< 2 Wafalme 2 >
1 Wakati Bwana alipokuwa karibu kumchukua Eliya mbinguni kwa upepo wa kisulisuli, Eliya na Elisha walikuwa njiani wakitoka Gilgali.
Lorsque Yahweh fit monter Elie au ciel dans un tourbillon, Elie s’en allait de Galgala avec Elisée.
2 Eliya akamwambia Elisha, “Kaa hapa. Bwana amenituma Betheli.” Lakini Elisha akasema, “Kwa hakika, kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Kwa hiyo wakaenda Betheli pamoja.
Elie dit à Elisée: « Reste ici, je te prie, car Yahweh m’envoie jusqu’à Béthel. » Elisée répondit: « Yahweh est vivant et ton âme est vivante! Je ne te quitterai point! » Et ils descendirent à Béthel.
3 Wana wa manabii waliokuwako huko Betheli wakamjia Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Elisha akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
Les fils des prophètes qui étaient à Béthel sortirent vers Elisée, et lui dirent: « Sais-tu que Yahweh enlèvera aujourd’hui ton maître de dessus ta tête? » Il répondit: « Je le sais aussi; tenez-vous en paix. »
4 Kisha Eliya akamwambia, “Baki hapa, Elisha. Bwana amenituma Yeriko.” Naye akajibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko.
Elie lui dit: « Elisée, reste ici, je te prie, car Yahweh m’envoie à Jéricho. » Il répondit: « Yahweh est vivant et ton âme est vivante! Je ne te quitterai point! » Et ils arrivèrent à Jéricho.
5 Wana wa manabii waliokuwako huko Yeriko wakamwendea Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
Les fils des prophètes qui étaient à Jéricho s’approchèrent d’Elisée et lui dirent: « Sais-tu que Yahweh enlèvera aujourd’hui ton maître de dessus ta tête? » Il répondit: « Je le sais aussi; tenez-vous en paix. »
6 Kisha Eliya akamwambia, “Kaa hapa. Bwana amenituma kwenda Yordani.” Naye akamjibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wote wawili wakaendelea pamoja.
Elie lui dit: « Reste ici, je te prie, car Yahweh m’envoie au Jourdain. » Il répondit: « Yahweh est vivant et ton âme est vivante! Je ne te quitterai point! » Et ils s’en allèrent tous deux.
7 Wana hamsini wa manabii wakaenda na kusimama kwa mbali, kuelekea mahali ambapo Eliya na Elisha walikuwa wamesimama kando ya Mto Yordani.
Cinquante hommes d’entre les fils des prophètes allèrent après eux et se tinrent à distance, à l’opposé, et eux deux s’arrêtèrent au bord du Jourdain.
8 Eliya akachukua vazi lake, akalisokota na kupiga nalo maji. Maji yakagawanyika upande wa kuume na upande wa kushoto, nao wawili wakavuka pakavu.
Alors Elie, prenant son manteau, le roula et en frappa les eaux, qui se partagèrent d’un côté et de l’autre, et ils passèrent tous deux à sec.
9 Walipokwisha kuvuka, Eliya akamwambia Elisha, “Niambie, nikufanyie nini kabla sijaondolewa kutoka kwako?” Elisha akajibu, “Naomba nirithi sehemu maradufu ya roho yako.”
Lorsqu’ils eurent passé, Elie dit à Elisée: « Demande ce que tu veux que je fasse pour toi, avant que je sois enlevé d’avec toi. » Elisée répondit: « Que vienne sur moi une double portion de ton esprit? »
10 Eliya akasema, “Umeomba jambo gumu. Lakini kama utaniona wakati ninapoondolewa kutoka kwako litakuwa lako. La sivyo, hautalipata.”
Elie dit: « Tu demandes une chose difficile. Si tu me vois pendant que je serai enlevé d’avec toi, il t’arrivera ainsi; sinon, cela n’arrivera pas. »
11 Walipokuwa wakitembea pamoja na kuzungumza, ghafula gari la moto na farasi wa moto vilitokea na kuwatenganisha wao wawili, naye Eliya akapanda mbinguni katika upepo wa kisulisuli.
Ils continuaient de marcher en s’entretenant, et voici qu’un char de feu et des chevaux de feu les séparèrent l’un de l’autre, et Elie monta au ciel dans un tourbillon.
12 Elisha aliona hili, naye akapaza sauti, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya Israeli na wapanda farasi wake!” Naye Elisha hakumwona tena. Kisha akazishika nguo zake mwenyewe na kuzirarua.
