< 2 Wafalme 2 >

1 Wakati Bwana alipokuwa karibu kumchukua Eliya mbinguni kwa upepo wa kisulisuli, Eliya na Elisha walikuwa njiani wakitoka Gilgali.
Comme Yahvé était sur le point d'enlever Élie au ciel par un tourbillon, Élie partit de Gilgal avec Élisée.
2 Eliya akamwambia Elisha, “Kaa hapa. Bwana amenituma Betheli.” Lakini Elisha akasema, “Kwa hakika, kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Kwa hiyo wakaenda Betheli pamoja.
Élie dit à Élisée: « Attends ici, car Yahvé m'a envoyé jusqu'à Béthel. » Élisée dit: « Aussi vrai que Yahvé est vivant et que ton âme est vivante, je ne te quitterai pas. » Ils descendirent donc à Béthel.
3 Wana wa manabii waliokuwako huko Betheli wakamjia Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Elisha akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
Les fils des prophètes qui étaient à Béthel sortirent vers Élisée et lui dirent: « Sais-tu que Yahvé va enlever aujourd'hui ton maître de dessus toi? » Il a dit: « Oui, je le sais. Tiens-toi tranquille. »
4 Kisha Eliya akamwambia, “Baki hapa, Elisha. Bwana amenituma Yeriko.” Naye akajibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko.
Élie lui dit: « Élisée, attends ici, car l'Éternel m'a envoyé à Jéricho. » Il dit: « Aussi vrai que Yahvé est vivant et que ton âme est vivante, je ne te quitterai pas. » Ils arrivèrent donc à Jéricho.
5 Wana wa manabii waliokuwako huko Yeriko wakamwendea Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
Les fils des prophètes qui étaient à Jéricho s'approchèrent d'Élisée et lui dirent: « Sais-tu que Yahvé va enlever aujourd'hui ton maître de dessus toi? » Il a répondu: « Oui, je le sais. Tiens-toi tranquille. »
6 Kisha Eliya akamwambia, “Kaa hapa. Bwana amenituma kwenda Yordani.” Naye akamjibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wote wawili wakaendelea pamoja.
Élie lui dit: « Attends ici, car l'Éternel m'a envoyé au Jourdain. » Il dit: « Aussi vrai que Yahvé vit et que ton âme vit, je ne te quitterai pas. » Et ils partirent tous deux.
7 Wana hamsini wa manabii wakaenda na kusimama kwa mbali, kuelekea mahali ambapo Eliya na Elisha walikuwa wamesimama kando ya Mto Yordani.
Cinquante hommes d'entre les fils des prophètes allèrent se placer à distance en face d'eux, et ils se tinrent tous deux au bord du Jourdain.
8 Eliya akachukua vazi lake, akalisokota na kupiga nalo maji. Maji yakagawanyika upande wa kuume na upande wa kushoto, nao wawili wakavuka pakavu.
Élie prit son manteau, l'enroula, et frappa les eaux; elles se divisèrent ici et là, et ils passèrent tous deux à sec.
9 Walipokwisha kuvuka, Eliya akamwambia Elisha, “Niambie, nikufanyie nini kabla sijaondolewa kutoka kwako?” Elisha akajibu, “Naomba nirithi sehemu maradufu ya roho yako.”
Lorsqu'ils eurent traversé, Élie dit à Élisée: « Demande ce que je peux faire pour toi, avant que je sois enlevé d'avec toi. » Elisha a dit, « S'il te plaît, qu'une double portion de ton esprit soit sur moi. »
10 Eliya akasema, “Umeomba jambo gumu. Lakini kama utaniona wakati ninapoondolewa kutoka kwako litakuwa lako. La sivyo, hautalipata.”
Il dit: « Tu as demandé une chose difficile. Si tu me vois quand on m'enlèvera de toi, il en sera ainsi pour toi; sinon, il n'en sera pas ainsi. »
11 Walipokuwa wakitembea pamoja na kuzungumza, ghafula gari la moto na farasi wa moto vilitokea na kuwatenganisha wao wawili, naye Eliya akapanda mbinguni katika upepo wa kisulisuli.
Comme ils continuaient à parler, voici qu'un char de feu et des chevaux de feu les séparèrent; et Élie monta au ciel dans un tourbillon.
12 Elisha aliona hili, naye akapaza sauti, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya Israeli na wapanda farasi wake!” Naye Elisha hakumwona tena. Kisha akazishika nguo zake mwenyewe na kuzirarua.
Élisée le vit, et il s'écria: « Mon père, mon père, les chars d'Israël et ses cavaliers! » Il ne le vit plus. Puis il saisit ses propres vêtements et les déchira en deux morceaux.
13 Akaliokota lile vazi lililoanguka kutoka kwa Eliya, kisha akarudi na kusimama ukingoni mwa Yordani.
Il prit aussi le manteau d'Élie qui était tombé de lui, et s'en retourna se placer sur la rive du Jourdain.
