< 2 Wafalme 2 >
1 Wakati Bwana alipokuwa karibu kumchukua Eliya mbinguni kwa upepo wa kisulisuli, Eliya na Elisha walikuwa njiani wakitoka Gilgali.
Quand l’Eternel fit monter Elie au ciel dans un tourbillon, Elle et Elisée quittaient Ghilgal.
2 Eliya akamwambia Elisha, “Kaa hapa. Bwana amenituma Betheli.” Lakini Elisha akasema, “Kwa hakika, kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Kwa hiyo wakaenda Betheli pamoja.
Elie dit à Elisée: "Reste ici, de grâce, car l’Eternel m’a donné une mission pour Béthel. Vive Dieu et par ta propre vie! répondit Elisée, je ne te quitterai pas." Et ils se rendirent ensemble à Béthel.
3 Wana wa manabii waliokuwako huko Betheli wakamjia Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Elisha akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
Les jeunes prophètes établis à Béthel allèrent au-devant d’Elisée et lui dirent: "Sais-tu que l’Eternel t’enlève aujourd’hui ton maître, ton guide?" Il répondit: "Silence, oui, je le sais."
4 Kisha Eliya akamwambia, “Baki hapa, Elisha. Bwana amenituma Yeriko.” Naye akajibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko.
Elie reprit: "Elisée, reste ici, car l’Eternel m’a confié une mission pour Jéricho. Vive l’Eternel, répliqua-t-il, et par ta propre vie! Je ne te quitterai pas." Et ils vinrent ensemble à Jéricho.
5 Wana wa manabii waliokuwako huko Yeriko wakamwendea Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
Les jeunes prophètes établis à Jéricho se rendirent auprès d’Elisée et lui dirent: "Sais-tu que l’Eternel t’enlève aujourd’hui ton maître, ton guide? Silence, répondit-il, oui, je le sais."
6 Kisha Eliya akamwambia, “Kaa hapa. Bwana amenituma kwenda Yordani.” Naye akamjibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wote wawili wakaendelea pamoja.
Et Elie dit de nouveau: "Reste ici, je te prie, car l’Eternel m’envoie du côté du Jourdain." Il répondit: "Vive l’Eternel et par ta propre vie! Je ne te quitterai pas." Et ils continuèrent ensemble leur route.
7 Wana hamsini wa manabii wakaenda na kusimama kwa mbali, kuelekea mahali ambapo Eliya na Elisha walikuwa wamesimama kando ya Mto Yordani.
Cinquante jeunes prophètes allèrent, de leur côté, et se placèrent en vue d’eux à une certaine distance; les deux prophètes s’étaient arrêtés près du Jourdain.
8 Eliya akachukua vazi lake, akalisokota na kupiga nalo maji. Maji yakagawanyika upande wa kuume na upande wa kushoto, nao wawili wakavuka pakavu.
Elie prit son manteau, le roula, en frappa les eaux, qui se séparèrent en deux, et ils passèrent ensemble à pieds secs.
9 Walipokwisha kuvuka, Eliya akamwambia Elisha, “Niambie, nikufanyie nini kabla sijaondolewa kutoka kwako?” Elisha akajibu, “Naomba nirithi sehemu maradufu ya roho yako.”
Pendant qu’ils traversaient, Elie dit à Elisée: "Exprime un désir; que puis-je faire pour toi avant que je te sois enlevé?" Elisée répondit: "Puissé-je avoir une double part de l’esprit qui t’inspire!
10 Eliya akasema, “Umeomba jambo gumu. Lakini kama utaniona wakati ninapoondolewa kutoka kwako litakuwa lako. La sivyo, hautalipata.”
Tu as demandé quelque chose de difficile, répondit Elie; tu seras cependant satisfait si tu me vois disparaître à tes yeux, mais sinon, non."
11 Walipokuwa wakitembea pamoja na kuzungumza, ghafula gari la moto na farasi wa moto vilitokea na kuwatenganisha wao wawili, naye Eliya akapanda mbinguni katika upepo wa kisulisuli.
Ils, poursuivaient leur chemin en conversant, quand tout à coup un char de feu, attelé de chevaux de feu, les sépara l’un de l’autre, et Elie monta au ciel dans un tourbillon.
12 Elisha aliona hili, naye akapaza sauti, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya Israeli na wapanda farasi wake!” Naye Elisha hakumwona tena. Kisha akazishika nguo zake mwenyewe na kuzirarua.
A cette vue, Elisée s’écria: "Mon père, mon père! Char et cavalerie d’Israël!" Et il ne le vit plus. Alors il saisit ses vêtements, et les déchira de part en part.
13 Akaliokota lile vazi lililoanguka kutoka kwa Eliya, kisha akarudi na kusimama ukingoni mwa Yordani.
Puis il ramassa le manteau qui était tombé des épaules d’Elie, et retourna sur les rives du Jourdain, où il s’arrêta.