Elisée regardait et criait: « Mon père! mon père! Char d’Israël et ses cavaliers! » Et il ne le vit plus. Il saisit alors ses vêtements et les déchira en deux morceaux,
13 Akaliokota lile vazi lililoanguka kutoka kwa Eliya, kisha akarudi na kusimama ukingoni mwa Yordani.
et il releva le manteau d’Elie qui était tombé de dessus lui. Puis, étant revenu au Jourdain, il s’arrêta sur le bord;
14 Ndipo akalichukua lile vazi ambalo lilikuwa limeanguka kutoka kwa Eliya, naye akayapiga yale maji nalo. Akauliza, “Yuko wapi sasa Bwana, Mungu wa Eliya?” Elisha alipoyapiga maji, yakagawanyika kulia na kushoto, naye akavuka.
et, prenant le manteau d’Elie qui était tombé de dessus lui, il en frappa les eaux et dit: « Où est Yahweh, le Dieu d’Elie? Où est-il? » Lorsqu’il eut frappé les eaux, elles se partagèrent d’un côté et de l’autre, et Elisée passa.
15 Wale wana wa manabii kutoka Yeriko waliokuwa wakitazama wakasema, “Roho wa Eliya inamkalia Elisha.” Nao wakaenda kumlaki na kusujudu hadi nchi mbele yake.
Les fils des prophètes qui étaient à Jéricho, à l’opposé, le virent et dirent: « L’esprit d’Elie repose sur Elisée; » et, allant à sa rencontre, ils se prosternèrent contre terre devant lui.
16 Wakasema, “Tazama, sisi watumishi wako tunao watu hamsini wenye uwezo. Waruhusu waende kumtafuta bwana wako. Labda Roho wa Bwana amemtwaa na kumweka katika mlima fulani au bonde fulani.” Elisha akajibu, “Hapana, msiwatume.”
Ils lui dirent: « Voici qu’il y a parmi tes serviteurs cinquante hommes vaillants: qu’ils aillent donc chercher ton maître. Peut-être que l’Esprit de Yahweh, l’ayant emporté, l’a jeté sur une des montagnes ou dans une des vallées. » Il répondit: « Ne les envoyez pas. »
17 Lakini wakasisitiza, mpaka akaona aibu kuwakatalia. Hivyo akasema, “Watumeni.” Nao wakawatuma watu hamsini, wakamtafuta kwa siku tatu, lakini hawakumpata.
Mais ils le pressèrent jusqu’à le couvrir de confusion, et il leur dit: « Envoyez-les. » Ils envoyèrent cinquante hommes, qui cherchèrent Elie pendant trois jours, sans le trouver.
18 Walipomrudia Elisha, ambaye alikuwa akingojea huko Yeriko, akawaambia, “Je, sikuwaambia msiende?”
Lorsqu’ils furent de retour auprès d’Elisée, — car il demeurait à Jéricho, — il leur dit: « Ne vous avais-je pas dit: N’allez pas? »
19 Watu wa mji wakamwambia Elisha, “Tazama, bwana wetu, mahali mji huu ulipojengwa ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo, lakini maji yake ni mabaya, na nchi haizai.”
Les gens de la ville dirent à Elisée: « Le séjour de la ville est bon, comme le voit mon seigneur; mais les eaux sont mauvaises et le pays est stérile. »
20 Akasema, “Nileteeni bakuli mpya, mweke chumvi ndani yake.” Kwa hiyo wakamletea.
Il dit: « Apportez-moi une écuelle neuve, et mettez-y du sel. » Et ils la lui apportèrent.
21 Kisha akaenda kwenye chemchemi na kuitupa ile chumvi ndani yake, akisema, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nimeyaponya maji haya. Kamwe hayatasababisha mauti tena wala kutozaa.’”
Il alla vers la source des eaux et, y ayant jeté du sel, il dit: « Ainsi dit Yahweh: J’assainis ces eaux; il n’en proviendra plus ni mort, ni stérilité. »
22 Nayo yale maji yakaponywa mpaka leo, sawasawa na neno la Elisha alilokuwa amesema.
Et les eaux furent assainies jusqu’à ce jour, selon la parole qu’Elisée avait dite.
23 Kutoka huko Elisha akakwea kwenda Betheli. Ikawa alipokuwa akitembea barabarani, baadhi ya vijana wakatoka mjini na kumfanyia mzaha. Wakasema, “Paa, wewe mwenye upaa! Paa, wewe mwenye upaa!”
Il monta de là à Béthel; et comme il montait par la route, des petits garçons sortirent de la ville et se moquèrent de lui; ils lui disaient: « Monte, chauve! monte, chauve! »
24 Akageuka, akawatazama na kuwalaani kwa Jina la Bwana. Kisha dubu wawili wa kike wakatokea mwituni na kuwararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao.
Il se retourna pour les regarder, et il les maudit au nom de Yahweh. Et deux ours sortirent de la forêt et déchirèrent quarante-deux de ces enfants.
25 Naye akaondoka huko, akaenda Mlima Karmeli, na kutoka huko akarudi Samaria.
De là il alla sur la montagne de Carmel, et de là il revint à Samarie.