14 Ndipo akalichukua lile vazi ambalo lilikuwa limeanguka kutoka kwa Eliya, naye akayapiga yale maji nalo. Akauliza, “Yuko wapi sasa Bwana, Mungu wa Eliya?” Elisha alipoyapiga maji, yakagawanyika kulia na kushoto, naye akavuka.
Il prit le manteau d'Élie qui était tombé de lui, frappa les eaux, et dit: « Où est Yahvé, le Dieu d'Élie? » Quand il eut aussi frappé les eaux, elles se séparèrent, et Élisée passa outre.
15 Wale wana wa manabii kutoka Yeriko waliokuwa wakitazama wakasema, “Roho wa Eliya inamkalia Elisha.” Nao wakaenda kumlaki na kusujudu hadi nchi mbele yake.
Lorsque les fils des prophètes qui étaient à Jéricho, en face de lui, le virent, ils dirent: « L'esprit d'Élie repose sur Élisée. » Ils vinrent à sa rencontre et se prosternèrent à terre devant lui.
16 Wakasema, “Tazama, sisi watumishi wako tunao watu hamsini wenye uwezo. Waruhusu waende kumtafuta bwana wako. Labda Roho wa Bwana amemtwaa na kumweka katika mlima fulani au bonde fulani.” Elisha akajibu, “Hapana, msiwatume.”
Ils lui dirent: « Vois maintenant, il y a avec tes serviteurs cinquante hommes forts. Laisse-les, je te prie, aller chercher ton maître. Peut-être l'Esprit de Yahvé l'a-t-il enlevé et déposé sur quelque montagne ou dans quelque vallée. » Il a dit: « Ne les envoyez pas. »
17 Lakini wakasisitiza, mpaka akaona aibu kuwakatalia. Hivyo akasema, “Watumeni.” Nao wakawatuma watu hamsini, wakamtafuta kwa siku tatu, lakini hawakumpata.
Comme ils le pressaient jusqu'à la honte, il dit: « Envoyez-les. » Ils envoyèrent donc cinquante hommes; ils cherchèrent pendant trois jours, mais ne le trouvèrent pas.
18 Walipomrudia Elisha, ambaye alikuwa akingojea huko Yeriko, akawaambia, “Je, sikuwaambia msiende?”
Ils revinrent vers lui pendant qu'il restait à Jéricho, et il leur dit: « Ne vous ai-je pas dit: « N'y allez pas? »
19 Watu wa mji wakamwambia Elisha, “Tazama, bwana wetu, mahali mji huu ulipojengwa ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo, lakini maji yake ni mabaya, na nchi haizai.”
Les hommes de la ville dirent à Élisée: « Voici, je vous en prie, la situation de cette ville est agréable, comme le voit mon seigneur; mais l'eau est mauvaise, et le pays est stérile. »
20 Akasema, “Nileteeni bakuli mpya, mweke chumvi ndani yake.” Kwa hiyo wakamletea.
Il dit: « Apportez-moi une jarre neuve, et mettez-y du sel. » On la lui apporta.
21 Kisha akaenda kwenye chemchemi na kuitupa ile chumvi ndani yake, akisema, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nimeyaponya maji haya. Kamwe hayatasababisha mauti tena wala kutozaa.’”
Il sortit vers la source des eaux, y jeta du sel, et dit: « L'Éternel dit: 'J'ai guéri ces eaux. Il n'y aura plus de mort ni de désert à partir de là ».
22 Nayo yale maji yakaponywa mpaka leo, sawasawa na neno la Elisha alilokuwa amesema.
Et les eaux furent guéries jusqu'à ce jour, selon la parole qu'Élisée avait prononcée.
23 Kutoka huko Elisha akakwea kwenda Betheli. Ikawa alipokuwa akitembea barabarani, baadhi ya vijana wakatoka mjini na kumfanyia mzaha. Wakasema, “Paa, wewe mwenye upaa! Paa, wewe mwenye upaa!”
De là, il monta à Béthel. Comme il montait par le chemin, des jeunes gens sortirent de la ville, se moquèrent de lui et lui dirent: « Monte, chauve! Monte, chauve! »
24 Akageuka, akawatazama na kuwalaani kwa Jina la Bwana. Kisha dubu wawili wa kike wakatokea mwituni na kuwararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao.
Il regarda derrière lui et les vit, et il les maudit au nom de Yahvé. Deux ourses sortirent alors des bois et déchiquetèrent quarante-deux de ces jeunes gens.
25 Naye akaondoka huko, akaenda Mlima Karmeli, na kutoka huko akarudi Samaria.
De là, il se rendit au Carmel et de là, il retourna à Samarie.

< 2 Wafalme 2 >