14 Ndipo akalichukua lile vazi ambalo lilikuwa limeanguka kutoka kwa Eliya, naye akayapiga yale maji nalo. Akauliza, “Yuko wapi sasa Bwana, Mungu wa Eliya?” Elisha alipoyapiga maji, yakagawanyika kulia na kushoto, naye akavuka.
Il prit le manteau qui était tombé des épaules d’Elie, et en frappa les eaux en s’écriant: "Où est l’Eternel, le Dieu d’Elie?" et sous ses coups les eaux se séparèrent devant lui également, et il passa.
15 Wale wana wa manabii kutoka Yeriko waliokuwa wakitazama wakasema, “Roho wa Eliya inamkalia Elisha.” Nao wakaenda kumlaki na kusujudu hadi nchi mbele yake.
Les jeunes prophètes de Jéricho avaient vu de loin ce qui s’était passé, et ils dirent: "L’Esprit d’Elie repose sur Elisée." Ils allèrent à sa rencontre, et se prosternèrent devant lui jusqu’à terre.
16 Wakasema, “Tazama, sisi watumishi wako tunao watu hamsini wenye uwezo. Waruhusu waende kumtafuta bwana wako. Labda Roho wa Bwana amemtwaa na kumweka katika mlima fulani au bonde fulani.” Elisha akajibu, “Hapana, msiwatume.”
Ils lui dirent: "Il y a parmi tes serviteurs cinquante hommes vaillants: laisse-les donc aller à la recherche de ton maître. Peut-être le souffle de l’Eternel l’a-t-il emporté et jeté sur une des montagnes, ou dans une des vallées. N’Envoyez personne," répliqua-t-il.
17 Lakini wakasisitiza, mpaka akaona aibu kuwakatalia. Hivyo akasema, “Watumeni.” Nao wakawatuma watu hamsini, wakamtafuta kwa siku tatu, lakini hawakumpata.
Mais ils insistèrent au point de l’embarrasser, et il dit: "Envoyez!" Ils envoyèrent cinquante hommes, qui cherchèrent le prophète pendant trois jours, mais sans le trouver.
18 Walipomrudia Elisha, ambaye alikuwa akingojea huko Yeriko, akawaambia, “Je, sikuwaambia msiende?”
Quand ils revinrent auprès d’Elisée, qui était resté à Jéricho, il leur dit: "Ne vous avais-je pas conseillé de ne pas aller?"
19 Watu wa mji wakamwambia Elisha, “Tazama, bwana wetu, mahali mji huu ulipojengwa ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo, lakini maji yake ni mabaya, na nchi haizai.”
Or, les habitants de Jéricho dirent à Elisée: "Le séjour de cette ville est agréable, comme mon seigneur le voit; mais l’eau y est malsaine et le sol meurtrier."
20 Akasema, “Nileteeni bakuli mpya, mweke chumvi ndani yake.” Kwa hiyo wakamletea.
Il répondit: "Apportez-moi une cruche neuve que vous remplirez de sel;" et on la lui apporta.
21 Kisha akaenda kwenye chemchemi na kuitupa ile chumvi ndani yake, akisema, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nimeyaponya maji haya. Kamwe hayatasababisha mauti tena wala kutozaa.’”
Il alla vers la source d’où venait l’eau et y jeta le sel en disant: "Telle est la parole de l’Eternel: Je vais rendre ces eaux salubres, et elles ne causeront plus ni mort ni ravages."
22 Nayo yale maji yakaponywa mpaka leo, sawasawa na neno la Elisha alilokuwa amesema.
Les eaux devinrent salubres, jusqu’au jour présent, selon la prédiction faite par Elisée.
23 Kutoka huko Elisha akakwea kwenda Betheli. Ikawa alipokuwa akitembea barabarani, baadhi ya vijana wakatoka mjini na kumfanyia mzaha. Wakasema, “Paa, wewe mwenye upaa! Paa, wewe mwenye upaa!”
Il se rendit de là à Béthel. Il suivait la montée, quand de jeunes garçons, sortant de la ville, l’insultèrent en ces termes: "Monte, chauve, monte, chauve!"
24 Akageuka, akawatazama na kuwalaani kwa Jina la Bwana. Kisha dubu wawili wa kike wakatokea mwituni na kuwararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao.
Il se retourna pour les voir, et les maudit au nom de l’Eternel. Aussitôt, deux ours sortirent de la forêt et mirent en pièces quarante-deux de ces enfants.
25 Naye akaondoka huko, akaenda Mlima Karmeli, na kutoka huko akarudi Samaria.
De là, il se dirigea vers le mont Carmel, d’où il revint à Samarie.