, akamtumia Hezekia barua na zawadi, kwa sababu alikuwa amesikia habari za kuugua kwa Hezekia.
En ce même temps, Mérodach-Baladan, fils de Baladan, roi de Babylone, envoya une lettre et des présents à Ezéchias, parce qu'il avait appris qu'Ezéchias était malade.
13 Hezekia akawapokea wale wajumbe na kuwaonyesha vitu vyote vile vilivyokuwa katika ghala zake: yaani fedha, dhahabu, vikolezo na mafuta safi, ghala la silaha na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hapakuwa na kitu chochote katika jumba lake la kifalme au katika ufalme wake wote ambacho Hezekia hakuwaonyesha.
Ezéchias se réjouit de la venue des envoyés, et il leur montra toute la maison de son trésor, l'argent et l'or, les aromates et l'huile de prix, tout son arsenal et tout ce qui se trouvait dans ses trésors; il n'y eut rien qu'Ezéchias ne leur fit voir dans sa maison et dans tous ses domaines.
14 Ndipo nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza, “Watu hao walisema nini, na wametoka wapi?” Hezekia akamjibu, “Wametoka nchi ya mbali. Walikuja kutoka Babeli.”
Mais Isaïe, le prophète, vint auprès du roi Ezéchias, et lui dit: « Qu'ont dit ces gens-là, et d'où sont-ils venus vers toi? » Ezéchias répondit: « Ils sont venus d'un pays éloigné, de Babylone. »
15 Nabii akauliza, “Waliona nini katika jumba lako la kifalme?” Hezekia akajibu, “Waliona kila kitu katika jumba langu la kifalme. Hakuna kitu chochote katika hazina yangu ambacho sikuwaonyesha.”
Et Isaïe dit: « Qu'ont-ils vu dans ta maison? » Et Ezéchias répondit: « Ils ont vu tout ce qui est dans ma maison; il n'y a rien dans mes trésors que je ne leur aie fait voir. »
16 Ndipo Isaya akamwambia Hezekia, “Sikia neno la Bwana:
Et Isaïe dit à Ezéchias: « Ecoute la parole de Yahweh:
17 Hakika wakati unakuja ambapo vitu vyote katika jumba lako la kifalme, na vyote ambavyo baba zako waliweka akiba mpaka siku hii, vitachukuliwa kwenda Babeli. Hakuna chochote kitakachosalia, asema Bwana.
Voici que des jours viendront où l'on emportera à Babylone tout ce qui est dans ta maison et ce que tes pères ont amassé jusqu'à ce jour; il n'en restera rien, dit Yahweh.
18 Nao baadhi ya wazao wako, nyama yako na damu yako mwenyewe watakaozaliwa kwako, watachukuliwa mbali, nao watakuwa matowashi katika jumba la mfalme wa Babeli.”
Et l'on prendra de tes fils, qui seront sortis de toi, que tu auras engendrés, pour en faire des eunuques dans le palais du roi de Babylone. »
19 Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la Bwana ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Lakini si patakuwa na amani na usalama wakati wa uhai wangu?”
Ezéchias répondit à Isaïe: « La parole de Yahweh que tu as prononcée est bonne. » Et il ajouta: « Oui, car la paix et la stabilité seront avec moi pendant ma vie. »
20 Matukio mengine ya utawala wa Hezekia, mafanikio yake yote, na jinsi alivyotengeneza bwawa na mfereji ambao ulileta maji katika mji, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
Le reste des actes d'Ezéchias, tous ses exploits, et comment il fit l'étang et l'aqueduc et amena les eaux dans la ville, cela n'est-il pas écrit dans le livre des Chroniques des rois de Juda?
21 Hezekia akafa, akazikwa pamoja na baba zake. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.
Ezéchias se coucha avec ses pères, et Manassé, son fils, régna à sa place.

< 2 Wafalme 20 >